BENKI YA ABSA YAUNGANA NA TPSF KUWANOA WAJASIRIAMALI WANAWAKE

Meneja Miradi wa Benki ya Absa, Bi. Munira Chambuso akizungumza katika semina iliyoandaliwa na benki hiyo kwa kushirikiana na Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania (TPSF) kwa wanawake wajasiriamali wadogo na wa kati, ikihuhusu elimu ya fedha na usimamizi wa uwekezaji, jijini Dar es Salaam jana.

DAR ES SALAAM | Wanawake wafanyabiashara kutoka sekta mbalimbali nchini wamehimizwa kuendelea kujengewa uwezo wa elimu ya fedha ili kuwawezesha kufanya maamuzi sahihi ya kifedha, kukuza biashara zao na kuongeza mchango wao katika maendeleo ya uchumi wa taifa.

Wito huo umetolewa na Meneja wa Huduma za Jamii na Matukio wa Benki ya Absa Tanzania, Bi. Abigail Lukuvi, wakati wa mafunzo ya elimu ya fedha yaliyoandaliwa kwa ushirikiano kati ya Benki ya Absa Tanzania na Shirikisho la Sekta Binafsi Tanzania (TPSF).

Akizungumza katika mafunzo hayo, Bi. Lukuvi amesema mpango huo ulianza mwaka jana kama sehemu ya ajenda ya uwajibikaji kwa jamii ya benki hiyo, inayolenga kuwawezesha wananchi, hususan wanawake wajasiriamali, kupata maarifa ya kifedha yatakayowasaidia kuwekeza kwa ufanisi na kuimarisha biashara zao.

Amesema mafunzo hayo yamewakutanisha wanawake wamiliki wa biashara kutoka sekta mbalimbali kwa lengo la kuwapa elimu kuhusu usimamizi wa fedha, uwekezaji na mikakati ya kuongeza mapato pamoja na kukuza biashara zao kwa njia endelevu.

Tunafurahi kuona wanawake wengi wakishiriki mafunzo haya. Tunaamini elimu ya fedha ni nyenzo muhimu katika kuwajengea uwezo wa kufikia mafanikio ya kiuchumi na kuimarisha ustawi wa biashara zao,” amesema Bi. Lukuvi.

Aidha, ameishukuru TPSF kwa ushirikiano wake katika kufanikisha mafunzo hayo na kubainisha kuwa ushirikiano huo utaendelea ili kuwafikia wanawake wengi zaidi na kuwapa fursa ya kupata elimu ya fedha na uwekezaji.

Mafunzo hayo yamewaleta pamoja wanawake kutoka sekta mbalimbali ikiwemo biashara, viwanda vidogo, madini, utalii, sekta za ubunifu na ukandarasi, wakiwakilisha wanachama wa TPSF.

Katika mafunzo hayo, wataalamu wa Absa walitoa elimu kuhusu usimamizi wa fedha ikijumuisha masuala ya bajeti, akiba na uwekezaji kwa lengo la kusaidia wajasiriamali kukuza biashara zao na kuongeza ufanisi katika shughuli zao za kiuchumi.

Kwa upande wake, mwakilishi wa TPSF, Kinanasi Seif, amesema shirikisho hilo litaendelea kushirikiana na wadau mbalimbali katika kuwawezesha wanawake wajasiriamali kupitia programu za mafunzo na elimu zinazolenga kukuza biashara na kuimarisha uchumi wao.

Amesema TPSF imekuwa ikitekeleza programu mbalimbali za kuwawezesha wanawake katika nyanja tofauti za biashara huku ikitambua mchango mkubwa wa wanawake katika maendeleo ya sekta binafsi na uchumi wa taifa kwa ujumla.

Tumefanikiwa kuwaleta pamoja wanawake wajasiriamali kutoka vyama mbalimbali ili wapate mafunzo ya elimu ya fedha na uwekezaji kutoka Benki ya Absa. Tunaamini maarifa haya yatawasaidia kufanya maamuzi sahihi ya kifedha na kukuza biashara zao,” amesema Seif.

Ameongeza kuwa ushirikiano kati ya TPSF na Benki ya Absa ni hatua muhimu katika kuhakikisha wanawake wanapata fursa za kujengewa uwezo na kufikia maendeleo endelevu katika shughuli zao za kiuchumi.

Wakati huo huo, wataalamu kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) walitoa elimu kuhusu utii wa kodi kwa biashara ndogo na za kati (SMEs), wakisisitiza umuhimu wa kuzingatia sheria za kodi katika kujenga biashara imara na endelevu.

