AKIBA COMMERCIAL BANK YAUNGANA NA VYOMBO VYA HABARI KUTOA ELIMU YA KIFEDHA NCHINI.


Dar es Salaam, Tanzania; 16 Februari 2026 – Akiba Commercial Bank Plc (ACB) imeendelea kuimarisha ushirikiano wake na wadau wa vyombo vya habari kama sehemu ya juhudi zake za kuendeleza Elimu ya Fedha na kukuza huduma jumuishi za kifedha. 

Kwa kutambua mchango wa vyombo vya habari kama daraja muhimu kati ya taasisi za kifedha na umma, Benki inathamini na kutambua umuhimu  wa vyombo vya habari  katika kueneza ujumbe wa elimu ya fedha. Kupitia magazeti, runinga, redio na majukwaa ya kidijitali, vyombo vya habari vina uwezo wa kufikia hadhira mbalimbali na kueneza Elimu ya Fedha na hivyo kuwezesha jamii 

 kufanya maamuzi sahihi ya maswala ya kifedha.
Akizungumza wakati wa kikao na vyombo mbali mbali  vya  habari, Dora Saria, Mkuu wa Masoko na Mawasiliano, alisisitiza kuwa elimu ya fedha ni kipaumbele cha kimkakati kinacholenga.


 kuiwezesha jamii kuwa na uelewa wa maswala ya  akiba, ukopaji na uwajibikaji, huduma za kifedha za kidijitali, fursa za uwekezaji na mbinu bora za usimamizi wa fedha. Aliongeza kuwa kwa kukuza utoaji wa Elimu za Fedha na kuhimiza matumizi makini ya huduma za kibenki jamii itaweza kunufaika kiuchumi na kimaendeleo.

Alibainisha zaidi kuwa kadiri taswira ya kifedha nchini Tanzania inavyobadilika, hasa kupitia  kuongezeka kwa matumizi ya kidijitali, umuhimu wa elimu ya kifedha unaongezeka sambamba na mabadiliko hayo na hivyo kupelekea kuongezeka kwa juhudi na kipaumbele cha  kuelemisha jamii katika uelewa wa Elimu ya Fedha.


Kupitia mkutano huo, Benki pia ilishirikisha vyombo vya habari vipaumbele vyake vya kimkakati kwa mwaka 2026, kwa kuainisha  ukuzaji na upanuzi wa huduma za Kidijitali kwa ajili ya kuleta ufanisi  na  kuimarisha uzoefu wa wateja na viwango vya uridhikaji katika utoaji huduma.

Akiba Commercial Bank Plc itaendelea  kushirikiana kwa karibu na wadau wa vyombo vya habari ili kuimarisha uwazi, kujenga imani ya umma katika sekta ya kifedha na kutoa ya elimu ya kifedha nchini.


Kuhusu Akiba Commercial Bank Plc (ACB)
Akiba Commercial Bank Plc ni benki ya kibiashara inayolenga  kuhudumia watu kutoka makundi  mbalimbali, ikiwa ni pamoja na wateja binafsi, SMEs,Makampuni makubwa  na taasisi za Serikali, ikizingatia  uwezeshaji wa tabaka la wajasiriamali (SMEs) ili kukuza  biashara, ajira na maendeleo jumuishi.

Share:

AIR FRANCE-KLM WAWEKEZA KATIKA NDOTO ZA MAMA VIJANA TANZANIA

 Katika jamii nyingi, kuwa mama katika umri mdogo huambatana na changamoto kubwa—kutengwa kijamii, ukosefu wa kipato na kukatizwa kwa masomo. Hata hivyo, kupitia ushirikiano kati ya Air France, KLM Royal Dutch Airlines na Forward Motion (FOMO), zaidi ya mama vijana 20 nchini Tanzania sasa wana sababu mpya ya kutazama kesho kwa matumaini.




