JIONI YA BARAKA FAMILIA YA OYA YASHIRIKI IFTAR NA JAMII

   Taasisi ya Oya Micro-crediti imeandaa futari maalum kwa wateja wake na jamii kwa ujumla tukio lililolenga kuimarisha mshikamano wa kijamii.

Watoto kutoka kituo cha kulelea watoto mayatima kinondoni,wakitabasam kufurahia iftar iliyoandaliwa na taasisi ya  Oya Micro-Credit ikiwa nikurudisha kwa jamii hasa katika mwezi huu mtukufu wa Ramadhani na Kwaresma


Mwezi Mtukufu wa Ramadhan ni wakati wa kutafakari, kushukuru, na kushirikiana na jamii katika kujitoa kwenye mambo mablimbali. Kwetu OYA, tunaamini kuwa mafanikio ya kweli hayapimwi tu kwa ukuaji wa biashara, bali pia kwa mchango chanya tunaoutoa kwa jamii inayotuzunguka.


Oya Micro-crediti tulipata heshima ya kuandaa Iftar dinner maalum iliyowaleta pamoja watumishi wetu, baadhi ya wateja na wageni maalum katika mazingira ya mshikamano na furaha.


Moja ya sehemu iliyogusa mioyo ya wengi ilikuwa uwepo wa watoto wazuri kutoka kituo cha kulelea watoto yatima kilichopo Kinondoni watoto hao walionesha Tabasamu lao lililota furaha kubwa na kutukumbusha maana halisi ya  ya Mwezi Mtukufu wa Ramadhan — huruma, upendo, na kushirikiana.

Haikua tu hafla ya kufuturu pamoja, bali pia ya kuimarisha mahusiano, kujenga mshikamano wa kijamii, na kueneza matumaini matukio kama haya yanatukumbusha kuwa hata matendo madogo ya wema yanaweza kuleta furaha kubwa kwa wengine.

Tunatoa shukrani zetu za dhati kwa kila mmoja aliyeshiriki na kuchangia kufanya siku hii iwe ya kipekee kadri mwezi wa Ramadhan unavyoendelea, OYA itaendelea kujitahidi kushirikiana na jamii na kuendeleza maadili ya umoja, huruma, na kusaidiana.


Kwa niaba ya familia nzima ya OYA, tunawatakia wote Ramadhan yenye baraka na amani. Alisema Mkurugenzi wa OYA Bwana. Alpha Peter



Ramadan Kareem. 🌙

Share:

BENKI YA ABSA TANZANIA YALENGA KUWEZESHA WASICHANA 5,000 KUPATA UJUZI WA AI KUPITIA MPANGO WA ELEVATEHER

Benki ya Absa Tanzania, kwa ushirikiano na Microsoft na Women in Tech, imezindua rasmi Mpango wa ElevateHer AI nchini Tanzania, ambao unalenga kuwawezesha wasichana 5,000 wa Kitanzania kupata ujuzi na cheti cha Akili Mnemba (AI).

Mpango huu ni sehemu ya juhudi pana za kiafrika zinazolenga kutoa mafunzo kwa wanawake 50,000 barani Afrika ili waweze kushiriki kikamilifu katika uchumi wa kidijitali unaokua kwa kasi.

Kupitia mpango wa ElevateHer, washiriki watapata fursa ya kujifunza mtandaoni kwa njia ya kujitegemea bila malipo, ambapo watapata maarifa ya msingi ya AI, matumizi ya AI katika biashara, na maendeleo ya taaluma katika mazingira ya kazi yanayoendeshwa na teknolojia ya AI. Mpango huu utakuwa wazi kwa mwaka mzima.

Ofisa Mkuu wa Uendeshaji wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Oscar Mwamfwagasi, amesema mpango huu unaakisi dhamira ya benki kuhakikisha wasichana wanapata ujuzi wa kidijitali unaohitajika kwa siku za usoni. “Artificial intelligence inabadilisha jinsi uchumi unavyofanya kazi na jinsi watu wanavyofanya kazi.

