Mkurugenzi Mtendaji wa Absa Bank akutana na Mkurugenzi wa Benki ya Dunia kwa Tanzania, Malawi, Zambia na Zimbabwe kuimarisha Mahusiano ya kibiashara.

   

Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Obedi Laiser (kulia), akiagana na Bw. Nathan Belete, Mkurugenzi wa Benki ya Dunia anayesimamia Malawi, Tanzania, Zambia na Zimbabwe, baada ya mkutano wa kimkakati wa kibiashara uliofanyika hivi karibuni katika Hoteli ya Hyatt Regency Park jijini Dar es Salaam. Mkutano huo ulilenga kuimarisha ushirikiano kati ya taasisi hizo mbili.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Obedi Laiser (kushoto), akizungumza na Bw. Nathan Belete, Mkurugenzi wa Benki ya Dunia anayesimamia Malawi, Tanzania, Zambia na Zimbabwe, baada ya mkutano wa kimkakati wa kibiashara uliofanyika hivi karibuni katika Hoteli ya Hyatt Regency Park jijini Dar es Salaam. Mkutano huo ulilenga kuimarisha ushirikiano kati ya taasisi hizo mbili.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Obedi Laiser (kushoto), akiwa na Bw. Nathan Belete, Mkurugenzi wa Benki ya Dunia anayesimamia Malawi, Tanzania, Zambia na Zimbabwe, baada ya mkutano wa kimkakati wa kibiashara uliofanyika hivi karibuni katika Hoteli ya Hyatt Regency Park jijini Dar es Salaam. Mkutano huo ulilenga kuimarisha ushirikiano kati ya taasisi hizo mbili.
Share:

APeF Yazindua Mfuko wa Ziada Kupanua wigo wa uwekaji Akiba, Uwekezaji na Ulinzi

    

Ofisa Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Masoko ya Mitaji na Dhamana, (CMSA), CPA Nicodemus Mkama, akikabidhi waraka wa ofa kwa Kaimu Mwenyekiti wa Bodi ya Africa Pension Fund (APeF), Dkt. Hamisi Kibola (wa tatu kushoto), kuashiria uzinduzi rasmi wa Mfuko wa Uwekezaji wa Pamoja wa Ziada Fund, jijini Dar es Salaam leo. Wa pili kushoto ni Ofisa Mtendaji Mkuu wa APeF, Bw. Mfaume Kimario, pamoja na wadau wengine wa Mfuko wa Ziada; kuanzia kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Alliance Life, Bw. Byford Mutikwasa, Bi. Tupokigwe Mwalwisi kutoka NBC na Bw. Lusungu.

DAR ES SALAAM, 26 Januari 2026. Africa Pension Fund Limited (APeF) leo imezindua rasmi Mfuko wa Ziada, ambao ni mfuko wa kwanza wa uwekezaji wa pamoja katika soko la fedha nchini Tanzania unaojumuisha mafao ya bima ya maisha, hatua inayoweka alama muhimu katika kupanua upatikanaji wa suluhisho za uwekezaji zilizo chini ya udhibiti. Hafla ya uzinduzi imefanyika katika Hoteli ya KingJada, Morocco Square, jijini Dar es Salaam. Kipindi cha awali cha uuzaji wa vipande kupitia mfuko huu kinaanza leo tarehe 26 Januari hadi 25 Februari 2026.

Hafla ya uzinduzi huo ilihudhuriwa na mgeni rasmi, Ofisa Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Masoko ya Mitaji na Dhamana (CMSA), CPA Nicodemus Mkama, ikihudhuriwa pia na wawakilishi kutoka Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE), mifuko ya hifadhi ya jamii, wasimamizi wa mifuko, madalali, taasisi za kibenki na bima, pamoja na wanahabari.

Mfuko wa Ziada umebuniwa kuwasaidia wawekezaji kuweka akiba na kukuza fedha zao kupitia uwekezaji wenye nidhamu katika soko la fedha, ukiwa na faida ya ziada ya ulinzi wa bima ya maisha kwa wawekezaji binafsi wanaokidhi vigezo. Mfuko huu umerahisishwa kiutendaji, kwa kuwawezesha wawekezaji kuanza kwa urahisi, kuongeza uwekezaji wakati wowote, na kupata fedha zao ndani ya siku tatu za kazi.

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Ofisa Mtendaji Mkuu wa APeF, Bw. Mfaume Kimario, alisema, Ziada imeundwa kwa wawekezaji wanaotaka njia rahisi na za kuaminika za kukuza fedha zao bila kupoteza uwezo wa kupata fedha zao pindi zinapohitajika. Huu ni mfuko imara katika soko la fedha unaopatikana kwa urahisi, wenye ulinzi wa bima ya maisha kwa wawekezaji wanaokidhi vigezo ukianzia na thamani halisi ya uwekezaji (vipande), ya chini kabisa ya shilingi 250,000. Bima hiyo hutoa kinga sawa na asilimia 50 ya thamani halisi ya uwekezaji (vipande) hadi kiwango cha juu cha thamani kilichohakikishwa cha shilingi milioni 100, na kiwango cha juu cha malipo ya bima cha shilingi milioni 50.

