BENKI ZA ABSA NA TCB KUIMARISHA MAHUSIANO YA USHIRIKIANO WA KIMKAKATI

Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Obedi Laiser (kushoto), akisalimiana na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya TCB, Bw. Adam Mihayo, mara baada ya Bw. Laiser pamoja na ujumbe wake kumtembelea ofisini kwake, jijini Dar es Salaam jana, kwa mazungumzo yenye lengo la kuimarisha mahusiano ya ushirikiano wa kimkakati kati ya taasisi hizo mbili katika kuangalia fursa za kibiashara.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Obedi Laiser (kushoto), akimsikiliza Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya TCB, Bw. Adam Mihayo, mara baada ya Bw. Laiser pamoja na ujumbe wake kumtembelea ofisini kwake jijini Dar es Salaam jana, kwa mazungumzo yenye lengo la kuimarisha mahusiano ya ushirikiano wa kimkakati kati ya taasisi hizo mbili katika kuangalia fursa za kibiashara.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Obedi Laiser (wa pili kushoto), akizungumza na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya TCB, Bw. Adam Mihayo (kushoto), pamoja na baadhi ya maofisa wa benki hiyo, mara baada ya Bw. Laiser pamoja na ujumbe wake kumtembelea ofisini kwake jijini Dar es Salaam jana, kwa mazungumzo yenye lengo la kuimarisha mahusiano ya ushirikiano wa kimkakati kati ya taasisi hizo mbili katika kuangalia fursa za kibiashara.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Obedi Laiser (wa nne kushoto), Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya TCB, Bw. Adam Mihayo (wa tano kushoto), pamoja na baadhi ya maofisa kutoka benki zote mbili, wakipiga picha ya kumbukumbu mara baada ya Bw. Laiser pamoja na ujumbe wake kutembelea ofisini za TCB, jijini Dar es Salaam jana, kwa mazungumzo yenye lengo la kuimarisha mahusiano ya ushirikiano wa kimkakati kati ya taasisi hizo mbili katika kuangalia fursa za kibiashara.
Share:

BENKI ABSA TANZANIA YAENDELEA KUJIZATITI KUTOA HUDUMA BORA KWA WATEJA

Mtendaji Mkuu wa Kitengo Cha Wateja wa Makampuni (CIB), wa Absa Group kutoka Afrika Kusini, Bw. Zaid Moola (wa pili kulia), akizungumza na baadhi ya wateja wa makampuni (CIB), katika hafla iliyoandaliwa na Benki ya Absa Tanzania jijini Dar es Salaam leo, kama sehemu ya kudumisha ushikiriano wa kibiashara baina yao. kikao hicho pia kiliwakutanisha wateja hao na watendaji wakuu wa kitengo cha CIB kutoka Absa Group, waliopo nchini kwa ziara ya kikazi.

Katika kuendeleza ushirikiano na kutambua mchango mkubwa wa wateja wake wa Kitengo cha Corporate and Investment Banking (CIB), Benki ya Absa Tanzania leo imeandaa kikao cha kifungua kinywa cha kukutanisha wadau wa biashara jijini Dar es Salaam.

Kikao hicho kimetoa fursa kwa viongozi wa benki na wateja kufanya majadiliano ya wazi kuhusu fursa za ukuaji wa biashara, mwenendo wa masoko, pamoja na mustakabali wa sekta ya biashara nchini Tanzania.

Akizungumza katika hafla hiyo, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Obedi Laiser, amesema benki hiyo inaendelea kutoa huduma mbalimbali za kifedha zinazolenga kukidhi mahitaji ya wateja wake, hususan makampuni na taasisi zinazofanya biashara kubwa.

Aidha, hafla hiyo ilitumika kuwatambulisha viongozi waandamizi kutoka Kitengo cha Corporate and Investment Banking cha Absa Group, wakiongozwa na Mtendaji Mkuu wake, Bw. Zaid Moola, ambao walipata nafasi ya kukutana na kufanya mazungumzo ya moja kwa moja na wateja wakati wa ziara yao ya kikazi nchini Tanzania.

