Absa Bank Tanzania Celebrates Record-Breaking Success at the 2026 Tanzania Pickleball Open, Reinforcing Nation’s Vision as a Regional Sports Hub

ATTRACTING pickleball players from more than seven countries, the Tanzania Pickleball Open 2026 tournament backed by Absa Bank Tanzania, underscoring the growing popularity of the sport and Tanzania’s ambitions to become a regional sports and tourism hub.

The five-day tournament, held at the Gymkhana Club grounds in Dar es Salaam, brought together elite pickleball players from Kenya, Uganda, Rwanda, South Africa, the Democratic Republic of Congo, India, Turkey and Dubai for one of East Africa’s largest pickleball competitions.

Organised through a partnership between the Tanzania Pickleball Association (TPA) and the East Africa Racket Sports Club (EARSC), the event featured a corporate prize pool of US$15,000 and premium playing equipment, attracting both international competitors and local spectators.

As the tournament’s title sponsor, Absa Bank Tanzania said its support reflects a broader commitment to youth development, community engagement and the promotion of emerging sports in the country.

Speaking during the closing ceremony, Absa Bank Tanzania Marketing and Communications Manager, Mr Beda Biswalo, said the tournament had demonstrated the growing potential of pickleball to unite communities and create opportunities for young people.

“We are inspired by the remarkable energy, discipline and international talent displayed throughout the tournament,” said Mr Biswalo. “Our partnership reflects a deeper purpose—championing a sport that unites communities while creating meaningful opportunities for young people.”

He encouraged more Tanzanians, particularly youth, to embrace the sport, noting that pickleball offers opportunities for recreation, fitness and professional development.

Sports stakeholders say the rapid growth of pickleball is creating new opportunities for athletes through international rankings, scholarships and participation in an expanding global professional circuit. The sport’s accessibility and relatively low cost have also contributed to its increasing popularity across different age groups.

The tournament's success aligns with Tanzania’s broader efforts to strengthen sports as a contributor to economic growth and tourism. Through support from government institutions and private-sector partners, the country has increasingly hosted regional and international sporting events aimed at showcasing Tanzania as a destination for sports tourism.

“Absa Bank investment in the tournament supports the Government’s agenda of developing sports infrastructure, nurturing local talent and positioning sports as a driver of economic activity. The initiative is in line with ongoing efforts by the National Sports Council (BMT) to expand opportunities for athletes and sports organisations”, Mr Biswalo added.

The bank also acknowledged the contributions of the Government of Tanzania, co-sponsors Pepsi and CBD Hotel, technology partner Courtly, tournament organisers and fans whose support contributed to the successful staging of the championship.

Following the success of the 2026 edition, Absa Bank remains committed to supporting the growth of pickleball and is optimistic that the Tanzania Pickleball Open will continue to attract increased international participation, help develop the next generation of Tanzanian athletes, and elevate the country's profile on the global sporting stage.

On his part, the President of Tanzania Pickleball Association and the East Africa Rackets Sports Club Director, Kartik Kapor, stated that the Tanzania Pickleball Open 2026 was a resounding success and marked only the beginning of Tanzania’s journey toward becoming a global pickleball powerhouse.

During the finals Women’s Doubles, Rakshika/Agni won 1st place, Sally/Rinaaz won 2nd place and Edna/Ester, WON 3rd place. On men’s Double category, Yuvraj/Purvansh won 1st place, Fifi/Shane won 2nd place and Kartik/Dev won 3rd place.

On the Men’s Singles; Purvansh won 1st place, Fifi 2nd and Dev won 3rd place. International Mixed Doubles; Shaheed/Deandra won 1st place, Ahmad/Zainab 2nd and Lisa/Zuber won 3rd place. Open Women’s Singles; Agni won 1st place, Tamara won 2nd and Sally won 3rd place.

On Mix Doubles winners; Rakshika/Dev won 1st place, 2nd place went to Alikhan/Sally and Yuvraj/Agni won 3rd place.
President of Tanzania Pickleball Association and the East Africa Rackets Sports Club Chairman, Kartik Kapor, shakes hands with Absa Bank Tanzania Head of Large Corporates, Christopher Mgani (right), during the closing ceremony of the Tanzania Pickleball Open 2026, sponsored by the financial institution, at the Dar es Salaam Gymkhana Club.
Absa Bank Tanzania Head of Large Corporates, Christopher Mgani (left), presents awards to winners of the Tanzania Pickleball Open 2026 during the closing ceremony at the Dar es Salaam Gymkhana Club. The tournament was sponsored by Absa Bank.



Absa Bank Tanzania Head of Large Corporates, Christopher Mgani (right), presents trophies to one of the winners of the Tanzania Pickleball Open 2026 during the closing ceremony at the Dar es Salaam Gymkhana Club. The tournament was sponsored by Absa Bank.
Pickleball players in action during the finals of the Tanzania Pickleball Open 2026, sponsored by Absa Bank Tanzania, at the Dar es Salaam Gymkhana grounds.

A pickleball player showcases her skills during the finals of the Tanzania Pickleball Open 2026, sponsored by Absa Bank Tanzania, at the Dar es Salaam Gymkhana grounds.

Cheerful winners of the recently concluded Tanzania Pickleball Open 2026 pose during the closing ceremony at the Dar es Salaam Gymkhana Club. The tournament was sponsored by Absa Bank
Share:

BENKI YA ABSA TANZANIA YAZINDUA HUDUMA YA MIKOPO ISIYO NA DHAMANA ILI KUKUZA BIASHARA ZA WAFANYABIASHARA WADOGO NA WA KATI.