Kupitia mchango wa mashine 15 za kushona, programu ya mafunzo ya ushonaji ya FOMO imepata nguvu mpya. Hii si tu kuhusu vifaa—ni kuhusu kujenga stadi zinazoweza kubadilisha maisha. Ujuzi wa ushonaji unafungua milango ya ajira binafsi, ubunifu wa bidhaa na hatimaye kipato cha kujitegemea.
Meneja Mkaazi wa Air France-KLM nchini Tanzania, Rajat Kumar (kulia), akikabidhi Moja ya mashine ya kushonea kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Forward Motion FOMO Vivian Sirikwa, wakati wa hafla ya kukabidhi msaada huo uliotolewa na Air France-KLM Kwa kushirikiana na FOMO ili kusaidia kuinua wanawake na wasichana walioko katika mazingira magumu, hususan akina mama vijana, kupitia msaada wa kisaikolojia na kijamii, elimu ya afya ya uzazi na masuala ya kijinsia, ukuzaji wa stadi za maisha, pamoja na uwezeshaji kiuchumi kushoto ni Meneja wa Air France -KLM ukanda wa Afrika mashariki Bw. Viyalrth Abbas, hafla hiyo imefanyika hivi karibuni jijini Dar es Salaam.





Wawakilishi wa Air France-KLM Group hawakukabidhi tu mashine; walitumia muda wao kuzungumza na mama vijana hao, wakitoa ushauri na kuwatia moyo. Kwa wengi wao, ujumbe kwamba wanathaminiwa na kuaminiwa ulikuwa na uzito mkubwa kama msaada wa kifaa chenyewe.




Mashine hizo zitasalia kuwa mali ya FOMO, zikihakikisha kuwa hata baada ya kundi la kwanza kuhitimu, makundi mengine yataendelea kunufaika. Huu ni uwekezaji wa muda mrefu katika rasilimali watu.




Kwa Air France-KLM Group, hatua hii ni sehemu ya dhamira pana ya uwajibikaji wa kijamii—kuhakikisha kuwa uwepo wake katika masoko mbalimbali unaacha alama chanya kwa jamii.




Kwa FOMO, ni hatua nyingine kuelekea lengo lao la kuona mama vijana wakirejea katika jamii wakiwa na kujiamini, ujuzi na uwezo wa kujitegemea.




Katika ulimwengu unaokabiliwa na changamoto nyingi za kijamii na kiuchumi, ushirikiano kama huu unaonesha kuwa mabadiliko ya kweli huanza pale taasisi na jamii zinapounganisha nguvu—kuwekeza si tu katika miundombinu, bali katika watu na ndoto zao.
Share:

.Air France na KLM Wawekeza katika Ndoto za Mama na Vijana Tanzania


Katika jamii nyingi, kuwa mama katika umri mdogo huambatana na changamoto kubwa—kutengwa kijamii, ukosefu wa kipato na kukatizwa kwa masomo. Hata hivyo, kupitia ushirikiano kati ya Air France, KLM Royal Dutch Airlines na Forward Motion (FOMO), zaidi ya mama vijana 20 nchini Tanzania sasa wana sababu mpya ya kutazama kesho kwa matumaini.



Kupitia mchango wa mashine 15 za kushona, programu ya mafunzo ya ushonaji ya FOMO imepata nguvu mpya. Hii si tu kuhusu vifaa—ni kuhusu kujenga stadi zinazoweza kubadilisha maisha. Ujuzi wa ushonaji unafungua milango ya ajira binafsi, ubunifu wa bidhaa na hatimaye kipato cha kujitegemea.
Meneja Mkaazi wa Air France-KLM nchini Tanzania, Rajat Kumar (kulia), akikabidhi Moja ya mashine ya kushonea kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Forward Motion FOMO Vivian Sirikwa, wakati wa hafla ya kukabidhi msaada huo uliotolewa na Air France-KLM Kwa kushirikiana na FOMO ili kusaidia kuinua wanawake na wasichana walioko katika mazingira magumu, hususan akina mama vijana, kupitia msaada wa kisaikolojia na kijamii, elimu ya afya ya uzazi na masuala ya kijinsia, ukuzaji wa stadi za maisha, pamoja na uwezeshaji kiuchumi kushoto ni Meneja wa Air France -KLM ukanda wa Afrika mashariki Bw. Viyalrth Abbas, hafla hiyo imefanyika hivi karibuni jijini Dar es Salaam.