Akizungumza katika semina hiyo, Afisa wa TRA, Zephaniah Usange Jamange, amesema kuwa pamoja na walipakodi kutekeleza wajibu wao wa kulipa kodi, ni muhimu pia kufahamu haki zao wanazostahili kupata kutoka kwa mamlaka hiyo.

Amesema miongoni mwa haki hizo ni usiri wa taarifa za kikodi, ambapo taarifa zote zinazowasilishwa na mlipakodi zinapaswa kubaki siri na haziwezi kutolewa kwa watu wasiohusika. Aidha, walipakodi wote wanapaswa kuhudumiwa kwa usawa bila upendeleo wowote.

Walipakodi pia wana haki ya kupinga maamuzi yanayotolewa na maafisa wa kodi pale wanapoona hawajaridhika nayo. Maamuzi ya awali si ya mwisho, hivyo kuna fursa ya kukata rufaa kwa kufuata taratibu zilizowekwa,” amesema Jamange.

Kwa upande wa wajibu, TRA imewakumbusha wafanyabiashara kuhakikisha wanajisajili kwa TIN ndani ya siku tano tangu waanze biashara. Pia wafanyabiashara wanaofikia mauzo yanayostahili kwa mujibu wa sheria wanapaswa kutumia mashine za kutolea risiti za kielektroniki (EFD) na kujisajili kwa Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) pale inapohitajika.

Mafunzo hayo ni sehemu ya juhudi za pamoja za kukuza ushiriki wa wanawake katika shughuli za kiuchumi kwa kuwapatia ujuzi wa usimamizi wa fedha, uwekezaji, utii wa kodi na uendeshaji bora wa biashara, hatua inayotarajiwa kuchochea ukuaji wa biashara zao na maendeleo ya uchumi wa taifa.
Meneja wa Huduma za Jamii na Matukio wa Benki ya Absa Tanzania, Bi. Abigail Lukuvi (wa pili kutoka kushoto), akizungumza na baadhi ya washiriki, katika semina iliyoandaliwa na benki hiyo kwa kushirikiana na Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania (TPSF) kwa wanawake wajasiriamali wadogo na wa kati ikihusu elimu ya fedha na usimamizi wa uwekezaji, jijini Dar es Salaam jana.
Mkurugenzi wa Wanachama wa Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania (TPSF), Bi. Kinanasy Seif akizngumza katika semina iliyoandaliwa na Benki ya Absa Tanzania kwa kushirikiana na taasisi hiyo kwa wanawake wajasiriamali wadogo na wa kati, ikihusu elimu ya fedha na usimamizi wa uwekezaji, jijini Dar es Salaam jana.
Meneja Bidhaa Kitengo cha Biashara wa Benki ya Absa Tanzania, Bi. Devroda Kagusa, akizungumza katika semina iliyoandaliwa na benki hiyo kwa kushirikiana na Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania (TPSF), kwa wanawake wajasiriamali wadogo na wa kati, Ikihusu elimu ya fedha na usimamizi wa uwekezaji, jijini Dar es Salaam jana.
Ofisa Elimu kwa Mlipa Kodi na Mawasiliano wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Bw. Zephania Mange, akitoa elimu kuhusu wajibu wa mlipa kodi katika semina iliyoandaliwa na Benki ya Absa Tanzania kwa kushirikiana na Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania (TPSF), kwa wanawake wajasiriamali wadogo na wa kati, Ikihusu elimu ya fedha na usimamizi wa uwekezaji, jijini Dar es Salaam jana.
Wawakilishi kutoka Benki ya Absa na TPSF, wakipiga picha ya kumbukumbu pamoja na washiriki wa semina hiyo pamoja na wawezeshaji wengine, mara baada ya kumalizika kwa semina hiyo, jijini Dar es Salaam jana.
Share:

BENKI YA ABSA TANZANIA YAENDELEZA HUDUMA ZA AFYA YA MAMA NA MTOTO KUPITIA UTOAJI WA VIFAA VYA HOSPITALI

  

