WAKULIMA KARATU KUNUFAIKA NA MAPINDUZI YA KIDIJITALI KUPITIA MIXX BY YAS

Meneja wa Mahusiano ya Biashara na Serikali wa Mixx by Yas, Suleiman Asilia (wa tatu kushoto), na Meneja wa Kibiashara Kanda ya Kaskazini wa Mixx by Yas, Eric Sosteness (kushoto kwake), pamoja na Kaimu Mkuu wa COPRA Kanda ya Kaskazini, Famia Amiri, wakimkabidhi runinga janja (Smart TV) Mwenyekiti wa ACU, Shedrack Asseri (mwenye koti jeusi), kwa ajili ya urushaji wa moja kwa moja wa minada ya mazao ya kilimo ili kuongeza uwazi na ushiriki wakati wa msimu wa mazao mbalimbali, ikiwemo ufuta.

Arusha - Wakulima wa Wilaya ya Karatu wanatarajiwa kunufaika kwa kiasi kikubwa na upatikanaji bora wa taarifa za masoko pamoja na kuongezeka kwa uwazi katika biashara ya mazao, kufuatia kuanzishwa kwa mpango wa kidijitali unaoongozwa na Mixx by Yas kwa kushirikiana na wadau wa sekta ya kilimo.

Mpango huo ulizinduliwa rasmi kupitia hafla ya makabidhiano ya runinga janja (Smart TV) iliyotolewa kwa Chama Kikuu cha Ushirika Arusha (ACU) kwa kushirikiana na Mamlaka ya Udhibiti wa Nafaka na Mazao Mchanganyiko (COPRA). Hatua hii inalenga kuboresha upatikanaji wa taarifa muhimu za masoko kwa wakulima na kuongeza ushiriki wao katika mifumo rasmi ya biashara.

Akizungumza katika hafla hiyo, Meneja wa Kibiashara Kanda ya Kaskazini wa Mixx by YasEric Sosteness, alisema kuwa suluhisho za kidijitali zinatoa fursa mpya kwa wakulima kufikia masoko kwa urahisi zaidi.

Kupitia Mixx by Yas, tumejikita kuwawezesha wakulima kwa kuwapatia suluhisho zinazowaleta karibu zaidi na masoko. Upatikanaji wa taarifa za mnada kwa wakati utawasaidia wakulima kufanya maamuzi sahihi na kuongeza kipato chao,” alisema.

Runinga hiyo janja inatarajiwa kuwa chombo muhimu katika kurusha moja kwa moja minada ya mazao ya kilimo. Kupitia teknolojia hiyo, wakulima wa Karatu na maeneo jirani wataweza kufuatilia mwenendo wa bei na shughuli za biashara bila kulazimika kuwepo katika eneo la mnada. Hatua hii inatarajiwa kuongeza uwazi, kupunguza upotoshaji wa taarifa, na kuimarisha ushindani wa haki katika soko.

Kwa upande wake, Meneja wa Mahusiano ya Biashara na Serikali wa Mixx by YasSuleiman Asilia, alisisitiza umuhimu wa ushirikiano kati ya sekta binafsi na taasisi za umma katika kuleta mageuzi ya kiuchumi kwa wakulima.

Ushirikiano huu unaonesha jinsi teknolojia na ubia vinavyoweza kufungua fursa mpya kwa wakulima. Lengo letu ni kuhakikisha wakulima wanaunganishwa zaidi, wanapata taarifa sahihi na wanajumuishwa kifedha,” alieleza.

Naye Kaimu Mkuu wa COPRA Kanda ya Kaskazini, Famia Amiri, alibainisha kuwa urushaji wa moja kwa moja wa minada utaongeza uwazi na kujenga imani katika mfumo wa biashara ya mazao, hususan katika kipindi hiki ambacho nchi inaelekea msimu wa ufuta.