   

Mkuu wa Kitengo cha Bidhaa na Njia za Malipo wa Benki ya Absa Tanzania, Jane Kalumuna (wa tatu kushoto) na wengine kutoka kushoto; Meneja Masoko, Mawasiliano na Chapa, Beda Biswalo, Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Wateja Wadogo na wa Kati, Scolastica Dominic na Meneja Mauzo wa Kitengo cha machine za malipo (POS), Edward Edwine, wakionesha mashine hizo kama ishara ya uzinduzi rasmi wa huduma ya mikopo isiyo na dhamana yenye lengo la kukuza biashara za wafanyabiashara wadogo na wa kati wanaofanya mauzo kwa kutumia POS za Absa. Hafla hiyo ilifanyika jijini Dar es Salaam leo.

Benki ya Absa Tanzania imezindua rasmi suluhisho bunifu la mikopo ya muda mfupi inayolenga kuwawezesha wafanyabiashara wadogo na wa kati kukuza biashara zao bila hitaji la dhamana.

Huduma hiyo mpya imeundwa mahsusi kwa wafanyabiashara wanaojihusisha na biashara ya bidhaa na huduma, wakiwemo wauzaji wa jumla, wasambazaji, mawakala na wauzaji wa rejareja wanaotumia mashine za malipo zinazotolewa na benki hiyo, Absa Point-of-Sale (POS) pamoja na njia nyingine za kidijitali za malipo.

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo jijini Dar es Salaam, Mkuu wa Kitengo cha Bidhaa na Njia za Malipo wa Benki ya Absa Tanzania, Jane Kalumuna, alisema huduma hiyo inalenga kuondoa changamoto kubwa inayowakabili wafanyabiashara wengi ya kushindwa kupata mikopo kutokana na kukosa dhamana za kawaida.

Alisema wafanyabiashara wengi wamekuwa wakifanya mauzo ya kila siku yenye mtiririko mzuri wa fedha, lakini bado wamekuwa wakikosa fursa za kupata mikopo kwa sababu mifumo mingi ya kifedha hutegemea zaidi dhamana kuliko uwezo halisi wa biashara.

Kwa muda mrefu, biashara nyingi zenye mtiririko mzuri wa fedha zimekuwa zikikosa huduma za kifedha kwa sababu hazina dhamana za kawaida. Kupitia Absa huduma hii, tunabadilisha simulizi hilo kwa kutambua na kuthamini utendaji halisi wa biashara,” alisema Bi. Jane.

Aliongeza kuwa huduma hiyo inatumia historia ya miamala ya POS kupima uwezo wa mfanyabiashara kukopa, hivyo kuwezesha wafanyabiashara kupata fedha kwa haraka kulingana na mwenendo halisi wa biashara zao.

Naye Meneja Masoko na Mawasiliano na Chapa wa Benki ya Absa Tanzania, Beda Biswalo, alisema huduma hiyo ni sehemu ya dhamira ya benki hiyo ya kuwezesha ukuaji wa biashara na uchumi wa Tanzania kwa ujumla.

Kwa kuondoa kikwazo cha dhamana na kubadilisha mauzo ya kila siku kupitia POS kuwa chanzo cha haraka cha mtaji, tunabadilisha namna biashara zinavyopata huduma za kifedha nchini Tanzania. Tunaamini kuwa kila mfanyabiashara ana simulizi muhimu, na suluhisho hili linaakisi ahadi yetu ya kusikiliza na kusaidia ukuaji wao,” alisema Biswalo.

Aliongeza kuwa kupitia huduma hiyo, Absa inaendeleza dhamira yake ya ‘Kuiwezesha Afrika ya Kesho Pamoja, Hatua Moja baada ya Nyingine’ kwa kusaidia biashara kukua, kupanuka na kuchangia maendeleo ya uchumi wa taifa.

Huduma ya Absa Merchant Financing inatarajiwa kusaidia kuziba pengo la upatikanaji wa mikopo kwa wafanyabiashara wengi nchini huku ikiimarisha ujumuishaji wa kifedha na mahusiano ya muda mrefu kati ya benki na wateja wake.
Mkuu wa Kitengo cha Bidhaa na Njia za Malipo wa Benki ya Absa Tanzania, Jane Kalumuna (wa tatu kushoto) na wengine kutoka kushoto; Meneja Masoko, Mawasiliano na Chapa, Beda Biswalo, Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Wateja Wadogo na wa Kati, Scolastica Dominic na Meneja Mauzo wa Kitengo cha machine za manunuzi (POS), Edward Edwine, wakiwa katika mkutano na waandishi wa habari, jijini Dar es leo, katika hafla ya uzinduzi rasmi wa huduma ya mikopo isiyo na dhamana yenye lengo la kukuza biashara za wafanyabiashara wadogo na wa kati wanaofanya mauzo kwa kutumia POS za Absa.
Mkuu wa Kitengo cha Bidhaa na Njia za Malipo wa Benki ya Absa Tanzania, Jane Kalumuna (wa tatu kushoto, waliokaa) na wengine kutoka kushoto; Meneja Masoko, Mawasiliano na Chapa, Beda Biswalo, Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Wateja Wadogo na wa Kati, Scolastica Dominic na Meneja Mauzo wa Kitengo cha machine za manunuzi (POS), Edward Edwine, wakionesha mashine hizo kama ishara ya uzinduzi rasmi wa huduma ya mikopo isiyo na dhamana yenye lengo la kukuza biashara za wafanyabiashara wadogo na wa kati wanaofanya mauzo kwa kutumia POS za Absa. Hafla hiyo ilifanyika jijini Dar es Salaam leo. Wengine ni baadhi ya wafanyakazi wa kitengo cha biashara.
Share:

BENKI YA ABSA TANZANIA YATHIBITISHA UPYA DHAMIRA YAKE KUKUZA VIPAJI VYA NDANI NCHINI TANZANIA

 

Mkurugenzi wa Rasilimali Watu wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Patrick Foya (wa tano kushoto), akipokea tuzo ya shukrani ya udhamini kutoka kwa Mwanzilishi wa Jukwaa la Fanisi, Bi. Sarah Majengo, wakati wa sherehe za kutimiza miaka mitano ya Fanisi jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki. Pichani (wa tatu kulia) ni Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Uwekezaji na Kanda Maalum za Kiuchumi (TISEZA), Bw. Gilead Teri, pamoja na wafanyakazi kutoka Absa.

