ACI FMA Tanzania yathibitisha kuunga mkono maendeleo ya masoko ya fedha nchini

 

Ofisa Mtendaji Mkuu wa Soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE), Bw. Peter Nalitolela (kulia), Rais wa ACI FMA Global Bw. Rui Correia, na Rais wa ACI FMA Tanzania Bw. Farid Yahya Ally wakichukua chakula cha futari katika hafla iliyoandaliwa na ACI FMA Tanzania jijini Dar es Salaam jana. Hafla hiyo iliwakutanisha wadau wa masoko ya fedha, watunga sera na wadhibiti ili kuimarisha ushirikiano na kukuza mazingira imara ya masoko ya fedha nchini.

ACI FMA Tanzania imethibitisha tena dhamira yake ya kuunga mkono ukuaji endelevu wa masoko ya fedha ya Tanzania na kuchangia kwa maana katika maendeleo endelevu ya uchumi wa taifa.

Hayo yalibainishwa na Rais wa chama hicho, Bw. Farid Yahya Ally, wakati wa hafla ya futari iliyofanyika Dar es Salaam mwishoni mwa wiki. Hafla hiyo ilijumuisha mjadala wa jopo kuhusu maendeleo na changamoto zinazoikabili sekta ya masoko ya fedha nchini Tanzania na iliwakutanisha wadau wa soko, watunga sera na wadhibiti wa sekta hiyo.

Kupitia ushirikiano endelevu na wadhibiti, watunga sera pamoja na wadau wa sekta, chama kitaendelea kuunga mkono mipango inayolingana na malengo ya muda mrefu ya maendeleo ya Tanzania, ikiwemo azma ya Dira 2050 ambayo inalenga kujenga uchumi wa dola trilioni moja,” alisema Bw. Ally.

Akihutubia wawakilishi mashuhuri kutoka Benki Kuu ya Tanzania, Soko la Hisa la Dar es Salaam, pamoja na Wakuu wa Masoko ya Kimataifa kutoka taasisi mbalimbali za kifedha, Bw. Ally alibainisha kuwa kama chombo cha kitaaluma kinachowakilisha wataalamu wa masoko ya fedha, ACI FMA Tanzania inatambua jukumu lake muhimu katika kuimarisha maendeleo na uadilifu wa masoko ya fedha nchini.

Kuimarisha ushirikiano na watunga sera pamoja na wadhibiti ni sehemu muhimu ya dhamira yetu ya kukuza kanuni bora za uendeshaji wa soko na kuhakikisha Tanzania inaendelea kuwa na mazingira rafiki kwa wawekezaji wa ndani na wa kimataifa,” alisema.

Hafla ya futari ilikuwa jukwaa muhimu la majadiliano na ushirikiano kati ya washiriki wa soko, watunga sera na wadhibiti. Majadiliano yalilenga kutafuta njia za kuziba mapengo ya kitaasisi yaliyopo na kuimarisha ushirikiano katika kujenga mazingira imara na yenye ustahimilivu kwa masoko ya fedha.

Wakati wa majadiliano hayo, washiriki walibainisha changamoto kadhaa zinazoathiri sekta ya masoko ya fedha, ikiwemo ukosefu wa utofauti wa bidhaa za kifedha, taratibu ngumu za udhibiti kwa washiriki wapya wa soko, pamoja na utegemezi mkubwa wa ufadhili unaotolewa na taasisi za kifedha.

Akijibu hoja hizo, Mtendaji Mkuu wa Soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE), Bw. Peter Nalitolela, alikiri kuwa ingawa masoko ya mitaji nchini Tanzania yanaendelea kukua, uelewa wa wawekezaji wadogo kuhusu soko hilo bado ni mdogo.

Alisema kuwa licha ya idadi ya akaunti za Central Depository System (CDS) kuwa ndogo kwa kiasi, hivi karibuni soko limeanza kushuhudia ongezeko la wawekezaji wapya wanaoingia kwenye soko la hisa.

Ingawa wawekezaji wengi zaidi wanaonesha nia ya kuingia sokoni, changamoto kadhaa bado zinaendelea kuwepo, ikiwemo ukosefu wa utofauti wa bidhaa za kifedha na maandalizi ya soko kukidhi ongezeko la ushiriki wa wawekezaji,” alisema.

