Light Upon Light Summit in Zanzibar Set to Inspire and Unite Global Muslim Community12th & 13th October 2024.

 

Zanzibar, Tanzania – The much-anticipated Light Upon Light Summit is set to take place on the beautiful island of Zanzibar on 12th and 13th October 2024. Organized by Light Upon Light (London) in collaboration with The Grand Mufti's Office of Zanzibar, this prestigious event will bring together leading Islamic scholars, thought leaders, and over 15,000 attendees for two transformative days of learning, reflection, and spiritual growth. The summit’s featured guest will be the renowned Islamic scholar, Sheikh Ismail ibn Musa Menk (Mufti Menk), Grand Mufti of Zimbabwe.


The Light Upon Light Summit will address crucial societal topics such as Unity, Peace and Respect. Additionally, the summit in Collaboration with The Zanzibar Commission for Tourism will promote the growth of Halaal Tourism in Zanzibar, a sector currently valued globally at USD 250 billion. Attendees from Tanzania, East Africa, the United Kingdom, and GCC nations will converge for this unique opportunity to engage in knowledge exchange, foster social unity, and explore investment opportunities.


• Day 1 (12th October 2024):


The summit will take place at Amani Stadium, Zanzibar, where participants will engage with Islamic scholars through inspirational sermons, Quran recitations, and captivating Nasheed performances.


• Day 2 (13th October 2024):


A more exclusive Gala Dinner and Motivational Evening will be held at Hotel Verde, limited to 400 attendees. This exclusive gathering will allow participants to connect with scholars and explore the potential for Muslim-Friendly Tourism investments in Zanzibar.



Get Your Tickets Now!


Tickets are available online at www.nilipe.co.tz or at the following physical locations:


Dar-es-Salaam:


• Karak House - Masaki


• Taste Me - Coco Beach


• Kanzu Point - City Mall


Zanzibar:


• Poaz Grill - Mlandege


• Taste Me - Mazizini


This is an opportunity not to be missed! Engage with world-renowned scholars, contribute to essential social discussions, and help shape the future of Zanzibar’s tourism and social unity. Purchase your tickets today and be part of this extraordinary event.



Thank You to Our Sponsors:


We would like to extend our heartfelt gratitude to the following sponsors for their generous support in making this event possible:


• Silent Ocean


• KCB Bank


• CRDB Bank


• Ashton Media


• Mjini FM


• Clouds Media


• Vista Print


• Infinity Development


• Azam


Your contributions are helping to make this event a truly remarkable and impactful gathering.
Share:

Benki ya Biashara DCB kuendelea kuboresha Maisha ya Watanzania

Mwenyekiti wa Bodi ya Benki ya Biashara ya DCB, Bi. Zawadia Nanyaro (wa nne kulia) akishikana mikono na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Biashara ya DCB, Bw. Sabasaba Moshingi baada ya kumaliza Mkutano Mkuu wa 22 wa Mwaka wa Wanahisa wa benki hiyo uliofanyika kwa njia ya mtandao jijini Dar es Salaam leo.

*Yajivunia kutoa Mikopo ya zaidi ya Shs Bilioni 740 Tokea Ilipoanzishwa

BENKI YA BIASHARA YA DCB imesema itaendelea kusimamia misingi ya kuanzishwa kwake ambayo ni kusaidia miradi endelevu ya kupunguza umasikini, kuendeleza jamii na kutoa huduma bora zinazokidhi mahitaji halisi ya kila siku ya wateja wao.

Akizungumza jijini Dar es Salaam leo wakati wa Mkutano Mkuu wa 22 wa Mwaka wa Wanahisa wa benki ya Biashara DCB, Mkurugenzi Mtendaji wa benki hiyo, Bw. Sabasaba Moshingi alisema, tokea kuanzishwa kwa DCB, takriban miaka 22 iliyopita benki hiyo imeendelea kukua mwaka hadi mwaka ikiendelea kutoa masuluhisho tofauti kwa wateja wake wa kada zote na hivyo kudhihirisha ukweli kuwa DCB ni ‘Mkombozi wa Kweli’ wa maisha ya watanzania.

Ikiwa ni Mkutano wake Mkuu wa kwanza tokea ajiunge na DCB, Bw. Moshingi akileta uzoefu wake wa miongo kadhaa katika tasnia za kibenki anasema benki inaendelea kujivunia kuwa kiongozi katika kuleta ufumbuzi wa tatizo la mitaji ya kibiashara kwa wajasiriamali wadogo wadogo kwa kuingiza sokoni bidhaa zenye ubunifu na kwa kutumia teknolojia za kisasa zinazoendana na mageuzi ya sayansi na teknolojia yanayoendelea duniani kote.

Benki ya Biashara DCB imekuwa mstari wa mbele katika kutoa mikopo kwa wajasiriamali wadogo wanaopata changamoto za kupata huduma hizo katika baadhi ya taasisi za kifedha kutokana na kutokidhi masharti waliyoweka, lakini pia tumeendelea kufanya vizuri katika mikopo ya watu binafsi na vikundi vya wajasiriamali huku tukiendelea kuboresha mikopo hiyo ili iendane na mahitaji yao, kwa kipindi cha miaka 22 tokea DCB imeanzishwa, tunajivunia kutoa mikopo yenye thamani ya zaidi ya shs bilioni 741 iliyowanufaisha zaidi ya watanzania 420,000”, alisema Bwana Moshingi.

