



Arusha - Wakulima wa Wilaya ya Karatu wanatarajiwa kunufaika kwa kiasi kikubwa na upatikanaji bora wa taarifa za masoko pamoja na kuongezeka kwa uwazi katika biashara ya mazao, kufuatia kuanzishwa kwa mpango wa kidijitali unaoongozwa na Mixx by Yas kwa kushirikiana na wadau wa sekta ya kilimo.
Mpango huo ulizinduliwa rasmi kupitia hafla ya makabidhiano ya runinga janja (Smart TV) iliyotolewa kwa Chama Kikuu cha Ushirika Arusha (ACU) kwa kushirikiana na Mamlaka ya Udhibiti wa Nafaka na Mazao Mchanganyiko (COPRA). Hatua hii inalenga kuboresha upatikanaji wa taarifa muhimu za masoko kwa wakulima na kuongeza ushiriki wao katika mifumo rasmi ya biashara.
Akizungumza katika hafla hiyo, Meneja wa Kibiashara Kanda ya Kaskazini wa Mixx by Yas, Eric Sosteness, alisema kuwa suluhisho za kidijitali zinatoa fursa mpya kwa wakulima kufikia masoko kwa urahisi zaidi.
“Kupitia Mixx by Yas, tumejikita kuwawezesha wakulima kwa kuwapatia suluhisho zinazowaleta karibu zaidi na masoko. Upatikanaji wa taarifa za mnada kwa wakati utawasaidia wakulima kufanya maamuzi sahihi na kuongeza kipato chao,” alisema.
Runinga hiyo janja inatarajiwa kuwa chombo muhimu katika kurusha moja kwa moja minada ya mazao ya kilimo. Kupitia teknolojia hiyo, wakulima wa Karatu na maeneo jirani wataweza kufuatilia mwenendo wa bei na shughuli za biashara bila kulazimika kuwepo katika eneo la mnada. Hatua hii inatarajiwa kuongeza uwazi, kupunguza upotoshaji wa taarifa, na kuimarisha ushindani wa haki katika soko.
Kwa upande wake, Meneja wa Mahusiano ya Biashara na Serikali wa Mixx by Yas, Suleiman Asilia, alisisitiza umuhimu wa ushirikiano kati ya sekta binafsi na taasisi za umma katika kuleta mageuzi ya kiuchumi kwa wakulima.
Naye Kaimu Mkuu wa COPRA Kanda ya Kaskazini, Famia Amiri, alibainisha kuwa urushaji wa moja kwa moja wa minada utaongeza uwazi na kujenga imani katika mfumo wa biashara ya mazao, hususan katika kipindi hiki ambacho nchi inaelekea msimu wa ufuta.“Ushirikiano huu unaonesha jinsi teknolojia na ubia vinavyoweza kufungua fursa mpya kwa wakulima. Lengo letu ni kuhakikisha wakulima wanaunganishwa zaidi, wanapata taarifa sahihi na wanajumuishwa kifedha,” alieleza.
Mbali na mpango huo, Mixx by Yas inaendelea kutoa huduma mbalimbali zinazolenga kumwezesha mkulima, ikiwemo Mixx Kilimo inayorahisisha miamala, Afya Mkulima inayolenga ustawi wa wakulima, pamoja na Kilimo Pesa inayowezesha upatikanaji wa huduma za kifedha kwa urahisi zaidi.
Kwa ujumla, mpango huu unaakisi mwelekeo wa sekta ya kilimo nchini kuelekea matumizi makubwa ya teknolojia katika kuboresha mifumo ya biashara. Kadri suluhisho hizi zinavyozidi kuenea, zinatarajiwa kuongeza tija, kuimarisha kipato cha wakulima, na kuwapa nafasi kubwa zaidi katika uchumi wa kisasa unaozidi kuwa wa kidijitali.












Taasisi ya Oya Micro-crediti imeandaa futari maalum kwa wateja wake na jamii kwa ujumla tukio lililolenga kuimarisha mshikamano wa kijamii.
Watoto kutoka kituo cha kulelea watoto mayatima kinondoni,wakitabasam kufurahia iftar iliyoandaliwa na taasisi ya Oya Micro-Credit ikiwa nikurudisha kwa jamii hasa katika mwezi huu mtukufu wa Ramadhani na Kwaresma
Mwezi Mtukufu wa Ramadhan ni wakati wa kutafakari, kushukuru, na kushirikiana na jamii katika kujitoa kwenye mambo mablimbali. Kwetu OYA, tunaamini kuwa mafanikio ya kweli hayapimwi tu kwa ukuaji wa biashara, bali pia kwa mchango chanya tunaoutoa kwa jamii inayotuzunguka.
Oya Micro-crediti tulipata heshima ya kuandaa Iftar dinner maalum iliyowaleta pamoja watumishi wetu, baadhi ya wateja na wageni maalum katika mazingira ya mshikamano na furaha.
Moja ya sehemu iliyogusa mioyo ya wengi ilikuwa uwepo wa watoto wazuri kutoka kituo cha kulelea watoto yatima kilichopo Kinondoni watoto hao walionesha Tabasamu lao lililota furaha kubwa na kutukumbusha maana halisi ya ya Mwezi Mtukufu wa Ramadhan — huruma, upendo, na kushirikiana.
Haikua tu hafla ya kufuturu pamoja, bali pia ya kuimarisha mahusiano, kujenga mshikamano wa kijamii, na kueneza matumaini matukio kama haya yanatukumbusha kuwa hata matendo madogo ya wema yanaweza kuleta furaha kubwa kwa wengine.Tunatoa shukrani zetu za dhati kwa kila mmoja aliyeshiriki na kuchangia kufanya siku hii iwe ya kipekee kadri mwezi wa Ramadhan unavyoendelea, OYA itaendelea kujitahidi kushirikiana na jamii na kuendeleza maadili ya umoja, huruma, na kusaidiana.
Kwa niaba ya familia nzima ya OYA, tunawatakia wote Ramadhan yenye baraka na amani. Alisema Mkurugenzi wa OYA Bwana. Alpha Peter
Ramadan Kareem. 🌙