Akizungumza kwa niaba ya Mwenyekiti na Bodi ya Wakurugenzi, Dkt. Hamisi Kibola, Mjumbe wa Bodi ya APeF, aliipongeza CMSA kwa hatua zilizofikiwa katika kuendeleza masoko ya mitaji nchini Tanzania na kwa kukuza ukuaji na uhai unaoonekana sokoni kwa sasa. Alibainisha kuwa kiwango cha uwekaji akiba nchini Tanzania bado kiko chini ya asilimia 3, na akatoa wito wa kuimarishwa kwa ushirikiano kati ya wasimamizi na wadau wa sekta ya fedha ili kujenga utamaduni imara wa kujiwekea akiba unaojengwa juu ya taaluma, uaminifu, elimu ya fedha na upatikanaji rahisi wa huduma. Aliongeza kuwa ndiyo sababu APeF ilianzishwa, ubunifu ukiwa kama msingi wake, ili kuongeza wigo kwa vitendo njia za uwekaji akiba na uwekezaji kupitia mifuko ya uwekezaji wa pamoja, mipango binafsi ya pensheni inayounganisha suluhisho za bima na masoko ya mitaji.

Mfuko wa Ziada umeandaliwa kwa ushirikiano na taasisi washirika muhimu, ambapo Alliance Life Assurance Limited ni mtoa bima, Benki ya Taifa ya Biashara (NBC) ni Mtunza Dhamana na Mdhamini. Wawekezaji wanaweza kupata huduma za Mfuko wa Ziada kupitia benki wakusanyaji zikiwemo CRDB Bank, NMB Bank, Exim Bank, Azania Bank, COOP Bank, NBC na Mwanga Hakika Bank, pamoja na kupitia mawakala walioidhinishwa na DSE na majukwaa ya kidijitali ya APeF.

Tunaalika Watanzania kufanya suala la kuweka akiba kuwa utamaduni wao kupitia Ziada. Unapoweka akiba kwa uthabiti, unaimarisha familia yako, kuinua jamii yako, na kuunga mkono maendeleo ya taifa. Ziada inakupa mahali rahisi pa kuanzia, kukua hatua kwa hatua, na kulinda kile kilicho muhimu zaidi,” aliongeza Ofisa Mtendaji Mkuu wa APef, Bw. Kimario.

Kwa upande wake Ofisa Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Masoko ya Mitaji na Dhamana (CMSA), CPA. Nicodemus Mkama alisema kuidhinishwa kwa mfuko wa ziada kunaendelea kuleta chachu zaidi katika maendeleo ya uwekezaji kwenye mifuko hiyo na kuifanya idadi ya mifuko hiyo ya uwekezaji wa pamoja kufikia 26.

Kuhusu APeF

Africa Pension Fund Limited (APeF) ni msimamizi wa mifuko aliyeidhinishwa, anayetoa huduma za usimamizi wa mifuko, mifuko ya uwekezaji wa pamoja, suluhisho za pensheni binafsi, usimamizi wa mali, na ushauri wa kifedha. APeF imejizatiti kuimarisha usalama wa kifedha kupitia suluhisho za uwekezaji bunifu, zenye uwazi na zinazozingatia misingi bora ya suluhisho za uwekezaji.
Ofisa Mtendaji Mkuu wa Africa Pension Fund (APeF), Bw. Mfaume Kimario, akizungumza wakati wa hafla ya uzinduzi rasmi wa Mfuko wa Uwekezaji wa Pamoja wa Ziada Fund, jijini Dar es Salaam leo.
Kaimu Mwenyekiti wa Bodi ya Africa Pension Fund (APeF), Dkt. Hamisi Kibola akizungumza wakati wa hafla ya uzinduzi rasmi wa Mfuko wa Uwekezaji wa Pamoja wa Ziada Fund, jijini Dar es Salaam leo.
Baadhi ya wadau wakihudhuria hafla ya uzinduzi rasmi wa Mfuko wa Uwekezaji wa Pamoja wa Ziada Fund unaoendeshwa na Africa Pension Fund (APeF).
Ofisa Mtendaji Mkuu wa Africa Pension Fund (APeF), Bw. Mfaume Kimario (kushoto) akizungumza na baadhi ya wadau wa Mfuko wa Uwekezaji wa Pamoja wa Ziada Fund wakati wa hafla ya uzinduzi wa mfuko huo, jijini Dar es Salaam leo.
Ofisa Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Masoko ya Mitaji na Dhamana, (CMSA), CPA Nicodemus Mkama (katikati), Kaimu Mwenyekiti wa Bodi ya Africa Pension Fund (APeF), Dkt. Hamisi Kibola (wa nne kushoto) na Ofisa Mtendaji Mkuu wa APeF, Bw. Mfaume Kimario (wa nne kulia) wakipiga picha ya pamoja na baadhi ya wafanyakazi wa taasisi hiyo baada uzinduzi rasmi wa Mfuko wa Uwekezaji wa Pamoja wa Ziada Fund, jijini Dar es Salaam leo.
Share:

ABSA BANK TANZANIA YAFUNGA KAMPENI YA 'UJANJA NI KUSWIPE NA KADI YA ABSA' KWA DROO YA MWISHO NA KUTANGAZWA KWA MSHINDI WA ZAWADI KUU

Mkuu wa Masoko na Mahusiano wa Benki yaAbsaTanzania, Bw. Aron Luhanga (kushoto), akifanya droo ya mwisho ya kampeni ya benki ya miezi mitatu ya 'Ujanja ni Kuswipe na Kadi ya Absa', jijini Dar es Salaam jana. Mteja wa benki hiyo, Bi. Nasreen Karim Abdallah, alijinyakulia zawadi kuu ya Tsh 30,000,000. Kampeni hiyo ililenga kuwahamasisha wateja kuongeza matumizi ya kadi za debit na credit za Absa pamoja na huduma za kibenki kwa njia za kidigitali za benki hiyo.

Benki ya Absa Tanzania imehitimisha rasmi kampeni yake ya 'Ujanja ni Kuswipe na Kadi ya Absa' iliyodumu Kwa miezi mitatu baada ya kufanyika kwa droo ya tatu na ya mwisho katika hafla Iliyofanyika jijini Dar es Salaam, jana.

Droo ya mwisho imehitimisha kampeni ya miezi mitatu iliyolenga kuwazawadia wateja kwa kufanya miamala na huduma za kibenki kwa njia za kidijitali ikiwa ni pamoja na matumizi ya kadi, huku ikithibitisha dhamira ya Absa ya kuhimiza miamala salama, rahisi na isiyotumia fedha taslimu.

Katika hafla hiyo, Absa ilifanya droo ya mwisho ya kila mwezi na kutoa jumla ya shilingi milioni 18 za Kitanzania (TZS 18 milioni) kwa wateja watatu walioibuka washindi kutokana na ushiriki wao katika mwezi wa mwisho wa kampeni.

Washindi hao ni Bw. Abdulrazak Ali Seif (TZS 10 milioni), Bi. Aysha Mbarak Meghji (TZS 5 milioni), na Bw. Gibbons Samuel Katule (TZS 3 milioni). Droo hiyo ilifanyika kwa kuzingatia Masharti na Vigezo vya kampeni na mbele ya mwakilishi wa Bodi ya Michezo ya Kubahatisha Tanzania, ili kuhakikisha uwazi na haki katika mchakato wa uchaguzi wa washindi.

Katika tukio lililosubiriwa kwa hamu zaidi wakati wa kilele cha kampeni hiyo, Bi. Nasreen Karim Abdallah aliibuka Mshindi wa Zawadi Kuu, akiondoka na shilingi milioni 30 za Kitanzania (TZS 30 milioni). Ushindi huo umetokana na matumizi yake ya mara kwa mara ya huduma za benki za kidijitali na kadi za Absa katika kipindi chote cha kampeni, na unaonesha jinsi miamala ya kila siku inaweza kuleta mabadiliko makubwa katika maisha.

Akizungumza katika hafla hiyo, Mkurugenzi wa Masoko na Mahusiano wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Aron Luhanga, alisisitiza mchango mkubwa wa wateja katika mafanikio ya kampeni hiyo:

Kampeni hii imekuwa na Manufaa mkubwa kwa wateja wetu tangu mwanzo. Tumehamasishwa kuona jinsi wengi wao wakichangamkia njia rahisi, salama na zisizotumia fedha taslimu katika kufanya miamala. Play Your Cards Right imeonesha kuwa pale wateja wanapochagua benki ya kidijitali, kila mtu hunufaika, kuanzia urahisi wa huduma hadi kuimarika kwa ujumuishaji wa kifedha.

"Tunawashukuru kwa dhati wateja wetu kwa kuendelea kuiamini Absa na kuwa sehemu ya safari hii.

Kwa upande wake, Mkuu wa Usimamizi wa Taarifa na Uchambuzi wa Takwimu (MI & Analytics), Bw. Denis Kessy, alieleza athari pana ya kampeni hiyo:

Absa tunaamini kuwa kila mteja ana Stori yenye thamani. Kampeni hii imetupa fursa ya kusherehekea Stori hizo, kubwa na ndogo, kwa kuwazawadia wateja wetu kwa kutumia tu huduma zetu za benki.

Tunapohitimisha kampeni hii leo, tunajivunia si mshindi wa zawadi kuu pekee, bali kila mteja aliyeshiriki.