Benki ya Absa Tanzania imethibitisha upya dhamira yake ya kukuza vipaji vya ndani na kuimarisha maendeleo ya nafasi za uongozi nchini Tanzania kupitia ushirikiano wake na jukwaa la Fanisi.

Akizungumza wakati wa sherehe za kutimiza miaka mitano ya Jukwaa la Fanisi jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Rasilimali Watu wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Patrick Foya, alisema benki hiyo inajivunia kushirikiana na mpango unaoendelea kulea kizazi kipya cha viongozi nchini.

Akihutubia wageni, washirika, wahitimu na washiriki wa jukwaa hilo, Bw. Foya alisifu maono ya mwanzilishi wa Fanisi, Bi. Sarah Majengo, na kusema kuwa katika kipindi cha miaka mitano iliyopita, jukwaa hilo limewabadilisha wataalamu wa ngazi ya kati kuwa viongozi imara wa mashirika kwa kuziba mapengo ya vipaji na kufafanua upya uongozi wa kisasa katika ukanda huu.

Alibainisha kuwa ushirikiano wa Absa na Fanisi unalingana na dhamira ya benki ya kuimarisha mustakabali wa Afrika kupitia uwekezaji kwa watu na maendeleo ya uongozi.

Katika Absa, dhamira yetu ni ‘kuimarisha Afrika ya Kesho, Pamoja, Hatua moja baada ya Nyingine’, na kwetu yote huanzia kwa watu wetu,” alisema. “Tunakusudia kujenga viongozi kutoka ndani. Tunaita kukuza idadi yetu wenyewe, ikimaanisha kuwekeza kwa watu wetu na kuwasaidia kukua kuwa viongozi imara.”

Bw. Foya alitanabaisha kuwa tangu kuanza kushirikiana na Fanisi mwaka 2024, benki hiyo tayari imeona takribani wafanyakazi 40 wakihitimu kupitia jukwaa hilo, huku wengine 28 wakiwa wamejiunga katika awamu mpya.

Kama wadhamini, uamuzi wetu wa kuwekeza katika Fanisi ulikuwa rahisi; tunaamini kuwa kuimarisha vipaji vya ndani ndiyo njia bora zaidi ya kuendesha ukuaji endelevu wa uchumi,” alisema.

Awali, Mwanzilishi wa Jukwaa la Fanisi, Bi. Sarah Majengo alisema jukwaa hilo la kujifunza lilianzishwa ili kuziba pengo kati ya malengo ya kitaifa ya Tanzania na mahitaji ya maendeleo ya rasilimali watu nchini.

Alisema kuwa biashara ndogo na za kati (SMEs) zinachangia zaidi ya asilimia 90 ya biashara nchini Tanzania, zinawaajiri zaidi ya watu milioni tano na kuchangia kwa kiasi kikubwa katika Pato la Taifa (GDP).

Hata hivyo, biashara nyingi bado zinakabiliwa na changamoto ya kupata wataalamu wenye nidhamu na uwezo licha ya kuongezeka kwa kiwango cha elimu. Utafiti wa Benki ya Dunia unasema vyeti vya kitaaluma pekee havichukuliwi tena kama viashiria vya kuaminika vya uwezo, huku kampuni nyingi zikihangaika kupata wafanyakazi wenye ujuzi na uwezo,” alisema.

Akihusisha suala hilo na matarajio makubwa ya maendeleo ya Tanzania chini ya mpango wa Taifa wa Vision 2050, unaolenga kujenga uchumi wa trilioni moja unaoendeshwa na tija na ubunifu, Bi. Sarah alibainisha kuwa mijadala mingi kuhusu Vision 2050 inalenga iwapo Tanzania inaweza kukuza watu wake kwa haraka vya kutosha ili kudumisha matarajio hayo. Alisisitiza kuwa pengo kati ya matarajio ya Tanzania na rasilimali watu wake ndilo hasa pengo ambalo Fanisi ipo kulishughulikia.

Alisema kuwa Fanisi katika kipindi cha miaka mitano iliyopita imeendesha programu zinazowanufaisha vijana na watu wazima, huku ikiendelea kuboresha dhamira yake kama kichocheo cha maendeleo ya watu.

Kwa upande wetu Fanisi, tumejizatiti zaidi kuhakikisha watu wengi wanapata nafasi ya kufikia uwezo wao kamili,” aliongeza.

Fanisi ni jukwaa la kujifunza na mshirika aliyewekeza katika kukuza vipaji kwa makampuni na watu wenye malengo ya ukuaji, ikitoa mafunzo maalum, fursa za mtandao na uwekaji wa kimkakati.
Mkurugenzi wa Rasilimali Watu wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Patrick Foya (kushoto), akihutubia washiriki wakati wa sherehe za kutimiza miaka mitano ya Jukwaa la Fanisi, zilizodhaminiwa na benki hiyo, jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki.
Mkurugenzi wa Rasilimali Watu wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Patrick Foya (kulia), akibadilishana mawazo na washiriki wakati wa sherehe za kutimiza miaka mitano ya Jukwaa la Fanisi, zilizodhaminiwa na benki hiyo, jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki.
Mkurugenzi wa Rasilimali Watu wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Patrick Foya (kushoto), akisalimiana na washiriki wakati wa sherehe za kutimiza miaka mitano ya Fanisi Platform, zilizodhaminiwa na Absa Bank, jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki. Katikati ni Bw. Christopher Shayo na Bw. Rwebu Mutahaba.
Mwanzilishi wa Jukwaa la Fanisi, Bi. Sarah Majengo (kushoto), akihutubia washiriki wakati wa sherehe za kutimiza miaka mitano ya jukwaa hilo, zilizodhaminiwa na Benki ya Absa, jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki.
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Uwekezaji na Kanda Maalum za Kiuchumi (TISEZA), Bw. Gilead Teri (katikati), pamoja na Mwanzilishi wa Jukwaa la Fanisi, Bi. Sarah Majengo (kulia kwake), wakipiga picha ya kumbukumbu na washirika, wahitimu na wadau wa jukwaa hilo wakati wa sherehe za kutimiza miaka mitano ya Fanisi Platform, zilizodhaminiwa na Benki ya Absa, jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki.
Share:

BENKI YA ABSA KUENDELEA KUSAPOTI SEKTA YA AFYA NCHINI

   

Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Bw Obedi Laiser (kulia), akichuana pamoja na washiriki wengine wa Mbio za Kilomita 10 za Absa Dar City Marathon 2026, jijini Dar es Salaam jana. Benki ya Absa ni mdhamini mkuu wa Mbio hizo, zilizoshirikisha zaidi ya wakimbiaji 3000 kutoka maeneo mbalimbali nchini.

BENKI ya Absa Tanzania imesema itendelea kusapoti juhudi zenye lengo la kuboresha afya za watanzania ikienda pamoja na ahadi ya chapa ya benki hiyo isemayo ‘Stori yako ina Thamani.

Hayo yalisemwa na Mkurugenzi na Masoko na Mawasiliano wa benki hiyo, Bw. Aron Luhanga wakati wa hafla ya mbio za Absa Dar City Marathon 2026 zilizoshirikisha zaidi ya wakimbiaji 3000 kutoka mikoa mbalimbali nchini jijini Dar es Salaam jana.

Leo tumehitimisha mbio hizi za Absa Dar City Marathon kama wadhamini wakuu, sisi Absa tunasema ‘stori yako ina thamani’, tunaamini kila mtanzania, kila mwananchi ana stori ya kuandika katika maisha yake, na ukiwa huna afya njema huwezi kuandika stori hizo kwa mafanikio, na sisi tumejikita kuhakikisha watanzania wanapata afya njema."

Kinachotokea ni kwamba, kile ambacho kimekusanywa, yale mapato yaliyokusanywa kupitia tukio hili, yanakwenda kusaidia kununua vifaa tiba kwa ajili ya wodi ya wanawake na watoto katika Hospitali ya Mnazi Mmoja”, alisema Bw. Luhanga.

Akizungumza siri ya ushindi wake, mshindi wa Mbio za Kilomita 21, Cecilia Panga kutoka Arusha alisema hii ni mara yake ya pili kushinda mbio hizo na kinachomsaidia ni kuweka bidii kubwa katika mazoezi.

Naye Katibu Mkuu wa Chama cha Riadha Mkoa wa Dar es Salaam (DAA), Felix Chunga alisema Mbio za Absa Dar City Marathon zimezidi kukua mwaka hadi mwaka hii ikiwa ni mwaka wake wa sita na zimekuwa na ushiriki mkubwa kutoka kwa wanariadha kutokana na kuwa na udhamini mzuri unaotolewa na benki hiyo unaoambatana na zawadi nzuri pamoja na ubora wa taratibu za mashindano ambao pia umewawezesha washiriki wake kufanya vizuri katika mashindano ya kitaifa na kimataifa.

Katika mbio za Absa Dar City Marathon mwaka huu, washindi wa kilomita 5 upande wa wanaume ni Nicholaus Zakaria (20:08:06) na Maria Joseph (23:15:55) upande wa wanawake huku mshindi wa Kilomita 10 wanaume ni Jumanne Mnada (28:37:03) kutoka Mara na upande wa wanawake ni Anastasia Nolomongo (35:14:91), akitokea Arusha.

Kwa upande wa mbio za Kilomita 21, John Nahhai kutoka Manyara, aliibuka kidedea kwa upande wa wanaume akitumia muda wa (1:03:53:18), huku kwa upande wa wanawake, Cecilia Panga kutoka Arusha, akiondoka kifua mbele kwa kushinda mbio hizo akitumia muda wa (1:12:49:28).
Mshindi wa kilomita 21 wanawake wa Mbio za Absa Dar City Marathon 2026, Bi. Cecilia Panga (kulia), kutoka Arusha, akipokea zawadi ya pesa taslimu kiasi cha shs 1,500,000 kutoka Kwa Mkurugenzi wa Masoko na Mawasiliano wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Aron Luhanga, mara baada ya kumalizika kwa mbio hizo, jijini Dar es Salaam jana. Benki ya Absa ni mdhamini mkuu wa Mbio hizo zilizoshirikisha zaidi ya wakimbiaji 3000 kutoka maeneo mbalimbali nchini.
Mkurugenzi wa Fedha wa Benki ya Absa Tanzania, Bernard Tesha, akishiriki Mbio za Absa Dar City Marathon 2026 pamoja na wanariadha wengine jijini Dar es Salaam jana. Benki ya Absa ni mdhamini mkuu wa Mbio hizo zilizoshirikisha zaidi ya wakimbiaji 3000 kutoka maeneo mbalimbali nchini.
Ofisa Mkuu wa Uendeshaji wa Benki ya Absa Tanzania, Oscar Mwamfwagasi (kushoto), akikabidhi zawadi Kwa mmoja wa washindi wa Mbio za Absa Dar City Marathon 2026, jijini Dar es Salaam leo. Benki ya Absa ni mdhamini mkuu wa mbio hizo zilizoshirikisha zaidi ya wakimbiaji 3000 kutoka maeneo mbalimbali nchini.
Mkurugenzi wa Sheria na Udhibiti wa Benki ya Absa Tanzania, Alistides Kashasira (kushoto), akikabidhi zawadi Kwa mmoja wa washindi wa Mbio za Absa Dar City Marathon 2026, jijini Dar es Salaam leo. Benki ya Absa ni mdhamini mkuu wa mbio hizo zilizoshirikisha zaidi ya wakimbiaji 3000 kutoka maeneo mbalimbali nchini.
Mkurugenzi wa Kitengo cha Huduma kwa Wateja na Huduma za Kidigitali wa Benki ya Absa Tanzania, Samuel Mkuyu (kushoto), akikabidhi zawadi Kwa mmoja wa washindi wa Mbio za Absa Dar City Marathon 2026, jijini Dar es Salaam leo. Benki ya Absa ni mdhamini mkuu wa mbio hizo zilizoshirikisha zaidi ya wakimbiaji 3000 kutoka maeneo mbalimbali nchini
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Obedi Laiser, pamoja na wafanyakazi walioshiriki Mbio za mwaka huu za Absa Dar City Marathon, wakipozi kwa picha ya kumbukumbu mara baada ya kumalizika kwa mbio hizo, jijini Dar es Salaam jana. Benki hiyo ni mdhanini mkuu wa mbio hizo.
Share:

ABSA YAONA MSIMAMO WA UCHUMI WA DUNIA KUIPA TANZANIA FURSA YA USHINDANI WA KIBIASHARA

 

Mkurugenzi wa Kitengo cha Mashirika Makubwa wa Benki ya Absa Tanzania, Bi. Nellyana Mmanyi (kulia), akizungumza katika mkutano ulioandaliwa na benki hiyo kwa viongozi waandamizi wa sekta za kibiashara ikilenga kujadili namna biashara za Tanzania zinavyoweza kubadili hali ya sintofahamu ya uchumi wa dunia kuwa fursa za kimkakati. Hafla hiyo ilifanyika jijini Dar es Salaam leo.

Benki ya Absa Tanzania⁠, imeeleza kuwa changamoto na misukosuko ya uchumi wa dunia zinaweza kuwa fursa muhimu kwa Tanzania kujijengea ushindani wa kiuchumi na biashara katika soko la kimataifa.

Kauli hiyo ilitolewa jijini Dar es Salaam leo katika hafla iliyoandaliwa na benki hiyo kwa viongozi waandamizi wa sekta za kibiashara ikilenga kujadili namna biashara za Tanzania zinavyoweza kubadili hali ya sintofahamu ya uchumi wa dunia kuwa fursa za kimkakati.

Mkutano huo uliwakutanisha wataalamu wa uchumi wa jumla kutoka Absa Group⁠ nchini Afrika Kusini

pamoja na wataalamu wa ndani, ambao walijadili mwenendo wa uchumi wa dunia na kutoa mbinu za kusaidia biashara kukabiliana na changamoto zinazotokana na siasa za kimataifa, mfumuko wa bei, mabadiliko ya tabianchi na kuyumba kwa masoko ya fedha.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa kikao hicho, Mkurugenzi wa Kitengo cha Mashirika Makubwa wa Benki ya Absa Tanzania, Bi. Nellyana Mmanyi, alisema kutokuwa na uhakika katika uchumi wa dunia sasa si jambo la muda mfupi bali ni hali ya kudumu inayohitaji biashara kuwa na uwezo wa kujipanga kimkakati.

Alisema mafanikio ya biashara katika mazingira ya sasa yatategemea uwezo wa taasisi kubadili changamoto kuwa fursa za ushindani.

Misukosuko ya kiuchumi duniani si hali ya mpito tena, bali ni uhalisia wa kudumu. Kwa Tanzania, huu ni wakati wa kuhitaji uongozi wenye taarifa sahihi, wepesi wa kufanya maamuzi ya kimkakati, na ushirikiano unaounganisha uzoefu wa kimataifa na utekelezaji wa ndani,” alisema Bi. Nellyana.

Katika kikao hicho, timu ya watafiti wa uchumi kutoka Absa Group iliwasilisha tathmini ya hali ya uchumi wa dunia na Afrika, ikieleza namna mvutano wa kisiasa duniani unavyoathiri masoko ya nishati, kuongeza mfumuko wa bei, pamoja na changamoto za viwango vya riba na athari zake kwa uhimilivu wa madeni.

Majadiliano pia yaligusia athari za mabadiliko ya tabianchi katika usalama wa chakula na uthabiti wa kijamii, huku ikielezwa kuwa utegemezi mkubwa wa Afrika kwa bidhaa za nje na mazingira ya kifedha ya kimataifa unaongeza shinikizo kwa uchumi wa bara hilo.

Hata hivyo, wataalamu hao walieleza kuwa Tanzania inaendelea kuonesha uimara wa kiuchumi kutokana na mazingira tulivu ya sera za fedha, ukuaji mzuri wa pato la taifa ukilinganishwa na nchi nyingine za ukanda huo, pamoja na nafasi yake ya kimkakati katika mabadiliko ya biashara na nishati duniani.

Aidha Bi. Nellyana alisema Tanzania ina msingi imara wa kiuchumi ambao unaweza kusaidia nchi kunufaika na mabadiliko ya sasa ya uchumi wa dunia kupitia uwekezaji, biashara na ukuaji wa muda mrefu.

Pamoja na hayo, wataalamu wa Trade Finance na Global Markets wa Absa waliwasilisha mbinu mbalimbali za kusaidia biashara kujikinga dhidi ya hatari za kiuchumi, ikiwemo suluhisho za mtaji wa biashara, ulinzi wa minyororo ya usambazaji, pamoja na matumizi ya mifumo ya kudhibiti hatari za ubadilishaji wa fedha za kigeni, viwango vya riba na masoko ya fedha.

