MRADI WA COOKFUND WALETA MAGEUZI YA MATUMIZI YA NISHATI KATIKA TAASISI ZA UMMA

Mshauri Mkuu wa Kiufundi wa UNCDF, Bw. Peter Malika, akizungumza wakati wa makabidhiano ya vifaa vya teknolojia ya upishi salama kwa Shule ya Msingi Bunge jijini Dar es Salaam jana. Serikali ya Tanzania, kwa ufadhili wa Umoja wa Ulaya (EU) kupitia Ujumbe wake nchini, na usimamizi wa programu ukifanywa na Mfuko wa Maendeleo wa Mitaji wa Umoja wa Mataifa (UNCDF), inatekeleza Programu ya CookFund ili kuharakisha mpito wa matumizi ya nishati safi ya kupikia katika kaya na taasisi za umma, hususan mashuleni. Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba (wa pili kutoka kulia), alikuwa mgeni rasmi.

Dar es Salaam, Tanzania | Zaidi ya wanafunzi 62,000 kote Tanzania sasa wananufaika na majiko salama na safi zaidi kufuatia usakinishaji wa zaidi ya majiko ya kisasa 170 ya nishati safi ya kupikia katika shule na taasisi za umma zaidi ya 45. Hatua hii muhimu iliadhimishwa katika hafla ya makabidhiano iliyofanyika katika Shule ya Msingi Bunge jijini Dar es Salaam, ikionesha mchango wa mpango huu katika kupunguza matumizi ya kuni na mkaa na hivyo kukabiliana na ukataji wa miti.

Mpango huu unafadhiliwa na Umoja wa Ulaya (EU) na kutekelezwa na Serikali ya Tanzania kwa kushirikiana na Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo ya Mitaji (UNCDF) kupitia programu ya CookFund.

Akizungumza katika hafla hiyo, Naibu Waziri wa Nishati, Mheshimiwa Salome Makamba alisema:

Mapinduzi haya kuelekea matumizi ya nishati safi ya kupikia ni kipaumbele cha kimkakati cha taifa kinachochangia kulinda mazingira, kuboresha afya ya umma na kuongeza ufanisi wa kiuchumi. Kwa kuzipatia shule na taasisi za umma teknolojia za kisasa za kupikia, tunalenga kulinda misitu yetu, kupunguza hewa chafuzi, na kuboresha mazingira ya kujifunzia kwa watoto wetu. Serikali itaendelea kushirikiana na wadau wa maendeleo kupanua upatikanaji wa nishati safi ya kupikia kwa kuzingatia Mkakati wa Taifa wa Nishati Safi ya Kupikia (2024–2034).

Jitihada za nishati safi ya kupikia nchini zinaongozwa na Wizara ya Nishati kwa kushirikiana na wizara na taasisi nyingine za Serikali, ikiwemo Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI, Wizara ya Maliasili na Utalii, Ofisi ya Makamu wa Rais – Mazingira, pamoja na taasisi nyingine za umma. Hadi sasa, msaada huu kwa taasisi za umma, hususan shule, unalenga taasisi zote zinazohudumia watu zaidi ya 100 kwa wakati mmoja ili kuachana na matumizi ya kuni na mkaa.

Hatua hizi zinaendana na vipaumbele vya kitaifa vya kupunguza ukataji wa miti, kupunguza uzalishaji wa gesi chafuzi, na kuongeza ufanisi katika utoaji wa huduma za umma. Matumizi ya kuni na mkaa huzalisha chembechembe hatarishi zinazoweza kusababisha magonjwa mbalimbali ya mfumo wa upumuaji kama pumu na saratani ya mapafu.

Kupitia programu ya CookFund, inayofadhiliwa na Umoja wa Ulaya, hatua hizi zinalenga kupunguza matumizi ya nishati za kuni na mkaa kwenda kwenye teknolojia bora na zenye ufanisi zaidi kama majiko yanayotumia mkaa mbadala, majiko ya umeme (electric pressure cookers), biyoethano, majiko banifu, pamoja na gesi. Teknolojia hizi zinatarajiwa kupunguza shinikizo kwa rasilimali za misitu, kuboresha ubora wa hewa jikoni, na kuongeza afya na usalama wa wanafunzi na watumishi. Hadi sasa, taasisi 45 zimeboresha mifumo yao ya upishi, nyingi zikiwa ni shule za msingi na sekondari.