Wawakilishi wa Air France-KLM Group hawakukabidhi tu mashine; walitumia muda wao kuzungumza na mama vijana hao, wakitoa ushauri na kuwatia moyo. Kwa wengi wao, ujumbe kwamba wanathaminiwa na kuaminiwa ulikuwa na uzito mkubwa kama msaada wa kifaa chenyewe.




Mashine hizo zitasalia kuwa mali ya FOMO, zikihakikisha kuwa hata baada ya kundi la kwanza kuhitimu, makundi mengine yataendelea kunufaika. Huu ni uwekezaji wa muda mrefu katika rasilimali watu.




Kwa Air France-KLM Group, hatua hii ni sehemu ya dhamira pana ya uwajibikaji wa kijamii—kuhakikisha kuwa uwepo wake katika masoko mbalimbali unaacha alama chanya kwa jamii.




Kwa FOMO, ni hatua nyingine kuelekea lengo lao la kuona mama vijana wakirejea katika jamii wakiwa na kujiamini, ujuzi na uwezo wa kujitegemea.




Katika ulimwengu unaokabiliwa na changamoto nyingi za kijamii na kiuchumi, ushirikiano kama huu unaonesha kuwa mabadiliko ya kweli huanza pale taasisi na jamii zinapounganisha nguvu—kuwekeza si tu katika miundombinu, bali katika watu na ndoto zao.
Share:

Portwest Deepens East African Footprint with Apparel Manufacturing Investment in TanzaniaDar es Salaam, Tanzania

The Deputy Minister for Industry and Trade, Hon. Denis Londo (center), cuts the ribbon to mark the official opening of Afriport’s occupational safety garments manufacturing factory located in Ubungo, Dar es Salaam. Second from the right is the company’s Chief Executive Officer, Mr. Henry Huge, together with other company officials and government representatives.
Portwest, the world’s fastest-growing manufacturer and distributor of workwear, safety wear and personal protective equipment (PPE), has strengthened its presence in East Africa with the operationalization of a new apparel manufacturing facility in Dar es Salaam, Tanzania—positioning the country as a strategic hub within the company’s global supply chain.

The investment has received strong support from the Government of Tanzania, which reiterated its commitment to creating a conducive environment for local and foreign investors.

Speaking during the official visit to the facility, Assistant Minister for Industry and Trade, Hon. Denis Londo, said the Government will continue to implement investor-friendly policies and legal frameworks to attract industrial investments.

The Government of the United Republic of Tanzania, through the Ministry of Industry and Trade, will continue to put in place enabling policies, laws and regulations to attract investors and support the establishment of industries in the country,” said Hon. Londo.

Investments such as this apparel manufacturing facility demonstrate growing confidence in Tanzania’s industrial environment and our commitment to building a strong manufacturing base that creates jobs and adds value locally.

Founded in 1904 in Ireland and still owned and managed by the Hughes family, Portwest operates in more than 150 countries and employs over 5,500 people globally. The company is internationally recognised for innovation in occupational safety solutions, producing flame-resistant and high-visibility clothing, safety footwear, PPE accessories and fall-protection equipment.

The Dar es Salaam facility is currently employing 200 workers, with existing infrastructure capable of scaling up to 1,000 direct jobs. The investment is expected to contribute significantly to skills development, technology transfer and value addition, in line with Tanzania’s industrialisation agenda and the objectives of the East African Community (EAC).