Meneja wa Huduma za Jamii na Matuko wa Benki ya Absa Tanzania, Bi. Abigail Lukuvi (wa pili kutoka kushoto), akikabidhi vifaa vya hospitali kwa Muuguzi Kiongozi wa Hospitali ya Mnazi Mmoja, Bi. Shufaa Kaniki (kulia), katika hafla iliyofanyika jijini Dar es Salaam jana. Kushoto ni Makamu wa Rais wa The Runners Club, Bw. Godfrey Mwangungulu, pamoja na baadhi ya wafanyakazi wa hospitali. Utoaji huu wa vifaa, wenye lengo la kuimarisha huduma za afya ya mama na mtoto, umefuatia mafanikio ya mbio za Absa Dar City Marathon zilizofanyika tarehe 3 Mei 2026 jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya wafanyakazi wa Hospitali ya Mnazi Mmoja wakionesha vifaa vipya vya hospitali walivyokabidhiwa na Meneja Huduma za Jamii na Matukio wa Benki ya Absa Tanzania, Bi. Abigail Lukuvi (kushoto), katika hafla iliyofanyika jijini Dar es Salaam jana. Utoaji huu, wenye dhamira ya kuimarisha huduma za afya ya mama na mtoto, umewezekana kufuatia mafanikio ya mbio za Absa Dar City Marathon zilizofanyika tarehe 3 Mei 2026, jijini Dar es Salaam.
Makamu wa Rais wa The Runners Club, Bw. Godfrey Mwangungulu, akitoa hotuba yake wakati wa hafla ya makabidhiano ya vifaa vya hospitali vilivyotolewa na Benki ya Absa Tanzania jijini Dar es Salaam jana. Mchango huu Kutoka Benki ya Absa, wenye lengo la kuunga mkono huduma za afya ya mama na mtoto, umewezekana kufuatia mafanikio ya mbio za Absa Dar City Marathon zilizofanyika tarehe 3 Mei 2026 jijini Dar es Salaam.
Muuguzi Kiongozi wa Hospitali ya Mnazi Mmoja, Bi. Shufaa Kaniki, akitoa shukrani zake baada ya kupokea msaada wa vifaa vya hospitali kutoka kwa Meneja Huduma za Jamii na Matukio wa Benki ya Absa Tanzania, Bi. Abigail Lukuvi (kushoto), katika hafla iliyofanyika jijini Dar es Salaam jana. Utoaji huu, unaolenga kuimarisha huduma za afya ya mama na mtoto, umefuatia mafanikio ya mbio za Absa Dar City Marathon zilizofanyika tarehe 3 Mei 2026 jijini Dar es Salaam.
Share:

KIKUNDI CHA DIAMOND DIVAS CHAWATAKA WANAWAKE KUCHANGAMKIA FURSA ZA UWEKEZAJI

Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Dar es Salaam na Mwenyekiti wa Kikundi cha Vicoba cha Diamond Divas Group, Mhe. Janeth Elias Mahawanga, akizungumza katika semina iliyoandaliwa na kikundi hicho ikihusu elimu ya kifedha na jinsi ya kuwekeza katika mifuko ya uwekezaji iliyofanyika jijini Dar es Salaam jana.

WITO umetolewa kwa wanawake nchini kuchangamkia fursa za uwekezaji katika mifuko mbalimbali ya uwekezaji, Ili kufikia Dira ya Maendeleo ya Taifa 2050 na kuliwezesha Taifa kuwa na uchumi shirikishi wa viwanda unaowezeshwa na ushirikishwaji mpana wa huduma za kifedha.

Wito huo umetolewa na Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Dar es Salaam na Mwenyekiti wa Kikundi cha Wanawake cha Huduma ndogo za kifedha cha Diamond Divas, Mhe. Janeth Elias Mahawanga wakati wa semina kuhusu Uwekezaji wa wanawake katika mifuko ya uwekezaji akisema uwekezaji huo utawasaidia kuongeza Mitaji ya biashara zao hivyo kujiinua kiuchumi.

Tunapozungumzia Dira ya Maendeleo ya Taifa 2050 kwa upande wa wanawake, Dira inasema Uchumi wa wananchi mmoja mmoja unakwenda kuongezeka, na Uchumi wa Taifa, lakini pia viwanda vidogo vidogo, Rais Samia Suluhu Hassan alikuwa na maono ya kuwa na dira ya Taifa, utekeleza wa dira unatutegemea sisi wananchi, sisi wanawake tunataka kuingia moja kwa moja katika utekelezaji wa dira, tunataka kuingia katika uchumi wa viwanda tukawe wawekezaji katika Taifa letu."

Kupitia semina kama hizi, ili kuwaandaa wanawake kushiriki kikamiifu, ni lazima kuwajengea uwezo kufahamu elimu ya fedha, biashara, fursa mbalimbali na uwekezaji, na ndio maana kwenye elimu hii sisi kama kikundi cha Diamond Divas tunataka kuwa wawekezaji, tunataka kuanzisha viwanda, tuanzishe taasisi yetu ndogo ya fedha, ili tuweze kuyafanya yote haya lazima tujikite zaidi katika elimu ya fedha, biashara, fursa na uwekezaji,” alisema Mhe Janeth.