Aidha, kupitia CookFund, UNCDF inatoa msaada wa kifedha na kiufundi kwa makampuni na wajasiriamali wanaokidhi vigezo ili kuongeza usambazaji wa nishati safi ya kupikia. Msaada huu unajumuisha uwekezaji wa mtaji na mtaji wa uendeshaji kwa ajili ya kuimarisha uwezo wa biashara zinazojihusisha na uzalishaji, uagizaji, usambazaji na uuzaji wa majiko, mafuta na bidhaa au huduma zinazohusiana na nishati safi ya kupikia.

Kwa upande wake, Mkuu wa Ushirikiano wa Umoja wa Ulaya nchini Tanzania, Marc Stalmans, alisema:

Umoja wa Ulaya umejikita kikamilifu katika kuendeleza hatua za kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi duniani, na Tanzania siyo tofauti. Mpango huu ni sehemu ya juhudi zetu za kusaidia mpito kuelekea nishati safi. Kupitia msaada wa Umoja wa Ulaya, jamii zinazingatia mbinu endelevu zinazolinda mazingira, huku zikichochea ukuaji wa uchumi, kukuza ajira, na kuboresha upatikanaji wa nishati mashuleni, kwenye biashara pamoja na kaya.

Naye Mshauri Mkuu Maswala Kiufundi wa UNCDF, Bw. Peter Malika, alibainisha kuwa pamoja na msaada uliotolewa kwa taasisi 45 katika wilaya 14 za Dar es Salaam, Pwani, Morogoro, Dodoma na Mwanza, programu hiyo imewekeza dola milioni 10.1 katika biashara ndogo na za kati 102.

Nishati safi ya kupikia inapunguza utegemezi wa kuni na mkaa huku ikiboresha usalama, afya na ufanisi wa majiko shuleni,” alisema Bw. Malika. “CookFund inaonesha wazi kuwa teknolojia za kisasa za nishati zinaweza kuleta mageuzi makubwa katika taasisi za umma na kuboresha moja kwa moja mazingira ya kujifunzia kwa maelfu ya wanafunzi.

Kwa ujumla, programu hii imeleta matokeo chanya na yenye mageuzi makubwa, ikichangia uundaji wa ajira 27,005 (za moja kwa moja na zisizo za moja kwa moja), jumla ya biashara 4,933 katika mnyororo wa thamani wa nishati safi ya kupikia, kufikia kaya zaidi ya 482,089, na kupunguza zaidi ya tani 3,911,450 za uzalishaji wa hewa ukaa. Mafanikio haya yanaonesha mchango mkubwa wa programu hii katika maendeleo endelevu, ustawi wa jamii na hatua za kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi nchini Tanzania.
Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba, akitoa hotuba yake wakati wa makabidhiano ya vifaa vya teknolojia ya upishi salama kwa Shule ya Msingi Bunge jijini Dar es Salaam jana. Serikali ya Tanzania, kwa ufadhili wa Umoja wa Ulaya (EU) kupitia Ujumbe wake nchini, na usimamizi wa programu ukifanywa na Mfuko wa Maendeleo wa Mitaji wa Umoja wa Mataifa (UNCDF), inatekeleza Programu ya CookFund ili kuharakisha kipindi cha mpito wa matumizi ya nishati safi ya kupikia katika kaya na taasisi za umma, hususan mashuleni.
Mkuu wa Ushirikiano wa Ujumbe wa EU nchini Tanzania, Bw. Marc Stalmans, akihutubia hadhira wakati wa makabidhiano ya vifaa vya teknolojia ya upishi salama kwa Shule ya Msingi Bunge jijini Dar es Salaam jana. Serikali ya Tanzania, kwa ufadhili wa Umoja wa Ulaya (EU) kupitia Ujumbe wake nchini, na usimamizi wa programu ukifanywa na Mfuko wa Maendeleo wa Mitaji wa Umoja wa Mataifa (UNCDF), inatekeleza Programu ya CookFund ili kuharakisha kipindi cha mpito wa matumizi ya nishati safi ya kupikia katika kaya na taasisi za umma, hususan shule. Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba (wa tatu kutoka kulia), alikuwa mgeni rasmi.
Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba (kushoto), anapika wali akitumia jiko linalotumia nishati salama ya kupikia, wakati wa hafla ya makabidhiano ya vifaa vya teknolojia ya upishi salama katika Shule ya Msingi Bunge jijini Dar es Salaam jana. Serikali ya Tanzania, kwa ufadhili wa Umoja wa Ulaya (EU) kupitia Ujumbe wake nchini, na kwa usimamizi wa programu kutoka Mfuko wa Umoja wa Mataifa wa Kuendeleza Mitaji (UNCDF), inatekeleza Mpango wa CookFund ili kuharakisha kipindi cha mpito cha matumizi ya upishi safi katika kaya na taasisi za umma, hususan mashuleni. Kutoka kulia ni Bw. Marc Stalmans, Mkuu wa Ushirikiano wa Umoja wa Ulaya (EU) nchini Tanzania, akiwa pamoja na Mshauri Mkuu wa Kiufundi wa UNCDF, Bw. Peter Malika.
Share:

WAKULIMA KARATU KUNUFAIKA NA MAPINDUZI YA KIDIJITALI KUPITIA MIXX BY YAS

Meneja wa Mahusiano ya Biashara na Serikali wa Mixx by Yas, Suleiman Asilia (wa tatu kushoto), na Meneja wa Kibiashara Kanda ya Kaskazini wa Mixx by Yas, Eric Sosteness (kushoto kwake), pamoja na Kaimu Mkuu wa COPRA Kanda ya Kaskazini, Famia Amiri, wakimkabidhi runinga janja (Smart TV) Mwenyekiti wa ACU, Shedrack Asseri (mwenye koti jeusi), kwa ajili ya urushaji wa moja kwa moja wa minada ya mazao ya kilimo ili kuongeza uwazi na ushiriki wakati wa msimu wa mazao mbalimbali, ikiwemo ufuta.

Arusha - Wakulima wa Wilaya ya Karatu wanatarajiwa kunufaika kwa kiasi kikubwa na upatikanaji bora wa taarifa za masoko pamoja na kuongezeka kwa uwazi katika biashara ya mazao, kufuatia kuanzishwa kwa mpango wa kidijitali unaoongozwa na Mixx by Yas kwa kushirikiana na wadau wa sekta ya kilimo.

Mpango huo ulizinduliwa rasmi kupitia hafla ya makabidhiano ya runinga janja (Smart TV) iliyotolewa kwa Chama Kikuu cha Ushirika Arusha (ACU) kwa kushirikiana na Mamlaka ya Udhibiti wa Nafaka na Mazao Mchanganyiko (COPRA). Hatua hii inalenga kuboresha upatikanaji wa taarifa muhimu za masoko kwa wakulima na kuongeza ushiriki wao katika mifumo rasmi ya biashara.

Akizungumza katika hafla hiyo, Meneja wa Kibiashara Kanda ya Kaskazini wa Mixx by YasEric Sosteness, alisema kuwa suluhisho za kidijitali zinatoa fursa mpya kwa wakulima kufikia masoko kwa urahisi zaidi.

Kupitia Mixx by Yas, tumejikita kuwawezesha wakulima kwa kuwapatia suluhisho zinazowaleta karibu zaidi na masoko. Upatikanaji wa taarifa za mnada kwa wakati utawasaidia wakulima kufanya maamuzi sahihi na kuongeza kipato chao,” alisema.

Runinga hiyo janja inatarajiwa kuwa chombo muhimu katika kurusha moja kwa moja minada ya mazao ya kilimo. Kupitia teknolojia hiyo, wakulima wa Karatu na maeneo jirani wataweza kufuatilia mwenendo wa bei na shughuli za biashara bila kulazimika kuwepo katika eneo la mnada. Hatua hii inatarajiwa kuongeza uwazi, kupunguza upotoshaji wa taarifa, na kuimarisha ushindani wa haki katika soko.

Kwa upande wake, Meneja wa Mahusiano ya Biashara na Serikali wa Mixx by YasSuleiman Asilia, alisisitiza umuhimu wa ushirikiano kati ya sekta binafsi na taasisi za umma katika kuleta mageuzi ya kiuchumi kwa wakulima.

Ushirikiano huu unaonesha jinsi teknolojia na ubia vinavyoweza kufungua fursa mpya kwa wakulima. Lengo letu ni kuhakikisha wakulima wanaunganishwa zaidi, wanapata taarifa sahihi na wanajumuishwa kifedha,” alieleza.

