BENKI YA ABSA TANZANIA YAKABIDHI WODI YA WAZAZI ILIYOKARABATIWA KATIKA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA TEMEKE

   

Mkurugenzi wa Rasilimali Watu wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Patrick Foya (kushoto), na Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Temeke, Dk. Mfaume Kibwana (Katikati), wakifungua pazia kuashiria makabidhiano rasmi ya Wodi ya Wazazi, iliyofanyiwa ukarabati na Benki ya Absa. Hafla hiyo ilifanyika hospitalini hapo, Temeke, Dar es Salaam leo. Kulia ni Mkurugenzi wa Masoko na Mahusiano wa benki hiyo, Bw. Aron Luhanga.

Benki ya Absa Bank Tanzania leo imekabidhi rasmi wodi iliyokarabatiwa ya Wazazi katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Temeke, ikiwa ni sehemu ya mpango wa kijamii unaoongozwa na wafanyakazi wa benki hiyo, wenye lengo la kuboresha mazingira ya huduma kwa kina mama, watoto pamoja na wahudumu wa afya.

Ukarabati huo umetekelezwa kupitia mpango wa Absa unaojulikana kama “Adopt a Ward”, ambao unaendeshwa na wafanyakazi wenyewe kwa kubaini mahitaji ya jamii, kukusanya rasilimali na kushirikiana na benki katika kuleta mabadiliko chanya yenye tija kwa jamii.

Kazi za ukarabati zilizofanyika katika wodi hiyo ni pamoja na akarabati wa paa na dari, uwekaji wa vigae kwenye kuta za vyoo, ukarabati wa madirisha, kazi za nje za mabomba maalumu ya plastiki (PVC), ukarabati wa mifumo ya umeme, kazi za mabomba ya maji, ufungaji wa milango ya alumini, ufungaji wa viti vya vyoo na sinki pamoja na uchoraji wa majengo.

Akizungumza wakati wa hafla ya makabidhiano, Mkurugenzi wa Rasilimali Watu wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Patrick Foya, alisema kuwa mpango huo unaonyesha imani ya muda mrefu ya benki kwamba jamii huimarika pale taasisi na watu binafsi wanapowekeza pamoja katika suluhisho za vitendo zinazoboresha maisha.

Katika Absa, tunaamini kuwa ‘Stori yako ina Thamani’, na leo tunakumbushwa kuwa hadithi za kina mama, watoto, familia na wahudumu wa afya zina umuhimu mkubwa. Ukarabati huu ni utekelezaji wa dhana yetu ya ‘Kuwezesha Afrika ya Kesho, Pamoja, Hatua Moja baada ya nyingine’. Pia unaonyesha utamaduni tunaoujenga Absa, ambapo watu wetu wanachukua jukumu la kubaini mahitaji ya jamii, kuhamasisha msaada na kushirikiana na benki kuleta mabadiliko endelevu.

Aliongeza kuwa mradi huo unaakisi ajenda pana ya uwajibikaji wa kijamii na uendelevu ya Absa, kwa kusaidia kuboresha mazingira ya huduma kwa heshima na ustahiki kwa wanawake na watoto, sambamba na kuimarisha mchango wa benki katika ustawi wa jamii.

Huu ni mfano halisi wa namna Absa inavyokuwa nguvu chanya katika jamii. Kwa kuboresha wodi ya Mama na Mtoto, tunawaunga mkono wahudumu wa afya wanaohudumia jamii kila siku, na pia kuboresha uzoefu wa huduma kwa kina mama na watoto. Tunaamini uwekezaji wa pamoja wa aina hii ni muhimu katika kujenga jamii imara na yenye afya.

Mpango huo uliwakutanisha wafanyakazi wa Absa kutoka idara mbalimbali, ukiakisi utamaduni wa ndani wa taasisi hiyo unaowahamasisha wafanyakazi kushiriki kikamilifu katika miradi ya maendeleo ya jamii, huku benki ikiongeza nguvu katika jitihada zao ili kuongeza athari chanya.

Mfumo huu wa utoaji unaoongozwa na wafanyakazi pamoja na msaada wa taasisi, umeendelea kuwa sehemu ya mkakati mpana wa Benki ya Absa Tanzania katika uwajibikaji kwa jamii, unaojikita katika ushirikiano, ujumuishi na uundaji wa thamani ya muda mrefu kwa jamii.