Ziara ya viongozi hao wa Absa Group inaonesha dhamira ya benki hiyo ya kuendelea kuimarisha mahusiano na wateja wake pamoja na kutoa suluhisho bunifu za kifedha zitakazosaidia biashara kukua na kustawi.

Hatua hiyo pia inaakisi dira ya Absa ya "Kuwezesha Afrika ya Kesho, Pamoja... Hadithi Moja Baada ya Nyingine."
Mtendaji Mkuu wa Kitengo cha Wateja wa Makampuni (CIB), wa Absa Group Kutoka Afrika Kusini, Bw. Zaid Moola (katikati), Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Obedi Laiser (kulia) na Mkurugenzi Mtendaji wa Wateja wa Makampuni wa Kanda ya Afrika, Bw. Sola Adegbesan, wakifurahi katika hafla iliyoandaliwa na Benki ya Absa jijini Dar es Salaam leo kwa wateja wa makampuni, kama sehemu ya kudumisha ushikiriano wa kibiashara baina yao. kikao hicho pia kiliwakutanisha wateja hao na watendaji hao kutoka absa group, waliopo nchini kwa ziara ya kikazi.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Obedi Laiser (kulia), akimsikiliza Ofisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi inayotoa huduma za kifedha ya ASA Microfinance, Bw. Muhammad Shah Newaj, katika hafla iliyoandaliwa na benki hiyo kwa wateja wake wa makampuni (CIB), jijini Dar es Salaam leo, kama sehemu ya kudumisha ushirikiano wa kibiashara baina yao. Kikao hicho pia kiliwakutanisha wateja hao na watendaji wakuu wa CIB kutoka Absa Group, waliopo nchini kwa ziara ya kikazi. Katikati ni Mkurugenzi wa Kitengo cha Masoko ya Fedha za Kigeni wa Benki ya Absa Tanzania, Bi. Irene Rwegalulira.
Mkurugenzi wa Masoko na Mahusiano wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Aron Luhanga akizungumza katika hafla waliyowaandaliwa wateja wa makampuni (CIB), jijini Dar es Salaam leo, kama sehemu ya kudumisha ushikiriano wa kibiashara baina yao. kikao hicho pia kiliwakutanisha wateja hao na watendaji wakuu wa kitengo cha CIB kutoka Absa Group, waliopo nchini kwa ziara ya kikazi.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Obedi Laiser (wa pili kushoto), akimsikiliza Mkurugenzi wa Kitengo cha Masoko ya Fedha za Kigeni wa benki hiyo, Bi. Irene Rwegalulira, wakati wa hafla iliyoandaliwa na benki hiyo kwa wateja wake wa makampuni (CIB), jijini Dar es Salaam leo. Wengine kutoka Kushoto ni Mkurugenzi wa Wateja wa Makampuni wa Absa Tanzania, Bi. Nellyana Mmanyi, Mkurugenzi wa Masoko na Mahusiano, Bw. Aron Luhanga na Mkuu wa Kitengo cha Shughuli za kibenki wa benki hiy, Bw. Alred Urasa.
Mkurugenzi Mtendaji wa Mtandao wa Wateja wa Absa Group, Bw. Clive Potter (kushoto), akizungumza na baadhi ya wateja wa makampuni (CIB), katika hafla iliyoandaliwa na Benki ya Absa Tanzania jijini Dar es Salaam leo, kama sehemu ya kudumisha ushikiriano wa kibiashara baina yao. Katikati ni Mkurugenzi wa Fedha wa Amref Health Africa, Bw. Damas Nugashe na Mkurugenzi Mtendaji wa Savanna Fibre Tanzania, Bw. Thomas Wenanga.
Mtendaji Mkuu wa Wateja wa Makampuni (CIB) wa Absa Group, Bw. Zaid Moola, baadhi ya watendaji wakuu kutoka Absa Group, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Obedi Laiser, baadhi ya wafanyakazi na wateja wa CIB, wakipiga picha ya pamoja mara baada ya kumalizika kwa kikao hicho jijini Dar es Salaam leo.
Share:

WAZIRI MASAUNI AONGOZA SAVE SOIL WALKATHON, ATOA WITO WA KULINDA UDONGO NA MAZINGIRA

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Mhe. Mhandisi Hamad Yussuf Masauni, ameongoza mamia ya wananchi na wadau mbalimbali wa mazingira katika matembezi ya Save Soil Walkathon, huku akitoa wito kwa Watanzania kushiriki kikamilifu katika juhudi za kulinda udongo na mazingira kwa ajili ya maendeleo endelevu ya taifa.

Mhe. Masauni, ambaye alikuwa mgeni rasmi wa tukio hilo, alishiriki matembezi hayo yaliyoandaliwa na Lions Club of Dar es Salaam Mazingira chini ya kaulimbiu ya “Save Soil, Save Our Future” (Linda Udongo, Linda Mustakabali Wetu).
Tukio hilo liliwakutanisha wadau wa mazingira, taasisi mbalimbali, sekta binafsi na wananchi katika kampeni ya kuongeza uelewa kuhusu umuhimu wa kuhifadhi afya ya udongo na matumizi endelevu ya rasilimali za asili.

Akizungumza baada ya matembezi hayo, Mhe. Masauni alisema afya ya udongo ni msingi wa usalama wa chakula, uhifadhi wa mazingira na ustawi wa uchumi wa taifa, hivyo kuna umuhimu wa kila Mtanzania kushiriki katika juhudi za kuutunza.

"Udongo ni rasilimali muhimu inayobeba maisha yetu ya kila siku. Bila udongo wenye afya hatuwezi kuwa na usalama wa chakula, mazingira bora wala maendeleo endelevu. Ni wajibu wa kila Mtanzania kushiriki katika juhudi za kulinda mazingira na kutumia ardhi kwa njia zinazohifadhi uhai wake kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho," alisema Mhe. Masauni.

Katika kuonesha kwa vitendo dhamira ya kulinda mazingira, Mhe. Masauni pia alipanda mti ikiwa ni ishara ya kujitolea katika uhifadhi wa udongo na mazingira pamoja na kuhamasisha wananchi kushiriki katika upandaji miti kama sehemu ya juhudi za kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi na uharibifu wa ardhi.
Kwa upande wake, Rais wa Lions Club of Dar es Salaam Mazingira, Lion Ramadevi, alisema Save Soil Walkathon ni sehemu ya kampeni pana inayolenga kuhamasisha jamii kutambua mchango mkubwa wa udongo katika maendeleo ya kiuchumi, kijamii na kimazi-ngira.

"Save Soil Walkathon si matembezi pekee, bali ni harakati ya kuhamasisha mabadiliko ya tabia na kuwajengea wananchi uelewa wa umuhimu wa kulinda udongo. Tunataka kuona jamii, taasisi na sekta binafsi zikichukua hatua za pamoja katika kuhifadhi mazingira kwa mustakabali wa taifa letu," alisema Lion Ramadevi.

Naye Esther Msuya, Meneja wa Afya, Usalama, Ulinzi na Mazingira (HSSE) wa GSG Energies, alisema kampuni hiyo itaendelea kuunga mkono mipango na kampeni zinazolenga uhifadhi wa mazingira na maendeleo endelevu nchini.

"Kulinda mazingira ni jukumu la kila mmoja wetu. GSG Energies tunaamini kuwa maendeleo ya kweli lazima yaende sambamba na uhifadhi wa mazingira."

"Ushiriki wetu katika Save Soil Walkathon unaonesha dhamira yetu ya kusaidia juhudi za kuongeza uelewa wa jamii na kulinda rasilimali za asili kwa manufaa ya vizazi vijavyo."