Kupitia Mpango wa ElevateHer AI, Benki ya Absa Tanzania inalenga kuhakikisha wasichana wa Kitanzania wanapata ujuzi na kujiamini kushiriki kikamilifu katika uchumi wa kidijitali na kuchangia ubunifu na ukuaji.

Juhudi hii inaendeleza michango ya Absa Tanzania ya kukuza ushiriki wa wanawake katika teknolojia, ikiwa ni pamoja na GirlCode Hackathon ya mwaka jana, ambapo wasichana wabunifu walikusanyika ili kutengeneza suluhisho za kiteknolojia.

Mpango wa ElevateHer unatoa njia tatu za kujifunza: AI kwa Wote, AI kwa Biashara, na AI kwa Ukuaji wa Kitaaluma, na kutoa fursa kwa washiriki kujenga maarifa ya vitendo na kutumia zana za AI katika safari zao za kitaaluma au za ujasiriamali.

Bi. Tiara Pathon, Mkurugenzi wa Ujuzi wa AI katika Microsoft Elevate, Microsoft Afrika Kusini, amesema upatikanaji wa ujuzi wa kidijitali kwa kila mmoja ni muhimu kwa ushiriki wa Afrika katika uchumi wa AI duniani. “Ukuaji wa uchumi jumuishi katika zama za AI unahitaji kujenga ujuzi kwa wingi katika masoko yanayokua. Kwa Afrika, hii inamaanisha kuwekeza kwa makusudi katika ujuzi wa kidijitali na AI kwa wanawake. Kupitia ushirikiano wetu na Absa na Women in Tech, mpango wa ElevateHer unawawezesha wanawake barani kote kupata ujuzi wa vitendo unaohitajika kazini na kuimarisha nafasi ya Afrika katika ajira za baadaye.

Mpango huu pia unasaidiwa na Women in Tech Global, shirika linalojitolea kuwawezesha wanawake na wasichana milioni tano katika Sayansi, Teknolojia, Uhandisi, na Hisabati (STEM) kufikia mwaka 2030.

Wanawake wanaopenda kushiriki wanaweza kujisajili mtandaoni kupitia: https://elevateher-in-africa.org/⁠
Share:

ACI FMA Tanzania yathibitisha kuunga mkono maendeleo ya masoko ya fedha nchini

 

Ofisa Mtendaji Mkuu wa Soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE), Bw. Peter Nalitolela (kulia), Rais wa ACI FMA Global Bw. Rui Correia, na Rais wa ACI FMA Tanzania Bw. Farid Yahya Ally wakichukua chakula cha futari katika hafla iliyoandaliwa na ACI FMA Tanzania jijini Dar es Salaam jana. Hafla hiyo iliwakutanisha wadau wa masoko ya fedha, watunga sera na wadhibiti ili kuimarisha ushirikiano na kukuza mazingira imara ya masoko ya fedha nchini.

ACI FMA Tanzania imethibitisha tena dhamira yake ya kuunga mkono ukuaji endelevu wa masoko ya fedha ya Tanzania na kuchangia kwa maana katika maendeleo endelevu ya uchumi wa taifa.

Hayo yalibainishwa na Rais wa chama hicho, Bw. Farid Yahya Ally, wakati wa hafla ya futari iliyofanyika Dar es Salaam mwishoni mwa wiki. Hafla hiyo ilijumuisha mjadala wa jopo kuhusu maendeleo na changamoto zinazoikabili sekta ya masoko ya fedha nchini Tanzania na iliwakutanisha wadau wa soko, watunga sera na wadhibiti wa sekta hiyo.

Kupitia ushirikiano endelevu na wadhibiti, watunga sera pamoja na wadau wa sekta, chama kitaendelea kuunga mkono mipango inayolingana na malengo ya muda mrefu ya maendeleo ya Tanzania, ikiwemo azma ya Dira 2050 ambayo inalenga kujenga uchumi wa dola trilioni moja,” alisema Bw. Ally.