Kwa upande wake, Mchumi Mwandamizi katika masuala ya Uchumi wa Absa Group, Bw. Phumelele Mbiyo, alisema utekelezaji wa mikakati ndiyo jambo muhimu zaidi katika mazingira ya sasa ya uchumi wa dunia.

Alisema Absa inaendelea kushirikiana na wateja wake si tu kwa kutoa huduma za kifedha, bali pia kwa kuwapatia utaalamu, taarifa na mifumo ya kufanya maamuzi sahihi hata katika mazingira yenye sintofahamu kubwa.

Kupitia kikao hicho, Absa ilisisitiza dhamira yake ya “Kuiwezesha Afrika ya kesho, pamoja… hatua moja baada ya nyingine,” ikiwa ni sehemu ya juhudi za benki hiyo kusaidia biashara za Tanzania kupitia tafiti za kiuchumi, utaalamu wa kitaalamu na ushirikiano wa muda mrefu.
Mkurugenzi wa Kitengo cha Mashirika Makubwa wa Benki ya Absa Tanzania, Bi. Nellyana Mmanyi (wa pili kushoto), akizungumza na baadhi ya washiriki katika mkutano ulioandaliwa na benki hiyo kwa viongozi waandamizi wa sekta za kibiashara ikilenga kujadili namna biashara za Tanzania zinavyoweza kubadili hali ya sintofahamu ya uchumi wa dunia kuwa fursa za kimkakati. Hafla hiyo ilifanyika jijini Dar es Salaam leo.
Mkurugenzi wa Masoko na Mahusiano ya Kibiashara wa Benki ya Absa Tanzania,Bw. Aron Luhanga (Katikati), akizungumza na baadhi ya washiriki katika mkutano ulioandaliwa na benki hiyo kwa viongozi waandamizi wa sekta za kibiashara ikilenga kujadili namna biashara za Tanzania zinavyoweza kubadili hali ya sintofahamu ya uchumi wa dunia kuwa fursa za kimkakati. Hafla hiyo ilifanyika jijini Dar es Salaam leo.
Mchumi Mwandamizi katika masuala ya Uchumi wa Absa Group, Bw. Phumelele Mbiyo, akijibu maswali kutoka kwa washiriki, washiriki katika mkutano ulioandaliwa na Benki ya Absa Tanzania kwa viongozi waandamizi wa sekta za kibiashara ikilenga kujadili namna biashara za Tanzania zinavyoweza kubadili hali ya sintofahamu ya uchumi wa dunia kuwa fursa za kimkakati. Hafla hiyo ilifanyika jijini Dar es Salaam leo.
Mkuu wa Masoko ya Kigeni wa Benki ya Absa Tanzania, Bi. Elisia Temu, akizungumza katika mkutano ulioandaliwa na benki hiyo kwa viongozi waandamizi wa sekta za kibiashara ikilenga kujadili namna biashara za Tanzania zinavyoweza kubadili hali ya sintofahamu ya uchumi wa dunia kuwa fursa za kimkakati. Hafla hiyo ilifanyika jijini Dar es Salaam leo.
Mkurugenzi wa Kitengo cha Mashirika Makubwa wa Benki ya Absa Tanzania, Bi. Nellyana Mmanyi (wa pili kulia) Mkurugenzi wa Masoko ya Fedha wa Benki ya Absa Tanzania, Bi. Irene Rwegalulira (wa pili kushoto), na Mkurugenzi wa Wateja Binafsi wa benki hiyo, Bi. Ndabu Swere (wa tatu kushoto), wakiwa na baadhi wa washiriki wa mkutano huo jijini Dar es Salaam leo. Mkutano huo ulilenga kujadili namna biashara za Tanzania zinavyoweza kubadili hali ya sintofahamu ya uchumi wa dunia kuwa fursa za kimkakati.
Share:

Benki ya Absa Tanzania Yazindua Huduma Iliyoboreshwa ya Prestige Banking ikitoa suluhisho jumuishi za kifedha

  

Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Obedi Laiser (wa tano kutoka kushoto), akiwa pamoja na maafisa wa benki na wateja, wakishuhudia tukio la uzinduzi rasmi wa Huduma ya Prestige Banking iliyoboreshwa kwa Wataalamu na Wajasiriamali jijini Dar es Salaam jana. Huduma hii imebuniwa kwa ajili ya wataalamu wanaopokea mishahara kati ya TZS milioni 2.5 na TZS milioni 5.99, pamoja na wajasiriamali waliojiajiri, ikiwa na msisitizo mkubwa katika kukuza ukwasi, uwekezaji, na uendelezaji wa biashara.

Benki ya Absa Tanzania leo imezindua rasmi huduma yake iliyoboreshwa ya Prestige Banking, kifurushi cha huduma za kifedha chenye mtazamo mpana wa maisha, kilichobuniwa kukidhi mahitaji mbalimbali ya wataalamu na wajasirimali wenye malengo makubwa nchini kote.

Huduma hii mpya inalenga wataalamu walio katika ajira rasmi wenye kipato cha kati ya Shilingi milioni 2.5 hadi milioni 5.99 kwa mwezi, pamoja na wajasiriamali waliojiajiri, ikiwa na msisitizo mkubwa katika kukuza ukwasi, uwekezaji, na uendelezaji wa biashara. Pia inalenga kuziba pengo linalokua sokoni kwa kutoa suluhisho jumuishi zinazosaidia ukuaji wa kifedha, ustawi wa maisha, na usalama wa muda mrefu.

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Obedi Laiser, alisema huduma hiyo inaakisi dira ya benki inayoweka mteja mbele na kuongozwa na kusudi.