Katika kipindi hiki cha mwaka mmoja tokea mkurugenzi mtendaji huyu mpya aingie madarakani, Benki ya biashara DCB imepiga hatua kadhaa za maendeleo ikiwa ni pamoja uimarishaji wa huduma za kibenki kwa njia za kidigitali pamoja na kuanzisha mikopo yenye lengo la kuinua maisha ya makundi maalumu hususan wanawake wajasiriamali.

Tumeanzisha huduma maalumu iitwayo ‘Tausi’ ikiwalenga wanawake yenye lengo la kuinua vipato vya wanawake wajasiriamali wadogo, tukianzia na mikoa ya Dar es Salaam, Pwani na Dodoma kwa kutoa mikopo ya kuendeleza biashara zao, kuwapa elimu ya kifedha pamoja na mbinu za uendeshaji wa biashara".

Sifa za kuwa mwanachama lazima uwe mkazi wa eneo husika, uwe na biashara, tukitumia mfumo wa kikundi kinachoanzia watu 15 hadi 30 wenye umri kuanzia miaka 18 mpaka 65, huku mikopo ikianzia 300,000 hadi milioni 1 kutegemea na aina ya biashara ya mteja na marejesho ni kati ya miezi mitano hadi 10”.

Bwana Moshingi anaongeza kuwa mbali na mikopo ya wanawake, DCB pia imeendelea kufanya vizuri katika mikopo mingine ya vikundi, mikopo ya nyumba, mikopo ya wafanyakazi hususan walimu, mikopo ya guta, pikipiki na bajaji na mingineyo.

Kwa upande wa huduma za jamii, benki yetu imekuwa mstari wa mbele pia katika kuisaidia serikali yetu katika kuwaletea watu wake maendelea hususan katika nyanja za elimu na afya kupitia miradi yetu mbalimbali inayoendelea, bila kusahau akaunti maalumu ya elimu ya DCB Skonga yenye lengo la kuboresha elimu ya watoto wetu".

Mwaka jana tulikabidhi madawati katika shule tano za Manispaa zote za jiji la Dar es Salaam na kauli mbiu isemayo ‘Elimu Mpango Mzima na Mama Samia’ tukikusudia kukabidhi madawati 1000 katika shule mbalimbali nchini kati ya mwaka 2023 na 2025, mradi huu unaendelea vizuri na wiki ijayo tutakabidhi baadhi ya madawati haya katika Shule ya Msingi ya Msisiri B, Kinondoni, jijini Dar es Salaam”, alisema.

Aidha anaongeza, “Ukiacha hayo benki yetu imeendelea kuwa mstari wa mbele katika kuuunga mkono serikali yetu katika miradi yake ya kimkakati kama tulivyofanya hivi karibuni tulipodhamini walimu 1000 kutoka Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam kwenda kufanya utalii katika mbuga za mikumi kwa kutumia treni ya SGR, kwa kufanya hivyo tunasaidia kuitangaza treni hii pamoja na utalii wa nchi yetu ndani na nje ya Tanzania”.

Pamoja na hayo mkurugenzi huyo anasema DCB imeendelea pia kufanya vizuri katika huduma na akaunti nyingine zikiwemo; Wahi Akaunti, akaunti ya mshahara, mikopo ya nusu mshahara, akaunti za wastaafu, huduma za malipo ya serikali (GePG) pamoja na malipo mengine kwa watoa huduma mbalimbali yanayofanyika katika matawi ya benkina kwa njia za mtandao.

Kaimu Mkurugenzi wa Fedha DCB, Bwana Siriaki Surumbu alisema benki imeendelea kukuza mapato ikijikita katika shughuli za utoaji mikopo yenye ubora hasa kwa vikundi maalum vya wanawake na wajasiliamali mbalimbali. Maboresho katika vitengo mbalimbali vya huduma hususan huduma za kidigitali ambazo zitaongeza ufanisi katika utoaji huduma na kuongeza mapato ya benki.

Naye Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya DCB, Bi. Zawadia Nanyaro alisema benki imekuwa mstari wa mbele katika kuunga mkono juhudi za serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan katika ajenda yake ya kuona huduma za kibenki zinawafikia watanzania wote wakifanya huduma zao za kibenki kwa njia za kidigitali kuwa bora zaidi na zenye gharama nafuu.

Bi Nanyaro alisema kwa sasa mkakati wa kuhahakisha huduma zake zinapatikana nchi nzima unaendelea vizuri ukiwezeshwa na uimarishaji wa huduma hizo, kusambaa kwa mtandao wa mawakala zaidi ya 1000 nchini kote pamoja na vituo vidogo 1500 vya kutolea huduma katika maeneo ya kimkakati.

Nipende kutoa shukurani kwa serikali yetu chini ya uongozi wa Mheshimiwa Rais wetu Mama Samia Suluhu Hassan kwa kuweka mazingira yanayosaidia sekta ya fedha kufanya biashara katika mazingira bora na wezeshi, lakini pia kwa kuona umuhimu wa kushirikisha sekta binafasi katika miradi ya kimkakati inayoendelea kwa mafanikio katika sehemu mbalimbali nchini".