Naye Kaimu Mkuu wa COPRA Kanda ya Kaskazini, Famia Amiri, alibainisha kuwa urushaji wa moja kwa moja wa minada utaongeza uwazi na kujenga imani katika mfumo wa biashara ya mazao, hususan katika kipindi hiki ambacho nchi inaelekea msimu wa ufuta.

Mbali na mpango huo, Mixx by Yas inaendelea kutoa huduma mbalimbali zinazolenga kumwezesha mkulima, ikiwemo Mixx Kilimo inayorahisisha miamala, Afya Mkulima inayolenga ustawi wa wakulima, pamoja na Kilimo Pesa inayowezesha upatikanaji wa huduma za kifedha kwa urahisi zaidi.

Kwa ujumla, mpango huu unaakisi mwelekeo wa sekta ya kilimo nchini kuelekea matumizi makubwa ya teknolojia katika kuboresha mifumo ya biashara. Kadri suluhisho hizi zinavyozidi kuenea, zinatarajiwa kuongeza tija, kuimarisha kipato cha wakulima, na kuwapa nafasi kubwa zaidi katika uchumi wa kisasa unaozidi kuwa wa kidijitali.

Share:

BENKI YA ABSA YAJIZATITI KUENDELEA KUWAWEZESHA WANAWAKE

  

Ofisa Mkuu wa Teknolojia wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Emmanuel Mwinuka, akitoa mada katika kongamano la wanawake lililopewa jina la ‘Accelerate Women Summit’ na kufanyika hivi karibuni jijini Dar es Salaam. Likidhaminiwa na Benki ya Absa, kongamano hilo liliwaleta pamoja viongozi wanawake kujadili namna teknolojia, uongozi na ujumuishwaji vinavyounda mustakabali wa taifa.
Meneja Huduma za Jamii na Matukio wa Benki ya Absa Tanzania, Bi. Abigail Lukuvi (wa pili kulia), akipokea cheti cha shukrani kwa udhamini kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Acceleration Foundation, Bi. Bernice Fernandos, wakati wa Kongamanao la wanawake lililoitwa ‘Accelerate Women Summit’ na kufanyika hivi karibuni jijini Dar es Salaam. Likidhaminiwa na Benki ya Absa, kongamano hilo liliwaleta pamoja viongozi wanawake kujadili namna teknolojia, uongozi na ujumuishwaji vinavyounda mustakabali wa taifa. Wanaoshuhudia kutoka kushoto ni Meneja anayeshughulikia miradi wa Benki ya Absa, Bi. Munira Chambuso, Ofisa Mkuu wa Teknolojia, Bw. Emmanuel Mwinuka, na Bi. Cygrade Othman pia kutoka benki hiyo.
Ofisa Mkuu wa Teknolojia wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Emmanuel Mwinuka (katikati), na Bi. Munira Chambuso (kushoto) kutoka Absa, wakimsikiliza mfanyabiashara na Mkurugenzi wa Masoko wa MeTL Group, Bi. Fatema Dewji, wakati wa Kongamano la wanawake lililoitwa ‘Accelerate Women Forum’ na kufanyika hivi karibuni jijini Dar es Salaam. Likidhaminiwa na Benki ya Absa, kongamano hilo liliwaleta pamoja viongozi wanawake kujadili namna teknolojia, uongozi na ujumuishwaji vinavyounda mustakabali wa taifa.
Bi. Thamrat Khamis (kushoto), anayeshughulikia akaunti za biashara ndogo na za kati (SME) akizungumza na mmoja wa washiriki wa Kongamano la wanawake lililoitwa ‘Accelerate Women Forum’ na kufanyika hivi karibuni jijini Dar es Salaam. Ukidhaminiwa na Benki ya Absa, mkutano huo uliwaleta pamoja viongozi wanawake kuchunguza namna teknolojia, uongozi na ujumuishwaji vinavyosukuma mustakabali wa taifa.
Wakishangilia, ni timu ya timu kutoka Benki ya Absa, ikiongozwa na Ofisa Mkuu wa Teknolojia, Bw. Emmanuel Mwinuka (wa pili kushoto), wakipiga picha ya kumbukumbu baada ya Kongamano la wanawake lililopewa jina la ‘Accelerate Women Forum’ likifanyika hivi karibuni jijini Dar es Salaam. Likidhaminiwa na Benki ya Absa, kongamano hilo, liliwaleta pamoja viongozi wanawake kujadili namna teknolojia, uongozi na ujumuishwaji vinavyounda mustakabali wa taifa.
Share:

BENKI YA ABSA TANZANIA YADUMISHA USHIRIKANO NA WATEJA WAKE

 

Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Obedi Laiser (kushoto), Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam, Walid Alhad Omar, pamoja na wageni wengine wakichukua chakula cha futari katika hafla iliyoandaliwa na benki kwa wateja wake jijini Dar es Salaam hivi karibuni.
Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam, Walid Alhad Omar (kulia), akipokelewa na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Obedi Laiser, wakati wa hafla ya futari, iliyoandaliwa na benki kwa wateja wake jijini Dar es Salaam hivi karibuni. Katikati ni Mdhibiti wa Masuala ya Fedha wa benki hiyo, Bw. Muhsin Kaye.
Mkurugenzi wa Wateja Binafsi wa Benki ya Absa Tanzania, Bi. Ndabu Swere (wa tatu kushoto), pamoja na baadhi ya wafanyakazi wa benki na wageni wengine, wakichukua chakula cha futari, katika hafla iliyoandaliwa na benki kwa wateja wake jijini Dar es Salaam hivi karibuni.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benkiy a Absa Tanzania, Bw. Obedi Laiser, akiwahutubia wateja na wageni waalikwa, katika hafla ya futari iliyoandaliwa na benki hiyo kwa wateja wake, jijini Dar es Salaam hivi karibuni.
Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam, Walid Alhad Omar, akihutubia baadhi ya wateja na wafanyakazi wa Benkiy a Absa Tanzania, wakati wa hafla ya futari iliyoandaliwa na benki hiyo kwa wateja wake jijini Dar es Salaam hivi karibuni.
Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam, Walid Alhad Omar (katikati), Mkurugenzi Mtendaji wa Absa Bank Tanzania, Bw. Obedi Laiser (wa pili kushoto), pamoja na baadhi ya wakurugenzi wa benki hiyo wakipiga picha ya pamoja baada ya hafla ya futari, iliyoandaliwa na benki kwa wateja wake jijini Dar es Salaam hivi karibuni.
Mdhibiti wa Masuala ya Fedha wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Muhsin Kaye (kushoto), akimuaga Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam, Walid Alhad Omar, huku Mkurugenzi Mtendaji wa benki, Bw. Obedi Laiser, akiangalia, baada ya hafla ya futari iliyoandaliwa na benki kwa wateja wake jijini Dar es Salaam hivi karibuni.
Share:

JIONI YA BARAKA FAMILIA YA OYA YASHIRIKI IFTAR NA JAMII

   Taasisi ya Oya Micro-crediti imeandaa futari maalum kwa wateja wake na jamii kwa ujumla tukio lililolenga kuimarisha mshikamano wa kijamii.

Watoto kutoka kituo cha kulelea watoto mayatima kinondoni,wakitabasam kufurahia iftar iliyoandaliwa na taasisi ya  Oya Micro-Credit ikiwa nikurudisha kwa jamii hasa katika mwezi huu mtukufu wa Ramadhani na Kwaresma


Mwezi Mtukufu wa Ramadhan ni wakati wa kutafakari, kushukuru, na kushirikiana na jamii katika kujitoa kwenye mambo mablimbali. Kwetu OYA, tunaamini kuwa mafanikio ya kweli hayapimwi tu kwa ukuaji wa biashara, bali pia kwa mchango chanya tunaoutoa kwa jamii inayotuzunguka.


Oya Micro-crediti tulipata heshima ya kuandaa Iftar dinner maalum iliyowaleta pamoja watumishi wetu, baadhi ya wateja na wageni maalum katika mazingira ya mshikamano na furaha.


Moja ya sehemu iliyogusa mioyo ya wengi ilikuwa uwepo wa watoto wazuri kutoka kituo cha kulelea watoto yatima kilichopo Kinondoni watoto hao walionesha Tabasamu lao lililota furaha kubwa na kutukumbusha maana halisi ya  ya Mwezi Mtukufu wa Ramadhan — huruma, upendo, na kushirikiana.

Haikua tu hafla ya kufuturu pamoja, bali pia ya kuimarisha mahusiano, kujenga mshikamano wa kijamii, na kueneza matumaini matukio kama haya yanatukumbusha kuwa hata matendo madogo ya wema yanaweza kuleta furaha kubwa kwa wengine.