Katika Absa, kusudi letu ni kuiwezesha Afrika ya kesho, pamoja… hatua moja baada ya nyingine. Huduma hii ya Prestige iliyoboreshwa, imeundwa kuendana na ndoto halisi za wataalamu na wajasiriamali wa Kitanzania wanaojenga mustakabali wao na kutamani kufika mbali zaidi. Hivi ndivyo tunavyotekeleza kwa vitendo ahadi yetu ya chapa isemayo ‘Stori yako ina Thamani,” alisema Bw. Laiser.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Wateja Binafsi wa benki hiyo, Bi. Ndabu Swere, alieleza kuwa huduma hiyo imeundwa mahsusi kuzingatia mitindo ya maisha na matarajio yanayokua ya wateja waliopo kwenye mkondo wa mafanikio.

Wataalamu na wajasiriamali wa leo wanatarajia zaidi kutoka kwenye benki zao kuliko huduma za miamala tu. Wanahitaji suluhisho zinazolingana na malengo yao, kusaidia uundaji wa ukwasi, kulinda kile wanachokijenga, na kuboresha mitindo yao ya maisha. Huduma ya Prestige inaleta yote haya kwa pamoja, ikiunganisha huduma rahisi za benki, suluhisho maalum za ukwasi, manufaa ya maisha, na ushauri wa kitaalamu katika kifurushi kimoja cha kiwango cha juu,” alisema Bi. Ndabu.

Baadhi ya manufaa ya huduma hiyo ni pamoja na Akaunti ya Prestige inayounganishwa na majukwaa ya kidijitali ya Absa, pamoja na kadi ya Platinum inayotoa urahisi, usalama, na upatikanaji wa taarifa papo hapo.

Ikitoa suluhisho za kukuza ukwasi kupitia Akaunti za akiba za Prestige, amana za muda maalum, mikopo ya nyumba iliyoboreshwa, na kadi za mkopo za Platinum zinazosaidia kufikia malengo ya kifedha yanayokua.

Huduma hiyo pia hutoa zawadi mbalimbali na manufaa ya Kipekee ya Mtindo wa Maisha kupitia Programu ya Twin Rewards inayoongeza uwezo wa kupata pointi, ofa za kurejeshewa fedha, punguzo maalum kutoka kwa washirika, pamoja na mikopo ya magari inayofanya manunuzi ya vitu vya thamani kuwa rahisi zaidi.

Huduma ya Prestige iliyoboreshwa hutoa pia Suluhisho za Ulinzi kupitia Bima mbalimbali zinazosaidia kulinda mali, afya, na urithi wa kifedha wa mteja.

Kupitia huduma hiyo mteja anaweza kupata Ushauri wa kitaalamu ikiwemo uandaaji wa wosia, mipango ya urithi na uendelevu wa mali, pamoja na uwezekano wa kujiunga na klabu maalum ya afya ili kukuza maisha yenye viwango.

Benki ya Absa Tanzania imeeleza kuwa huduma hii mpya ni sehemu ya mkakati wake mpana wa kutoa huduma za kifedha zinazomweka mteja katikati, zikivuka mipaka ya bidhaa za kawaida kwa kushughulikia mahitaji kamili ya kifedha na mitindo ya maisha ya wateja.

Huduma hii inaonyesha dhamira yetu ya kuwa mshirika wa kifedha anayeaminika katika kila hatua ya maisha ya wateja wetu,” aliongeza Bi. Ndabu. “Kadiri malengo yao yanavyokua, nasi tunakua pamoja nao.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Obedi Laiser, akihutubia wageni waalikwa wakati wa uzinduzi rasmi wa Huduma ya Prestige Banking iliyoboreshwa kwa Wataalamu na Wajasiriamali jijini Dar es Salaam jana. Huduma hii imebuniwa kwa ajili ya wataalamu wanaopokea mishahara kati ya TZS milioni 2.5 na TZS milioni 5.99, pamoja na wajasiriamali waliojiajiri, ikiwa na msisitizo mkubwa katika kukuza ukwasi, uwekezaji, na uendelezaji wa biashara.
Mkuu wa Kitengo cha Wateja Maalum wa Benki ya Absa Tanzania, Bi. Thereza Majinge, akitoa ufafanuzi kuhusu Huduma ya Prestige Banking iliyoboreshwa kwa Wataalamu na Wajasiriamali iliyozinduliwa jijini Dar es Salaam jana. Huduma hii imebuniwa kwa ajili ya wataalamu wanaopokea mishahara kati ya TZS milioni 2.5 na TZS milioni 5.99, pamoja na wajasiriamali waliojiajiri, ikiwa na msisitizo mkubwa katika kukuza ukwasi, uwekezaji, na uendelezaji wa biashara.
Mkurugenzi wa Wateja Binafsi wa Benki ya Absa Tanzania, Bi. Ndabu Swere (katikati), akizungumza na baadhi ya wageni waalikwa wakati wa uzinduzi rasmi wa Huduma ya Prestige Banking iliyoboreshwa kwa Wataalamu na Wajasiriamali jijini Dar es Salaam jana. Huduma hii imebuniwa kwa ajili ya wataalamu wanaopokea mishahara kati ya TZS milioni 2.5 na TZS milioni 5.99, pamoja na wajasiriamali waliojiajiri, ikiwa na msisitizo mkubwa katika kukuza ukwasi, uwekezaji, na uendelezaji wa biashara.
Share:

RC SINGIDA APONGEZA JITIHADA ZA NBC KUCHOCHEA MAPINDUZI YA KILIMO

 

Mkuu wa Mkoa wa Singida, Bi. Halima Dendego (wa tatu kulia), akionesha baadhi ya zawadi zinazotolewa kwa washindi kampeni ya “Wekeza NBC Shambani Ushinde” inayoratibiwa na Benki ya NBC. Wengine pichani ni Mkuu wa Kanda ya Kati wa NBC, Bw. Miraji Msuya (wa tatu kushoto), Mkuu wa Idara ya Bima wa NBC, Bw. Benjamini Nkaka (wa pili kushoto) Mkuu wa Kitengo cha Wateja Wadogo na Wakulima wa NBC, Bw. Raymond Urassa (kushoto), Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Chama Kikuu cha Ushirika cha Wakulima wa Mkoa wa Singida (SIFACU) Bw. Julius Kitundu (kulia) na Mrajisi Msaidizi wa Mkoa wa Singida Bi. Nuria Gulamali (wa pili kulia).
Mkuu wa Mkoa wa Singida, Bi. Halima Dendego (katikati), akipokea zawadi maalum ya picha yake kutoka kwa wafanyakazi wa benki ya NBC wakiongozwa na Mkuu wa Kanda ya Kati wa NBC, Bw. Miraji Msuya (kushoto) wakati wa hafla ya uzinduzi wa kampeni ya “Wekeza NBC Shambani Ushinde” inayoratibiwa na Benki ya NBC.