Nipende pia kuwahakikishia wanahisa wetu, wateja wetu na wadau wetu kuwa benki yenu ipo katika mikono salama na inaendelea vizuri chini ya uongozi wa Bwana Moshingi, menejimenti, wafanyakazi wote pamoja na Bodi ya wakurugenzi".

Tunachohitaji tu ni ushirikiano kutoka kwenu wanahisa wote, wadau pamoja na wateja wetu ili benki yetu izidi kufanya vizuri sokoni na kutekeleza mikakati yote ya maendeleo tuliyojiwekea".

Natoa wito kwa watanzania wote kujiunga na benki yetu na kufaidika na fursa mbalimbali za huduma bora za kibenki tunazozitoa, DCB ni Mkombozi wa Kweli kwa watanzania wote, Wajasiriamali wadogo na wa kati, wanawake na vijana, DCB ni Mkombozi wa Kweli kwa wafanyabiashara wa kada zote”, anamaliza Bi Nanyaro.
Mwenyekiti wa Bodi ya Benki ya Biashara ya DCB, Bi. Zawadia Nanyaro, akizungumza na wanahisa wakati wa Mkutano Mkuu wa 22 wa mwaka wa Wanahisa wa benki hiyo uliofanyika kwa jijini Dar es Salaam leo. Bi Zawadia alisema DCB Itaendelea kusimamia misingi ya kuanzishwa kwake ambayo ni kusaidia miradi endelevu ya kupunguza umasikini, kuendeleza jamii na kutoa huduma bora zinazokidhi mahitaji halisi ya kila siku ya wateja wao.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Biashara ya DCB, Bw. Sabasaba Moshingi , akizungumza na wanahisa wakati wa Mkutano Mkuu wa 22 wa mwaka wa Wanahisa wa benki hiyo uliofanyika jijini Dar es Salaam leo. Bwana Moshingi aliwaambia wanahisa kuwa DCB chini ya uongozi wake, kwa kushirikiana na Bodi pamoja na wafanyakazi wote wamejizatiti kuandika upya historia ya benki hiyo na hii ikianza kuonekana baada ya DCB kufanya vizuri katika robo ya kwanza na ya pili mwaka huu.
Mwanasheria Mshauri wa Benki ya Biashara ya DCB, Bw. Alex Mgongolwa, akizungumza na wanahisa wakati wa Mkutano Mkuu wa 22 wa mwaka wa Wanahisa wa benki uliofanyika jijini Dar es Salaam leo.
Mwenyekiti wa Kamati ya Bodi ya Ukaguzi na Usimamizi wa Benki ya Biashara ya DCB, Prof. Tadeo Satta, akizungumza na wanahisa wakati wa Mkutano Mkuu wa 22 wa mwaka wa Wanahisa wa benki hiyo uliofanyika jijini Dar es Salaam leo.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Biashara ya DCB, Bw. Sabasaba Moshingi (kulia) akizungumza na baadhi ya wawakilishi wa wanahisa wa benki hiyo wakati wa Mkutano Mkuu wa 22 wa mwaka wa Wanahisa wa benki hiyo uliofanyika jijini Dar es Salaam leo. Kutoka kushoto ni Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Jiji la Dar es Salaam, Bw. Selemani Kateti, Mwakilishi kutoka UTT AMIS, Bw. Medson Enock na Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Manispaa ya Kigamboni, Bw. Rajab Gondomo.

Kuhusu DCB

Benki ya Biashara ya DCB ilianzishwa mwaka 2002 na mwaka unaofuata kupewa leseni ya kujiendesha kama benki ya kijamii, ikijulikana kama Benki ya Watu wa Dar es Salaam ‘Dar es Salaam Community Bank’ ambayo wanahisa wake waanzilishi wakiwa ni Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam pamoja na Manispaa zake za Ilala, Kinondoni na Temeke. Wanahisa wengine ni Mifuko ya NHIF na UTT AMIS pamoja na wananchi wa kawaida.

Kuanzishwa kwa DCB kulitokana na maono ya Rais mstaafu wa awamu za tatu, Hayati Benjamin William Mkapa kutoka na kilio cha wananchi wenye kipato cha chini na cha kati kukosa mikopo ya mitaji katika benki za kibiashara kutokana na kutokidhi vigezo vilivyowekwa.

Katika miaka hii 22 tokea kuanzishwa kwa DCB, benki imepitia hatua mbalimbali; ilikuwa benki ya kwanza kuorodheshwa katika Soko la Hisa la Dar es salaam (DSE) mnamo mwaka 2008, ambapo Februari 2012 ilifanikiwa kuhuisha leseni yake kutoka benki ya kijamii na kuwa benki kamili ya kibiashara na kubadilisha jina kutoka Benki ya Watu wa Dar es Salaam na kuwa Benki ya Biashara ya DCB.

Benki ya DCB ina mtandao wa matawi 9 ya kibenki ndani na nje ya Dar es Salaam ikiwa na mtandao wa mawakala 1000 na vituo vya kutolea huduma 1500 sehemu mbalimbali nchini. Ina zaidi ya mashine 280 za ATM zilizounganishwa na Umoja Switch, lakini pia inatumia Kadi za Visa zinazoweza kutumika katika mashine zinazosapoti kadi hizo ndani na nje ya nchi.
Share:

Mkurugenzi mshauri wa USAID afanya ziara kukagua miradi ya USAID Afya Yangu na Kizazi Hodari Kanda ya Kusini

MSHAURI Mkuu wa kiufundi wa watoto yatima na walioko katika mazingira magumu kutoka USAID Sarah Dastur akiwa kwenye picha na baadhi ya wanafunzi wa shule ya msingi ya JJ Mungai iliyopo Manispaa ya Iringa baada ya kuwatembelea walengwa wanaonufaika na miradi ya USAID Afya yangu na Kizazi Hodari, Kanda ya Kusini mwishoni mwa wiki.