Meanwhile, Human Resources Manager of the facility, Ms. Anna Lucas, revealed that the company has invested more than USD 8.8 million in the project.

This investment reflects our long-term commitment to Tanzania. Beyond production, we are creating sustainable employment opportunities for Tanzanian youth and contributing to skills development within the local workforce,” she said.

Some employees also noted that the factory has played a vital role in addressing youth unemployment by providing stable jobs and professional training opportunities.
Share:

BENKI YA ABSA TANZANIA YAKABIDHI ZAWADI YA FEDHA TZS MILIONI 48, IKIHITIMISHA KAMPENI YA “UJANJA NI KUSWIPE NA KADI YA ABSA”

   

Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Obedi Laiser, akikabidhi mfano wa hundi ya shs 30,000,000 kwa mshindi wa droo kubwa ya kampeni ya ‘Ujanja ni Kuswipe na Kadi ya Absa’ Bi.Nasreen Karim Abdallah (wa pili kushoto), katika hafla iliyofanyika jijini Dar es Salaam jana. Katika kampeni hiyo ya miezi mitatu iliyokuwa na lengo la kuhamasisha wateja wa benki hiyo na watanzania kutumia huduma za kibenki kwa njia za kidigitali, zawadi zenye jumla ya shs 120,000,000 zilitolewa. Kushoto ni Mkurugenzi wa Wateja Binafsi, Bi. Ndabu Swere na kulia ni Mkurugenzi wa Masoko na Mahusiano, Bw. Aron Luhanga.

Benki ya Absa Tanzania imekabidhi zawadi kwa washindi wa kampeni yake ya “Ujanja ni Kuswipe na Kadi ya Absa”, ikihitimisha kampeni yake ya miezi mitatu iliyokuwa na lengo la kuhamasisha wateja na watanzania kutumia huduma za kibenki kwa njia za kidigitali katika kufanya miamala mbalimbali ya kifedha.

Katika hafla hiyo, mteja wa benki hiyo, Bi. Nasreen Karim Abdallah alikabidhiwa mfano wa hundi yenye thamani ya shilingi milioni 30, baada ya kuibuka mshindi wa droo kubwa iliyofanyika januari 21 mwaka huu, huku washindi wengine wa kila mwezi akiwemo Bw. Abdulrazak Ali Seif aliyepata TZS milioni 10, Bi. Aysha Mbarak Meghji aliyepata TZS milioni 5, na Bw. Gibbons Samuel Katule aliyepata TZS milioni 3 na wote kwa pamoja wakithibisha fedha hizo kuingizwa katika akaunti zao.

Akizungumza katika hafla hiyo, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Obedi Laiser alisema, kampeni hiyo ililenga katika kuwazawadia wateja wao kwa kuendelea kutumia huduma za kibenki zilizo salama, rahisi na za kisasa; “Zaidi ya zawadi, tunajivunia mabadiliko chanya tuliyoyaona kuelekea matumizi ya miamala isiyo ya fedha taslimu, ambayo huokoa muda, hupunguza hatari na kuchangia ujumuishi wa kifedha, hafla ya leo inaashiria mafanikio ya kampeni ambayo yamebadilisha maisha ya watu wengi.

Dhamira yetu iko wazi, Kuiwezesha Afrika ya kesho, pamoja, hatua moja baada ya nyingine. Kila kampeni, kila ubunifu na kila zawadi tunayotoa inaongozwa na imani yetu kwamba Stori yako ina thamani”, alisema Bw. Laiser.

Kampeni hiyo ilionesha ongezeko kubwa la matumizi ya kadi na huduma za kidijitali, ikithibitisha mwelekeo unaokua wa wateja kupendelea huduma za kibenki zinazopatikana muda wowote na mahali popote, huku zikisaidia kupunguza foleni ndefu katika matawi na kuongeza kasi, usalama na urahisi wa huduma.