Akizungumzia nini kifanyike Ili kuongeza kasi ya watanzania hususan wanawake kuwekeza katika mifuko ya uwekezaji na Masoko ya mitaji, Mkufunzi wa Masuala ya kifedha, uchumi na uwekezaji, Bw. Emilian Busara alitaja suala la utoaji wa elimu kuhusu mifuko hiyo kupewa kipaumbele zaidi Ili wanaotaka kuwekeza wachague ni aina gani ya mfuko unawafaa.

Cha kwanza watanzania wanahitaji elimu ya fedha, bila kuwapa watu elimu, hakuna namna nyingine ambayo watu wanaweza kuijua mifuko ya uwekezaji, jinsi ya kuwekeza na manufaa yake, na la pili ni kuchukua hatua ya kuwekeza, huwezi kujifunza kuendesha baisketi kwa kusoma kwenye vitabu, lakini tatu ni yule anayejua basi amuelimisha mwingine, yakifanyika haya, sina shaka idadi ya watanzania hususan wanawake watakaojiunga na mifuko hii itaongezeka,” alisema Bw. Busara akitoa pongezi kwa kikundi cha Diamond Divas kwa kuonesha njia.

Kwa upande wake, mmoja wa washiriki katika semina hiyo, Bi. Hellen Siria alitoa ushauri kwa wanawake walio katika vikundi vya kuwezeshana katika Jamii kuvirasimisha Ili viweze kunufaika na fursa mbalimbali zinazotolewa ikiwemo fursa za kupata mitaji, mikopo ya aina mbalimbali na fursa nyinginezo zitakazowasaidia kuinua biashara na maisha yao.

Wito wangu kwa wanawake wenzangu, hasa kwenye vile vikundi vilivyopo katika jamii, tuvirasimishe ili iwe rahisi kunufaika na fursa mbalimbali zinazojitokeza zinazowahusu wanawake wajasiriamali, lakini kilicho muhimu zaidi kwa wanawake tuhakikishe tunajikita katika uwekezaji,” alisema Bi. Hellen.
Katibu wa Kikundi cha Vicoba cha Diamond Divas Group, Bi.Noryne Mmasi, akizungumza katika semina iliyoandaliwa na kikundi hicho ikihusu elimu ya kifedha na jinsi ya kuwekeza katika mifuko ya uwekezaji iliyofanyika jijini Dar es Salaam jana.
Mkufunzi wa Masuala ya kifedha, uchumi na uwekezaji, Bw. Emilian Busara, akitoa elimu ya fedha na uwekezaji katika semina iliyoandaliwa na Kikundi cha Vicoba cha Diamond Divas Group ikihusu elimu ya kifedha na uwekezaji iliyofanyika jijini Dar es Salaam jana.
Baadhi ya wanachama wa Kikundi cha Vicoba cha Diamond Divas Group wakisikiliza mada iliyokuwa ikitolewa na Mkufunzi wa Masuala ya kifedha, uchumi na uwekezaji, Bw. Emilian Busara katika semina kuhusu elimu ya kifedha na jinsi ya kuwekeza katika mifuko mbalimbali ya uwekezaji, iliyofanyika jijini Dar es Salaam jana.
Wanachama wa Kikundi cha Vicoba cha Diamond Divas Group, wakipozi mbele ya wapigapicha mara baada ya kumalizika kwa semina iliyoandaliwa na kikundi hicho kuhusu elimu ya kifedha na jinsi ya kuwekeza katika mifuko mbalimbali ya uwekezaji, iliyofanyika jijini Dar es Salaam jana.
Share:

WATENDAJI WA BENKI YA ABSA TANZANIA WALIVYOSHIRIKI KIKAO CHA BAJETI JIJINI DODOMA JANA

    

Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (katikati), akipozi kwa picha ya kumbukumbu na Ofisa Mkuu wa Fedha wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Bernard Tesha (kushoto), na Mkuu wa Mikakati na Data wa benki hiyo, Bw. John Mosha, ndani ya viwanja vya bunge, mara baada ya mheshimiwa waziri, kuwasilisha bajeti ya serikali ya Sh 63.2 trilioni, itakayotumika katika Mwaka 2026/2027, bungeni, jijini Dodoma, jana.
Ofisa Mkuu wa Fedha wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Bernard Tesha (kulia), Mkuu wa Mikakati na Data wa benki hiyo, Bw. John Mosha (wa tatu kulia), pamoja na baadhi ya wawakilishi kutoka taasisi za fedha, wakimsikiliza kwa makini, Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar, wakati akiwasilisha bajeti ya serikali ya Sh 63.2 trillioni, itakayotumika katika Mwaka 2026/2027, bungeni, jijini Dodoma, jana.
Ofisa Mkuu wa Fedha wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Bernard Tesha (kulia, mstari wa nyuma) na Mkuu wa Mikakati na Data wa benki hiyo, Bw. John Mosha (wa tatu kulia, mstari wa nyuma), pamoja na baadhi ya wawakilishi kutoka taasisi za fedha, wakisimama kwa utambulisho, kabla Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar, hajawasilisha bajeti ya serikali ya Mwaka 2026/2027, bungeni, jijini Dodoma, jana.
Ofisa Mkuu wa Fedha wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Bernard Tesha (wa tatu kushoto), akibadilishana mawazo na baadhi ya wawakilishi kutoka taasisi mbalimbali waliohudhuria uwasilishwaji wa bajeti ya serikali ya Mwaka 2026/2027, bungeni, jijini Dodoma, jana, uliofanywa na Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar.
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Ndege la Air Tanzania Company Limited (ATCL) Mhandisi Peter Ulanga (Katikati), akipiga picha ya kumbukumbu na Ofisa Mkuu wa Fedha wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Bernard Tesha (kulia kwake) na Mkuu wa Mikakati na Data wa benki hiyo, Bw. John Mosha, ndani ya viwanja vya bunge, muda mfupi baada ya Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar, kuwasilisha bajeti ya serikali ya Mwaka 2026/2027, bungeni, jijini Dodoma, jana.
Share:

Absa Bank Tanzania Celebrates Record-Breaking Success at the 2026 Tanzania Pickleball Open, Reinforcing Nation’s Vision as a Regional Sports Hub

ATTRACTING pickleball players from more than seven countries, the Tanzania Pickleball Open 2026 tournament backed by Absa Bank Tanzania, underscoring the growing popularity of the sport and Tanzania’s ambitions to become a regional sports and tourism hub.

The five-day tournament, held at the Gymkhana Club grounds in Dar es Salaam, brought together elite pickleball players from Kenya, Uganda, Rwanda, South Africa, the Democratic Republic of Congo, India, Turkey and Dubai for one of East Africa’s largest pickleball competitions.

Organised through a partnership between the Tanzania Pickleball Association (TPA) and the East Africa Racket Sports Club (EARSC), the event featured a corporate prize pool of US$15,000 and premium playing equipment, attracting both international competitors and local spectators.

As the tournament’s title sponsor, Absa Bank Tanzania said its support reflects a broader commitment to youth development, community engagement and the promotion of emerging sports in the country.

Speaking during the closing ceremony, Absa Bank Tanzania Marketing and Communications Manager, Mr Beda Biswalo, said the tournament had demonstrated the growing potential of pickleball to unite communities and create opportunities for young people.

“We are inspired by the remarkable energy, discipline and international talent displayed throughout the tournament,” said Mr Biswalo. “Our partnership reflects a deeper purpose—championing a sport that unites communities while creating meaningful opportunities for young people.”

He encouraged more Tanzanians, particularly youth, to embrace the sport, noting that pickleball offers opportunities for recreation, fitness and professional development.

Sports stakeholders say the rapid growth of pickleball is creating new opportunities for athletes through international rankings, scholarships and participation in an expanding global professional circuit. The sport’s accessibility and relatively low cost have also contributed to its increasing popularity across different age groups.

The tournament's success aligns with Tanzania’s broader efforts to strengthen sports as a contributor to economic growth and tourism. Through support from government institutions and private-sector partners, the country has increasingly hosted regional and international sporting events aimed at showcasing Tanzania as a destination for sports tourism.

“Absa Bank investment in the tournament supports the Government’s agenda of developing sports infrastructure, nurturing local talent and positioning sports as a driver of economic activity. The initiative is in line with ongoing efforts by the National Sports Council (BMT) to expand opportunities for athletes and sports organisations”, Mr Biswalo added.

The bank also acknowledged the contributions of the Government of Tanzania, co-sponsors Pepsi and CBD Hotel, technology partner Courtly, tournament organisers and fans whose support contributed to the successful staging of the championship.

Following the success of the 2026 edition, Absa Bank remains committed to supporting the growth of pickleball and is optimistic that the Tanzania Pickleball Open will continue to attract increased international participation, help develop the next generation of Tanzanian athletes, and elevate the country's profile on the global sporting stage.

On his part, the President of Tanzania Pickleball Association and the East Africa Rackets Sports Club Director, Kartik Kapor, stated that the Tanzania Pickleball Open 2026 was a resounding success and marked only the beginning of Tanzania’s journey toward becoming a global pickleball powerhouse.