"Tutaendelea kushirikiana na Serikali, taasisi na wadau mbalimbali katika kutekeleza miradi na kampeni zinazochochea utunzaji wa mazingira, matumizi bora ya rasilimali za asili na maendeleo endelevu nchini," alisema Esther Msuya.
Save Soil Walkathon imeonesha nguvu ya ushirikiano kati ya Serikali, asasi za kiraia, sekta binafsi na wananchi katika kuendeleza agenda ya utunzaji wa mazingira. Washiriki walihamasishwa kuchukua hatua za vitendo ikiwemo upandaji miti, matumizi bora ya ardhi, uhifadhi wa vyanzo vya maji na ulinzi wa rasilimali za asili kwa ajili ya mustakabali wa taifa.

Wadhamini wa Save Soil Walkathon:
  • GSG Energies
  • META JCB
  • SRL
  • UHAI Pure Drinking Water
  • ISUZU Tanzania

Share:

PROF. NAGU ARIDHISHWA NA HUDUMA ZINAZOTOLEWA BANDA JUMUISHI LA OFISI YA WAZIRI MKUU SABASABA

     

Na. Mwandishi Wetu - Dar es Salaam | Naibu Katibu Mkuu anayeshughulikia Afya katika Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI, Prof. Tumaini Nagu, ametembelea Banda Jumuishi la Ofisi ya Waziri Mkuu na Taasisi zake katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara (Sabasaba 2026) yanayoendelea katika Viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere, jijini Dar es Salaam, na kupongeza ubora wa huduma zinazotolewa kwa wananchi.

Akiwa katika ziara hiyo, Prof. Nagu amepata fursa ya kutembelea sehemu mbalimbali za banda hilo na kupokea maelezo kuhusu huduma na mifumo mbalimbali inayowezesha wananchi kupata taarifa na huduma zinazotolewa na Ofisi ya Waziri Mkuu pamoja na taasisi zake.

Amesema banda hilo limekuwa jukwaa muhimu la kuwaelimisha wananchi kuhusu utekelezaji wa programu na miradi ya maendeleo inayolenga kuboresha utoaji wa huduma za kijamii, hususan katika sekta ya afya, elimu, utawala bora na maendeleo ya serikali za mitaa.

Prof. Nagu amewapongeza watumishi wanaohudumu katika banda hilo kwa kujituma, kutoa elimu kwa ufasaha na kuhakikisha kila mwananchi anayefika anapata huduma na taarifa sahihi zinazomwezesha kufahamu shughuli zinazotekelezwa na Serikali kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu.

Aidha, amewataka kuendelea kutumia maonesho hayo kama fursa ya kusikiliza maoni ya wananchi, kupokea changamoto zao na kutoa ufafanuzi wa kina kuhusu huduma zinazotolewa, ili kuongeza uelewa na kuimarisha uhusiano kati ya Serikali na wananchi.

"Banda Jumuishi la Ofisi ya Waziri Mkuu limeendelea kuvutia maelfu ya wananchi wanaotembelea Maonesho ya Sabasaba, ambapo wamekuwa wakipata elimu na huduma mbalimbali zinazotolewa na Ofisi hii pamoja na taasisi zake kwa lengo la kuboresha ustawi wa wananchi na kuharakisha maendeleo ya Taifa, hivyo wananchi endeleeni kuitumia fursa ya uwepo wa ofisi hii katika maonesho haya," alisema Dkt. Nagu

Aidha,ametumia nafasi hiyo kuipongeza Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TANTRADE) pamoja na Taasisi nyingine zilizowezesha mafanikio ya maonesho hayo huku akiiasa jamii kuendelea kutembelea banda hilo na kupata elimu.

Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam yanaendelea katika viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere chini ya kaulimbiu isemayo, "Maonesho ya Biashara ya Kimataifa ya Sabasaba ni Fahari ya Tanzania," yakilenga kukuza biashara, uwekezaji na ubunifu nchini.