Aliendelea kusisitiza ukubwa wa mafanikio ya kampeni hiyo kwa kusema:

Kupitia kampeni hii, Absa iliwazawadia washindi 72 wa kila wiki, washindi tisa wa kila mwezi na mshindi mmoja wa Zawadi Kuu, kwa jumla ya shilingi milioni 120 za Kitanzania (TZS 120 milioni) zilizorejeshwa kwa wateja wetu.

Huu ni uthibitisho dhahiri kuwa kuchagua Absa kunalipa.

Kampeni ya Play Your Cards Right ilikuwa kampeni ya zawadi kwa wateja iliyodumu kwa miezi mitatu kuanzia Oktoba hadi Desemba 2025, ikiwa na lengo la kuhamasisha matumizi ya malipo ya kidijitali na yasiyotumia fedha taslimu. Wateja walipata nafasi ya kushiriki katika droo za kila wiki na kila mwezi kwa kutumia kadi zao za debit au credit za Absa kupitia malipo ya kuswipe, kutap (tap) au ununuzi mtandaoni.

Kwa kukamilika kwa droo ya mwisho, kampeni ya Play Your Cards Right imefikia tamati rasmi. Washindi waliotangazwa katika droo ya mwisho watatambuliwa rasmi katika hafla maalum ya kukabidhi zawadi itakayofanyika mwezi Februari, na hivyo kuhitimisha kampeni hii kwa namna ya kukumbukwa, ikiwa ni uthibitisho wa dhamira ya Absa ya kuwaweka wateja katikati ya kila zawadi na kila hatua ya safari yake.
Mmoja wa washindi wa kila mwezi wa kampeni ya miezi mitatu ya benki ya Absa Tanzania iitwayo 'Ujanja ni Kuswipe na Benki ya Absa' Bw. George Kivaria, akichukua tiketi ya bahati nasibu ili kumpata mshindi wa droo Kuu wakati wa droo ya mwisho iliyofanyika jijini Dar es Salaam jana. Mteja wa benki hiyo, Bi. Nasreen Karim Abdallah, alishinda zawadi kuu ya Tsh 30,000,000. Kampeni hiyo ililenga kuwahamasisha wateja kuongeza matumizi ya kadi za debit na credit za Absa pamoja na pamoja na huduma za kibenki kwa njia za kidigitali za benki hiyo. Kushoto ni Mkuu wa Masoko na Mahusiano wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Aron Luhanga.
Mkuu wa Usimamizi wa Taarifa na Uchambuzi wa Takwimu wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Dennis Kessy (wa tatu kushoto), akikabidhi hundi ya mfano ya Tsh 500,000/- kwa Bw. George Kivaria (wa pili kushoto), mmoja wa washindi wa kampeni ya miezi mitatu ya benki hiyo iitwayo 'Ujanja ni Kuswipe na Benki ya Absa' wakati wa hafla iliyofanyika jijini Dar es Salaam jana. Kampeni hiyo ililenga kuwahamasisha wateja kuongeza matumizi ya kadi za debit na credit za Absa pamoja na huduma za kibenki kwa njia za kidigitali za benki hiyo.
Mkuu wa Usimamizi wa Taarifa na Uchambuzi wa Takwimu wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Dennis Kessy, akikabidhi hundi ya mfano ya Tsh 500,000/- kwa Bw. Mohammed Zulfikar Hemani (kushoto), mmoja wa washindi wa kampeni ya miezi mitatu ya benki hiyo iitwayo 'Ujanja ni Kuswipe na Benki ya Absa', wakati wa hafla iliyofanyika jijini Dar es Salaam jana. Kulia ni Mkuu wa Masoko na Mahusiano wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Aron Luhanga.
Share:

BENKI YA ABSA YAIPONGEZA BLACK SWAN KWA USHINDI WA BARA AFRIKA, YATHIBITISHA DHAMIRA YA KUKUZA SAFARI YA UBUNIFU WA TEKNOLOJIA YA KIFEDHA (FINTECH) TANZANIA

Benki ya Absa Tanzania imeipongeza Black Swan kwa kuibuka mshindi wa jumla wa Absa–MEST Africa Challenge 2025, shindano la ubunifu linalojumuisha nchi mbalimbali barani Afrika na linaloendeshwa kwa ushirikiano na Meltwater Entrepreneurial School of Technology (MEST Africa). Black Swan pia ilikuwa miongoni mwa washindi watatu bora wa Absa Wazo Challenge Tanzania 2025.

Ushindi huo wa ngazi ya bara, uliopatikana kupitia kampuni ya Black Swan iliyosajiliwa nchini Mauritius, ni hatua muhimu kwa teknolojia ya fedha (fintech), ambayo safari yake ilianza kutambulika ndani ya nchi kupitia Wazo Challenge Tanzania ya Absa Bank Tanzania. Mafanikio hayo yanaonesha nafasi ya Absa kama kichocheo cha ubunifu, kutoka uthibitisho wa ndani hadi ukuaji wa kiwango cha bara.