During the finals Women’s Doubles, Rakshika/Agni won 1st place, Sally/Rinaaz won 2nd place and Edna/Ester, WON 3rd place. On men’s Double category, Yuvraj/Purvansh won 1st place, Fifi/Shane won 2nd place and Kartik/Dev won 3rd place.

On the Men’s Singles; Purvansh won 1st place, Fifi 2nd and Dev won 3rd place. International Mixed Doubles; Shaheed/Deandra won 1st place, Ahmad/Zainab 2nd and Lisa/Zuber won 3rd place. Open Women’s Singles; Agni won 1st place, Tamara won 2nd and Sally won 3rd place.

On Mix Doubles winners; Rakshika/Dev won 1st place, 2nd place went to Alikhan/Sally and Yuvraj/Agni won 3rd place.
President of Tanzania Pickleball Association and the East Africa Rackets Sports Club Chairman, Kartik Kapor, shakes hands with Absa Bank Tanzania Head of Large Corporates, Christopher Mgani (right), during the closing ceremony of the Tanzania Pickleball Open 2026, sponsored by the financial institution, at the Dar es Salaam Gymkhana Club.
Absa Bank Tanzania Head of Large Corporates, Christopher Mgani (left), presents awards to winners of the Tanzania Pickleball Open 2026 during the closing ceremony at the Dar es Salaam Gymkhana Club. The tournament was sponsored by Absa Bank.



Absa Bank Tanzania Head of Large Corporates, Christopher Mgani (right), presents trophies to one of the winners of the Tanzania Pickleball Open 2026 during the closing ceremony at the Dar es Salaam Gymkhana Club. The tournament was sponsored by Absa Bank.
Pickleball players in action during the finals of the Tanzania Pickleball Open 2026, sponsored by Absa Bank Tanzania, at the Dar es Salaam Gymkhana grounds.

A pickleball player showcases her skills during the finals of the Tanzania Pickleball Open 2026, sponsored by Absa Bank Tanzania, at the Dar es Salaam Gymkhana grounds.

Cheerful winners of the recently concluded Tanzania Pickleball Open 2026 pose during the closing ceremony at the Dar es Salaam Gymkhana Club. The tournament was sponsored by Absa Bank
Share:

BENKI YA ABSA TANZANIA YAZINDUA HUDUMA YA MIKOPO ISIYO NA DHAMANA ILI KUKUZA BIASHARA ZA WAFANYABIASHARA WADOGO NA WA KATI.

   

Mkuu wa Kitengo cha Bidhaa na Njia za Malipo wa Benki ya Absa Tanzania, Jane Kalumuna (wa tatu kushoto) na wengine kutoka kushoto; Meneja Masoko, Mawasiliano na Chapa, Beda Biswalo, Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Wateja Wadogo na wa Kati, Scolastica Dominic na Meneja Mauzo wa Kitengo cha machine za malipo (POS), Edward Edwine, wakionesha mashine hizo kama ishara ya uzinduzi rasmi wa huduma ya mikopo isiyo na dhamana yenye lengo la kukuza biashara za wafanyabiashara wadogo na wa kati wanaofanya mauzo kwa kutumia POS za Absa. Hafla hiyo ilifanyika jijini Dar es Salaam leo.

Benki ya Absa Tanzania imezindua rasmi suluhisho bunifu la mikopo ya muda mfupi inayolenga kuwawezesha wafanyabiashara wadogo na wa kati kukuza biashara zao bila hitaji la dhamana.

Huduma hiyo mpya imeundwa mahsusi kwa wafanyabiashara wanaojihusisha na biashara ya bidhaa na huduma, wakiwemo wauzaji wa jumla, wasambazaji, mawakala na wauzaji wa rejareja wanaotumia mashine za malipo zinazotolewa na benki hiyo, Absa Point-of-Sale (POS) pamoja na njia nyingine za kidijitali za malipo.

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo jijini Dar es Salaam, Mkuu wa Kitengo cha Bidhaa na Njia za Malipo wa Benki ya Absa Tanzania, Jane Kalumuna, alisema huduma hiyo inalenga kuondoa changamoto kubwa inayowakabili wafanyabiashara wengi ya kushindwa kupata mikopo kutokana na kukosa dhamana za kawaida.

Alisema wafanyabiashara wengi wamekuwa wakifanya mauzo ya kila siku yenye mtiririko mzuri wa fedha, lakini bado wamekuwa wakikosa fursa za kupata mikopo kwa sababu mifumo mingi ya kifedha hutegemea zaidi dhamana kuliko uwezo halisi wa biashara.