Mbali na mpango huo, Mixx by Yas inaendelea kutoa huduma mbalimbali zinazolenga kumwezesha mkulima, ikiwemo Mixx Kilimo inayorahisisha miamala, Afya Mkulima inayolenga ustawi wa wakulima, pamoja na Kilimo Pesa inayowezesha upatikanaji wa huduma za kifedha kwa urahisi zaidi.

Kwa ujumla, mpango huu unaakisi mwelekeo wa sekta ya kilimo nchini kuelekea matumizi makubwa ya teknolojia katika kuboresha mifumo ya biashara. Kadri suluhisho hizi zinavyozidi kuenea, zinatarajiwa kuongeza tija, kuimarisha kipato cha wakulima, na kuwapa nafasi kubwa zaidi katika uchumi wa kisasa unaozidi kuwa wa kidijitali.

Share:

BENKI YA ABSA YAJIZATITI KUENDELEA KUWAWEZESHA WANAWAKE

  

Ofisa Mkuu wa Teknolojia wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Emmanuel Mwinuka, akitoa mada katika kongamano la wanawake lililopewa jina la ‘Accelerate Women Summit’ na kufanyika hivi karibuni jijini Dar es Salaam. Likidhaminiwa na Benki ya Absa, kongamano hilo liliwaleta pamoja viongozi wanawake kujadili namna teknolojia, uongozi na ujumuishwaji vinavyounda mustakabali wa taifa.
Meneja Huduma za Jamii na Matukio wa Benki ya Absa Tanzania, Bi. Abigail Lukuvi (wa pili kulia), akipokea cheti cha shukrani kwa udhamini kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Acceleration Foundation, Bi. Bernice Fernandos, wakati wa Kongamanao la wanawake lililoitwa ‘Accelerate Women Summit’ na kufanyika hivi karibuni jijini Dar es Salaam. Likidhaminiwa na Benki ya Absa, kongamano hilo liliwaleta pamoja viongozi wanawake kujadili namna teknolojia, uongozi na ujumuishwaji vinavyounda mustakabali wa taifa. Wanaoshuhudia kutoka kushoto ni Meneja anayeshughulikia miradi wa Benki ya Absa, Bi. Munira Chambuso, Ofisa Mkuu wa Teknolojia, Bw. Emmanuel Mwinuka, na Bi. Cygrade Othman pia kutoka benki hiyo.
Ofisa Mkuu wa Teknolojia wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Emmanuel Mwinuka (katikati), na Bi. Munira Chambuso (kushoto) kutoka Absa, wakimsikiliza mfanyabiashara na Mkurugenzi wa Masoko wa MeTL Group, Bi. Fatema Dewji, wakati wa Kongamano la wanawake lililoitwa ‘Accelerate Women Forum’ na kufanyika hivi karibuni jijini Dar es Salaam. Likidhaminiwa na Benki ya Absa, kongamano hilo liliwaleta pamoja viongozi wanawake kujadili namna teknolojia, uongozi na ujumuishwaji vinavyounda mustakabali wa taifa.
Bi. Thamrat Khamis (kushoto), anayeshughulikia akaunti za biashara ndogo na za kati (SME) akizungumza na mmoja wa washiriki wa Kongamano la wanawake lililoitwa ‘Accelerate Women Forum’ na kufanyika hivi karibuni jijini Dar es Salaam. Ukidhaminiwa na Benki ya Absa, mkutano huo uliwaleta pamoja viongozi wanawake kuchunguza namna teknolojia, uongozi na ujumuishwaji vinavyosukuma mustakabali wa taifa.
Wakishangilia, ni timu ya timu kutoka Benki ya Absa, ikiongozwa na Ofisa Mkuu wa Teknolojia, Bw. Emmanuel Mwinuka (wa pili kushoto), wakipiga picha ya kumbukumbu baada ya Kongamano la wanawake lililopewa jina la ‘Accelerate Women Forum’ likifanyika hivi karibuni jijini Dar es Salaam. Likidhaminiwa na Benki ya Absa, kongamano hilo, liliwaleta pamoja viongozi wanawake kujadili namna teknolojia, uongozi na ujumuishwaji vinavyounda mustakabali wa taifa.
Share:

BENKI YA ABSA TANZANIA YADUMISHA USHIRIKANO NA WATEJA WAKE

 

Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Obedi Laiser (kushoto), Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam, Walid Alhad Omar, pamoja na wageni wengine wakichukua chakula cha futari katika hafla iliyoandaliwa na benki kwa wateja wake jijini Dar es Salaam hivi karibuni.
Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam, Walid Alhad Omar (kulia), akipokelewa na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Obedi Laiser, wakati wa hafla ya futari, iliyoandaliwa na benki kwa wateja wake jijini Dar es Salaam hivi karibuni. Katikati ni Mdhibiti wa Masuala ya Fedha wa benki hiyo, Bw. Muhsin Kaye.
Mkurugenzi wa Wateja Binafsi wa Benki ya Absa Tanzania, Bi. Ndabu Swere (wa tatu kushoto), pamoja na baadhi ya wafanyakazi wa benki na wageni wengine, wakichukua chakula cha futari, katika hafla iliyoandaliwa na benki kwa wateja wake jijini Dar es Salaam hivi karibuni.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benkiy a Absa Tanzania, Bw. Obedi Laiser, akiwahutubia wateja na wageni waalikwa, katika hafla ya futari iliyoandaliwa na benki hiyo kwa wateja wake, jijini Dar es Salaam hivi karibuni.
Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam, Walid Alhad Omar, akihutubia baadhi ya wateja na wafanyakazi wa Benkiy a Absa Tanzania, wakati wa hafla ya futari iliyoandaliwa na benki hiyo kwa wateja wake jijini Dar es Salaam hivi karibuni.
Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam, Walid Alhad Omar (katikati), Mkurugenzi Mtendaji wa Absa Bank Tanzania, Bw. Obedi Laiser (wa pili kushoto), pamoja na baadhi ya wakurugenzi wa benki hiyo wakipiga picha ya pamoja baada ya hafla ya futari, iliyoandaliwa na benki kwa wateja wake jijini Dar es Salaam hivi karibuni.
Mdhibiti wa Masuala ya Fedha wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Muhsin Kaye (kushoto), akimuaga Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam, Walid Alhad Omar, huku Mkurugenzi Mtendaji wa benki, Bw. Obedi Laiser, akiangalia, baada ya hafla ya futari iliyoandaliwa na benki kwa wateja wake jijini Dar es Salaam hivi karibuni.
Share:

JIONI YA BARAKA FAMILIA YA OYA YASHIRIKI IFTAR NA JAMII

   Taasisi ya Oya Micro-crediti imeandaa futari maalum kwa wateja wake na jamii kwa ujumla tukio lililolenga kuimarisha mshikamano wa kijamii.

Watoto kutoka kituo cha kulelea watoto mayatima kinondoni,wakitabasam kufurahia iftar iliyoandaliwa na taasisi ya  Oya Micro-Credit ikiwa nikurudisha kwa jamii hasa katika mwezi huu mtukufu wa Ramadhani na Kwaresma


Mwezi Mtukufu wa Ramadhan ni wakati wa kutafakari, kushukuru, na kushirikiana na jamii katika kujitoa kwenye mambo mablimbali. Kwetu OYA, tunaamini kuwa mafanikio ya kweli hayapimwi tu kwa ukuaji wa biashara, bali pia kwa mchango chanya tunaoutoa kwa jamii inayotuzunguka.


Oya Micro-crediti tulipata heshima ya kuandaa Iftar dinner maalum iliyowaleta pamoja watumishi wetu, baadhi ya wateja na wageni maalum katika mazingira ya mshikamano na furaha.


Moja ya sehemu iliyogusa mioyo ya wengi ilikuwa uwepo wa watoto wazuri kutoka kituo cha kulelea watoto yatima kilichopo Kinondoni watoto hao walionesha Tabasamu lao lililota furaha kubwa na kutukumbusha maana halisi ya  ya Mwezi Mtukufu wa Ramadhan — huruma, upendo, na kushirikiana.