Hatua hiyo ya makabidhiano pia inaendana na lengo la Absa ya “Kuiwezesha Afrika ya Kesho, Pamoja, Hatua Moja baada ya nyingine” pamoja na ahadi yake ya chapa ya “Stori yako ina Thamani”, ambayo ni msingi wa namna benki hiyo inavyotoa thamani kwa wateja, jamii na wadau wake.

Kupitia uboreshaji wa mazingira katika sekta muhimu ya afya, Benkiy a Absa Tanzania inalenga kuchangia katika kuboresha huduma za afya ya mama na mtoto, huku ikiimarisha umuhimu wa ushirikiano wa pamoja katika kutatua changamoto za jamii.
Mkurugenzi wa Rasilimali Watu wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Patrick Foya (katikati), akikata utepe kuashiria makabidhiano rasmi ya Wodi ya Wazazi ya Hosptali ya Rufaa ya Mkoa Temeke, iliyofanyiwa ukarabati na Benki ya Absa. Hafla hiyo, ilifanyika hospitalini hapo, Temeke, Dar es Salaam leo. Kulia ni na Mganga Mfawidhi wa hospitali hiyo, Dk. Mfaume Kibwana na kushoto ni Mkurugenzi wa Masoko na Mahusiano wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Aron Luhanga.
Mkuu wa Udhibiti ya Udhibiti Ubora wa, Bw. Hosptali ya Rufaa ya Mkoa Temeke, Dk. Selemani Kivoja, akisalimiana na Mkurugenzi wa Rasilimali Watu wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Patrick Foya (kushoto), huku Mganga Mfawidhi wa hospitali hiyo, Dk. Mfaume Kibwana (kushoto), akiangalia, katika hafla ambayo beni hiyo ilikabidhi jengo la wodi ya wazazi lililokarabatiwa na benki hiyo, katika hafla hiyo ilifanyika hospitalini hapo, Temeke, Dar es Salaam leo. Kulia ni Mkurugenzi wa Masoko na Mahusiano wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Aron Luhanga.
Baadhi ya wafanyakazi wa Benki ya Absa Tanzania wakiongozwa na Mkurugenzi wa Rasilimali Watu, Bw. Patrick Foya, pamoja na watumishi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Temeke, wakipiga picha ya pamoja mara baada ya kumalizika kwa hafla ya makabidhiano ya Wodi ya Wazazi iliyofanyiwa ukarabati na benki hiyo.
Share:

BENKI YA ABSA YAENDELEA KUWAWEZESHA WANAWAKE WAJASIRIMALI KIUCHUMI

Meneja Bidhaa wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Bryton Kimemeta (kushoto), akizungumza na baadhi ya wanawake wajasiriamali, wanachama wa Taasisi inayotoa huduma za kifedha ya ASA Microfinance Tanzania, katika semina iliyoandaliwa na taasisi hiyo kwa uwezeshaji wa benki hiyo ikihusu elimu ya kifedha na jinsi ya kusimamia biashara kwa ufanisi, jijini Dar es Salaam jana. Mafunzo hayo ni sehemu ya mikakati ya Benki ya Absa ya kuwawezesha wajasiriamali nchini sambamba na Lengo la benki hiyo la Kuiwezesha Afrika ya Kesho, Pamoja, hatua moja baada ya nyingine, kupitia chapa ya benki hiyo inayosema 'Stori yako ni ya thamani'.
Meneja Msaidizi wa Uhakiki wa Biashara wa Benki ya Absa Tanzania. Bi. Miriam Ngajilo (kushoto), akizungumza na baadhi ya wanawake wajasiriamali, wanachama wa Taasisi inayotoa huduma za kifedha ya ASA Microfinance Tanzania, katika semina iliyoandaliwa na taasisi hiyo kwa uwezeshaji wa benki hiyo ikihusu elimu ya kifedha na jinsi ya kusimamia biashara kwa ufanisi, jijini Dar es Salaam jana. Mafunzo haya ni sehemu ya mikakati ya benki hiyo ya kuwawezesha wajasiriamali nchini sambamba na Lengo la Benki ya Absa la Kuiwezesha Afrika ya Kesho, Pamoja, hatua moja baada ya nyingine, kupitia chapa ya benki hiyo inayosema 'Stori yako ni ya thamani'.
Mkurugenzi wa Uendeshaji wa Taasisi inayotoa huduma za kifedha ya ASA Microfinance Tanzania, Bw. Hafizur Milon (kushoto), akizungumza kuhusu mahusiano ya kibiashara kati ya taasisi hiyo na Benki ya Absa Tanzania, wakati wa semina ya wanawake wajasiriamali wanachama wa taasisi hiyo kuhusu elimu ya kifedha na jinsi ya kusimamia biashara kwa ufanisi, jijini Dar es Salaam jana. Mafunzo haya ni sehemu ya mikakati ya Benki ya Absa katika kuwawezesha wajasiriamali nchini sambamba na Lengo la benki hiyo la 'Kuiwezesha Afrika ya Kesho, Pamoja, hatua moja baada ya nyingine', kupitia chapa ya benki hiyo inayosema 'Stori yako ni ya thamani'.
Mtaalamu wa Mafunzo wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Hussein Said (kulia), akizungumza na baadhi ya wanawake wajasiriamali, wanachama wa Taasisi inayotoa huduma za kifedha ya ASA Microfinance Tanzania, katika semina iliyoandaliwa na taasisi hiyo kwa uwezeshaji wa benki hiyo ikihusu elimu ya kifedha na jinsi ya kusimamia biashara kwa ufanisi, jijini Dar es Salaam jana. Mafunzo haya ni sehemu ya mikakati ya benki hiyo ya kuwawezesha wajasiriamali nchini sambamba na Lengo la Benki ya Absa la Kuiwezesha Afrika ya Kesho, Pamoja, hatua moja baada ya nyingine, kupitia chapa ya benki hiyo inayosema 'Stori yako ni ya thamani'.
Mmoja wa wanawake wajasiariamali mwanachama wa Taasisi ya huduma za kifedha ya ASA Microfinance Tanzania, Amina Makongoro akichangia hoja wakati wa semina kuhusu elimu ya kifedha na usimamizi wa biashara wenye tija, iliyoandaliwa na taasisi hiyo ikiwezeshwa na Benki ya Absa Tanzania, jijini Dar es Salaam jana. Mafunzo haya ni sehemu ya mikakati ya benki hiyo katika kuwawezesha wajasiriamali nchini sambamba na Lengo la benki hiyo la 'Kuiwezesha Afrika ya Kesho, Pamoja, hatua moja baada ya nyingine', kupitia chapa ya benki hiyo inayosema 'Stori yako ni ya thamani'.
Baadhi ya wanawake wajasiriamali wanachama wa Taasisi ya huduma za kifedha ya ASA Microfinance Tanzania, wakisikiliza, wakati Meneja Bidhaa wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Bryton Kimemeta, akizungumza nao wakati wa semina kuhusu elimu ya kifedha na jinsi ya kusimamia biashara kwa ufanisi, iliyoandaliwa na Taasisi ya ASA Microfinance Tanzania kwa uwezeshaji wa benki hiyo, jijini Dar es Salaam jana. Semina hiyo ni sehemu ya mikakati ya benki hiyo katika kuwawezesha wajasiriamali nchini sambamba na Lengo la benki hiyo la 'Kuiwezesha Afrika ya Kesho, Pamoja, hatua moja baada ya nyingine', kupitia chapa ya benki hiyo inayosema 'Stori yako ni ya thamani'.
Share:

MRADI WA COOKFUND WALETA MAGEUZI YA MATUMIZI YA NISHATI KATIKA TAASISI ZA UMMA

Mshauri Mkuu wa Kiufundi wa UNCDF, Bw. Peter Malika, akizungumza wakati wa makabidhiano ya vifaa vya teknolojia ya upishi salama kwa Shule ya Msingi Bunge jijini Dar es Salaam jana. Serikali ya Tanzania, kwa ufadhili wa Umoja wa Ulaya (EU) kupitia Ujumbe wake nchini, na usimamizi wa programu ukifanywa na Mfuko wa Maendeleo wa Mitaji wa Umoja wa Mataifa (UNCDF), inatekeleza Programu ya CookFund ili kuharakisha mpito wa matumizi ya nishati safi ya kupikia katika kaya na taasisi za umma, hususan mashuleni. Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba (wa pili kutoka kulia), alikuwa mgeni rasmi.