Bw. Nalitolela pia alibainisha kuwa mauzo ya awali ya hisa kwa umma (IPOs) yamepungua si Tanzania pekee bali pia kimataifa, hali inayoakisi mwenendo mpana wa masoko duniani.

Hata hivyo, alisisitiza kuwa Tanzania inaendelea kubadilika taratibu kutoka katika mfumo wa uchumi unaoongozwa zaidi na serikali kuelekea uchumi unaochochewa zaidi na sekta binafsi, hatua ambayo tayari imeanza kuleta mwamko chanya katika masoko ya mitaji na hisa.

Wakati huohuo, Rais wa ACI FMA Duniani, Bw. Rui Correia, alitangaza kuwa chama hicho kitaanzisha mpango wa ufadhili wa masomo kwa wanawake barani Afrika ili kusaidia wataalamu wanawake katika sekta ya masoko ya fedha.

Hili ni jambo tunalotaka kufanya hasa tunapokaribia Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani. Kwa mwaka huu tutazingatia ufadhili wa masomo kwa wanawake barani Afrika, na mwaka ujao tutaanzisha mpango mwingine,” alisema Bw. Correia.

Alisisitiza kuwa chama hicho kinathamini sana ushirikishwaji wa maarifa na maendeleo ya kitaaluma ndani ya jamii ya wataalamu wa masoko ya fedha.

Kwetu sisi, elimu si kupata vyeti pekee. Ni kuhusu kubadilishana utaalamu, maarifa na uzoefu katika nyanja mbalimbali za masoko ya fedha,” aliongeza.

ACI FMA Tanzania ni shirika lisilo la kiserikali linalofanya kazi chini ya mwavuli wa ACI FMA Global. Chama hicho kinakuza kanuni bora za uendeshaji wa soko kwa kuwapatia wataalamu wa masoko ya fedha mafunzo, fursa za kushiriki katika shughuli za kitaaluma pamoja na vyeti vinavyotambulika kimataifa.
Rais wa ACI FMA Tanzania, Bw. Farid Yahya Ally, akizungumza na washiriki wakati wa hafla ya futari, iliyofanyika Dar es Salaam jana. Hafla hiyo iliwakutanisha wadau wa masoko ya fedha, watunga sera na wadhibiti ili kuimarisha ushirikiano na kukuza mazingira imara ya masoko ya fedha nchini.
Rais wa ACI FMA Tanzania Bw. Farid Yahya Ally (kulia) akibadilishana mawazo na Rais wa ACI FMA Duniani, Bw. Rui Correia (kushoto) pamoja na Mchambuzi Mwandamizi wa Masuala ya Fedha kutoka Benki Kuu ya Tanzania, Bw. Stanslaus Shenyali, wakati wa hafla ya futari, iliyoandaliwa na ACI FMA Tanzania Dar es Salaam jana.
Ofisa Mtendaj Mkuu wa Soko la Hisa la Dar es Salaam Bw. Peter Nalitolela (kulia) akizungumza wakati wa mjadala uliofanyika pamoja futari iliyoandaliwa na ACI FMA Tanzania jijini Dar es Salaam jana. Hafla hiyo iliwakutanisha wadau wa masoko ya fedha, watunga sera na wadhibiti ili kuimarisha ushirikiano na kukuza mazingira imara ya masoko ya fedha nchini.
Baadhi ya wageni waalikwa wakiwa katika hafla ya futari iliyoandaliwa na ACI FMA Tanzania, jijini Dar es Salaam jana. Hafla hiyo iliwakutanisha wadau wa masoko ya fedha, watunga sera na wadhibiti ili kuimarisha ushirikiano na kukuza mazingira imara ya masoko ya fedha nchini.
Rais wa ACI FMA Tanzania Bw. Farid Yahya Ally (wa nane kutoka kushoto), Rais wa ACI FMA Duniani, Bw. Rui Correia (wa sita kutoka kushoto), maofisa wa ACI na wageni wengine waalikwa wakipiga picha ya pamoja baada ya hafla ya futari iliyofanyika Dar es Salaam jana. Hafla hiyo iliwakutanisha wadau wa masoko ya fedha, watunga sera na wadhibiti ili kuimarisha ushirikiano na kukuza mazingira imara ya masoko ya fedha nchini.
Share:

BENKI YA ABSA TANZANIA YATAMBULIWA KWA DHAMIRA YAKE THABITI YA KUWAWEZESHA WANAWAKE NCHINI

  

Mkurugenzi Mtendaji wa Benkiy a Absa Tanzania, Bw. Obedi Laiser (wa sita kushoto), akionesha tuzo ya ‘Rising Women’ mara baada ya kukabidhiwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Mipango na Uwekezaji, Prof. Kitila Mkumbo (wa tano kushoto), jijini Dar es Salaam jana. Benki hiyo ilitambuliwa kwa dhamira yake thabiti ya kuwawezesha wanawake, kuendeleza ujumuishaji wa kifedha na kuunda fursa zenye maana kwa uwakilishi wa wanawake katika nafasi za uongozi.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Mipango na Uwekezaji, Prof. Kitila Mkumbo, akikabidhi tuzo ya ‘Rising Women’ kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Bww. Obedi Laiser (wa pili kulia), jijini Dar es Salaam jana. Benki hiyo ilitambuliwa kwa dhamira yake thabiti ya kuwawezesha wanawake, kuendeleza ujumuishaji wa kifedha na kuunda fursa zenye maana kwa uwakilishi wa wanawake katika nafasi za uongozi.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Mipango na Uwekezaji, Prof. Kitila Mkumbo, akikabidhi tuzo ya shukrani kwa Meneja Huduma za Jamii na Mtukio wa Benki ya Absa Tanzania, Bi. Abigail Lukuvi (kulia), kwa kutambua mchango wa benki hiyo katika Mpango wa Rising Women. Hafla hiyo ilifanyika jijini Dar es Salaam jana. Benki hiyo ilitambuliwa kwa dhamira yake thabiti ya kuwawezesha wanawake, kuendeleza ujumuishaji wa kifedha na kuunda fursa zenye maana kwa uwakilishi wa wanawake katika nafasi za uongozi.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Obedi Laiser (wa nne kushoto), na Meneja Huduma za Jamii na Matukio wa wa benki hiyo, Bi. Abigail Lukuvi (wa tatu kulia), pamoja na baadhi ya wafanyakazi wa Absa, wakipozi na tuzo za utambuzi za ‘Rising Women’ jijini Dar es Salaam jana. Benki hiyo ilitambuliwa kwa dhamira yake thabiti ya kuwawezesha wanawake, kuendeleza ujumuishaji wa kifedha na kuunda fursa zenye maana kwa uwakilishi wa wanawake katika nafasi za uongozi.
Share:

AKIBA COMMERCIAL BANK ENGAGES WOMEN ENTREPRENEURS AHEAD OF INTERNATIONAL WOMEN’S DAY

    

Akiba Commercial Bank’s Chief Commercial Officer, Wezi Mwazani speaks during the engagement.

In celebration of International Women’s Day, Akiba Commercial Bank Plc hosted a special engagement event in Dar es Salaam on 6 March 2026, bringing together female entrepreneurs served by the bank from various branches across the city.

The event formed part of the bank’s Lady Entrepreneur Campaign, an initiative aimed at strengthening relationships with women customers while promoting financial empowerment and business growth.

Supporting Women in Business

Speaking during the engagement, the Bank’s Chief Commercial Officer, Wezi Mwazani, highlighted the important role women play in economic development and community transformation.


She emphasized that women entrepreneurs remain a key focus for the bank as it continues to expand financial inclusion and support the growth of small and medium-sized enterprises (SMEs).

Mwazani noted that the bank is committed to providing tailored financial solutions designed to meet the needs of women at different stages of their entrepreneurial journey.


Women entrepreneurs continue to demonstrate resilience and innovation in business. At Akiba Commercial Bank, we are committed to supporting women with financial solutions, knowledge, and opportunities that help them grow their businesses and improve their livelihoods,” she said.

Entrepreneurs Share Their Experiences

During the engagement, customers expressed appreciation for the support extended by the bank through its financial services and advisory initiatives.

Participants noted that access to banking services and financing has enabled them to:

  • Strengthen and expand their businesses
  • Increase household income
  • Improve their standards of living

Some entrepreneurs also highlighted that the support received has helped them contribute more actively to community development and job creation, demonstrating the wider impact of empowering women in business.

Strengthening Customer Relationships

The engagement in Dar es Salaam brought together female customers from several branches across the city, reflecting the bank’s commitment to deepening relationships with its customers while gaining insights into their evolving financial needs.