Shindano la Absa–MEST Africa Challenge liliwakutanisha kampuni bunifu zinazojihusisha na teknolojia za kifedha zenye uwezo mkubwa kutoka katika nchi mbalimbali ambako Absa inafanya kazi. Black Swan ilijitofautisha kwa suluhisho lake la upimaji mbadala wa uaminifu wa mikopo linalotumia Akili Bandia (AI), linalolenga kupanua upatikanaji wa huduma za kifedha kwa watu na biashara ndogo na za kati (SMEs) ambazo hazijahudumiwa vya kutosha.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Obedi Laiser (kulia) akishikana mikono na Mkurugenzi wa Huduma Jumuishi za Fedha wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Bw. Kennedy Komba jijini Dar es Salaam hivi karibuni, wakati wa hafla ya uzinduzi wa mpango wa Wazo Challenge Tanzania, unaolenga kuimarisha ubunifu na ujasiriamali katika sekta ya Teknolojia ya Fedha (FinTech) na biashara changa (startup) nchini Tanzania. Kushoto ni Mkuu wa Kitengo cha Huduma kwa Wateja na Huduma za Kidigitali, Bw. Samuel Mkuyu. (Picha; Maktaba)

Akizungumza kuhusu mafanikio hayo, Sam Mkuyu, Mkuu wa Kitengo cha Huduma kwa Wateja na Huduma za Kidigitali wa Benki ya Absa Tanzania, Samuel Mkuyu, alisema: “Ushindi wa Black Swan ni uthibitisho madhubuti wa sababu za kuwepo kwa majukwaa kama Wazo Challenge Tanzania. Ubunifu haukui ukiwa peke yake, unahitaji upatikanaji wa utaalamu, matumizi halisi, na taasisi zilizo tayari kushirikiana. Kupitia Wazo Challenge Tanzania, tunaunda kwa makusudi mazingira yanayowezesha fintech kujaribu mawazo, kuimarisha mifumo yao ya kiteknolojia, na kujenga suluhisho zinazoweza kukua, salama, na zinazoendana na mustakabali wa sekta ya benki. Kuona ubunifu uliojikita Tanzania ukishinda katika ngazi ya bara ni matokeo hasa tuliyolenga kuyawezesha.

Wazo Challenge Tanzania, iliyoanzishwa na Benki ya Absa Tanzania kwa ushirikiano na Hindsight Ventures, ilibuniwa kusaidia teknolojia za kifedha na wabunifu wanaoendeleza suluhisho zinazolingana na kaulimbiu ya “Bank of the Future.” Tangu kuanzishwa kwake, mpango huu umejenga imani miongoni mwa wabunifu wa ndani, ukionesha kuwa kampuni zinzojishughulisha na teknolojia za kifedha za Tanzania zinaweza kushindana na kushinda katika majukwaa makubwa barani Afrika.

Zaidi ya Tanzania, Absa Group inaendelea kuchangia kwa kiwango kikubwa ukuaji wa fintech barani Afrika kupitia mipango kama MEST Africa Challenge, inayounganisha kampuni changa na mitaji, ushirikiano wa kibiashara wa kiwango cha taasisi, pamoja na fursa za kuvuka mipaka ya nchi.
Baadhi ya washiriki wa Wazo Challenge Tanzania 2025, wakiwa katika hafla ya makabidhiano ya zawadi kwa washindi, jijini Dar es Salaam hivi karibuni. (Picha; Absa Bank Tanzania)

Akizungumza kuhusu dhamira pana ya Absa na umuhimu wa kusimulia hadithi za ubunifu, Aron Luhanga, Mkurugenzi wa Masoko na Mahusiano wa Benki ya Absa Tanzania, alisema:

Safari ya Black Swan inaakisi kikamilifu ahadi ya chapa yetu isemayo ‘Stori yako ina thamani’. Kutoka katika mfumo wa ubunifu wa Tanzania hadi kutambulika katika ngazi ya bara, hii ni stori ya imani, ushirikiano na uwezekano. Katika Absa, dhamira yetu iko wazi, Kuiwezesha Afrika ya Kesho, pamoja, hatua moja baada ya nyingine. Stori za fintech kama Black Swan zinatuhamasisha kuendelea kuunga mkono ubunifu na kusimama bega kwa bega na wajasiriamali wanaounda mustakabali wa Afrika.

Absa Bank Tanzania pia imetangaza kuwa maandalizi ya toleo lijalo la Wazo Challenge Tanzania yanaendelea, likitarajiwa kufanyika mwaka 2026, likiwa na msisitizo mkubwa zaidi kwenye suluhisho za teknoljia za kifedha zinazoweza kukua, ujumuishi wa kidijitali, na ushirikiano unaozalisha matokeo chanya ya kiuchumi.