Tunatoa shukrani zetu za dhati kwa kila mmoja aliyeshiriki na kuchangia kufanya siku hii iwe ya kipekee kadri mwezi wa Ramadhan unavyoendelea, OYA itaendelea kujitahidi kushirikiana na jamii na kuendeleza maadili ya umoja, huruma, na kusaidiana.


Kwa niaba ya familia nzima ya OYA, tunawatakia wote Ramadhan yenye baraka na amani. Alisema Mkurugenzi wa OYA Bwana. Alpha Peter



Ramadan Kareem. 🌙

Share:

BENKI YA ABSA TANZANIA YALENGA KUWEZESHA WASICHANA 5,000 KUPATA UJUZI WA AI KUPITIA MPANGO WA ELEVATEHER

Benki ya Absa Tanzania, kwa ushirikiano na Microsoft na Women in Tech, imezindua rasmi Mpango wa ElevateHer AI nchini Tanzania, ambao unalenga kuwawezesha wasichana 5,000 wa Kitanzania kupata ujuzi na cheti cha Akili Mnemba (AI).

Mpango huu ni sehemu ya juhudi pana za kiafrika zinazolenga kutoa mafunzo kwa wanawake 50,000 barani Afrika ili waweze kushiriki kikamilifu katika uchumi wa kidijitali unaokua kwa kasi.

Kupitia mpango wa ElevateHer, washiriki watapata fursa ya kujifunza mtandaoni kwa njia ya kujitegemea bila malipo, ambapo watapata maarifa ya msingi ya AI, matumizi ya AI katika biashara, na maendeleo ya taaluma katika mazingira ya kazi yanayoendeshwa na teknolojia ya AI. Mpango huu utakuwa wazi kwa mwaka mzima.

Ofisa Mkuu wa Uendeshaji wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Oscar Mwamfwagasi, amesema mpango huu unaakisi dhamira ya benki kuhakikisha wasichana wanapata ujuzi wa kidijitali unaohitajika kwa siku za usoni. “Artificial intelligence inabadilisha jinsi uchumi unavyofanya kazi na jinsi watu wanavyofanya kazi.

Kupitia Mpango wa ElevateHer AI, Benki ya Absa Tanzania inalenga kuhakikisha wasichana wa Kitanzania wanapata ujuzi na kujiamini kushiriki kikamilifu katika uchumi wa kidijitali na kuchangia ubunifu na ukuaji.

Juhudi hii inaendeleza michango ya Absa Tanzania ya kukuza ushiriki wa wanawake katika teknolojia, ikiwa ni pamoja na GirlCode Hackathon ya mwaka jana, ambapo wasichana wabunifu walikusanyika ili kutengeneza suluhisho za kiteknolojia.

Mpango wa ElevateHer unatoa njia tatu za kujifunza: AI kwa Wote, AI kwa Biashara, na AI kwa Ukuaji wa Kitaaluma, na kutoa fursa kwa washiriki kujenga maarifa ya vitendo na kutumia zana za AI katika safari zao za kitaaluma au za ujasiriamali.

Bi. Tiara Pathon, Mkurugenzi wa Ujuzi wa AI katika Microsoft Elevate, Microsoft Afrika Kusini, amesema upatikanaji wa ujuzi wa kidijitali kwa kila mmoja ni muhimu kwa ushiriki wa Afrika katika uchumi wa AI duniani. “Ukuaji wa uchumi jumuishi katika zama za AI unahitaji kujenga ujuzi kwa wingi katika masoko yanayokua. Kwa Afrika, hii inamaanisha kuwekeza kwa makusudi katika ujuzi wa kidijitali na AI kwa wanawake. Kupitia ushirikiano wetu na Absa na Women in Tech, mpango wa ElevateHer unawawezesha wanawake barani kote kupata ujuzi wa vitendo unaohitajika kazini na kuimarisha nafasi ya Afrika katika ajira za baadaye.

Mpango huu pia unasaidiwa na Women in Tech Global, shirika linalojitolea kuwawezesha wanawake na wasichana milioni tano katika Sayansi, Teknolojia, Uhandisi, na Hisabati (STEM) kufikia mwaka 2030.