Akihutubia wawakilishi mashuhuri kutoka Benki Kuu ya Tanzania, Soko la Hisa la Dar es Salaam, pamoja na Wakuu wa Masoko ya Kimataifa kutoka taasisi mbalimbali za kifedha, Bw. Ally alibainisha kuwa kama chombo cha kitaaluma kinachowakilisha wataalamu wa masoko ya fedha, ACI FMA Tanzania inatambua jukumu lake muhimu katika kuimarisha maendeleo na uadilifu wa masoko ya fedha nchini.

Kuimarisha ushirikiano na watunga sera pamoja na wadhibiti ni sehemu muhimu ya dhamira yetu ya kukuza kanuni bora za uendeshaji wa soko na kuhakikisha Tanzania inaendelea kuwa na mazingira rafiki kwa wawekezaji wa ndani na wa kimataifa,” alisema.

Hafla ya futari ilikuwa jukwaa muhimu la majadiliano na ushirikiano kati ya washiriki wa soko, watunga sera na wadhibiti. Majadiliano yalilenga kutafuta njia za kuziba mapengo ya kitaasisi yaliyopo na kuimarisha ushirikiano katika kujenga mazingira imara na yenye ustahimilivu kwa masoko ya fedha.

Wakati wa majadiliano hayo, washiriki walibainisha changamoto kadhaa zinazoathiri sekta ya masoko ya fedha, ikiwemo ukosefu wa utofauti wa bidhaa za kifedha, taratibu ngumu za udhibiti kwa washiriki wapya wa soko, pamoja na utegemezi mkubwa wa ufadhili unaotolewa na taasisi za kifedha.

Akijibu hoja hizo, Mtendaji Mkuu wa Soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE), Bw. Peter Nalitolela, alikiri kuwa ingawa masoko ya mitaji nchini Tanzania yanaendelea kukua, uelewa wa wawekezaji wadogo kuhusu soko hilo bado ni mdogo.

Alisema kuwa licha ya idadi ya akaunti za Central Depository System (CDS) kuwa ndogo kwa kiasi, hivi karibuni soko limeanza kushuhudia ongezeko la wawekezaji wapya wanaoingia kwenye soko la hisa.

Ingawa wawekezaji wengi zaidi wanaonesha nia ya kuingia sokoni, changamoto kadhaa bado zinaendelea kuwepo, ikiwemo ukosefu wa utofauti wa bidhaa za kifedha na maandalizi ya soko kukidhi ongezeko la ushiriki wa wawekezaji,” alisema.

Bw. Nalitolela pia alibainisha kuwa mauzo ya awali ya hisa kwa umma (IPOs) yamepungua si Tanzania pekee bali pia kimataifa, hali inayoakisi mwenendo mpana wa masoko duniani.

Hata hivyo, alisisitiza kuwa Tanzania inaendelea kubadilika taratibu kutoka katika mfumo wa uchumi unaoongozwa zaidi na serikali kuelekea uchumi unaochochewa zaidi na sekta binafsi, hatua ambayo tayari imeanza kuleta mwamko chanya katika masoko ya mitaji na hisa.

Wakati huohuo, Rais wa ACI FMA Duniani, Bw. Rui Correia, alitangaza kuwa chama hicho kitaanzisha mpango wa ufadhili wa masomo kwa wanawake barani Afrika ili kusaidia wataalamu wanawake katika sekta ya masoko ya fedha.

Hili ni jambo tunalotaka kufanya hasa tunapokaribia Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani. Kwa mwaka huu tutazingatia ufadhili wa masomo kwa wanawake barani Afrika, na mwaka ujao tutaanzisha mpango mwingine,” alisema Bw. Correia.

Alisisitiza kuwa chama hicho kinathamini sana ushirikishwaji wa maarifa na maendeleo ya kitaaluma ndani ya jamii ya wataalamu wa masoko ya fedha.

Kwetu sisi, elimu si kupata vyeti pekee. Ni kuhusu kubadilishana utaalamu, maarifa na uzoefu katika nyanja mbalimbali za masoko ya fedha,” aliongeza.