Haikua tu hafla ya kufuturu pamoja, bali pia ya kuimarisha mahusiano, kujenga mshikamano wa kijamii, na kueneza matumaini matukio kama haya yanatukumbusha kuwa hata matendo madogo ya wema yanaweza kuleta furaha kubwa kwa wengine.

Tunatoa shukrani zetu za dhati kwa kila mmoja aliyeshiriki na kuchangia kufanya siku hii iwe ya kipekee kadri mwezi wa Ramadhan unavyoendelea, OYA itaendelea kujitahidi kushirikiana na jamii na kuendeleza maadili ya umoja, huruma, na kusaidiana.


Kwa niaba ya familia nzima ya OYA, tunawatakia wote Ramadhan yenye baraka na amani. Alisema Mkurugenzi wa OYA Bwana. Alpha Peter



Ramadan Kareem. 🌙

Share:

BENKI YA ABSA TANZANIA YALENGA KUWEZESHA WASICHANA 5,000 KUPATA UJUZI WA AI KUPITIA MPANGO WA ELEVATEHER

Benki ya Absa Tanzania, kwa ushirikiano na Microsoft na Women in Tech, imezindua rasmi Mpango wa ElevateHer AI nchini Tanzania, ambao unalenga kuwawezesha wasichana 5,000 wa Kitanzania kupata ujuzi na cheti cha Akili Mnemba (AI).

Mpango huu ni sehemu ya juhudi pana za kiafrika zinazolenga kutoa mafunzo kwa wanawake 50,000 barani Afrika ili waweze kushiriki kikamilifu katika uchumi wa kidijitali unaokua kwa kasi.

Kupitia mpango wa ElevateHer, washiriki watapata fursa ya kujifunza mtandaoni kwa njia ya kujitegemea bila malipo, ambapo watapata maarifa ya msingi ya AI, matumizi ya AI katika biashara, na maendeleo ya taaluma katika mazingira ya kazi yanayoendeshwa na teknolojia ya AI. Mpango huu utakuwa wazi kwa mwaka mzima.

Ofisa Mkuu wa Uendeshaji wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Oscar Mwamfwagasi, amesema mpango huu unaakisi dhamira ya benki kuhakikisha wasichana wanapata ujuzi wa kidijitali unaohitajika kwa siku za usoni. “Artificial intelligence inabadilisha jinsi uchumi unavyofanya kazi na jinsi watu wanavyofanya kazi.

Kupitia Mpango wa ElevateHer AI, Benki ya Absa Tanzania inalenga kuhakikisha wasichana wa Kitanzania wanapata ujuzi na kujiamini kushiriki kikamilifu katika uchumi wa kidijitali na kuchangia ubunifu na ukuaji.

Juhudi hii inaendeleza michango ya Absa Tanzania ya kukuza ushiriki wa wanawake katika teknolojia, ikiwa ni pamoja na GirlCode Hackathon ya mwaka jana, ambapo wasichana wabunifu walikusanyika ili kutengeneza suluhisho za kiteknolojia.

Mpango wa ElevateHer unatoa njia tatu za kujifunza: AI kwa Wote, AI kwa Biashara, na AI kwa Ukuaji wa Kitaaluma, na kutoa fursa kwa washiriki kujenga maarifa ya vitendo na kutumia zana za AI katika safari zao za kitaaluma au za ujasiriamali.

Bi. Tiara Pathon, Mkurugenzi wa Ujuzi wa AI katika Microsoft Elevate, Microsoft Afrika Kusini, amesema upatikanaji wa ujuzi wa kidijitali kwa kila mmoja ni muhimu kwa ushiriki wa Afrika katika uchumi wa AI duniani. “Ukuaji wa uchumi jumuishi katika zama za AI unahitaji kujenga ujuzi kwa wingi katika masoko yanayokua. Kwa Afrika, hii inamaanisha kuwekeza kwa makusudi katika ujuzi wa kidijitali na AI kwa wanawake. Kupitia ushirikiano wetu na Absa na Women in Tech, mpango wa ElevateHer unawawezesha wanawake barani kote kupata ujuzi wa vitendo unaohitajika kazini na kuimarisha nafasi ya Afrika katika ajira za baadaye.