Dar es Salaam, Tanzania | Zaidi ya wanafunzi 62,000 kote Tanzania sasa wananufaika na majiko salama na safi zaidi kufuatia usakinishaji wa zaidi ya majiko ya kisasa 170 ya nishati safi ya kupikia katika shule na taasisi za umma zaidi ya 45. Hatua hii muhimu iliadhimishwa katika hafla ya makabidhiano iliyofanyika katika Shule ya Msingi Bunge jijini Dar es Salaam, ikionesha mchango wa mpango huu katika kupunguza matumizi ya kuni na mkaa na hivyo kukabiliana na ukataji wa miti.

Mpango huu unafadhiliwa na Umoja wa Ulaya (EU) na kutekelezwa na Serikali ya Tanzania kwa kushirikiana na Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo ya Mitaji (UNCDF) kupitia programu ya CookFund.

Akizungumza katika hafla hiyo, Naibu Waziri wa Nishati, Mheshimiwa Salome Makamba alisema:

Mapinduzi haya kuelekea matumizi ya nishati safi ya kupikia ni kipaumbele cha kimkakati cha taifa kinachochangia kulinda mazingira, kuboresha afya ya umma na kuongeza ufanisi wa kiuchumi. Kwa kuzipatia shule na taasisi za umma teknolojia za kisasa za kupikia, tunalenga kulinda misitu yetu, kupunguza hewa chafuzi, na kuboresha mazingira ya kujifunzia kwa watoto wetu. Serikali itaendelea kushirikiana na wadau wa maendeleo kupanua upatikanaji wa nishati safi ya kupikia kwa kuzingatia Mkakati wa Taifa wa Nishati Safi ya Kupikia (2024–2034).

Jitihada za nishati safi ya kupikia nchini zinaongozwa na Wizara ya Nishati kwa kushirikiana na wizara na taasisi nyingine za Serikali, ikiwemo Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI, Wizara ya Maliasili na Utalii, Ofisi ya Makamu wa Rais – Mazingira, pamoja na taasisi nyingine za umma. Hadi sasa, msaada huu kwa taasisi za umma, hususan shule, unalenga taasisi zote zinazohudumia watu zaidi ya 100 kwa wakati mmoja ili kuachana na matumizi ya kuni na mkaa.

Hatua hizi zinaendana na vipaumbele vya kitaifa vya kupunguza ukataji wa miti, kupunguza uzalishaji wa gesi chafuzi, na kuongeza ufanisi katika utoaji wa huduma za umma. Matumizi ya kuni na mkaa huzalisha chembechembe hatarishi zinazoweza kusababisha magonjwa mbalimbali ya mfumo wa upumuaji kama pumu na saratani ya mapafu.

Kupitia programu ya CookFund, inayofadhiliwa na Umoja wa Ulaya, hatua hizi zinalenga kupunguza matumizi ya nishati za kuni na mkaa kwenda kwenye teknolojia bora na zenye ufanisi zaidi kama majiko yanayotumia mkaa mbadala, majiko ya umeme (electric pressure cookers), biyoethano, majiko banifu, pamoja na gesi. Teknolojia hizi zinatarajiwa kupunguza shinikizo kwa rasilimali za misitu, kuboresha ubora wa hewa jikoni, na kuongeza afya na usalama wa wanafunzi na watumishi. Hadi sasa, taasisi 45 zimeboresha mifumo yao ya upishi, nyingi zikiwa ni shule za msingi na sekondari.

Aidha, kupitia CookFund, UNCDF inatoa msaada wa kifedha na kiufundi kwa makampuni na wajasiriamali wanaokidhi vigezo ili kuongeza usambazaji wa nishati safi ya kupikia. Msaada huu unajumuisha uwekezaji wa mtaji na mtaji wa uendeshaji kwa ajili ya kuimarisha uwezo wa biashara zinazojihusisha na uzalishaji, uagizaji, usambazaji na uuzaji wa majiko, mafuta na bidhaa au huduma zinazohusiana na nishati safi ya kupikia.

Kwa upande wake, Mkuu wa Ushirikiano wa Umoja wa Ulaya nchini Tanzania, Marc Stalmans, alisema:

Umoja wa Ulaya umejikita kikamilifu katika kuendeleza hatua za kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi duniani, na Tanzania siyo tofauti. Mpango huu ni sehemu ya juhudi zetu za kusaidia mpito kuelekea nishati safi. Kupitia msaada wa Umoja wa Ulaya, jamii zinazingatia mbinu endelevu zinazolinda mazingira, huku zikichochea ukuaji wa uchumi, kukuza ajira, na kuboresha upatikanaji wa nishati mashuleni, kwenye biashara pamoja na kaya.