ACI FMA Tanzania ni shirika lisilo la kiserikali linalofanya kazi chini ya mwavuli wa ACI FMA Global. Chama hicho kinakuza kanuni bora za uendeshaji wa soko kwa kuwapatia wataalamu wa masoko ya fedha mafunzo, fursa za kushiriki katika shughuli za kitaaluma pamoja na vyeti vinavyotambulika kimataifa.
Rais wa ACI FMA Tanzania, Bw. Farid Yahya Ally, akizungumza na washiriki wakati wa hafla ya futari, iliyofanyika Dar es Salaam jana. Hafla hiyo iliwakutanisha wadau wa masoko ya fedha, watunga sera na wadhibiti ili kuimarisha ushirikiano na kukuza mazingira imara ya masoko ya fedha nchini.
Rais wa ACI FMA Tanzania Bw. Farid Yahya Ally (kulia) akibadilishana mawazo na Rais wa ACI FMA Duniani, Bw. Rui Correia (kushoto) pamoja na Mchambuzi Mwandamizi wa Masuala ya Fedha kutoka Benki Kuu ya Tanzania, Bw. Stanslaus Shenyali, wakati wa hafla ya futari, iliyoandaliwa na ACI FMA Tanzania Dar es Salaam jana.
Ofisa Mtendaj Mkuu wa Soko la Hisa la Dar es Salaam Bw. Peter Nalitolela (kulia) akizungumza wakati wa mjadala uliofanyika pamoja futari iliyoandaliwa na ACI FMA Tanzania jijini Dar es Salaam jana. Hafla hiyo iliwakutanisha wadau wa masoko ya fedha, watunga sera na wadhibiti ili kuimarisha ushirikiano na kukuza mazingira imara ya masoko ya fedha nchini.
Baadhi ya wageni waalikwa wakiwa katika hafla ya futari iliyoandaliwa na ACI FMA Tanzania, jijini Dar es Salaam jana. Hafla hiyo iliwakutanisha wadau wa masoko ya fedha, watunga sera na wadhibiti ili kuimarisha ushirikiano na kukuza mazingira imara ya masoko ya fedha nchini.
Rais wa ACI FMA Tanzania Bw. Farid Yahya Ally (wa nane kutoka kushoto), Rais wa ACI FMA Duniani, Bw. Rui Correia (wa sita kutoka kushoto), maofisa wa ACI na wageni wengine waalikwa wakipiga picha ya pamoja baada ya hafla ya futari iliyofanyika Dar es Salaam jana. Hafla hiyo iliwakutanisha wadau wa masoko ya fedha, watunga sera na wadhibiti ili kuimarisha ushirikiano na kukuza mazingira imara ya masoko ya fedha nchini.
Share:

BENKI YA ABSA TANZANIA YATAMBULIWA KWA DHAMIRA YAKE THABITI YA KUWAWEZESHA WANAWAKE NCHINI

  

Mkurugenzi Mtendaji wa Benkiy a Absa Tanzania, Bw. Obedi Laiser (wa sita kushoto), akionesha tuzo ya ‘Rising Women’ mara baada ya kukabidhiwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Mipango na Uwekezaji, Prof. Kitila Mkumbo (wa tano kushoto), jijini Dar es Salaam jana. Benki hiyo ilitambuliwa kwa dhamira yake thabiti ya kuwawezesha wanawake, kuendeleza ujumuishaji wa kifedha na kuunda fursa zenye maana kwa uwakilishi wa wanawake katika nafasi za uongozi.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Mipango na Uwekezaji, Prof. Kitila Mkumbo, akikabidhi tuzo ya ‘Rising Women’ kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Bww. Obedi Laiser (wa pili kulia), jijini Dar es Salaam jana. Benki hiyo ilitambuliwa kwa dhamira yake thabiti ya kuwawezesha wanawake, kuendeleza ujumuishaji wa kifedha na kuunda fursa zenye maana kwa uwakilishi wa wanawake katika nafasi za uongozi.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Mipango na Uwekezaji, Prof. Kitila Mkumbo, akikabidhi tuzo ya shukrani kwa Meneja Huduma za Jamii na Mtukio wa Benki ya Absa Tanzania, Bi. Abigail Lukuvi (kulia), kwa kutambua mchango wa benki hiyo katika Mpango wa Rising Women. Hafla hiyo ilifanyika jijini Dar es Salaam jana. Benki hiyo ilitambuliwa kwa dhamira yake thabiti ya kuwawezesha wanawake, kuendeleza ujumuishaji wa kifedha na kuunda fursa zenye maana kwa uwakilishi wa wanawake katika nafasi za uongozi.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Obedi Laiser (wa nne kushoto), na Meneja Huduma za Jamii na Matukio wa wa benki hiyo, Bi. Abigail Lukuvi (wa tatu kulia), pamoja na baadhi ya wafanyakazi wa Absa, wakipozi na tuzo za utambuzi za ‘Rising Women’ jijini Dar es Salaam jana. Benki hiyo ilitambuliwa kwa dhamira yake thabiti ya kuwawezesha wanawake, kuendeleza ujumuishaji wa kifedha na kuunda fursa zenye maana kwa uwakilishi wa wanawake katika nafasi za uongozi.
Share:

AKIBA COMMERCIAL BANK ENGAGES WOMEN ENTREPRENEURS AHEAD OF INTERNATIONAL WOMEN’S DAY

    

Akiba Commercial Bank’s Chief Commercial Officer, Wezi Mwazani speaks during the engagement.

In celebration of International Women’s Day, Akiba Commercial Bank Plc hosted a special engagement event in Dar es Salaam on 6 March 2026, bringing together female entrepreneurs served by the bank from various branches across the city.

The event formed part of the bank’s Lady Entrepreneur Campaign, an initiative aimed at strengthening relationships with women customers while promoting financial empowerment and business growth.

Supporting Women in Business

Speaking during the engagement, the Bank’s Chief Commercial Officer, Wezi Mwazani, highlighted the important role women play in economic development and community transformation.


She emphasized that women entrepreneurs remain a key focus for the bank as it continues to expand financial inclusion and support the growth of small and medium-sized enterprises (SMEs).

Mwazani noted that the bank is committed to providing tailored financial solutions designed to meet the needs of women at different stages of their entrepreneurial journey.


Women entrepreneurs continue to demonstrate resilience and innovation in business. At Akiba Commercial Bank, we are committed to supporting women with financial solutions, knowledge, and opportunities that help them grow their businesses and improve their livelihoods,” she said.

Entrepreneurs Share Their Experiences

During the engagement, customers expressed appreciation for the support extended by the bank through its financial services and advisory initiatives.

Participants noted that access to banking services and financing has enabled them to:

  • Strengthen and expand their businesses
  • Increase household income
  • Improve their standards of living

Some entrepreneurs also highlighted that the support received has helped them contribute more actively to community development and job creation, demonstrating the wider impact of empowering women in business.

Strengthening Customer Relationships

The engagement in Dar es Salaam brought together female customers from several branches across the city, reflecting the bank’s commitment to deepening relationships with its customers while gaining insights into their evolving financial needs.

The bank also indicated that the event marks the beginning of broader outreach activities under the Lady Entrepreneur Campaign. Similar engagements are expected to be extended to customers in other regions where the bank operates.

Expanding Opportunities for Women Entrepreneurs

Through these continued engagements, Akiba Commercial Bank Plc aims to expand opportunities for women entrepreneurs by:

  • Promoting financial literacy and knowledge
  • Improving access to financial services
  • Supporting business growth and sustainability

The bank has also encouraged women entrepreneurs and business groups to visit its branches to explore the available banking solutions and take part in the ongoing Lady Entrepreneur Campaign as it expands to other regions across the country.











Share:

MKURUGENZI MTENDAJI WA BENKI YA ABSA TANZANIA NA UJUMBE WAKE WAMTEMBELEA MKUU WA MKOA WA MBEYA OFISINI KWAKE

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Mhe. Beno Malisa (kushoto), akimkaribisha Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Obedi Laiser, alipofika kumtembelea akiwa na ujumbe wake, ofisini kwake, mjini Mbeya jana. Bw. Laiser na ujumbe wake wapo mjini Mbeya kwa ziara ya kikazi.
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Mhe. Beno Malisa (kushoto), akisalimiana na Mkuu wa Uendeshaji wa Matawi wa Benki ya Absa Tanzania, Bi. Mwilongo Msungu, wakati Mkurugenzi Mtendaji wa benki hiyo, Bw. Obedi Laiser (Katikati), na ujumbe wake, ukimtembela mkuu wa mkoa huyo, ofisini kwake, mjini Mbeya jana. Bw. Laiser na ujumbe huo wapo mjini Mbeya kwa ziara ya kikazi.
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Mhe. Beno Malisa (kushoto), akiwa na baadhi ya wakurugenzi wa Benki ya Absa Tanzania, wakati wa ziara ya Mkurugenzi Mtendaji wa benki hiyo, Bw. Obedi Laiser (hayupo pichani), na ujumbe wake, walipomtembelea mkuu wa mkoa huyo, ofisini kwake, mjini Mbeya jana. Bw. Laiser na ujumbe huo wapo mjini Mbeya kwa ziara ya kibiashara. Katikati ni Mkurugenzi wa Wateja Binafsi, Bi. Ndabu Swere na Mkuu wa Uendeshaji wa Matawi, Bi. Mwilongo Msungu.
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Mhe. Beno Malisa (kulia), akiagana na Mkuu wa Mikakati na Data wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. John Mosha, wakati yeye, Mkurugenzi Mtendaji wa benki hiyo, Bw. Obedi Laiser pamoja na maofisa wengine wa benki hiyo, walipomtembelea mkuu wa mkoa huyo, ofisini kwake, mjini Mbeya jana. Bw. Laiser na ujumbe huo wapo mjini Mbeya kwa ziara ya kikazi.
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Mhe. Beno Malisa (kulia), akiagana na Meneja wa Benki ya Absa mkoani humo, Bw. Alto Hagamu, na Mkuu wa Kitengo cha Biashara wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Melvin Saprapasen (kushoto), wakati wao, Mkurugenzi Mtendaji wa benki hiyo, Bw. Obedi Laiser (hayupo pichani), pamoja na maofisa wengine wa benki hiyo, walipomtembelea mkuu wa mkoa huyo, ofisini kwake, mjini Mbeya jana. Bw. Laiser na ujumbe huo wapo mjini Mbeya kwa ziara ya kikazi.
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Mhe. Beno Malisa (wa sita kushoto), akipozi kwa picha ya kumbukumbu na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Obedi Laiser (kulia kwake), mara baada ya mkurugenzi huyo pamoja na ujumbe wake kumtembelea ofisini kwake mjini Mbeya jana wakiwa mkoani humo kwa ziara ya kikazi.
Share:

BENKI YA ABSA TANZANIA YATHIBITISHA DHAMIRA YA KUENDELEZA UWEZESHAJI WA WANAWAKE KIUCHUMI KAMA NGUZO YA UKUAJI WA TAIFA

Benki ya Absa Tanzania imethibitisha upya dhamira yake ya kuendeleza uwezeshaji wa wanawake kiuchumi, ikisisitiza kuwa ujumuishaji si tendo la hisani la taasisi bali ni mkakati muhimu wa kitaifa kwa ukuaji endelevu wa uchumi.

Akizungumza na vyombo vya habari jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki hiyo, Obedi Laiser, alieleza kuwa kuwawezesha wanawake ni msingi wa ushindani wa muda mrefu wa uchumi wa Tanzania.

Uwezeshaji wa wanawake si jambo la hiari katika ukuaji wa uchumi. Ni hitaji la lazima kwa ukuaji,” alisema Bw. Laiser. “Kuwaacha nje karibu nusu ya rasilimali watu wa taifa kushiriki kikamilifu katika uchumi kunasababisha hasara inayoonekana yenye tija.

Alibainisha kuwa katika Absa, dhana ya ujumuishaji imejengeka ndani ya mfumo wa uendeshaji wa benki hiyo, ikilenga ubunifu wa bidhaa, mifumo ya utoaji mikopo, maendeleo ya uongozi pamoja na ushirikiano wa kimkakati.