Iringa Jumatatu Agosti 5 2024, MSHAURI Mkuu wa kiufundi wa watoto yatima na walioko katika mazingira magumu kutoka USAID Sarah Dastur amefanya ziara ya siku moja ndani ya Mkoa wa Iringa kwa lengo la kuwatembelea walengwa wanaonufaika na miradi ya USAID Afya yangu na Kizazi Hodari, Kanda ya Kusini. Miradi hiyo miwili inatekelezwa na Deloitte Consulting Limited kupitia shirika la Msaada Kutoka Kwa Watu Wa Marekani.

Miradi hiyo inalenga kushughulikia utoaji wa huduma ya afya kwa wanaoishi na maambukizi ya UKIMWI, kifua kikuu, uzazi wa mpango pamoja na mapambano dhidi ya ukatili wa kijinsia Nchini Tanzania.

Sarah Dastur alitembelea shule ya Msingi ya JJ Mungai kuona miradi inavyowasaidia wanafunzi hao hasa katika mapambano ya ukatili wa kijinsia dhidi yao, aliwatembea walengwa wanaoishi na maambukizi ya UKIMWI eneo Isakalilo, pia alitembelea hospital ya Tosamaganga moja ya hospital zinazotoa huduma ya dawa kwa ya kufubaza virusi vya UKIMWI (ARV).

Moja ya wanaufaika wa mradi wa USAID Afya yangu ambaye ameomba kutotajwa jina lake wala kuchukuliwa picha ameshukuru mradi huo kuwa Mkombozi na Msaada Mkubwa kwa watanzania wengi hasa wale wenye uwezo wa chini kwa kuwarudushia tabasamu.

Aidha alitoa ombi kwa niaba ya wenzake uongezwe usiri kwa vituo/ club ambazo wanakutana vijana wanaoishi na maambukizi ya UKIMWI kwa lengo la kubadilishana mawazo kwani vingi vipo katikati ya muingiliano wa watu jambo ambalo linaondoa ufalagha wao akieleza linachochea hali ya unyanyapaa kwa watu wenye Elimu hasi.
Dkt Stella Mtera ambaye ni Msimamizi wa kitengo cha CTC hospitali ya Tosamaganga iliyopo manispaa ya Iringa akimsikiliza MSHAURI Mkuu wa kiufundi wa watoto yatima na walioko katika mazingira magumu kutoka USAID Sarah Dastur wakati alipotembelea walengwa wanaonufaika na miradi ya USAID Afya yangu na Kizazi Hodari, Kanda ya Kusini mwishoni mwa wiki.
Share:

Benki ya DCB yaunga mkono jitihada za serikali ujenzi wa Reli ya SGR

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mhe. Albert Chalamila, akihutubia mkoani humo jana, katika hafla ya kuwaaga walimu zaidi ya 1000 wa Mkoa huo kabla hawajaondoka Kwa treni ya SGR kuelekea Morogoro na baadae Mikumi katika ziara yao ilidhaminiwa na Benki ya Biashara ya DCB kusaidia mkakati wa kuitangaza SGR na utalii kupitia Royal Tour. Kutoka Morogoro, DCB ilitoa mabasi 30 kusafirisha walimu hao hadi Mikumi.

Katika kuunga mkono juhudi zilizofanywa na serikali inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan za ujenzi wa reli ya kisasa ya SGR pamoja na kukuza utalii kupitia Royal Tour, Benki ya Biashara ya DCB imedhamini safari ya walimu zaidi ya 1000 kutumia treni ya SGR kutoka Dar es Salaam hadi Morogoro na kisha Mikumi ili kukuza utalii wa ndani na kujifunza mambo yatakayowasaidia wanafunzi wao wawapo madarasani.

Akizungumza katika hafla ya kuwaaga walimu hao kutoka Jiji la Dar es Salaam, katika Stesheni ya SGR, jijini humo jana, Mkurugenzi Mtendaji wa DCB, Bw. Sabasaba Moshingi alisema taasisi yao imeshirikiana na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa huo kuwapa nafasi walimu hao kutembelea mbuga za wanyama ya Mikumi ili kujionea vivutio vya utalii vitakavyowasaidia kuwafundisha wanafunzi wa mashuleni.

Alisema DCB inamilikiwa na Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam ambalo ndiko wanakotoka walimu hao hivyo akawashauri kutumia huduma zilizoboreshwa za benki hiyo kama vile kuweka amana, bima mbalimbali na mikopo yenye masharti nafuu ili kuboresha maisha yao na kuacha kuangukia katika taasisi zinazotoa mikopo inayowaumiza na yenye masharti magumu.