Singida, Aprili 30, 2026 — Mkuu wa Mkoa wa Singida, Bi. Halima Dendego, amepongeza mchango wa wadau mbalimbali, hususan Benki ya Taifa ya Biashara (NBC), kwa kuunga mkono juhudi za Serikali katika kuharakisha maendeleo ya sekta ya kilimo. Ameitaja kampeni ya “Wekeza NBC Shambani Ushinde” kuwa kichocheo muhimu cha ustawi wa wakulima na ukuaji wa uchumi wa mkoa huo.

Akizungumza wakati wa uzinduzi rasmi wa kampeni hiyo uliofanyika jana mkoani Singida, Bi. Dendego alisema kuanzishwa kwa mpango huo kwa mara ya kwanza katika mkoa huo ni hatua muhimu inayosaidia kufanikisha malengo ya Serikali ya kuongeza uzalishaji wa mazao ya kimkakati pamoja na kuinua kipato cha wakulima.
Hafla hiyo iliwaleta pamoja wadau mbalimbali wa sekta ya kilimo, wakiwemo viongozi wa vyama vya msingi na vyama vikuu vya ushirika, wakulima, pamoja na wadau wengine katika mnyororo wa thamani wa kilimo. Uongozi wa NBC uliwakilishwa na Mkuu wa Idara ya Bima, Bw. Benjamini Nkaka, na Mkuu wa Kitengo cha Wateja Wadogo na Wakulima, Bw. Raymond Urassa, wakishirikiana na timu ya maofisa wa benki hiyo akiwemo Mkuu wa Kanda ya Kati, Bw. Miraji Msuya.

Kwa mujibu wa Bi. Dendego, kampeni hiyo inaendana na mafanikio ya jitihada za Serikali ambazo tayari zimeanza kuzaa matunda. Alitaja mafanikio hayo kuwa ni pamoja na usajili wa zaidi ya asilimia 92 ya wakulima mkoani Singida, utoaji wa ruzuku za pembejeo kama mbegu na mbolea, pamoja na uwekezaji katika huduma za ugani na kilimo cha umwagiliaji.

Kampeni ya NBC Shambani inakuja kuimarisha juhudi hizi kwa kuchochea ujumuishaji wa kifedha kwa wakulima. Hii ni hatua muhimu kuelekea kilimo chenye tija na chenye manufaa kwa wananchi mmoja mmoja, kaya na mkoa kwa ujumla,” alisisitiza Bi. Dendego.

Aidha, aliwahimiza wakulima kuchangamkia fursa zinazotolewa na kampeni hiyo, ikiwemo akaunti zisizo na makato ya kila mwezi, upatikanaji wa mikopo ya pembejeo na zana za kilimo, elimu ya fedha, pamoja na huduma za bima ya afya na mazao.

Akifafanua zaidi kuhusu kampeni hiyo, Bw. Nkaka alisema NBC inaendelea kubuni suluhisho za kifedha bunifu ili kuunga mkono azma ya Serikali ya kuongeza ukuaji wa sekta ya kilimo kutoka asilimia 5 hadi 10 ifikapo mwaka 2030. Aliongeza kuwa benki hiyo pia inawekeza katika utoaji wa elimu ya fedha, huduma za kidijitali, pamoja na bima zinazolenga kupunguza hatari kwa wakulima.

Kwa upande wake, Bw. Urassa alisema kampeni hiyo ya miezi minne inalenga wakulima wa mazao ya dengu, choroko, mbaazi, soya na ufuta. Alieleza kuwa wakulima wana nafasi ya kushiriki binafsi au kupitia vyama vya ushirika na kushinda zawadi mbalimbali, zikiwemo pikipiki na kompyuta mpakato (laptops).

Lengo kuu ni kuwahamasisha wakulima kutumia mifumo rasmi ya kifedha kwa kutunza fedha zao benki. Tunawakaribisha kufungua akaunti za NBC Shambani ili waweze kunufaika na huduma na fursa hizi,” alibainisha.

Baadhi ya wakulima walioshiriki katika hafla hiyo walieleza matumaini yao juu ya kampeni hiyo, wakiwahimiza wenzao kuitumia kikamilifu ili kunufaika na huduma za kifedha, elimu, bima pamoja na zawadi zinazotolewa.

Uzinduzi wa kampeni ya Wekeza NBC Shambani Ushinde unaashiria hatua mpya katika juhudi za kukuza sekta ya kilimo mkoani Singida. Kupitia ushirikiano kati ya sekta ya umma na binafsi, wakulima wanapata fursa ya kuimarisha uzalishaji wao, kuongeza kipato na kuchangia kwa kiasi kikubwa ukuaji wa uchumi wa taifa.
Share:

LILIAN-FAVOUR MAKAWA

LILIAN-FAVOUR MAKAWA

Popular Posts

Blog Archive

Labels

Recent Posts

Label Cloud

BIASHARA (321) BURUDANI (4) KIMATAIFA (10) KITAIFA (123) MICHEZO (40) SIASA (3)

Pages