The bank also indicated that the event marks the beginning of broader outreach activities under the Lady Entrepreneur Campaign. Similar engagements are expected to be extended to customers in other regions where the bank operates.

Expanding Opportunities for Women Entrepreneurs

Through these continued engagements, Akiba Commercial Bank Plc aims to expand opportunities for women entrepreneurs by:

  • Promoting financial literacy and knowledge
  • Improving access to financial services
  • Supporting business growth and sustainability

The bank has also encouraged women entrepreneurs and business groups to visit its branches to explore the available banking solutions and take part in the ongoing Lady Entrepreneur Campaign as it expands to other regions across the country.











Share:

MKURUGENZI MTENDAJI WA BENKI YA ABSA TANZANIA NA UJUMBE WAKE WAMTEMBELEA MKUU WA MKOA WA MBEYA OFISINI KWAKE

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Mhe. Beno Malisa (kushoto), akimkaribisha Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Obedi Laiser, alipofika kumtembelea akiwa na ujumbe wake, ofisini kwake, mjini Mbeya jana. Bw. Laiser na ujumbe wake wapo mjini Mbeya kwa ziara ya kikazi.
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Mhe. Beno Malisa (kushoto), akisalimiana na Mkuu wa Uendeshaji wa Matawi wa Benki ya Absa Tanzania, Bi. Mwilongo Msungu, wakati Mkurugenzi Mtendaji wa benki hiyo, Bw. Obedi Laiser (Katikati), na ujumbe wake, ukimtembela mkuu wa mkoa huyo, ofisini kwake, mjini Mbeya jana. Bw. Laiser na ujumbe huo wapo mjini Mbeya kwa ziara ya kikazi.
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Mhe. Beno Malisa (kushoto), akiwa na baadhi ya wakurugenzi wa Benki ya Absa Tanzania, wakati wa ziara ya Mkurugenzi Mtendaji wa benki hiyo, Bw. Obedi Laiser (hayupo pichani), na ujumbe wake, walipomtembelea mkuu wa mkoa huyo, ofisini kwake, mjini Mbeya jana. Bw. Laiser na ujumbe huo wapo mjini Mbeya kwa ziara ya kibiashara. Katikati ni Mkurugenzi wa Wateja Binafsi, Bi. Ndabu Swere na Mkuu wa Uendeshaji wa Matawi, Bi. Mwilongo Msungu.
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Mhe. Beno Malisa (kulia), akiagana na Mkuu wa Mikakati na Data wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. John Mosha, wakati yeye, Mkurugenzi Mtendaji wa benki hiyo, Bw. Obedi Laiser pamoja na maofisa wengine wa benki hiyo, walipomtembelea mkuu wa mkoa huyo, ofisini kwake, mjini Mbeya jana. Bw. Laiser na ujumbe huo wapo mjini Mbeya kwa ziara ya kikazi.
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Mhe. Beno Malisa (kulia), akiagana na Meneja wa Benki ya Absa mkoani humo, Bw. Alto Hagamu, na Mkuu wa Kitengo cha Biashara wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Melvin Saprapasen (kushoto), wakati wao, Mkurugenzi Mtendaji wa benki hiyo, Bw. Obedi Laiser (hayupo pichani), pamoja na maofisa wengine wa benki hiyo, walipomtembelea mkuu wa mkoa huyo, ofisini kwake, mjini Mbeya jana. Bw. Laiser na ujumbe huo wapo mjini Mbeya kwa ziara ya kikazi.
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Mhe. Beno Malisa (wa sita kushoto), akipozi kwa picha ya kumbukumbu na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Obedi Laiser (kulia kwake), mara baada ya mkurugenzi huyo pamoja na ujumbe wake kumtembelea ofisini kwake mjini Mbeya jana wakiwa mkoani humo kwa ziara ya kikazi.
Share:

BENKI YA ABSA TANZANIA YATHIBITISHA DHAMIRA YA KUENDELEZA UWEZESHAJI WA WANAWAKE KIUCHUMI KAMA NGUZO YA UKUAJI WA TAIFA

Benki ya Absa Tanzania imethibitisha upya dhamira yake ya kuendeleza uwezeshaji wa wanawake kiuchumi, ikisisitiza kuwa ujumuishaji si tendo la hisani la taasisi bali ni mkakati muhimu wa kitaifa kwa ukuaji endelevu wa uchumi.