Mpango huu pia unasaidiwa na Women in Tech Global, shirika linalojitolea kuwawezesha wanawake na wasichana milioni tano katika Sayansi, Teknolojia, Uhandisi, na Hisabati (STEM) kufikia mwaka 2030.

Wanawake wanaopenda kushiriki wanaweza kujisajili mtandaoni kupitia: https://elevateher-in-africa.org/⁠
Share:

ACI FMA Tanzania yathibitisha kuunga mkono maendeleo ya masoko ya fedha nchini

 

Ofisa Mtendaji Mkuu wa Soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE), Bw. Peter Nalitolela (kulia), Rais wa ACI FMA Global Bw. Rui Correia, na Rais wa ACI FMA Tanzania Bw. Farid Yahya Ally wakichukua chakula cha futari katika hafla iliyoandaliwa na ACI FMA Tanzania jijini Dar es Salaam jana. Hafla hiyo iliwakutanisha wadau wa masoko ya fedha, watunga sera na wadhibiti ili kuimarisha ushirikiano na kukuza mazingira imara ya masoko ya fedha nchini.

ACI FMA Tanzania imethibitisha tena dhamira yake ya kuunga mkono ukuaji endelevu wa masoko ya fedha ya Tanzania na kuchangia kwa maana katika maendeleo endelevu ya uchumi wa taifa.

Hayo yalibainishwa na Rais wa chama hicho, Bw. Farid Yahya Ally, wakati wa hafla ya futari iliyofanyika Dar es Salaam mwishoni mwa wiki. Hafla hiyo ilijumuisha mjadala wa jopo kuhusu maendeleo na changamoto zinazoikabili sekta ya masoko ya fedha nchini Tanzania na iliwakutanisha wadau wa soko, watunga sera na wadhibiti wa sekta hiyo.

Kupitia ushirikiano endelevu na wadhibiti, watunga sera pamoja na wadau wa sekta, chama kitaendelea kuunga mkono mipango inayolingana na malengo ya muda mrefu ya maendeleo ya Tanzania, ikiwemo azma ya Dira 2050 ambayo inalenga kujenga uchumi wa dola trilioni moja,” alisema Bw. Ally.

Akihutubia wawakilishi mashuhuri kutoka Benki Kuu ya Tanzania, Soko la Hisa la Dar es Salaam, pamoja na Wakuu wa Masoko ya Kimataifa kutoka taasisi mbalimbali za kifedha, Bw. Ally alibainisha kuwa kama chombo cha kitaaluma kinachowakilisha wataalamu wa masoko ya fedha, ACI FMA Tanzania inatambua jukumu lake muhimu katika kuimarisha maendeleo na uadilifu wa masoko ya fedha nchini.

Kuimarisha ushirikiano na watunga sera pamoja na wadhibiti ni sehemu muhimu ya dhamira yetu ya kukuza kanuni bora za uendeshaji wa soko na kuhakikisha Tanzania inaendelea kuwa na mazingira rafiki kwa wawekezaji wa ndani na wa kimataifa,” alisema.

Hafla ya futari ilikuwa jukwaa muhimu la majadiliano na ushirikiano kati ya washiriki wa soko, watunga sera na wadhibiti. Majadiliano yalilenga kutafuta njia za kuziba mapengo ya kitaasisi yaliyopo na kuimarisha ushirikiano katika kujenga mazingira imara na yenye ustahimilivu kwa masoko ya fedha.

Wakati wa majadiliano hayo, washiriki walibainisha changamoto kadhaa zinazoathiri sekta ya masoko ya fedha, ikiwemo ukosefu wa utofauti wa bidhaa za kifedha, taratibu ngumu za udhibiti kwa washiriki wapya wa soko, pamoja na utegemezi mkubwa wa ufadhili unaotolewa na taasisi za kifedha.