Akizungumzia mafanikio ya kampeni hiyo, Bi. Ndabu Swere alisema; Kampeni ya “Ujanja ni Kuswipe na Kadi ya Absa” inaonesha jinsi miamala midogo ya kila siku inavyoweza kuwa na nguvu kubwa. Wateja waliitikia vyema, wakidumu katika kufanya miamala kwa njia za kidijitali, na kwa upande wetu tuliweza kuwazawadia uaminifu wao kwa njia yenye maana.

Kwa upande wake, mshindi wa zawadi kubwa, Bi. Nasreen Karim Abdallah, aliishukuru Benki ya Absa kwa zawadi hiyo, akisema ushindi huo ni hatua muhimu katika maisha yake. Alibainisha pia urahisi wa kushiriki kampeni hiyo kwa kutumia tu kadi katika miamala ya kila siku.

Kilichonivutia zaidi ni urahisi wa kushiriki, ni kutumia tu kadi yangu kwenye matumizi ya kawaida. Zawadi hii haithibitishi tu umuhimu wa huduma za kidijitali katika maisha yetu ya kila siku, bali pia ni ya kubadilisha maisha,” alisema.

Benki ya Absa Tanzania imethibitisha dhamira yake ya kuendelea kubuni bidhaa na kampeni zinazowaletea wateja thamani zaidi, ikikumbusha kuwa mwaka 2024 benki hiyo ilitoa zawadi ya magari matatu na mwaka 2025 imetoa TZS milioni 120 kama zawadi za fedha taslimu.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Obedi Laiser, akizungumza katika hafla ambayo benki hiyo ilikabidhi mfano wa hundi ya shs 30,000,000 kwa mshindi wa droo kubwa ya kampeni ya ‘Ujanja ni Kuswipe na Kadi ya Absa’ Bi.Nasreen Karim Abdallah (kushoto), jijini Dar es Salaam jana. Katika kampeni ya miezi mitatu iliyokuwa na lengo la kuhamasisha wateja wa benki hiyo na watanzania kutumia huduma za kibenki kwa njia za kidigitali, zawadi zenye jumla ya shs 120,000,000 zilitolewa. Wa pili kushoto ni Mkurugenzi wa Wateja Binafsi, Bi. Ndabu Swere na kulia ni Mkurugenzi wa Masoko na Mahusiano, Bw. Aron Luhanga.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Obedi Laiser, akikabidhi mfano wa hundi ya shs 3,000,000 kwa mmoja wa washindi wa droo ya kila mwezi ya kampeni ya ‘Ujanja ni Kuswipe na Kadi ya Absa’ Bw. Gibbons Samuel Katule (wa pili kushoto), katika hafla iliyofanyika jijini Dar es Salaam jana. Katika kampeni hiyo ya miezi mitatu iliyokuwa na lengo la kuhamasisha wateja wa benki hiyo na watanzania kutumia huduma za kibenki kwa njia za kidigitali, zawadi zenye jumla ya shs 120,000,000 zilitolewa. Kushoto ni Mkurugenzi wa Wateja Binafsi, Bi. Ndabu Swere na kulia ni Mkurugenzi wa Masoko na Mahusiano, Bw. Aron Luhanga.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Obedi Laiser, akikabidhi mfano wa hundi ya shs 3,000,000 kwa mmoja wa washindi wa droo ya kila mwezi ya kampeni ya ‘Ujanja ni Kuswipe na Kadi ya Absa’ Bw. Gibbons Samuel Katule (wa pili kushoto), katika hafla iliyofanyika jijini Dar es Salaam jana. Katika kampeni hiyo ya miezi mitatu iliyokuwa na lengo la kuhamasisha wateja wa benki hiyo na watanzania kutumia huduma za kibenki kwa njia za kidigitali, zawadi zenye jumla ya shs 120,000,000 zilitolewa. Kushoto ni Mkurugenzi wa Wateja Binafsi, Bi. Ndabu Swere na kulia ni Mkurugenzi wa Masoko na Mahusiano, Bw. Aron Luhanga.
Mshindi wa droo kubwa ya kampeni ya ‘Ujanja ni Kuswipe na Kadi ya Absa’, Bi. Nasreen Karim Abdallah (kushoto), akizungumza baada ya kukabidhiwa zawadi yake ya shs 30,000,000 jijini Dar es Salaam jana. Kampeni hiyo ya miezi mitatu iliyokuwa na lengo la kuhamasisha wateja wa benki hiyo na watanzania kutumia huduma za kibenki kwa njia za kidigitali, zawadi zenye jumla ya shs 120,000,000 zilitolewa. Wa pili kushoto ni Mkurugenzi wa Wateja Binafsi, Bi. Ndabu Swere, Mkurugenzi Mtendaji wa benki hiyo, Bw. Obedi Laiser na Mkurugenzi wa Masoko na Mahusiano, Bw. Aron Luhanga.
Share:

Mkurugenzi Mtendaji wa Absa Bank akutana na Mkurugenzi wa Benki ya Dunia kwa Tanzania, Malawi, Zambia na Zimbabwe kuimarisha Mahusiano ya kibiashara.

   

Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Obedi Laiser (kulia), akiagana na Bw. Nathan Belete, Mkurugenzi wa Benki ya Dunia anayesimamia Malawi, Tanzania, Zambia na Zimbabwe, baada ya mkutano wa kimkakati wa kibiashara uliofanyika hivi karibuni katika Hoteli ya Hyatt Regency Park jijini Dar es Salaam. Mkutano huo ulilenga kuimarisha ushirikiano kati ya taasisi hizo mbili.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Obedi Laiser (kushoto), akizungumza na Bw. Nathan Belete, Mkurugenzi wa Benki ya Dunia anayesimamia Malawi, Tanzania, Zambia na Zimbabwe, baada ya mkutano wa kimkakati wa kibiashara uliofanyika hivi karibuni katika Hoteli ya Hyatt Regency Park jijini Dar es Salaam. Mkutano huo ulilenga kuimarisha ushirikiano kati ya taasisi hizo mbili.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Obedi Laiser (kushoto), akiwa na Bw. Nathan Belete, Mkurugenzi wa Benki ya Dunia anayesimamia Malawi, Tanzania, Zambia na Zimbabwe, baada ya mkutano wa kimkakati wa kibiashara uliofanyika hivi karibuni katika Hoteli ya Hyatt Regency Park jijini Dar es Salaam. Mkutano huo ulilenga kuimarisha ushirikiano kati ya taasisi hizo mbili.
Share:

APeF Yazindua Mfuko wa Ziada Kupanua wigo wa uwekaji Akiba, Uwekezaji na Ulinzi

    

Ofisa Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Masoko ya Mitaji na Dhamana, (CMSA), CPA Nicodemus Mkama, akikabidhi waraka wa ofa kwa Kaimu Mwenyekiti wa Bodi ya Africa Pension Fund (APeF), Dkt. Hamisi Kibola (wa tatu kushoto), kuashiria uzinduzi rasmi wa Mfuko wa Uwekezaji wa Pamoja wa Ziada Fund, jijini Dar es Salaam leo. Wa pili kushoto ni Ofisa Mtendaji Mkuu wa APeF, Bw. Mfaume Kimario, pamoja na wadau wengine wa Mfuko wa Ziada; kuanzia kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Alliance Life, Bw. Byford Mutikwasa, Bi. Tupokigwe Mwalwisi kutoka NBC na Bw. Lusungu.