Wanawake daima wameonesha uwezo na uthabiti. Nguvu ilikuwepo siku zote. Kilichokosekana mara nyingi ni fursa, fursa ya kupata mitaji, mitandao na mifumo rasmi,” alisema. “Tunapowawezesha wanawake, hatuchagui tu kundi fulani. Tunachagua mustakabali wa Tanzania.

Mfano halisi wa dhamira hiyo ni akaunti ya She Business Account, suluhisho maalum lililobuniwa kushughulikia vikwazo vinavyowazuia mara nyingi wanawake wajasiriamali kuingia katika mfumo rasmi wa benki. Bidhaa hiyo inapunguza gharama za uendeshaji wa akaunti huku ikihamasisha ujenzi wa historia ya miamala inayoongeza sifa za kustahili mikopo.

Kutambua kuwa masharti ya dhamana na hali ya kutokuwa rasmi kwa baadhi ya biashara hupunguza upatikanaji wa fedha, benki hiyo pia imeimarisha ushirikiano na taasisi za fedha ndogo. Kupitia mfumo huu wa ufadhili wa ngazi mbalimbali, Absa hutoa mitaji kwa wakopeshaji waliobobea ambao huwafikishia wanawake wajasiriamali katika ngazi za msingi.

Bw. Laiser pia alitofautiana na mtazamo kwamba wanawake ni wakopaji wenye hatari kubwa zaidi. “Dhana kwamba wanawake ni wakopaji hatarishi zaidi haiendani na takwimu za utendaji. Biashara zinazoongozwa na wanawake mara nyingi huonesha nidhamu kubwa ya marejesho ya mikopo na mwenendo endelevu wa kuwekeza tena.

Mbali na suluhisho za kifedha, Absa inaweka ujumuishaji katika misingi ya taasisi kupitia mipango ya kukuza uongozi. Bw. Laiser ni mdhamini wa programu ya ndani ya ulezi inayojulikana kama “ElevateHer,” inayowawezesha mameneja wanawake wa ngazi ya kati kujenga uwepo wa kiuongozi, kuimarisha ushiriki katika vikao vya bodi, na kuongeza mwonekano wa kimkakati.

Benki hiyo pia huwezesha uhusiano wa ulezi kati ya wakurugenzi wanawake waandamizi na viongozi chipukizi, hatua inayokuza mwendelezo wa uongozi na uhamishaji wa maarifa. Dhamira hii imejikita katika madhumuni ya taasisi ya Absa, ‘Kuiwezesha Afrika ya Kesho Pamoja, hatua moja baada ya nyingine’, na ahadi yake ya chapa, ‘Stori yako ina thamani’.

Madhumuni yetu yanaakisi imani kwamba ukuaji endelevu hupatikana kwa kufungua uwezo wa mtu mmoja mmoja na wa pamoja. ‘Stori yako ina thamani’ inamaanisha kila mjasiriamali, kila kiongozi na kila ndoto inastahili kutambuliwa, kuungwa mkono na kupewa fursa,” alisema Bw. Laiser.
Aidha, Bw. Laiser alionya kuwa kupunguza kasi ya juhudi za makusudi za uwezeshaji kutaleta gharama zinazoonekana, ikiwemo kudhoofika kwa uthabiti wa kaya, kupungua kwa utofauti wa uongozi na kushuka kwa ushindani wa taifa.

Katika mazingira ya sasa ya kimataifa, ujumuishaji si suala la pembeni tena. Ni kiini cha uimara wa muda mrefu wa mizania ya kifedha na kasi ya uchumi wa taifa,” alisema.

Kwa Absa Bank Tanzania, uwezeshaji wa wanawake si kampeni ya msimu bali ni uwekezaji wa kimuundo, unaounganisha mafanikio ya kibiashara na maendeleo ya kijamii, na kuiweka benki hiyo kama kichocheo cha mageuzi jumuishi ya uchumi.
Share:

LILIAN-FAVOUR MAKAWA

LILIAN-FAVOUR MAKAWA

Popular Posts

Blog Archive

Labels

Blog Archive

Recent Posts

Label Cloud

BIASHARA (307) BURUDANI (4) KIMATAIFA (10) KITAIFA (121) MICHEZO (39) SIASA (3)

Pages