Miongoni mwa Taasisi za Ofisi ya Waziri Mkuu zilizoshiriki ni pamoja na PSSSF, WCF, NSSF, OSHA, NEEC, TNBC, CMA, TACAIDS, DCEA,Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa, DART, TARURA, Chuo cha Serikali za Mitaa(LGTI) pamoja na Shirika la Masoko Kariakoo.
Share:

DP WORLD YALETA MAPINDUZI MAKUBWA YA UTENDAJI KAZI NA UFANISI WA KIHISTORIA KATIKA BANDARI YA DAR ES SALAAM

Kupungua kwa zaidi ya asilimia 90 kwa muda wa upakuaji wa shehena kunadhihirisha mabadiliko ya kiutendaji yaliyofanyika ndani ya miaka miwili ya mageuzi ya uendeshaji.

DAR ES SALAAM, TANZANIA – 7 July 2026: Bandari ya Dar es Salaam imeshuhudia mapinduzi makubwa kiutendaji baada ya kampuni ya DP World kuweka rekodi mpya ya kasi ya kuhudumia meli na kupunguza muda wa kushusha mizigo kwa zaidi ya asilimia 90. Mafanikio haya ni hatua kubwa katika mageuzi ya bandari hiyo tangu kampuni hiyo ianze uendeshaji wake rasmi mnamo Aprili 2024.

Chini ya mkataba wa uendeshaji wa miaka 30, kampuni ya DP World inaendelea kuwekeza katika ukarabati na upanuzi wa bandari hiyo ili kuunga mkono malengo ya muda mrefu ya nchi kiuchumi na kibiashara.

Kupitia uhamishaji wa mifumo ya kisasa ya uendeshaji wa meli za mizigo ya magari (RoRo) unaowezesha bandari kuhudumia meli kubwa na zenye mahitaji ya hali ya juu kwa usalama zaidi, huku ikipunguza gharama za mnyororo wa ugavi, huku ikiongeza ushindani wa kibiashara na kuchochea ukuaji wa uchumi.

Mageuzi haya yameleta mapinduzi makubwa kwa kupunguza muda wa kushusha mizigo ya aina hiyo kwa zaidi ya asilimia 90—kutoka zaidi ya saa 300 hadi chini ya saa 28. Hatua hii imeweka kiwango kipya kabisa cha ufanisi katika bandari hiyo.
Meli hiyo yenye urefu wa mita 240, ndiyo meli ndefu zaidi kuwahi kutia nanga katika Bandari ya Dar es Salaam, ikiwa na uwezo wa kubeba hadi magari 7,790. Ilitumia muda wa saa 27 tu kukamilisha zoezi la kushusha shehena ya magari 779, ambayo mengi yake yalikuwa ni magari makubwa na mitambo mizito.

Akizungumzia hatua hiyo, Ofisa Mtendaji Mkuu wa DP World nchini Tanzania, Martin Jacob, alisema: “Katika kipindi cha miaka miwili iliyopita, tumefanya mapinduzi makubwa katika mfumo wa usafirishaji wa shehena kupitia Bandari ya Dar es Salaam. Kasi kubwa ya kuhudumia meli, kuongezeka kwa uwezo wa bandari, na uwezo wa kupokea meli kubwa zaidi zenye mizigo mchanganyiko, kunazidi kuimarisha nafasi ya Tanzania kama lango kuu la biashara katika ukanda wa Afrika Mashariki, huku kukileta tija kwa wateja, wafanyabiashara na uchumi kwa ujumla.