Naye Mshauri Mkuu Maswala Kiufundi wa UNCDF, Bw. Peter Malika, alibainisha kuwa pamoja na msaada uliotolewa kwa taasisi 45 katika wilaya 14 za Dar es Salaam, Pwani, Morogoro, Dodoma na Mwanza, programu hiyo imewekeza dola milioni 10.1 katika biashara ndogo na za kati 102.

Nishati safi ya kupikia inapunguza utegemezi wa kuni na mkaa huku ikiboresha usalama, afya na ufanisi wa majiko shuleni,” alisema Bw. Malika. “CookFund inaonesha wazi kuwa teknolojia za kisasa za nishati zinaweza kuleta mageuzi makubwa katika taasisi za umma na kuboresha moja kwa moja mazingira ya kujifunzia kwa maelfu ya wanafunzi.

Kwa ujumla, programu hii imeleta matokeo chanya na yenye mageuzi makubwa, ikichangia uundaji wa ajira 27,005 (za moja kwa moja na zisizo za moja kwa moja), jumla ya biashara 4,933 katika mnyororo wa thamani wa nishati safi ya kupikia, kufikia kaya zaidi ya 482,089, na kupunguza zaidi ya tani 3,911,450 za uzalishaji wa hewa ukaa. Mafanikio haya yanaonesha mchango mkubwa wa programu hii katika maendeleo endelevu, ustawi wa jamii na hatua za kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi nchini Tanzania.
Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba, akitoa hotuba yake wakati wa makabidhiano ya vifaa vya teknolojia ya upishi salama kwa Shule ya Msingi Bunge jijini Dar es Salaam jana. Serikali ya Tanzania, kwa ufadhili wa Umoja wa Ulaya (EU) kupitia Ujumbe wake nchini, na usimamizi wa programu ukifanywa na Mfuko wa Maendeleo wa Mitaji wa Umoja wa Mataifa (UNCDF), inatekeleza Programu ya CookFund ili kuharakisha kipindi cha mpito wa matumizi ya nishati safi ya kupikia katika kaya na taasisi za umma, hususan mashuleni.
Mkuu wa Ushirikiano wa Ujumbe wa EU nchini Tanzania, Bw. Marc Stalmans, akihutubia hadhira wakati wa makabidhiano ya vifaa vya teknolojia ya upishi salama kwa Shule ya Msingi Bunge jijini Dar es Salaam jana. Serikali ya Tanzania, kwa ufadhili wa Umoja wa Ulaya (EU) kupitia Ujumbe wake nchini, na usimamizi wa programu ukifanywa na Mfuko wa Maendeleo wa Mitaji wa Umoja wa Mataifa (UNCDF), inatekeleza Programu ya CookFund ili kuharakisha kipindi cha mpito wa matumizi ya nishati safi ya kupikia katika kaya na taasisi za umma, hususan shule. Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba (wa tatu kutoka kulia), alikuwa mgeni rasmi.
Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba (kushoto), anapika wali akitumia jiko linalotumia nishati salama ya kupikia, wakati wa hafla ya makabidhiano ya vifaa vya teknolojia ya upishi salama katika Shule ya Msingi Bunge jijini Dar es Salaam jana. Serikali ya Tanzania, kwa ufadhili wa Umoja wa Ulaya (EU) kupitia Ujumbe wake nchini, na kwa usimamizi wa programu kutoka Mfuko wa Umoja wa Mataifa wa Kuendeleza Mitaji (UNCDF), inatekeleza Mpango wa CookFund ili kuharakisha kipindi cha mpito cha matumizi ya upishi safi katika kaya na taasisi za umma, hususan mashuleni. Kutoka kulia ni Bw. Marc Stalmans, Mkuu wa Ushirikiano wa Umoja wa Ulaya (EU) nchini Tanzania, akiwa pamoja na Mshauri Mkuu wa Kiufundi wa UNCDF, Bw. Peter Malika.
Share:

WAKULIMA KARATU KUNUFAIKA NA MAPINDUZI YA KIDIJITALI KUPITIA MIXX BY YAS

Meneja wa Mahusiano ya Biashara na Serikali wa Mixx by Yas, Suleiman Asilia (wa tatu kushoto), na Meneja wa Kibiashara Kanda ya Kaskazini wa Mixx by Yas, Eric Sosteness (kushoto kwake), pamoja na Kaimu Mkuu wa COPRA Kanda ya Kaskazini, Famia Amiri, wakimkabidhi runinga janja (Smart TV) Mwenyekiti wa ACU, Shedrack Asseri (mwenye koti jeusi), kwa ajili ya urushaji wa moja kwa moja wa minada ya mazao ya kilimo ili kuongeza uwazi na ushiriki wakati wa msimu wa mazao mbalimbali, ikiwemo ufuta.

Arusha - Wakulima wa Wilaya ya Karatu wanatarajiwa kunufaika kwa kiasi kikubwa na upatikanaji bora wa taarifa za masoko pamoja na kuongezeka kwa uwazi katika biashara ya mazao, kufuatia kuanzishwa kwa mpango wa kidijitali unaoongozwa na Mixx by Yas kwa kushirikiana na wadau wa sekta ya kilimo.

Mpango huo ulizinduliwa rasmi kupitia hafla ya makabidhiano ya runinga janja (Smart TV) iliyotolewa kwa Chama Kikuu cha Ushirika Arusha (ACU) kwa kushirikiana na Mamlaka ya Udhibiti wa Nafaka na Mazao Mchanganyiko (COPRA). Hatua hii inalenga kuboresha upatikanaji wa taarifa muhimu za masoko kwa wakulima na kuongeza ushiriki wao katika mifumo rasmi ya biashara.

Akizungumza katika hafla hiyo, Meneja wa Kibiashara Kanda ya Kaskazini wa Mixx by YasEric Sosteness, alisema kuwa suluhisho za kidijitali zinatoa fursa mpya kwa wakulima kufikia masoko kwa urahisi zaidi.

Kupitia Mixx by Yas, tumejikita kuwawezesha wakulima kwa kuwapatia suluhisho zinazowaleta karibu zaidi na masoko. Upatikanaji wa taarifa za mnada kwa wakati utawasaidia wakulima kufanya maamuzi sahihi na kuongeza kipato chao,” alisema.

Runinga hiyo janja inatarajiwa kuwa chombo muhimu katika kurusha moja kwa moja minada ya mazao ya kilimo. Kupitia teknolojia hiyo, wakulima wa Karatu na maeneo jirani wataweza kufuatilia mwenendo wa bei na shughuli za biashara bila kulazimika kuwepo katika eneo la mnada. Hatua hii inatarajiwa kuongeza uwazi, kupunguza upotoshaji wa taarifa, na kuimarisha ushindani wa haki katika soko.

Kwa upande wake, Meneja wa Mahusiano ya Biashara na Serikali wa Mixx by YasSuleiman Asilia, alisisitiza umuhimu wa ushirikiano kati ya sekta binafsi na taasisi za umma katika kuleta mageuzi ya kiuchumi kwa wakulima.

Ushirikiano huu unaonesha jinsi teknolojia na ubia vinavyoweza kufungua fursa mpya kwa wakulima. Lengo letu ni kuhakikisha wakulima wanaunganishwa zaidi, wanapata taarifa sahihi na wanajumuishwa kifedha,” alieleza.

Naye Kaimu Mkuu wa COPRA Kanda ya Kaskazini, Famia Amiri, alibainisha kuwa urushaji wa moja kwa moja wa minada utaongeza uwazi na kujenga imani katika mfumo wa biashara ya mazao, hususan katika kipindi hiki ambacho nchi inaelekea msimu wa ufuta.

Mbali na mpango huo, Mixx by Yas inaendelea kutoa huduma mbalimbali zinazolenga kumwezesha mkulima, ikiwemo Mixx Kilimo inayorahisisha miamala, Afya Mkulima inayolenga ustawi wa wakulima, pamoja na Kilimo Pesa inayowezesha upatikanaji wa huduma za kifedha kwa urahisi zaidi.

Kwa ujumla, mpango huu unaakisi mwelekeo wa sekta ya kilimo nchini kuelekea matumizi makubwa ya teknolojia katika kuboresha mifumo ya biashara. Kadri suluhisho hizi zinavyozidi kuenea, zinatarajiwa kuongeza tija, kuimarisha kipato cha wakulima, na kuwapa nafasi kubwa zaidi katika uchumi wa kisasa unaozidi kuwa wa kidijitali.