Kwa muda mrefu, biashara nyingi zenye mtiririko mzuri wa fedha zimekuwa zikikosa huduma za kifedha kwa sababu hazina dhamana za kawaida. Kupitia Absa huduma hii, tunabadilisha simulizi hilo kwa kutambua na kuthamini utendaji halisi wa biashara,” alisema Bi. Jane.

Aliongeza kuwa huduma hiyo inatumia historia ya miamala ya POS kupima uwezo wa mfanyabiashara kukopa, hivyo kuwezesha wafanyabiashara kupata fedha kwa haraka kulingana na mwenendo halisi wa biashara zao.

Naye Meneja Masoko na Mawasiliano na Chapa wa Benki ya Absa Tanzania, Beda Biswalo, alisema huduma hiyo ni sehemu ya dhamira ya benki hiyo ya kuwezesha ukuaji wa biashara na uchumi wa Tanzania kwa ujumla.

Kwa kuondoa kikwazo cha dhamana na kubadilisha mauzo ya kila siku kupitia POS kuwa chanzo cha haraka cha mtaji, tunabadilisha namna biashara zinavyopata huduma za kifedha nchini Tanzania. Tunaamini kuwa kila mfanyabiashara ana simulizi muhimu, na suluhisho hili linaakisi ahadi yetu ya kusikiliza na kusaidia ukuaji wao,” alisema Biswalo.

Aliongeza kuwa kupitia huduma hiyo, Absa inaendeleza dhamira yake ya ‘Kuiwezesha Afrika ya Kesho Pamoja, Hatua Moja baada ya Nyingine’ kwa kusaidia biashara kukua, kupanuka na kuchangia maendeleo ya uchumi wa taifa.

Huduma ya Absa Merchant Financing inatarajiwa kusaidia kuziba pengo la upatikanaji wa mikopo kwa wafanyabiashara wengi nchini huku ikiimarisha ujumuishaji wa kifedha na mahusiano ya muda mrefu kati ya benki na wateja wake.
Mkuu wa Kitengo cha Bidhaa na Njia za Malipo wa Benki ya Absa Tanzania, Jane Kalumuna (wa tatu kushoto) na wengine kutoka kushoto; Meneja Masoko, Mawasiliano na Chapa, Beda Biswalo, Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Wateja Wadogo na wa Kati, Scolastica Dominic na Meneja Mauzo wa Kitengo cha machine za manunuzi (POS), Edward Edwine, wakiwa katika mkutano na waandishi wa habari, jijini Dar es leo, katika hafla ya uzinduzi rasmi wa huduma ya mikopo isiyo na dhamana yenye lengo la kukuza biashara za wafanyabiashara wadogo na wa kati wanaofanya mauzo kwa kutumia POS za Absa.
Mkuu wa Kitengo cha Bidhaa na Njia za Malipo wa Benki ya Absa Tanzania, Jane Kalumuna (wa tatu kushoto, waliokaa) na wengine kutoka kushoto; Meneja Masoko, Mawasiliano na Chapa, Beda Biswalo, Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Wateja Wadogo na wa Kati, Scolastica Dominic na Meneja Mauzo wa Kitengo cha machine za manunuzi (POS), Edward Edwine, wakionesha mashine hizo kama ishara ya uzinduzi rasmi wa huduma ya mikopo isiyo na dhamana yenye lengo la kukuza biashara za wafanyabiashara wadogo na wa kati wanaofanya mauzo kwa kutumia POS za Absa. Hafla hiyo ilifanyika jijini Dar es Salaam leo. Wengine ni baadhi ya wafanyakazi wa kitengo cha biashara.
Share:

MASHINDANO YA KUOGELEA YA SWAHILI TALENT YAMALIZIKA KWA MAFANIKIO MAKUBWA CHINI YA UDHAMINI YA ABSA BANK TANZANIA

   