Mabadiliko kuelekea matumizi ya meli maalum za kusafirisha magari na malori (PCTC), yaliyofanyika kwa ushirikiano na Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA), yamewezesha ushushaji wa magari na mitambo mizito kwa kasi, usalama na ufanisi mkubwa zaidi. Hatua hii ya kuacha mifumo ya zamani ya upakuaji mizigo ya kawaida imeleta mafanikio endelevu katika makundi yote ya shehena huku yakiimarisha nafasi ya Dar es Salaam kama kitovu cha biashara chenye ushindani mkubwa katika ukanda wa Afrika Mashariki.
Muhtasari wa Mageuzi na Matokeo
  • Kasi ya kushusha shehena kuongezeka kwa 90% – Muda wa kushusha mizigo ya aina hiyo umepungua kutoka zaidi ya saa 300 hadi chini ya saa 28.
  • Uwekaji wa rekodi mpya ya meli – Kufanikiwa kupokelewa na kuhudumiwa kwa meli ndefu zaidi kuwahi kufika bandarini, yenye urefu wa mita 240.
  • Upanuzi wa uwezo na ufanisi – Kuanza rasmi kwa uendeshaji wa meli maalum za magari (PCTC) kumeongeza kasi na usalama wa kazi.
  • Uchochezi wa ukuaji wa uchumi – Kupungua kwa gharama za usafirishaji kunasaidia kuongeza tija, kukuza Pato la Taifa, na kuleta ushindani wa kibiashara.
  • Kuendeleza wataalamu wazalendo – Zaidi ya Watanzania 2,900 wamepata ajira na wanaendelea kupatiwa mafunzo ya kiutendaji na usalama kazini.
Ili kukidhi ongezeko la shehena na ujio wa meli kubwa zaidi, DP World inaendelea kuwekeza katika kuwajengea uwezo wafanyakazi na kuimarisha usalama bandarini hapo. Kituo hicho kimeajiri zaidi ya Watanzania 2,900, ambao wanapatiwa vyeti vinavyotambulika kimataifa pamoja na mafunzo maalum ya kiutendaji na ukabilianaji wa dharura, kwa lengo la kuhakikisha shughuli za bandari zinakuwa salama, za ufanisi na za kuaminika.

Uwekezaji wetu endelevu katika Bandari ya Dar es Salaam unaonyesha dhamira ya muda mrefu ya DP World katika kuchochea ukuaji wa uchumi wa Afrika na kuiunganisha na mifumo ya biashara ya kimataifa. Kupitia ushirikiano wetu na Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA), hatuboreshi tu miundombinu hii muhimu, bali pia tunawezesha mtangamano wa kikanda, kupunguza vikwazo vya kibiashara, na kutengeneza fursa endelevu za kiuchumi," anasema Mohammed Akoojee, Ofisa Mtendaji Mkuu na Mkurugenzi Mkuu wa DP World kanda ya Afrika.
Kwa taarifa zaidi kuhusu jinsi DP World inavyoboresha biashara ya kimataifa, tembelea tovuti yetu: www.dpworld.com

Kwa maswali ya vyombo vya habari, tafadhali wasiliana na;

Keitumetse Masike
Mkurugenzi: Mawasiliano ya Biashara na Mikakati Afrika
Keitumetse.masike@dpworld.com
+27 61 831 8490

Kholiswa Hashe
Meneja Mwandamizi, Mawasiliano – Afrika Mashariki
Kholiswa.Hashe@dpworld.com
+27 72 741 0099

Fuatilia DP World kupitia:



Kuhusu DP World

DP World inabadilisha mustakabali wa biashara ya kimataifa ili kuboresha maisha ya watu kila mahali. Tukifanya kazi katika mabara sita tukiwa na timu ya wafanyakazi zaidi ya 125,000, tunajumuisha miundombinu ya kimataifa na uzoefu wa maeneo husika ili kutoa huduma jumuishi za ugavi. Kuanzia Bandari na Vituo vya Huduma (Terminals) hadi Huduma za Majini, Lojistiki na Teknolojia, tunatumia ubunifu kutengeneza njia bora zaidi za kufanya biashara—huku tukipunguza changamoto kuanzia kiwandani hadi mlangoni mwa mteja.

Katika kanda ya kusini mwa jangwa la Sahara, DP World imeajiri zaidi ya watu 28,000, ina magari zaidi ya 6,300, na inafanya kazi katika masoko 48.
TUNAFANIKISHA MTIRIRIKO WA BIASHARA
Share:

LILIAN-FAVOUR MAKAWA

LILIAN-FAVOUR MAKAWA

Popular Posts

Blog Archive

Labels

Blog Archive

Recent Posts

Label Cloud

BIASHARA (331) BURUDANI (4) KIMATAIFA (10) KITAIFA (129) MICHEZO (41) SIASA (3)

Pages