Wanawake wanaopenda kushiriki wanaweza kujisajili mtandaoni kupitia: https://elevateher-in-africa.org/⁠
Share:

ACI FMA Tanzania yathibitisha kuunga mkono maendeleo ya masoko ya fedha nchini

 

Ofisa Mtendaji Mkuu wa Soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE), Bw. Peter Nalitolela (kulia), Rais wa ACI FMA Global Bw. Rui Correia, na Rais wa ACI FMA Tanzania Bw. Farid Yahya Ally wakichukua chakula cha futari katika hafla iliyoandaliwa na ACI FMA Tanzania jijini Dar es Salaam jana. Hafla hiyo iliwakutanisha wadau wa masoko ya fedha, watunga sera na wadhibiti ili kuimarisha ushirikiano na kukuza mazingira imara ya masoko ya fedha nchini.

ACI FMA Tanzania imethibitisha tena dhamira yake ya kuunga mkono ukuaji endelevu wa masoko ya fedha ya Tanzania na kuchangia kwa maana katika maendeleo endelevu ya uchumi wa taifa.

Hayo yalibainishwa na Rais wa chama hicho, Bw. Farid Yahya Ally, wakati wa hafla ya futari iliyofanyika Dar es Salaam mwishoni mwa wiki. Hafla hiyo ilijumuisha mjadala wa jopo kuhusu maendeleo na changamoto zinazoikabili sekta ya masoko ya fedha nchini Tanzania na iliwakutanisha wadau wa soko, watunga sera na wadhibiti wa sekta hiyo.

Kupitia ushirikiano endelevu na wadhibiti, watunga sera pamoja na wadau wa sekta, chama kitaendelea kuunga mkono mipango inayolingana na malengo ya muda mrefu ya maendeleo ya Tanzania, ikiwemo azma ya Dira 2050 ambayo inalenga kujenga uchumi wa dola trilioni moja,” alisema Bw. Ally.

Akihutubia wawakilishi mashuhuri kutoka Benki Kuu ya Tanzania, Soko la Hisa la Dar es Salaam, pamoja na Wakuu wa Masoko ya Kimataifa kutoka taasisi mbalimbali za kifedha, Bw. Ally alibainisha kuwa kama chombo cha kitaaluma kinachowakilisha wataalamu wa masoko ya fedha, ACI FMA Tanzania inatambua jukumu lake muhimu katika kuimarisha maendeleo na uadilifu wa masoko ya fedha nchini.

Kuimarisha ushirikiano na watunga sera pamoja na wadhibiti ni sehemu muhimu ya dhamira yetu ya kukuza kanuni bora za uendeshaji wa soko na kuhakikisha Tanzania inaendelea kuwa na mazingira rafiki kwa wawekezaji wa ndani na wa kimataifa,” alisema.

Hafla ya futari ilikuwa jukwaa muhimu la majadiliano na ushirikiano kati ya washiriki wa soko, watunga sera na wadhibiti. Majadiliano yalilenga kutafuta njia za kuziba mapengo ya kitaasisi yaliyopo na kuimarisha ushirikiano katika kujenga mazingira imara na yenye ustahimilivu kwa masoko ya fedha.

Wakati wa majadiliano hayo, washiriki walibainisha changamoto kadhaa zinazoathiri sekta ya masoko ya fedha, ikiwemo ukosefu wa utofauti wa bidhaa za kifedha, taratibu ngumu za udhibiti kwa washiriki wapya wa soko, pamoja na utegemezi mkubwa wa ufadhili unaotolewa na taasisi za kifedha.

Akijibu hoja hizo, Mtendaji Mkuu wa Soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE), Bw. Peter Nalitolela, alikiri kuwa ingawa masoko ya mitaji nchini Tanzania yanaendelea kukua, uelewa wa wawekezaji wadogo kuhusu soko hilo bado ni mdogo.

Alisema kuwa licha ya idadi ya akaunti za Central Depository System (CDS) kuwa ndogo kwa kiasi, hivi karibuni soko limeanza kushuhudia ongezeko la wawekezaji wapya wanaoingia kwenye soko la hisa.

Ingawa wawekezaji wengi zaidi wanaonesha nia ya kuingia sokoni, changamoto kadhaa bado zinaendelea kuwepo, ikiwemo ukosefu wa utofauti wa bidhaa za kifedha na maandalizi ya soko kukidhi ongezeko la ushiriki wa wawekezaji,” alisema.

Bw. Nalitolela pia alibainisha kuwa mauzo ya awali ya hisa kwa umma (IPOs) yamepungua si Tanzania pekee bali pia kimataifa, hali inayoakisi mwenendo mpana wa masoko duniani.