DAR ES SALAAM, 26 Januari 2026. Africa Pension Fund Limited (APeF) leo imezindua rasmi Mfuko wa Ziada, ambao ni mfuko wa kwanza wa uwekezaji wa pamoja katika soko la fedha nchini Tanzania unaojumuisha mafao ya bima ya maisha, hatua inayoweka alama muhimu katika kupanua upatikanaji wa suluhisho za uwekezaji zilizo chini ya udhibiti. Hafla ya uzinduzi imefanyika katika Hoteli ya KingJada, Morocco Square, jijini Dar es Salaam. Kipindi cha awali cha uuzaji wa vipande kupitia mfuko huu kinaanza leo tarehe 26 Januari hadi 25 Februari 2026.

Hafla ya uzinduzi huo ilihudhuriwa na mgeni rasmi, Ofisa Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Masoko ya Mitaji na Dhamana (CMSA), CPA Nicodemus Mkama, ikihudhuriwa pia na wawakilishi kutoka Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE), mifuko ya hifadhi ya jamii, wasimamizi wa mifuko, madalali, taasisi za kibenki na bima, pamoja na wanahabari.

Mfuko wa Ziada umebuniwa kuwasaidia wawekezaji kuweka akiba na kukuza fedha zao kupitia uwekezaji wenye nidhamu katika soko la fedha, ukiwa na faida ya ziada ya ulinzi wa bima ya maisha kwa wawekezaji binafsi wanaokidhi vigezo. Mfuko huu umerahisishwa kiutendaji, kwa kuwawezesha wawekezaji kuanza kwa urahisi, kuongeza uwekezaji wakati wowote, na kupata fedha zao ndani ya siku tatu za kazi.

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Ofisa Mtendaji Mkuu wa APeF, Bw. Mfaume Kimario, alisema, Ziada imeundwa kwa wawekezaji wanaotaka njia rahisi na za kuaminika za kukuza fedha zao bila kupoteza uwezo wa kupata fedha zao pindi zinapohitajika. Huu ni mfuko imara katika soko la fedha unaopatikana kwa urahisi, wenye ulinzi wa bima ya maisha kwa wawekezaji wanaokidhi vigezo ukianzia na thamani halisi ya uwekezaji (vipande), ya chini kabisa ya shilingi 250,000. Bima hiyo hutoa kinga sawa na asilimia 50 ya thamani halisi ya uwekezaji (vipande) hadi kiwango cha juu cha thamani kilichohakikishwa cha shilingi milioni 100, na kiwango cha juu cha malipo ya bima cha shilingi milioni 50.

Akizungumza kwa niaba ya Mwenyekiti na Bodi ya Wakurugenzi, Dkt. Hamisi Kibola, Mjumbe wa Bodi ya APeF, aliipongeza CMSA kwa hatua zilizofikiwa katika kuendeleza masoko ya mitaji nchini Tanzania na kwa kukuza ukuaji na uhai unaoonekana sokoni kwa sasa. Alibainisha kuwa kiwango cha uwekaji akiba nchini Tanzania bado kiko chini ya asilimia 3, na akatoa wito wa kuimarishwa kwa ushirikiano kati ya wasimamizi na wadau wa sekta ya fedha ili kujenga utamaduni imara wa kujiwekea akiba unaojengwa juu ya taaluma, uaminifu, elimu ya fedha na upatikanaji rahisi wa huduma. Aliongeza kuwa ndiyo sababu APeF ilianzishwa, ubunifu ukiwa kama msingi wake, ili kuongeza wigo kwa vitendo njia za uwekaji akiba na uwekezaji kupitia mifuko ya uwekezaji wa pamoja, mipango binafsi ya pensheni inayounganisha suluhisho za bima na masoko ya mitaji.

Mfuko wa Ziada umeandaliwa kwa ushirikiano na taasisi washirika muhimu, ambapo Alliance Life Assurance Limited ni mtoa bima, Benki ya Taifa ya Biashara (NBC) ni Mtunza Dhamana na Mdhamini. Wawekezaji wanaweza kupata huduma za Mfuko wa Ziada kupitia benki wakusanyaji zikiwemo CRDB Bank, NMB Bank, Exim Bank, Azania Bank, COOP Bank, NBC na Mwanga Hakika Bank, pamoja na kupitia mawakala walioidhinishwa na DSE na majukwaa ya kidijitali ya APeF.