Naye Mkurugenzi wa Biashara wa benki hiyo, Bw. Ramadhan Mganga alisema DCB ndio mkombozi halisi wa watanzania kwani wanazo huduma na bidhaa tofauti zinazokidhi mahitaji ya kibenki ya watanzania hivyo kutoa hamasa kwa walimu hao na kwa watanzania kwa ujumla kuchangamkia huduma hizo.

Aidha alisema ili kufanikisha safari hiyo wamedhamini mabasi 30 yatakayowasafirisha walimu hao kutoka Morogoro kwenda Mikumi ikiwa pia ni kutambua mchango wa walimu hao katika maendeleo ya benki yao.

Awali akizungumza katika hafla hiyo, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Bw. Albert Chalamila aliipongeza DCB Kwa kufanikisha safari hiyo ya walimu akisema ofisi yake itaendelea kuandaa safari kwa makundi mengine ikiwa ni sehemu ya mkakati wa muda mrefu wa kuitangaza treni ya SGR.

Ziara hii sio tu itaongeza maarifa kwa walimu kupitia ziara ya Mikumi, bali pia itaongeza chachu ya kampeni inayoendelea ya Royal Tour,”alisema.

Benki ya Biashara ya DCB ilianzishwa mwaka 2002 ikitokana na wito wa Rais wa awamu ya tatu, Hayati, William Benjamin Mkapa, kufuatia kilio cha mitaji cha wananchi wenye kipato cha chini na cha kati wa Jiji la Dar es Salaam kukosa mikopo katika benki nyingi za kibiashara kwa kutokidhi vigezo vilivyokuwa vikiweka na benki hizo.
Mkurugenzi wa Biashara wa Benki ya DCB, Bw. Ramadhan Mganga akizungumza kuhusu udhamini wa benki hiyo Kwa ziara ya walimu 1000 wa Mkoa wa Dar es Salaam kwa ziara yao kwenda Mikumi kwa kutumia treni ya SGR kutokea mkoani humo jana. Benki ya imedhamini mabasi 30 Ili kusafirisha walimu hao kutoka Morogoro kuelekea Mikumi Ili kusaidia mkakati wa kuitangaza SGR na utalii kupitia Royal Tour.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mhe. Albert Chalamila (katikati), akisalimiana na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya DCB, Bw. Sabasaba Moshi mkoani humo jana, wakati wa hafla ya kuwaaga walimu zaidi ya 1000 wa Mkoa huo kabla hawajaondoka katika stesheni ya SGR kuelekea Morogoro na baadae Mikumi katika ziara yao ilidhaminiwa na DCB kusaidia mkakati wa kuitangaza SGR na Royal Tour. Kutoka Morogoro, DCB ilitoa mabasi 30 kusafirisha walimu hao hadi Mikumi.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya DCB, Bw. Sabasaba Moshingi (kulia), akisalimiana na Katibu Tawala wa Mkoa wa Dar es Salaam, Dk. Toba Nguvila, mkoani humo jana, wakati wa hafla ya kuwaaga walimu zaidi ya 1000 wa Mkoa wa Dar es Salaam, kabla hawajaondoka kwa treni ya SGR kuelekea Morogoro na baadae Mikumi katika ziara yao ilidhaminiwa na Benki ya Biashara ya DCB ili kusaidia mkakati wa kuitangaza SGR na Royal Tour. Kutoka Morogoro, DCB ilitoa mabasi 30 kusafirisha walimu hao hadi Mikumi.
Baadhi ya walimu kutoka jijini Dar es Salaam wakiwasili kwa treni ya SGR mjini Morogoro jana, wakiwa safarini kuelekea katika mbuga za wanyama ya Mikumi. Benki ya Biashara ya DCB ili kusaidia mkakati wa kuitangaza SGR na Royal Tour imedhamini safari hiyo Kwa kutoa mabasi 30 kusafirisha walimu hao hadi mbugani huko kutoka Morogoro.
Share:

TCB YAINGIA MKATABA WA MAKUBALIANO NA ZEEA KUWEZESHA MIKOPO VIKUNDI MAALUM

Benki  ya Biashara Tanzania (TCB)  imesaini mkataba wa makubaliano (MOU) na Wakala wa serikali wa uwezeshaji wananchi kiuchumi zanzibar ( ZEEA) Makubaliano haya ya kimkakati yanalenga kuanzisha mpango maalum wa mikopo utakaonufaisha makundi maalum wakiwemo wanawake na vijana wanaojihusisha na shughuli za kiuchumi visiwani Zanzibar. Mpango huu unakusudia kuchochea ukuaji wa biashara, ongezeko la ajira, na maendeleo ya kiuchumi katika ukanda huu wa Afrika Mashariki.

Akishuhudia kusainiwa kwa hati hizo jijini Dar es salaam Katibu mkuu ofisi ya Raisi kazi uchumi na Uwekezaji zanzibar Mariam amesema tayari shilingi bilioni 2 zimeshakusanywa na halmashauri visiwani humo ili kuanza uwezeshaji akiitaka benki ya TCB kuhakikisha inafanya tathmini ya mikopo wanayotoa kwa makundi hayo ili ziweze kurejeshwa kwa wakati na wengine waweze kukopa .