Tunapoangalia mbele kuelekea Wazo Challenge Tanzania 2026, tunataka wabunifu wajue kuwa kuna taasisi katika soko hili zinazowaamini,” aliongeza Mkuyu. “Ubunifu hustawi pale imani inapokutana na fursa, na Absa imejidhatiti kutoa vyote viwili.

Kupitia mipango ya ngazi ya nchi na ya Kundi, Absa inaendelea kujiweka kama kinara wa fikra katika uwezeshaji wa fteknolojia za kifedha, ushirikiano wa ubunifu, na ujumuishi wa kifedha, ikihakikisha kuwa mawazo yanayozaliwa Tanzania yanaweza kukua na kuwa suluhisho zinazohudumia Afrika nzima.
Share:

AVODA BLUE TANZANIA GRADUATES FIRST COHORT OF ENTREPRENEURS

Unleashed Africa Social Enterprises Acting Board Chairperson, Ms. Ngianasia Minja (second right), presents a certificate to Ms. Esther Kolimba, a graduand of the four-month AVODA Blue Tanzania entrepreneurship program, during a function held in Dar es Salaam. The program aims to strengthen Tanzania’s business landscape through world-class strategy, operational excellence, and faith-based leadership principles. Looking on from left are Avoda Group Founder and CEO, Mr. Jun Shiomitsu, and Avoda Uganda Country Director, Mr. Joshua Agonya.

By Peter Mgongo | Dar es Salaam, Tanzania

The AVODA Blue Tanzania Program has celebrated the graduation of its first cohort of entrepreneurs, marking a major milestone in developing globally competitive and ethically grounded business leaders in the country. The ceremony held in Dar es Salaam recently, bringing together government leaders, business executives, investors, and development partners.

Launched earlier this year, AVODA Blue Tanzania is a four-month, execution-focused entrepreneurship program adapted from the Cambridge MBA and contextualized for African markets, the program aims to strengthen Tanzania’s business landscape through world-class strategy, operational excellence, and faith-based leadership principles.

Cohort 1 brought together founders from sectors including technology, food production, logistics, fashion, education, real estate advisory, and social enterprise. Over the past four months, participants completed intensive training sessions, virtual modules, one-on-one diagnostics, and practical assignments applied directly to their businesses.

Guest of Honor, Mr. Jason Ndanguzi who was representing the ICT Commission’s Director General, Dr. Nkundwe Mwasaga, underscored the importance of entrepreneurship in advancing the country’s digital economy.

This moment aligns with Tanzania’s broader vision, as a nation, we are accelerating the Digital Economy Framework, strengthening our ICT Policy, and preparing our people and enterprises for a knowledge-based, technology-enabled future. For the ICT Commission, this program demonstrates exactly the kind of capacity-building that Tanzania needs as we transition into a digital era."

Across global innovation economies, one pattern is clear; countries rise not because they have ideas, but because they have capable founders. Founders with strategic discipline. Founders who understand technology. Founders who lead with integrity. Founders who build enterprises that last. Avoda Blue is among the few programs in Tanzania addressing this with such depth, rigor, and intentionality”, he noted.

The ICT guru added; “As the ICT Commission, we stand ready to deepen collaboration with programs that strengthen digital capability, prepare entrepreneurs for scale, integrate emerging technologies, and support the creation of sustainable businesses. Tanzania’s rise depends on entrepreneurs who are ready to build boldly, adapt quickly, and innovate continuously."

To our graduates, today marks your transition into a new identity, you are no longer simply business owners, you are architects of Tanzania’s digital and economic future. Over the last four months, you have engaged with operational frameworks, financial discipline, AI tools, product refinement, Kingdom leadership principles, and investor readiness, this kind of preparation is rare in our market, and deeply necessary”, added Mr. Ndanguzi.

Earlier the Unleashed Africa CEO, Ms. Khalila Mbowe said her social ventures reaffirms its national commitment to building world-class programs that equip Tanzania’s youth, founders, and industry leaders with the skills, networks, and mindsets needed to build high-performing, future-ready enterprises

For too long, many African entrepreneurs including many of us have operated from the back benches of business excellence, that era must be history, across our brands; from RiseUp, to JUU’s creative economy work, to The Space and its flagship Nipe Dili program, Unleashed Africa has been steadily constructing a holistic empowerment ecosystem where young people can access opportunities, develop 21st-century skills, secure business support, and deepen their leadership potential”, said Ms. Khalila.

Avoda Group Founder and CEO Jun Shiomitsu expressed deep appreciation to Unleashed Africa for being the first organization in Tanzania to believe in and partner with the AVODA mission. He noted that although expanding the program beyond Uganda was initially considered difficult, the team’s prayers and the strong Christian entrepreneurial ecosystem helped pave the way. He added that their relationship with Unleashed Africa is already bearing visible fruit, demonstrating the powerful work taking place in Tanzania.