Akizungumza na vyombo vya habari jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki hiyo, Obedi Laiser, alieleza kuwa kuwawezesha wanawake ni msingi wa ushindani wa muda mrefu wa uchumi wa Tanzania.

Uwezeshaji wa wanawake si jambo la hiari katika ukuaji wa uchumi. Ni hitaji la lazima kwa ukuaji,” alisema Bw. Laiser. “Kuwaacha nje karibu nusu ya rasilimali watu wa taifa kushiriki kikamilifu katika uchumi kunasababisha hasara inayoonekana yenye tija.

Alibainisha kuwa katika Absa, dhana ya ujumuishaji imejengeka ndani ya mfumo wa uendeshaji wa benki hiyo, ikilenga ubunifu wa bidhaa, mifumo ya utoaji mikopo, maendeleo ya uongozi pamoja na ushirikiano wa kimkakati.

Wanawake daima wameonesha uwezo na uthabiti. Nguvu ilikuwepo siku zote. Kilichokosekana mara nyingi ni fursa, fursa ya kupata mitaji, mitandao na mifumo rasmi,” alisema. “Tunapowawezesha wanawake, hatuchagui tu kundi fulani. Tunachagua mustakabali wa Tanzania.

Mfano halisi wa dhamira hiyo ni akaunti ya She Business Account, suluhisho maalum lililobuniwa kushughulikia vikwazo vinavyowazuia mara nyingi wanawake wajasiriamali kuingia katika mfumo rasmi wa benki. Bidhaa hiyo inapunguza gharama za uendeshaji wa akaunti huku ikihamasisha ujenzi wa historia ya miamala inayoongeza sifa za kustahili mikopo.

Kutambua kuwa masharti ya dhamana na hali ya kutokuwa rasmi kwa baadhi ya biashara hupunguza upatikanaji wa fedha, benki hiyo pia imeimarisha ushirikiano na taasisi za fedha ndogo. Kupitia mfumo huu wa ufadhili wa ngazi mbalimbali, Absa hutoa mitaji kwa wakopeshaji waliobobea ambao huwafikishia wanawake wajasiriamali katika ngazi za msingi.

Bw. Laiser pia alitofautiana na mtazamo kwamba wanawake ni wakopaji wenye hatari kubwa zaidi. “Dhana kwamba wanawake ni wakopaji hatarishi zaidi haiendani na takwimu za utendaji. Biashara zinazoongozwa na wanawake mara nyingi huonesha nidhamu kubwa ya marejesho ya mikopo na mwenendo endelevu wa kuwekeza tena.

Mbali na suluhisho za kifedha, Absa inaweka ujumuishaji katika misingi ya taasisi kupitia mipango ya kukuza uongozi. Bw. Laiser ni mdhamini wa programu ya ndani ya ulezi inayojulikana kama “ElevateHer,” inayowawezesha mameneja wanawake wa ngazi ya kati kujenga uwepo wa kiuongozi, kuimarisha ushiriki katika vikao vya bodi, na kuongeza mwonekano wa kimkakati.

Benki hiyo pia huwezesha uhusiano wa ulezi kati ya wakurugenzi wanawake waandamizi na viongozi chipukizi, hatua inayokuza mwendelezo wa uongozi na uhamishaji wa maarifa. Dhamira hii imejikita katika madhumuni ya taasisi ya Absa, ‘Kuiwezesha Afrika ya Kesho Pamoja, hatua moja baada ya nyingine’, na ahadi yake ya chapa, ‘Stori yako ina thamani’.

Madhumuni yetu yanaakisi imani kwamba ukuaji endelevu hupatikana kwa kufungua uwezo wa mtu mmoja mmoja na wa pamoja. ‘Stori yako ina thamani’ inamaanisha kila mjasiriamali, kila kiongozi na kila ndoto inastahili kutambuliwa, kuungwa mkono na kupewa fursa,” alisema Bw. Laiser.
Aidha, Bw. Laiser alionya kuwa kupunguza kasi ya juhudi za makusudi za uwezeshaji kutaleta gharama zinazoonekana, ikiwemo kudhoofika kwa uthabiti wa kaya, kupungua kwa utofauti wa uongozi na kushuka kwa ushindani wa taifa.