Share:

BENKI YA ABSA YAJIZATITI KUENDELEA KUWAWEZESHA WANAWAKE

  

Ofisa Mkuu wa Teknolojia wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Emmanuel Mwinuka, akitoa mada katika kongamano la wanawake lililopewa jina la ‘Accelerate Women Summit’ na kufanyika hivi karibuni jijini Dar es Salaam. Likidhaminiwa na Benki ya Absa, kongamano hilo liliwaleta pamoja viongozi wanawake kujadili namna teknolojia, uongozi na ujumuishwaji vinavyounda mustakabali wa taifa.
Meneja Huduma za Jamii na Matukio wa Benki ya Absa Tanzania, Bi. Abigail Lukuvi (wa pili kulia), akipokea cheti cha shukrani kwa udhamini kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Acceleration Foundation, Bi. Bernice Fernandos, wakati wa Kongamanao la wanawake lililoitwa ‘Accelerate Women Summit’ na kufanyika hivi karibuni jijini Dar es Salaam. Likidhaminiwa na Benki ya Absa, kongamano hilo liliwaleta pamoja viongozi wanawake kujadili namna teknolojia, uongozi na ujumuishwaji vinavyounda mustakabali wa taifa. Wanaoshuhudia kutoka kushoto ni Meneja anayeshughulikia miradi wa Benki ya Absa, Bi. Munira Chambuso, Ofisa Mkuu wa Teknolojia, Bw. Emmanuel Mwinuka, na Bi. Cygrade Othman pia kutoka benki hiyo.
Ofisa Mkuu wa Teknolojia wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Emmanuel Mwinuka (katikati), na Bi. Munira Chambuso (kushoto) kutoka Absa, wakimsikiliza mfanyabiashara na Mkurugenzi wa Masoko wa MeTL Group, Bi. Fatema Dewji, wakati wa Kongamano la wanawake lililoitwa ‘Accelerate Women Forum’ na kufanyika hivi karibuni jijini Dar es Salaam. Likidhaminiwa na Benki ya Absa, kongamano hilo liliwaleta pamoja viongozi wanawake kujadili namna teknolojia, uongozi na ujumuishwaji vinavyounda mustakabali wa taifa.
Bi. Thamrat Khamis (kushoto), anayeshughulikia akaunti za biashara ndogo na za kati (SME) akizungumza na mmoja wa washiriki wa Kongamano la wanawake lililoitwa ‘Accelerate Women Forum’ na kufanyika hivi karibuni jijini Dar es Salaam. Ukidhaminiwa na Benki ya Absa, mkutano huo uliwaleta pamoja viongozi wanawake kuchunguza namna teknolojia, uongozi na ujumuishwaji vinavyosukuma mustakabali wa taifa.
Wakishangilia, ni timu ya timu kutoka Benki ya Absa, ikiongozwa na Ofisa Mkuu wa Teknolojia, Bw. Emmanuel Mwinuka (wa pili kushoto), wakipiga picha ya kumbukumbu baada ya Kongamano la wanawake lililopewa jina la ‘Accelerate Women Forum’ likifanyika hivi karibuni jijini Dar es Salaam. Likidhaminiwa na Benki ya Absa, kongamano hilo, liliwaleta pamoja viongozi wanawake kujadili namna teknolojia, uongozi na ujumuishwaji vinavyounda mustakabali wa taifa.
Share:

BENKI YA ABSA TANZANIA YADUMISHA USHIRIKANO NA WATEJA WAKE

 

Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Obedi Laiser (kushoto), Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam, Walid Alhad Omar, pamoja na wageni wengine wakichukua chakula cha futari katika hafla iliyoandaliwa na benki kwa wateja wake jijini Dar es Salaam hivi karibuni.
Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam, Walid Alhad Omar (kulia), akipokelewa na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Obedi Laiser, wakati wa hafla ya futari, iliyoandaliwa na benki kwa wateja wake jijini Dar es Salaam hivi karibuni. Katikati ni Mdhibiti wa Masuala ya Fedha wa benki hiyo, Bw. Muhsin Kaye.
Mkurugenzi wa Wateja Binafsi wa Benki ya Absa Tanzania, Bi. Ndabu Swere (wa tatu kushoto), pamoja na baadhi ya wafanyakazi wa benki na wageni wengine, wakichukua chakula cha futari, katika hafla iliyoandaliwa na benki kwa wateja wake jijini Dar es Salaam hivi karibuni.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benkiy a Absa Tanzania, Bw. Obedi Laiser, akiwahutubia wateja na wageni waalikwa, katika hafla ya futari iliyoandaliwa na benki hiyo kwa wateja wake, jijini Dar es Salaam hivi karibuni.
Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam, Walid Alhad Omar, akihutubia baadhi ya wateja na wafanyakazi wa Benkiy a Absa Tanzania, wakati wa hafla ya futari iliyoandaliwa na benki hiyo kwa wateja wake jijini Dar es Salaam hivi karibuni.
Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam, Walid Alhad Omar (katikati), Mkurugenzi Mtendaji wa Absa Bank Tanzania, Bw. Obedi Laiser (wa pili kushoto), pamoja na baadhi ya wakurugenzi wa benki hiyo wakipiga picha ya pamoja baada ya hafla ya futari, iliyoandaliwa na benki kwa wateja wake jijini Dar es Salaam hivi karibuni.
Mdhibiti wa Masuala ya Fedha wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Muhsin Kaye (kushoto), akimuaga Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam, Walid Alhad Omar, huku Mkurugenzi Mtendaji wa benki, Bw. Obedi Laiser, akiangalia, baada ya hafla ya futari iliyoandaliwa na benki kwa wateja wake jijini Dar es Salaam hivi karibuni.
Share:

JIONI YA BARAKA FAMILIA YA OYA YASHIRIKI IFTAR NA JAMII

   Taasisi ya Oya Micro-crediti imeandaa futari maalum kwa wateja wake na jamii kwa ujumla tukio lililolenga kuimarisha mshikamano wa kijamii.

Watoto kutoka kituo cha kulelea watoto mayatima kinondoni,wakitabasam kufurahia iftar iliyoandaliwa na taasisi ya  Oya Micro-Credit ikiwa nikurudisha kwa jamii hasa katika mwezi huu mtukufu wa Ramadhani na Kwaresma


Mwezi Mtukufu wa Ramadhan ni wakati wa kutafakari, kushukuru, na kushirikiana na jamii katika kujitoa kwenye mambo mablimbali. Kwetu OYA, tunaamini kuwa mafanikio ya kweli hayapimwi tu kwa ukuaji wa biashara, bali pia kwa mchango chanya tunaoutoa kwa jamii inayotuzunguka.


Oya Micro-crediti tulipata heshima ya kuandaa Iftar dinner maalum iliyowaleta pamoja watumishi wetu, baadhi ya wateja na wageni maalum katika mazingira ya mshikamano na furaha.


Moja ya sehemu iliyogusa mioyo ya wengi ilikuwa uwepo wa watoto wazuri kutoka kituo cha kulelea watoto yatima kilichopo Kinondoni watoto hao walionesha Tabasamu lao lililota furaha kubwa na kutukumbusha maana halisi ya  ya Mwezi Mtukufu wa Ramadhan — huruma, upendo, na kushirikiana.

Haikua tu hafla ya kufuturu pamoja, bali pia ya kuimarisha mahusiano, kujenga mshikamano wa kijamii, na kueneza matumaini matukio kama haya yanatukumbusha kuwa hata matendo madogo ya wema yanaweza kuleta furaha kubwa kwa wengine.

Tunatoa shukrani zetu za dhati kwa kila mmoja aliyeshiriki na kuchangia kufanya siku hii iwe ya kipekee kadri mwezi wa Ramadhan unavyoendelea, OYA itaendelea kujitahidi kushirikiana na jamii na kuendeleza maadili ya umoja, huruma, na kusaidiana.


Kwa niaba ya familia nzima ya OYA, tunawatakia wote Ramadhan yenye baraka na amani. Alisema Mkurugenzi wa OYA Bwana. Alpha Peter



Ramadan Kareem. 🌙

Share:

LILIAN-FAVOUR MAKAWA

LILIAN-FAVOUR MAKAWA

Popular Posts

Blog Archive

Labels

Recent Posts

Label Cloud

BIASHARA (311) BURUDANI (4) KIMATAIFA (10) KITAIFA (122) MICHEZO (39) SIASA (3)

Pages