Meneja wa Bidhaa wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. George Kaindoah, akimkabidhi tuzo Malachi Mwiki, mmoja wa washindi wa mashindano ya kuogelea ya Swahili Talent Swimming, yaliyodhaminiwa na Benki ya Absa na kumalizika jana katika viwanja vya Gymkhana Club jijini Dar es Salaam. Mashindano hayo yalishirikisha zaidi ya washiriki 300 kutoka shule zaidi ya 25, huku yakitoa kipaumbele maalum katika kuhamasisha ushirikishwaji kwa kuwajumuisha watoto wenye mahitaji maalum kutoka Dar es Salaam na Arusha, kwa lengo la kutambua na kukuza vipaji vya vijana katika mchezo wa kuogelea.
Muogeleaji chipukizi Cairo Erick Johannes, akionesha umahiri wake wakati wa mashindano ya kuogelea ya Swahili Talent Swimming, yaliyodhaminiwa na Benki ya Absa Tanzania na kumalizika jana katika viwanja vya Gymkhana Club jijini Dar es Salaam. Mashindano hayo yalishirikisha zaidi ya washiriki 300 kutoka shule zaidi ya 25, huku yakilenga kuhamasisha ushirikishwaji kwa kuwajumuisha watoto wenye mahitaji maalum kutoka Dar es Salaam na Arusha, kwa lengo la kutambua na kukuza vipaji vya vijana katika mchezo wa kuogelea.
Meneja wa Bidhaa wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. George Kaindoah, akimkabidhi tuzo Amran Suleiman, mmoja wa washindi wa mashindano ya kuogelea ya Swahili Talent Swimming, yaliyodhaminiwa na Benki ya Absa na kumalizika jana katika viwanja vya Gymkhana Club jijini Dar es Salaam. Washindi wengine wanaoonekana pichani ni Alssein Humudi (wa tatu kushoto) na Konhelli Mhella. Mashindano hayo yalishirikisha zaidi ya washiriki 300 kutoka shule zaidi ya 25, huku yakilenga kuhamasisha ushirikishwaji kwa kuwajumuisha watoto wenye mahitaji maalum kutoka Dar es Salaam na Arusha, kwa lengo la kutambua na kukuza vipaji vya vijana katika mchezo wa kuogelea.
Waogeleaji wakichuana wakati wa mashindano ya kuogelea ya Swahili Talent Swimming yaliyodhaminiwa na Benki ya Absa Tanzania na kumalizika jana katika viwanja vya Gymkhana Club jijini Dar es Salaam. Mashindano hayo yalishirikisha zaidi ya washiriki 300 kutoka shule zaidi ya 25, huku yakilenga kuhamasisha ushirikishwaji kwa kuwajumuisha watoto wenye mahitaji maalum kutoka Dar es Salaam na Arusha, kwa lengo la kutambua na kukuza vipaji vya vijana katika mchezo wa kuogelea.
Baadhi ya washiriki wenye mahitaji maalumu, wakipozi kwa picha ya kumbukumbu na Irene Mushi kutoka Benki ya Absa, baada ya kuwakabidhi medali zao, wakati wa mashindano ya kuogelea ya Swahili Talent Swimming, yaliyodhaminiwa na Benki ya Absa na kumalizika jana katika viwanja vya Gymkhana Club jijini Dar es Salaam. Mashindano hayo yalishirikisha zaidi ya washiriki 300 kutoka shule zaidi ya 25, huku yakilenga kuhamasisha ushirikishwaji kwa kuwajumuisha watoto wenye mahitaji maalum kutoka Dar es Salaam na Arusha, kwa lengo la kutambua na kukuza vipaji vya vijana katika mchezo wa kuogelea.
Muogeleaji chipukizi Malikah Kassim akionesha medali yake wakati wa mashindano ya kuogelea ya Swahili Talent Swimming yaliyodhaminiwa na Benki ya Absa Tanzania na kumalizika jana katika viwanja vya Gymkhana Club, jijini Dar es Salaam. Mashindano hayo yalishirikisha zaidi ya washiriki 300 kutoka shule zaidi ya 25, huku yakilenga kuhamasisha ushirikishwaji kwa kuwajumuisha watoto wenye mahitaji maalum kutoka Dar es Salaam na Arusha, kwa lengo la kutambua na kukuza vipaji vya vijana katika mchezo wa kuogelea.
Baadhi ya washindi wa mashindano ya kuogelea ya Swahili Talent Swimming Competition Season 3 yaliyomalizika jana, wakionesha medali zao wakati wa hafla ya utoaji wa tuzo katika viwanja vya Gymkhana Club, jijini Dar es Salaam. Mashindano hayo yalishirikisha zaidi ya washiriki 300 kutoka shule zaidi ya 25, huku yakilenga kuhamasisha ushirikishwaji kwa kuwajumuisha watoto wenye mahitaji maalum kutoka Dar es Salaam na Arusha, kwa lengo la kutambua na kukuza vipaji vya vijana katika mchezo wa kuogelea.
Share:

LILIAN-FAVOUR MAKAWA

LILIAN-FAVOUR MAKAWA

Popular Posts

Blog Archive

Labels

Blog Archive

Recent Posts

Label Cloud

BIASHARA (324) BURUDANI (4) KIMATAIFA (10) KITAIFA (124) MICHEZO (41) SIASA (3)

Pages