To the graduates; first of all, you believed in us. Now, as you graduate, it is our turn to believe in you, to ensure that your businesses find the customers they need and the capital they require. It is our turn now to place our trust in you. I am confident that your businesses will achieve great things, truly great things, and I stand firmly by that confidence. Christian connections around the world have already seen and experienced our services. By graduating from Avoda, you are being planted into a massive global ecosystem, in Asia, Europe, and the Americas, among people who share your faith and who want to see you succeed,” he said.

One of the graduands, Engineer Regina Fumbuka from Multi Genius Africa, an organization working to make mathematics more appealing and easier to teach said, the Avoda program has helped her learn how to become a good leader, build effective business systems, manage a business, and maintain proper financial records. She added that the program has enabled her to progress from one level to another in her entrepreneurial journey.

Three awards were presented during the ceremony; the Exceptional Performance Award, Business Growth Excellence Award, and Servant Leadership Award. Graduates also showcased their businesses, growth milestones, and investment or partnership needs through a three-minute pitch session.
Unleashed Africa Social Enterprises Acting Board Chairperson, Ms. Ngianasia Minja (second right), presents a certificate to Mr. Alexander Rwiza, a graduand of the four-month AVODA Blue Tanzania entrepreneurship program, during a function held in Dar es Salaam recently. The program aims to strengthen Tanzania’s business landscape through world-class strategy, operational excellence, and faith-based leadership principles. Looking on from left are Avoda Group Founder and CEO, Mr. Jun Shiomitsu, and Avoda Uganda Country Director, Mr. Joshua Agonya.
Unleashed Africa Chief Executive Officer, Ms. Khalila Mbowe (right), moderates a panel discussion during the four-month AVODA Blue Tanzania entrepreneurship program graduation, adapted from the Cambridge MBA and contextualized for African markets. The program aims to strengthen Tanzania’s business landscape through world-class strategy, operational excellence, and faith-based leadership principles. The event was held in Dar es Salaam recently. On her right are Avoda Uganda Country Director, Mr. Joshua Agonya; one of the graduands, Ms. Esther Kolimba and Avoda Group Founder and CEO, Mr. Jun Shiomitsu. (Photos by Peter Mgongo)
Share:

INNOVATION HUBS NETWORK STAKEHOLDERS RECOGNIZED FOR OUTSTANDING CONTRIBUTION

The Chairperson of the Board of the Tanzania Hubs Network (THN), Dr. Irene Shubi Isinika, speaking at the ceremony to commend pioneering innovation stakeholders held alongside the THN Annual General Meeting in Dar es Salaam recently. Since its establishment in 2020, THN has been at the forefront of building an innovation ecosystem by empowering innovation hubs to support innovators and entrepreneurs in driving social and economic development.
The Chairperson of the Board of the Tanzania Hubs Network (THN), Dr. Irene Shubi Isinika (right), presenting an honorary award to the Project Manager of the Funguo Program run by the United Nations Development Programme (UNDP), Mr. Joseph Manirakiza, in recognition of his contribution to innovation development in the country. This took place during the ceremony to commend innovation stakeholders held alongside the THN Annual General Meeting in Dar es Salaam recently.
Senior Lecturer at the College of Information and Communication Technologies of the University of Dar es Salaam and Innovation Coordinator through the university’s innovation hub (UDICTI), Dr. Moses Ismail (left), receiving an award presented by the Tanzania Hubs Network (THN) from the Country Director of the Westerwelle Tanzania Foundation, Mr. Isaack Shalo, at a ceremony organized by THN in Dar es Salaam to recognize pioneering stakeholders who have contributed to the advancement of innovation in the country.

By Peter Mgongo, Dar es Salaam

In recognizing the contribution of stakeholders who have supported the growth of innovation in the country, the Tanzania Hubs Network (THN) organized an official ceremony to commend pioneering innovation stakeholders, alongside the network’s annual general meeting.

Speaking at the ceremony in Dar es Salaam yesterday, the Executive Director of the network, Mr. Kiko Kiwanga, said the network, which was established in 2020, connects more than 62 hubs across Mainland Tanzania and Zanzibar, bringing together innovation hubs from universities, organizations, governmental bodies, and private centers.

Today is a very special day for our ecosystem because since we began, this is our first annual meeting, which started this morning with the guest of honor being the Director of the ICT Commission, Dr. Nkundwe Mwasaga. We are now doing something unique within our ecosystem to recognize stakeholders who have made significant contributions in advancing innovation and strengthening these hubs.

The contributions of these stakeholders have always been acknowledged, but today, for the first time, we are holding this event to recognize the pioneering stakeholders who have put great effort into ensuring that young innovators and startup entrepreneurs grow and receive support within our ecosystem,” said Mr. Kiwanga.