Akijibu hoja hizo, Mtendaji Mkuu wa Soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE), Bw. Peter Nalitolela, alikiri kuwa ingawa masoko ya mitaji nchini Tanzania yanaendelea kukua, uelewa wa wawekezaji wadogo kuhusu soko hilo bado ni mdogo.

Alisema kuwa licha ya idadi ya akaunti za Central Depository System (CDS) kuwa ndogo kwa kiasi, hivi karibuni soko limeanza kushuhudia ongezeko la wawekezaji wapya wanaoingia kwenye soko la hisa.

Ingawa wawekezaji wengi zaidi wanaonesha nia ya kuingia sokoni, changamoto kadhaa bado zinaendelea kuwepo, ikiwemo ukosefu wa utofauti wa bidhaa za kifedha na maandalizi ya soko kukidhi ongezeko la ushiriki wa wawekezaji,” alisema.

Bw. Nalitolela pia alibainisha kuwa mauzo ya awali ya hisa kwa umma (IPOs) yamepungua si Tanzania pekee bali pia kimataifa, hali inayoakisi mwenendo mpana wa masoko duniani.

Hata hivyo, alisisitiza kuwa Tanzania inaendelea kubadilika taratibu kutoka katika mfumo wa uchumi unaoongozwa zaidi na serikali kuelekea uchumi unaochochewa zaidi na sekta binafsi, hatua ambayo tayari imeanza kuleta mwamko chanya katika masoko ya mitaji na hisa.

Wakati huohuo, Rais wa ACI FMA Duniani, Bw. Rui Correia, alitangaza kuwa chama hicho kitaanzisha mpango wa ufadhili wa masomo kwa wanawake barani Afrika ili kusaidia wataalamu wanawake katika sekta ya masoko ya fedha.

Hili ni jambo tunalotaka kufanya hasa tunapokaribia Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani. Kwa mwaka huu tutazingatia ufadhili wa masomo kwa wanawake barani Afrika, na mwaka ujao tutaanzisha mpango mwingine,” alisema Bw. Correia.

Alisisitiza kuwa chama hicho kinathamini sana ushirikishwaji wa maarifa na maendeleo ya kitaaluma ndani ya jamii ya wataalamu wa masoko ya fedha.

Kwetu sisi, elimu si kupata vyeti pekee. Ni kuhusu kubadilishana utaalamu, maarifa na uzoefu katika nyanja mbalimbali za masoko ya fedha,” aliongeza.

ACI FMA Tanzania ni shirika lisilo la kiserikali linalofanya kazi chini ya mwavuli wa ACI FMA Global. Chama hicho kinakuza kanuni bora za uendeshaji wa soko kwa kuwapatia wataalamu wa masoko ya fedha mafunzo, fursa za kushiriki katika shughuli za kitaaluma pamoja na vyeti vinavyotambulika kimataifa.
Rais wa ACI FMA Tanzania, Bw. Farid Yahya Ally, akizungumza na washiriki wakati wa hafla ya futari, iliyofanyika Dar es Salaam jana. Hafla hiyo iliwakutanisha wadau wa masoko ya fedha, watunga sera na wadhibiti ili kuimarisha ushirikiano na kukuza mazingira imara ya masoko ya fedha nchini.
Rais wa ACI FMA Tanzania Bw. Farid Yahya Ally (kulia) akibadilishana mawazo na Rais wa ACI FMA Duniani, Bw. Rui Correia (kushoto) pamoja na Mchambuzi Mwandamizi wa Masuala ya Fedha kutoka Benki Kuu ya Tanzania, Bw. Stanslaus Shenyali, wakati wa hafla ya futari, iliyoandaliwa na ACI FMA Tanzania Dar es Salaam jana.
Ofisa Mtendaj Mkuu wa Soko la Hisa la Dar es Salaam Bw. Peter Nalitolela (kulia) akizungumza wakati wa mjadala uliofanyika pamoja futari iliyoandaliwa na ACI FMA Tanzania jijini Dar es Salaam jana. Hafla hiyo iliwakutanisha wadau wa masoko ya fedha, watunga sera na wadhibiti ili kuimarisha ushirikiano na kukuza mazingira imara ya masoko ya fedha nchini.
Baadhi ya wageni waalikwa wakiwa katika hafla ya futari iliyoandaliwa na ACI FMA Tanzania, jijini Dar es Salaam jana. Hafla hiyo iliwakutanisha wadau wa masoko ya fedha, watunga sera na wadhibiti ili kuimarisha ushirikiano na kukuza mazingira imara ya masoko ya fedha nchini.
Rais wa ACI FMA Tanzania Bw. Farid Yahya Ally (wa nane kutoka kushoto), Rais wa ACI FMA Duniani, Bw. Rui Correia (wa sita kutoka kushoto), maofisa wa ACI na wageni wengine waalikwa wakipiga picha ya pamoja baada ya hafla ya futari iliyofanyika Dar es Salaam jana. Hafla hiyo iliwakutanisha wadau wa masoko ya fedha, watunga sera na wadhibiti ili kuimarisha ushirikiano na kukuza mazingira imara ya masoko ya fedha nchini.
Share:

BENKI YA ABSA TANZANIA YATAMBULIWA KWA DHAMIRA YAKE THABITI YA KUWAWEZESHA WANAWAKE NCHINI

  

Mkurugenzi Mtendaji wa Benkiy a Absa Tanzania, Bw. Obedi Laiser (wa sita kushoto), akionesha tuzo ya ‘Rising Women’ mara baada ya kukabidhiwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Mipango na Uwekezaji, Prof. Kitila Mkumbo (wa tano kushoto), jijini Dar es Salaam jana. Benki hiyo ilitambuliwa kwa dhamira yake thabiti ya kuwawezesha wanawake, kuendeleza ujumuishaji wa kifedha na kuunda fursa zenye maana kwa uwakilishi wa wanawake katika nafasi za uongozi.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Mipango na Uwekezaji, Prof. Kitila Mkumbo, akikabidhi tuzo ya ‘Rising Women’ kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Bww. Obedi Laiser (wa pili kulia), jijini Dar es Salaam jana. Benki hiyo ilitambuliwa kwa dhamira yake thabiti ya kuwawezesha wanawake, kuendeleza ujumuishaji wa kifedha na kuunda fursa zenye maana kwa uwakilishi wa wanawake katika nafasi za uongozi.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Mipango na Uwekezaji, Prof. Kitila Mkumbo, akikabidhi tuzo ya shukrani kwa Meneja Huduma za Jamii na Mtukio wa Benki ya Absa Tanzania, Bi. Abigail Lukuvi (kulia), kwa kutambua mchango wa benki hiyo katika Mpango wa Rising Women. Hafla hiyo ilifanyika jijini Dar es Salaam jana. Benki hiyo ilitambuliwa kwa dhamira yake thabiti ya kuwawezesha wanawake, kuendeleza ujumuishaji wa kifedha na kuunda fursa zenye maana kwa uwakilishi wa wanawake katika nafasi za uongozi.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Obedi Laiser (wa nne kushoto), na Meneja Huduma za Jamii na Matukio wa wa benki hiyo, Bi. Abigail Lukuvi (wa tatu kulia), pamoja na baadhi ya wafanyakazi wa Absa, wakipozi na tuzo za utambuzi za ‘Rising Women’ jijini Dar es Salaam jana. Benki hiyo ilitambuliwa kwa dhamira yake thabiti ya kuwawezesha wanawake, kuendeleza ujumuishaji wa kifedha na kuunda fursa zenye maana kwa uwakilishi wa wanawake katika nafasi za uongozi.
Share:

LILIAN-FAVOUR MAKAWA

LILIAN-FAVOUR MAKAWA

Popular Posts

Blog Archive

Labels

Blog Archive

Recent Posts

Label Cloud

BIASHARA (309) BURUDANI (4) KIMATAIFA (10) KITAIFA (121) MICHEZO (39) SIASA (3)

Pages