Tunaalika Watanzania kufanya suala la kuweka akiba kuwa utamaduni wao kupitia Ziada. Unapoweka akiba kwa uthabiti, unaimarisha familia yako, kuinua jamii yako, na kuunga mkono maendeleo ya taifa. Ziada inakupa mahali rahisi pa kuanzia, kukua hatua kwa hatua, na kulinda kile kilicho muhimu zaidi,” aliongeza Ofisa Mtendaji Mkuu wa APef, Bw. Kimario.

Kwa upande wake Ofisa Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Masoko ya Mitaji na Dhamana (CMSA), CPA. Nicodemus Mkama alisema kuidhinishwa kwa mfuko wa ziada kunaendelea kuleta chachu zaidi katika maendeleo ya uwekezaji kwenye mifuko hiyo na kuifanya idadi ya mifuko hiyo ya uwekezaji wa pamoja kufikia 26.

Kuhusu APeF

Africa Pension Fund Limited (APeF) ni msimamizi wa mifuko aliyeidhinishwa, anayetoa huduma za usimamizi wa mifuko, mifuko ya uwekezaji wa pamoja, suluhisho za pensheni binafsi, usimamizi wa mali, na ushauri wa kifedha. APeF imejizatiti kuimarisha usalama wa kifedha kupitia suluhisho za uwekezaji bunifu, zenye uwazi na zinazozingatia misingi bora ya suluhisho za uwekezaji.
Ofisa Mtendaji Mkuu wa Africa Pension Fund (APeF), Bw. Mfaume Kimario, akizungumza wakati wa hafla ya uzinduzi rasmi wa Mfuko wa Uwekezaji wa Pamoja wa Ziada Fund, jijini Dar es Salaam leo.
Kaimu Mwenyekiti wa Bodi ya Africa Pension Fund (APeF), Dkt. Hamisi Kibola akizungumza wakati wa hafla ya uzinduzi rasmi wa Mfuko wa Uwekezaji wa Pamoja wa Ziada Fund, jijini Dar es Salaam leo.
Baadhi ya wadau wakihudhuria hafla ya uzinduzi rasmi wa Mfuko wa Uwekezaji wa Pamoja wa Ziada Fund unaoendeshwa na Africa Pension Fund (APeF).
Ofisa Mtendaji Mkuu wa Africa Pension Fund (APeF), Bw. Mfaume Kimario (kushoto) akizungumza na baadhi ya wadau wa Mfuko wa Uwekezaji wa Pamoja wa Ziada Fund wakati wa hafla ya uzinduzi wa mfuko huo, jijini Dar es Salaam leo.
Ofisa Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Masoko ya Mitaji na Dhamana, (CMSA), CPA Nicodemus Mkama (katikati), Kaimu Mwenyekiti wa Bodi ya Africa Pension Fund (APeF), Dkt. Hamisi Kibola (wa nne kushoto) na Ofisa Mtendaji Mkuu wa APeF, Bw. Mfaume Kimario (wa nne kulia) wakipiga picha ya pamoja na baadhi ya wafanyakazi wa taasisi hiyo baada uzinduzi rasmi wa Mfuko wa Uwekezaji wa Pamoja wa Ziada Fund, jijini Dar es Salaam leo.
Share:

LILIAN-FAVOUR MAKAWA

LILIAN-FAVOUR MAKAWA

Popular Posts

Blog Archive

Labels

Blog Archive

Recent Posts

Label Cloud

BIASHARA (295) BURUDANI (4) KIMATAIFA (10) KITAIFA (120) MICHEZO (39) SIASA (3)

Pages