Speaking about the THN Network, the director said that since its establishment, it has been at the forefront of building an innovation ecosystem by empowering innovation hubs to support innovators and entrepreneurs to drive social and economic development.

We call upon the government to increase investment in supporting youth through this network, enabling them to achieve their innovation goals and establish companies with great potential to create jobs and solve various societal challenges. These hubs have done tremendous work in preparing young people, many come in without any ideas at all, and they are supported until they develop concrete concepts.

Speaking at the event, one of the stakeholders who received an award, Dr. Moses Ismail, a Senior Lecturer at the College of Information and Communication Technologies of the University of Dar es Salaam and Innovation Coordinator through the university’s innovation hub (UDICTI), said that although the university engages in teaching, research, community service, and consultancy, with innovation and entrepreneurship taught to first-year students for many years, in 2010 the college established the UDICTI innovation hub with the aim of providing practical innovation training.

The hub provides a dedicated workspace, specialized training in developing innovative products, and linkages to innovation stakeholders who can support the work they undertake.

Innovation is a crucial tool for the development of a country and its people because it enhances the value of local innovative products. Many of us rely heavily on imported products, yet locally we have various innovative products that help our students become major contributors to the production of these products, which eventually grow into companies and help increase employment, especially at a time when we want our university graduates to be key drivers of job creation rather than job seekers,” said Dr. Ismail.

Meanwhile, the Chief Executive Officer of the Business Registrations and Licensing Agency (BRELA), Mr. Godfrey Nyaisa, speaking at the event, urged innovators, especially those running startups to register their businesses with BRELA so they can benefit from various guidelines that will enable them to operate efficiently. He also challenged the THN Network to involve government authorities in their day-to-day operations.

With a vision of strengthening collaboration, providing resources, and promoting knowledge exchange among its members, THN also collaborates with the Information and Communication Technologies Commission (ICTC) to strengthen the innovation environment and promote the establishment of innovation hubs in various regions.

Share:

Benki ya Absa Tanzania yang'ara tuzo za NBAA

   

Naibu Waziri wa Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. Laurent Luswetila (kulia), akikabidhi tuzo ya mshindi wa pili wa Uwasilishaji Bora wa Taarifa za Fedha katika kitengo cha Mabenki yenye Ukubwa wa Kati kwa Mwaka 2024 zinazotolewa na Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu (NBAA), kwa Mkuu wa Uchambuzi wa Utendaji wa Biashara wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Stivin Augustino (wa pili kushoto) na Mdhibiti wa Masuala ya Fedha wa benki hiyo, Bw. Muhsin Kaye, katika hafla iliyofanyika jijini Dar es Salaam jana. Wa tatu kushoto Mkurugenzi Mtendaji wa NBAA, CPA. Pius Maneno.
Mdhibiti wa Masuala ya Fedha wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Muhsin Kaye ( wa pili kushoto) akishikana mikono na Mwenyekiti wa Bodi ya NBAA, CPA Prof. Sylvia Temu, mara baada ya kupokea tuzo ya mshindi wa pili wa Uwasilishaji Bora wa Taarifa za Fedha katika kitengo cha Mabenki yenye Ukubwa wa Kati kwa Mwaka 2024 zinazotolewa na Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu (NBAA), katika hafla iliyofanyika jijini Dar es Salaam jana. Kutoka kulia ni Naibu Waziri wa Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. Laurent Luswetila, Mkurugenzi Mtendaji NBAA, CPA. Pius Maneno na Mkuu wa Uchambuzi wa Utendaji wa Biashara wa benki hiyo, Bw. Stivin Augustino.
Mkuu wa Uchambuzi wa Utendaji wa Biashara wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Stivin Augustino (kushoto) na Mdhibiti wa Masuala ya Fedha wa benki hiyo, Bw. Muhsin Kaye wakipozi mbele ya wapigapicha baada ya kukabidhiwa tuzo ya mshindi wa pili wa Uwasilishaji Bora wa Taarifa za Fedha katika kitengo cha Mabenki yenye Ukubwa wa Kati kwa Mwaka 2024, zinazotolewa na Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu (NBAA) katika hafla iliyofanyika jijini Dar es Salaam jana.
Mkuu wa Uchambuzi wa Utendaji wa Biashara wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Stivin Augustino (mstari wa mbele wa tatu kushoto) akipiga picha ya pamoja na washindi mbalimbali wa tuzo za Uwasilishaji Bora wa Taarifa za Fedha katika kitengo cha Mabenki yenye Ukubwa wa Kati kwa Mwaka 2024, zinazotolewa na Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu (NBAA), zilizofanyika jijini Dar es Salaam jana.
Share:

LILIAN-FAVOUR MAKAWA

LILIAN-FAVOUR MAKAWA

Popular Posts

Blog Archive

Labels

Recent Posts

Label Cloud

BIASHARA (291) BURUDANI (4) KIMATAIFA (10) KITAIFA (120) MICHEZO (39) SIASA (3)

Pages