Ameeleza kuwa mpango huu wa mikopo umekusudiwa kutia chachu juhudi za kijasiriamali,kuwapa wajasiriamali uthubutu wa kuanzisha na kupanua biashara zao. Malengo ya uwezeshaji huu ni kuwa chanzo cha mabadiliko mengine kama kuimarisha uchumi wa ndani, kuunga mkono juhudi za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kupambana na ukosefu wa ajira na kuleta maendeleo na kuwa Kupata fursa ya mikopo ni muhimu kwa maendeleo na ukuaji wa biashara ndogondogo na za kati

Kwa upande wake Afisa mtendaji mkuu wa TCB ADAM MIHAYO amesema Mkataba huu wa makubaliano unathibitisha dhamira ya Benki ya TCB kuwezesha uchumi jumuishi na maendeleo ya kiuchumi kwa ujumla na kwamba Mkataba huu wa makubaliano unathibitisha dhamira ya Benki ya TCB kuwezesha uchumi jumuishi na maendeleo ya kiuchumi kwa ujumla.

Amesema  mkataba huo utawezesha  kutoa mikopo nafuu kwa makundikiasi cha shilingi milioni 30 kwa kikundi, huku wakipewa muda miezi 24 sawa na miaka miwili Kwa kutoa mikopo nafuu kwa makundi hayo, TCB na ZEEA watawasaidia wajasiriamali kupanua biashara zao, kutengeneza fursa mpya za ajira, na hivyo kupunguza uhaba wa ajira.

Mpango huu pia utazisaidia biashara kujiendesha, kukabiliana na mfumuko wa bei, pamoja na kuwekeza katika vitendea kazi, na kuzipa ustahimilivu,Tuna furaha kushirikiana na ZEEA kuwainua wajasiriamali wanawake, vijana na makundi mengine maalum yaliyomo visiwani Zanzibar,” alisema Adam Mihayo,Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya TCB. 

Kwa upande wake mkurugenzi Mtendaji wa ZEEA Juma Burhan Mohamed amesema wanalenga kuipatia benki ya TCb kiasi cha shilingi bilioni 1.8 ili waanze utoaji wa mikopo hiyo  na kwamba Mpango huu unaendana na lengo  la kuwezesha maendeleo ya kiuchumi kwa kujenga uchumi jumuishi Kwa
kuyawezesha makundi maalum, wanaziinua biashara binafsi, pamoja na kuimarisha mfumo mzima wa uchumi na kutengeneza mazingira imara ya
kiuchumi.” alisema
Mbali na kuchangia maendeleo ya kiuchumi, makubaliano haya pia yanakusudia kuimarisha uchumi wa buluu visiwani Zanzibar. Kupitia mikopo hii itakayoinua biashara ndani katika sekta hii, TCB na ZEEA wanapigia chapuo eneo hili nyeti la shughuli za kiuchumi lenye uwezo wa kuchangia maendeleo kwa kiasi kikubwa.

Mchango wa Benki ya TCB katika kuunga mkono jitihada za Serikali katik na kupokea maombi ya mkopo yanayofikia wastani wa Mpango huu wa mikopo umekusudiwa kutia chachu juhudi za kijasiriamali, kuwapa wajasiriamali uthubutu wa kuanzisha na kupanua biashara zao Malengo ya uwezeshaji huu ni kuwa chanzo cha mabadiliko mengine kama kuimarisha biashara na uchumi.

Share:

UINGEREZA KUENDELEA KUFADHILI MIRADI YA UKIMWI NCHINI

Balozi wa Uingereza nchini Tanzania, Mhe. David Concar, akikabidhi cheti kwa mmoja wa washiriki wenye umri mdogo wa Kampeni ya kupanda mlima kilimanjaro ya GGM Kili Challenge, Regina Enos Baraka (kulia), mara baada ya kumaliza zoezi la kupanda na kushuka mlima huo, mjini Moshi, Kilimanjaro, hivi karibuni. Kampeni hiyo ya kila mwaka ina lengo la kusaidia miradi inayojikita katika kutokomeza VVU na Ukimwi imendaliwa na Kampuni ya Dhahabu ya Geita Gold Mining kwa kushirikiana na Tume ya Taifa ya Kudhibiti Ukimwi (TACAIDS) ambapo jumla ya wapanda mlima 48 na waendesha baisketi 23 walishiriki. Regina anaishi katika Kituo cha Moyo wa Huruma cha Geita kilichoanzishwa kwa msaada kutoka Mfuko wa Kili Challenge.

Balozi wa Uingereza nchini, Mhe. David Concar amesema nchi yake itaendelea kuunga mkono juhudi zinazofanywa na Serikali ya Tanzania katika kupambana na ugonjwa wa Ukimwi Ili kutimiza malengo ya Kimataifa ya muda wa kati na mrefu ili kuona hakuna maambukizi mapya, unyanyapaa na vifo vinavyohusiana na VVU .

Balozi Concar aliyasema hayo wakati wa mapokezi ya wapanda mlima Kilimanjaro 71 walikuwa wakishiriki Kampeni ya kila mwaka ya GGM Kili Challenge mjini Moshi, Kilimanjaro, inayoandaliwa na Kampuni ya Dhahabu ya Geita Gold Mining kwa kushirikiana na Tume ya Taifa ya Kupambana na Ukimwi (TACAIDS)

Njia kuu ambayo Uingereza inafanya ni kuwa mmoja wachangiaji wakubwa wa Mfuko wa Kimataifa wa kupambana na UKIMWI, Kifua Kikuu na Malaria, kwa miaka mitatu kutoka 2024 hadi 2026, Uingereza itatoa pauni bilioni 1 kwa mfuko huo, ambao kwa jumla utatoa dola milioni 602 kwa Tanzania."