Hata hivyo, alisisitiza kuwa Tanzania inaendelea kubadilika taratibu kutoka katika mfumo wa uchumi unaoongozwa zaidi na serikali kuelekea uchumi unaochochewa zaidi na sekta binafsi, hatua ambayo tayari imeanza kuleta mwamko chanya katika masoko ya mitaji na hisa.

Wakati huohuo, Rais wa ACI FMA Duniani, Bw. Rui Correia, alitangaza kuwa chama hicho kitaanzisha mpango wa ufadhili wa masomo kwa wanawake barani Afrika ili kusaidia wataalamu wanawake katika sekta ya masoko ya fedha.

Hili ni jambo tunalotaka kufanya hasa tunapokaribia Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani. Kwa mwaka huu tutazingatia ufadhili wa masomo kwa wanawake barani Afrika, na mwaka ujao tutaanzisha mpango mwingine,” alisema Bw. Correia.

Alisisitiza kuwa chama hicho kinathamini sana ushirikishwaji wa maarifa na maendeleo ya kitaaluma ndani ya jamii ya wataalamu wa masoko ya fedha.

Kwetu sisi, elimu si kupata vyeti pekee. Ni kuhusu kubadilishana utaalamu, maarifa na uzoefu katika nyanja mbalimbali za masoko ya fedha,” aliongeza.

ACI FMA Tanzania ni shirika lisilo la kiserikali linalofanya kazi chini ya mwavuli wa ACI FMA Global. Chama hicho kinakuza kanuni bora za uendeshaji wa soko kwa kuwapatia wataalamu wa masoko ya fedha mafunzo, fursa za kushiriki katika shughuli za kitaaluma pamoja na vyeti vinavyotambulika kimataifa.
Rais wa ACI FMA Tanzania, Bw. Farid Yahya Ally, akizungumza na washiriki wakati wa hafla ya futari, iliyofanyika Dar es Salaam jana. Hafla hiyo iliwakutanisha wadau wa masoko ya fedha, watunga sera na wadhibiti ili kuimarisha ushirikiano na kukuza mazingira imara ya masoko ya fedha nchini.
Rais wa ACI FMA Tanzania Bw. Farid Yahya Ally (kulia) akibadilishana mawazo na Rais wa ACI FMA Duniani, Bw. Rui Correia (kushoto) pamoja na Mchambuzi Mwandamizi wa Masuala ya Fedha kutoka Benki Kuu ya Tanzania, Bw. Stanslaus Shenyali, wakati wa hafla ya futari, iliyoandaliwa na ACI FMA Tanzania Dar es Salaam jana.
Ofisa Mtendaj Mkuu wa Soko la Hisa la Dar es Salaam Bw. Peter Nalitolela (kulia) akizungumza wakati wa mjadala uliofanyika pamoja futari iliyoandaliwa na ACI FMA Tanzania jijini Dar es Salaam jana. Hafla hiyo iliwakutanisha wadau wa masoko ya fedha, watunga sera na wadhibiti ili kuimarisha ushirikiano na kukuza mazingira imara ya masoko ya fedha nchini.
Baadhi ya wageni waalikwa wakiwa katika hafla ya futari iliyoandaliwa na ACI FMA Tanzania, jijini Dar es Salaam jana. Hafla hiyo iliwakutanisha wadau wa masoko ya fedha, watunga sera na wadhibiti ili kuimarisha ushirikiano na kukuza mazingira imara ya masoko ya fedha nchini.
Rais wa ACI FMA Tanzania Bw. Farid Yahya Ally (wa nane kutoka kushoto), Rais wa ACI FMA Duniani, Bw. Rui Correia (wa sita kutoka kushoto), maofisa wa ACI na wageni wengine waalikwa wakipiga picha ya pamoja baada ya hafla ya futari iliyofanyika Dar es Salaam jana. Hafla hiyo iliwakutanisha wadau wa masoko ya fedha, watunga sera na wadhibiti ili kuimarisha ushirikiano na kukuza mazingira imara ya masoko ya fedha nchini.
Share:

LILIAN-FAVOUR MAKAWA

LILIAN-FAVOUR MAKAWA

Popular Posts

Blog Archive

Labels

Blog Archive

Recent Posts

Label Cloud

BIASHARA (310) BURUDANI (4) KIMATAIFA (10) KITAIFA (121) MICHEZO (39) SIASA (3)

Pages