Katika mazingira ya sasa ya kimataifa, ujumuishaji si suala la pembeni tena. Ni kiini cha uimara wa muda mrefu wa mizania ya kifedha na kasi ya uchumi wa taifa,” alisema.

Kwa Absa Bank Tanzania, uwezeshaji wa wanawake si kampeni ya msimu bali ni uwekezaji wa kimuundo, unaounganisha mafanikio ya kibiashara na maendeleo ya kijamii, na kuiweka benki hiyo kama kichocheo cha mageuzi jumuishi ya uchumi.
Share:

Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar, Suleiman Abdulla awaongoza wateja, wadau wa NBC kushiriki hafla ya futari Zanzibar

 

Makamu wa Pili wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Mhe. Hemed Suleiman Abdulla (katikati) akipokea zawadi maalum kutoka kwa Mkurugenzi wa Idara ya Mikopo wa NBC, Bw Saleh Mohammed (kulia) wakati wa hafla ya futari iliyoandaliwa na benki hiyo kwa ajili ya wateja wake visiwani Zanzibar. Anaeshuhudia ni Naibu Mufti Mkuu wa Zanzibar, Sheikh Mahmoud Mussa Wadi. Hafla hiyo ilifanyika jana kwenye hotel ya Madinat Al Bahr, Zanzibar ikihusisha wateja na wadau mbalimbali wa benki hiyo wakiwemo viongozi wa serikali na dini.
  • Aipongeza NBC kwa Mchango wa Maendeleo Zanzibar.
Makamu wa Pili wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Mhe. Hemed Suleiman Abdulla jana aliwaongoza baadhi ya waislamu visiwani humo kushiriki hafla fupi ya futari iliyoandaliwa na Benki ya Taifa ya Biashara (NBC) kwa ajili ya wateja na wadau mbalimbali wa benki hiyo visiwani humo.

Hafla hiyo ilifanyika kwenye hotel ya Madinat Al Bahr, Zanzibar ikihusisha wateja na wadau mbalimbali wa benki hiyo wakiwemo viongozi wa serikali na dini akiwemo Naibu Mufti Mkuu wa Zanzibar, Sheikh Mahmoud Mussa Wadi. Mkurugenzi wa Idara ya Mikopo wa NBC, Bw Saleh Mohammed alimuwakilisha Mkurugenzi Mtendaji wa benki hiyo Bw Theobald Sabi kwenye hafla hiyo iliyohudhuriwa pia na wafanyakazi wa benki ya NBC.

Pamoja na ushiriki huo Mhe Abdulla aliishukuru na kuipongeza NBC kwa kuandaa tukio hilo la kiimani, akieleza kuwa ni ishara ya moyo wa kujali na kujenga mahusiano imara na jamii.

Alitoa shukrani za dhati kwa niaba ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kwa kutambua mchango wa NBC katika maendeleo ya visiwa hivyo—kuanzia msaada wa kifedha, ushauri wa kitaalamu, hadi ushiriki wake katika mipango mbalimbali ya kijamii na kiuchumi.

Kushiriki futari kama hii pamoja na wadau mbalimbali wakiwemo wateja wenu ni jambo la heri, hususan katika mwezi huu Mtukufu wa Ramadhani. Ni thamani kubwa kwenu kama waandaaji, kwetu kama walengwa, na mbele ya Mwenyezi Mungu pia… tunawashukuru sana,” alisema.

Aliongeza kuwa NBC imeendelea kujidhihirisha kama taasisi inayojitoa kwa dhati katika juhudi za kiimani na kimaendeleo, jambo lililomfanya kuupa kipaumbele mwaliko huo ili kufikisha shukrani zake binafsi na za serikali.

“Kupitia matukio kama haya, Wazanzibar wengi zaidi wanavutiwa kuwa karibu nanyi, si tu kibiashara bali kwa sababu mmeonesha kuwa uhusiano wenu na wateja ni zaidi ya miamala ya kibenki,” alisisitiza.

Aidha, alibainisha kuwa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar inaendelea kuweka mazingira wezeshi kwa taasisi za fedha ili ziweze kunufaika na ukuaji wa uchumi unaochochewa na miradi ya maendeleo pamoja na sekta muhimu kama utalii, biashara na uvuvi.