Nitoe pongezi kwa AngloGold Ashanti na Bodi ya Wadhamini ya Geita Gold Mining Limited Kilimanjaro Challenge dhidi ya HIV/AIDS pamoja na TACAIDS kwa kuifanya Kili Challenge kuwa tukio la kila mwaka la kupendeza likileta ujumbe wa nguvu kwa wanaoishi na VVU”, alisema.

Akizungumza katika hafla hiyo, Mwakilishi ukutoka Geita Gold Mining, Mhandisi Nzuamkende alisema kampeni hiyo inayofanyika Kwa mwaka wa 22, inalenga kukusanya fedha kuchangia jitihada za Serikali ya Tanzania kufikia malengo ya sifuri tatu (Maambukizi mapya Sifuri, Unyanyapaa Sifuri na vifo vinavyohusiana na UKIMWI Sifuri).

Tunapokusanyika hapa ili kusherehekea mafanikio yenu, ninatoa shukrani zangu za dhati kwa kila mmoja wenu kwa kukabiliana na hofu zenu, na kushinda mojawapo ya milima mirefu zaidi na yenye changamoto duniani."

Juhudi zenu, kwenye miteremko ya Mlima Kilimanjaro na kwenye njia tambarare za baiskeli, hazijadhihirisha tu nguvu ya uamuzi na umoja lakini pia zimeleta athari kubwa katika dhamira yetu ya pamoja ya kupambana na VVU na UKIMWI, mmetuonyesha kwamba hakuna changamoto isiyoweza kuzuilika tunapokutana kwa sababu moja na kwa hilo, nawapongeza nyote”, alisema.

Aidha aliwashukuru wafadhili na washiriki wote kutokana na michango yao inayoendelea kufanikisha Kampeni hiyo hadi kuufanya Mfuko wa Kili Challenge Against HIV/AIDS Trust kuwa mfuko wa kimataifa, unaohusisha wapanda mlima na waendesha baiskeli kutoka mabara yote na zaidi ya nchi 20.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TACAIDS, Dk. Jerome Kamwela alisema Tanzania inafanya vizuri kueleka malengo ya kimataifa ya muda mrefu na wa kati ambayo ni kufikia 95 tatu kufikia mwaka 2025 ambazo kama tawimu za karibuni zinavyoonesha kuwa kuna watu milioni 1.7 wanaishi na VVU, hivyo 95 ya kwanza ni kuona watu hao wanatambuliwa na kujua hali zao ambapo sasa imefika asilimia 83, huku 95 ya pili ni wale wanaoishi na VVU watumie dawa za kufubaza makali ya ukimwi (ARV) ambapo Tanzania imevuka lengo kwa kufikisha asilimia 98 na 95 ya tatu wale wanaotumia ARV asilimia 95 wawe wamefubaza virusi, utafiti wa mwisho unaonyesha maambukizi mapya yakipungua.

Nao baadhi ya washiriki wenye umri mdogo waliopanda Mlima Kilimanjaro, Regina Baraka na Baraka Erasto, kutoka kituo cha Moyo wa Huruma cha mkoani Geita, kilichoanzishwa kupitia mfuko wa Kili Challenge walielezwa kufurahishwa kwa uzoefu walioupata Kwa mara ya kwanza wakipanda mlimani hivyo kutoa hamasa Kwa vijana wadogo wenye umri kama wao kujitokeza kushiriki katika Kampeni hiyo Ili kuweza kuleta mabadiliko kwa wenye VVU.
Balozi wa Uingereza nchini Tanzania, Mhe. David Concar, akikabidhi cheti kwa mmoja wa washiriki wenye umri mdogo wa Kampeni ya kupanda mlima kilimanjaro ya GGM Kili Challenge, Baraka Erasto (kulia), mara baada ya kumaliza zoezi la kupanda na kushuka mlima huo, mjini Moshi, Kilimanjaro, hivi karibuni. Kampeni hiyo ya kila mwaka ina lengo la kusaidia miradi inayojikita katika kutokomeza VVU na Ukimwi imendaliwa na Kampuni ya Dhahabu ya Geita Gold Mining kwa kushirikiana na Tume ya Taifa ya Kudhibiti Ukimwi (TACAIDS) ambapo jumla ya wapanda mlima 48 na waendesha baisketi 23 walishiriki. anaishi katika Kituo cha Moyo wa Huruma cha Geita kilichoanzishwa kwa msaada kutoka Mfuko wa Kili Challenge.
Balozi wa Uingereza nchini Tanzania, Mhe. David Concar, akihutubia katika hafla ya kuwapokea wapanda mlima Kilimanjaro waliokuwa wakishiriki kampeni ya kila mwaka ya GGM Kili Challenge yenye lengo la kusaidia miradi inayojikita katika kutokomeza VVU na Ukimwi. Kampeni hiyo imendaliwa na Kampuni ya Dhahabu ya Geita Gold Mining kwa kushirikiana na Tume ya Taifa ya Kudhibiti Ukimwi (TACAIDS) ambapo jumla ya wapanda mlima 48 na waendesha baisketi 23 walishiriki zoezi hilo lilioanza Julai 19 kufikia tamati yake mjini humo hivi karibuni.
Share:

Benki ya Absa Tanzania Yazindua Akaunti ya Akiba ya Vijana

Mkuu wa Kitengo cha Wateja Binafsi wa Benki ya Absa Tanzania, Bi. Ndabu Swere (katikati), akizungumza na waandishi wa habari wakati wa uzinduzi wa akaunti ya akiba ya vijana ya benki hiyo, jijini Dar es Salaam leo. Kushoto ni Mkuu wa Masoko na Mahusiano, Bw. Aron Luhanga na Meneja Bidhaa, Bw. George Kaindoah.
Baadhi ya waandishi kutoka vyombo mbalimbali vya habari wakiwa kazini wakati wa uzinduzi wa akaunti ya akiba ya vijana ya Benki ya Absa, jijini Dar es Salaam leo.

Benki ya Absa Tanzania imezindua akaunti ya Akiba ya Vijana, bidhaa mpya ya kifedha iliyoundwa mahsusi kwa vijana wa Kitanzania wenye umri wa miaka 18 hadi 30. Hafla rasmi ya uzinduzi iliyofanyika leo, inaashiria hatua muhimu katika kujitolea kwa benki kuwawezesha vijana na kukuza utamaduni wa kuweka akiba.

Akizungumza katika hafla ya uzinduzi, Bi. Ndabu Swere, Mkuu wa Kitengo cha Wateja Binafsi wa Benki ya Absa Tanzania, alielezea furaha yake katika kuzindua bidhaa hii mpya na kusisitiza umuhimu wake. “Leo tuko hapa kushuhudia uzinduzi wa bidhaa ya kipekee kutoka Absa Bank Tanzania - Akaunti ya Akiba ya Vijana ya Absa. Akaunti hii inalenga vijana wenye umri wa miaka 18 hadi 30, kundi ambalo linawakilisha sehemu kubwa ya idadi ya Watanzania,” alisema Bi. Swere.

Akaunti ya Akiba ya Vijana ya Absa imeundwa ili kuziba pengo muhimu katika soko. Wakati Benki ya Absa inatoa Akaunti za Akiba kwa Watoto wenye umri chini ya miaka 18, zinazosimamiwa na wazazi au walezi, kumekuwa na uhaba wa bidhaa maalum kwa vijana. Pengo hili mara nyingi limewalazimu vijana kutafuta huduma za kifedha mahali pengine, jambo ambalo linaifanya benki kuwa na changamoto ya kuwavuta tena mara wanapomaliza masomo na kuanza ajira au kuanzisha biashara zao.

Akaunti yetu mpya ya Akiba ya Vijana inashughulikia suala hili, ikilingana na kujitolea kwetu katika kanuni za ESG na kuwaunga mkono vijana wa Tanzania,” aliongeza Bi. Swere. “Katika Benki ya Absa Tanzania, tunaongozwa na dhamira yetu kuu ya 'Kuwawezesha Afrika kesho, pamoja, stori moja baada ya nyingine.' Leo, tunachukua hatua ya ujasiri kwa kuanzisha Akaunti ya Akiba ya Vijana ya Absa, iliyoundwa kukuza utamaduni wa kuweka akiba miongoni mwa vijana wetu.

Akaunti ya Akiba ya Vijana ya Absa inatoa faida nyingi, zikiwemo kuweka amana bure kupitia Absa Wakala, ATM, na matawi, kupewa kadi ya debit ya bure mteja anapofungua akaunti, huduma za benki za simu na za mtandao bure, kutokukatwa ada ya kila mwezi, ufikiaji wa akaunti saa 24/7 kupitia majukwaa ya kidijitali ya Absa, ushiriki katika programu na shughuli zinazolenga vijana, kama vile maonyesho ya kazi, matukio ya vijana, na semina, na kufaidika na mpango wa kurudishiwa pesa wa Absa Twin Rewards.

Kwa upande wake, Bw. Aron Luhanga, Mkuu wa Kitengo cha Masoko na Mahusiano ya Kampuni wa Absa, alisisitiza ahadi ya chapa ya benki, "Hadithi yako ina thamani," au kwa Kiingereza, “Your story matters.” “Huu kwetu ni zaidi ya msemo; ni ahadi ya kutembea pamoja na vijana, kuwasaidia katika safari ya maisha ili kuwasaidia kuandika stori bora zaidi. Tunaelewa kijana alikotoka, tunaona anakotaka kwenda, na tunaahidi kumpa msaada anaohitaji kuandika hadithi nzuri ambayo tutajivunia kuwa sehemu yake,” alisema.

Katika hitimisho lake, Bi. Swere aliwaalika vijana wote wa Kitanzania kuchukua fursa hii na kufungua Akaunti ya Akiba ya Vijana ya Absa. Akaunti hii imeundwa kusaidia vijana kujenga tabia ya kuweka akiba na kufaidika na faida za kipekee zinazotolewa na Benki ya Absa Tanzania.
Share:

LILIAN-FAVOUR MAKAWA

LILIAN-FAVOUR MAKAWA

Popular Posts

Blog Archive

Labels

Recent Posts

Label Cloud

BIASHARA (275) BURUDANI (4) KIMATAIFA (10) KITAIFA (119) MICHEZO (38) SIASA (3)

Pages