Kwa upande wake, Bw. Saleh Mohammed alisema kuwa kuandaa futari katika mikoa mbalimbali, ikiwemo Zanzibar, ni sehemu ya utamaduni wa NBC unaolenga kuimarisha ukaribu na jamii.

Alieleza kuwa mafanikio ya benki hiyo, ikiwemo ongezeko la wateja mikoa mbalimbali pamoja na visiwani Zanzibar, yanatokana na mahusiano mazuri na utoaji wa huduma unaozingatia mahitaji halisi ya wateja, ikiwemo misingi ya kiimani.

Alitolea mfano huduma ya La’ Riba, inayowezesha wateja wenye imani ya Kiislamu kupata huduma za kifedha zinazoendana na misingi ya dini yao.

Sambamba na hilo, alibainisha kuwa NBC imeendelea kuboresha huduma za kidijitali ili kuwapa wateja urahisi zaidi, ikiwemo kufungua akaunti kwa njia ya mtandao, kufanya malipo ya serikali (GEPG), kununua umeme , pamoja na kulipa ankara mbalimbali kwa urahisi.

Tunaendelea kuwaalika wateja wetu kutumia NBC Kiganjani App, NBC Connect, mashine zetu za POS na kadi zetu za malipo ili kufurahia huduma za kibenki zilizo salama, za haraka na za kisasa zaidi,” alisema.

Hafla hiyo ilihitimishwa kwa utoaji wa zawadi kwa wageni waalikwa na kutoa fursa ya kubadilishana mawazo, kuimarisha mtandao wa kibiashara na kijamii, pamoja na kusherehekea kwa pamoja katika mwezi huu mtukufu wa Ramadhani.
Makamu wa Pili wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Mhe. Hemed Suleiman Abdulla (wa pili) akiwaongoza wageni waalikwa kupata futari wakati wa hafla ya futari iliyoandaliwa na benki ya NBC kwa ajili ya wateja wake visiwani Zanzibar. Pamoja nae pia yupo Mkurugenzi wa Idara ya Mikopo wa NBC, Bw Saleh Mohammed. Hafla hiyo ilifanyika jana kwenye hotel ya Madinat Al Bahr, Zanzibar ikihusisha wateja na wadau mbalimbali wa benki hiyo wakiwemo viongozi wa serikali na dini.



Makamu wa Pili wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Mhe. Hemed Suleiman Abdulla (pichani) akizungumza na wageni waalikwa wakati wa hafla ya futari iliyoandaliwa na Benki ya NBC kwa ajili ya wateja wake visiwani Zanzibar. Hafla hiyo ilifanyika jana kwenye hotel ya Madinat Al Bahr, Zanzibar ikihusisha wateja na wadau mbalimbali wa benki hiyo wakiwemo viongozi wa serikali na dini.
Mkurugenzi wa Idara ya Mikopo wa NBC, Bw Saleh Mohammed (pichani) akizungumza na wageni waalikwa wakati wa hafla ya futari iliyoandaliwa na Benki ya NBC kwa ajili ya wateja wake visiwani Zanzibar. Hafla hiyo ilifanyika jana kwenye hotel ya Madinat Al Bahr, Zanzibar ikihusisha wateja na wadau mbalimbali wa benki hiyo wakiwemo viongozi wa serikali na dini.
Makamu wa Pili wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Mhe. Hemed Suleiman Abdulla (katikati) sambamba na wageni wengine waalikwa wakiwa kwenye hafla ya futari iliyoandaliwa na Benki ya NBC kwa ajili ya wateja wake visiwani Zanzibar. Kushoto kwake yupo Naibu Mufti Mkuu wa Zanzibar, Sheikh Mahmoud Mussa Wadi na kulia kwake yupo Mkurugenzi wa Idara ya Mikopo wa NBC, Bw Saleh Mohammed. Hafla hiyo ilifanyika jana kwenye hotel ya Madinat Al Bahr, Zanzibar ikihusisha wateja na wadau mbalimbali wa benki hiyo wakiwemo viongozi wa serikali na dini.
Baadhi ya wageni waalikwa wakipata futari wakati wa hafla ya futari iliyoandaliwa na benki ya NBC kwa ajili ya wateja wake visiwani Zanzibar. Hafla hiyo ilifanyika jana kwenye hotel ya Madinat Al Bahr, Zanzibar ikihusisha wateja na wadau mbalimbali wa benki hiyo wakiwemo viongozi wa serikali na dini.
Makamu wa Pili wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Mhe. Hemed Suleiman Abdulla (katikati) akiwa kwenye picha ya pamoja na baadhi ya maofisa wa benki ya NBC wakiongozwa na Mkurugenzi wa Idara ya Mikopo wa NBC, Bw Saleh Mohammed wakati wa hafla ya futari iliyoandaliwa na Benki ya NBC kwa ajili ya wateja wake visiwani Zanzibar. Kushoto alieketi ni Naibu Mufti Mkuu wa Zanzibar, Sheikh Mahmoud Mussa Wadi. Hafla hiyo ilifanyika jana kwenye hotel ya Madinat Al Bahr, Zanzibar ikihusisha wateja na wadau mbalimbali wa benki hiyo wakiwemo viongozi wa serikali na dini.
Mkurugenzi wa Idara ya Mikopo wa NBC, Bw Saleh Mohammed (katikati walioketi) akiwa kwenye picha ya pamoja na baadhi ya maofisa wa benki ya NBC wakati wa hafla ya futari iliyoandaliwa na benki hiyo kwa ajili ya wateja wake visiwani Zanzibar. Hafla hiyo ilifanyika jana kwenye hotel ya Madinat Al Bahr, Zanzibar ikihusisha wateja na wadau mbalimbali wa benki hiyo wakiwemo viongozi wa serikali na dini.
Share:

Benki ya Absa kuendelea kushiriki mikakati ya kuboresha ustawi na maendeleo endelevu ya watoto, familia na jamii nchini

 

Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Obedi Laiser (kushoto), akimsikiliza Mkurugenzi wa Shirika la World Vision Tanzania, Bw. James Anditi, wakati wa uzinduzi rasmi wa Mkakati wa miaka mitano wa Jubilei (2026–2030) wa shirika hilo jijini Dar es Salaam jana, unaolenga kuboresha ustawi na maendeleo endelevu ya watoto, familia na jamii nchini. Ushiriki wa Benki ya Absa unaakisi dhamira ya benki hiyo kuwa chachu ya mabadiliko chanya kwa kuiwezesha jamii kupitia ushirikiano wenye malengo mahsusi unaopanua fursa, kuimarisha ustahimilivu na kusaidia athari endelevu za kijamii kwa muda mrefu, kwa kuiwezesha Afrika ya kesho, kwa pamoja.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Obedi Laiser, akizungumza wakati wa uzinduzi rasmi wa Mkakati wa miaka mitano wa Jubilei (2026–2030) wa Shirika la World Vision jijini Dar es Salaam jana, unaolenga kuboresha ustawi na maendeleo endelevu ya watoto, familia na jamii nchini. Ushiriki wa Benki ya Absa unaakisi dhamira ya benki hiyo kuwa chachu ya mabadiliko chanya kwa kuiwezesha jamii kupitia ushirikiano wenye malengo mahsusi unaopanua fursa, kuimarisha ustahimilivu na kusaidia athari endelevu za kijamii kwa muda mrefu, kwa kuiwezesha Afrika ya kesho, kwa pamoja.
Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Dkt. Doroth Gwajima (katikati, waliokaa), akiwa katika picha ya pamoja na viongozi waandamizi kutoka World Vision, Benki ya Absa pamoja na wadau wengine wakati wa uzinduzi rasmi wa Mkakati wa Jubilei (2026–2030) wa shirika hilo uliofanyika jana jijini Dar es Salaam jana, unaolenga kuboresha ustawi na maendeleo endelevu ya watoto, familia na jamii nchini. Ushiriki wa Benki ya Absa unaakisi dhamira ya benki hiyo kuwa chachu ya mabadiliko chanya kwa kuiwezesha jamii kupitia ushirikiano wenye malengo mahsusi unaopanua fursa, kuimarisha ustahimilivu na kusaidia athari endelevu za kijamii kwa muda mrefu, kwa kuiwezesha Afrika ya kesho, kwa pamoja.
Share:

LILIAN-FAVOUR MAKAWA

LILIAN-FAVOUR MAKAWA

Popular Posts

Blog Archive

Labels

Blog Archive

Recent Posts

Label Cloud

BIASHARA (305) BURUDANI (4) KIMATAIFA (10) KITAIFA (121) MICHEZO (39) SIASA (3)

Pages