Showing posts with label MICHEZO. Show all posts
Showing posts with label MICHEZO. Show all posts

Serikali ya Marekani Yashiriki Uzinduzi wa Ndondo Cup 2024, kupitia kampeni za SITETEREKI na FURAHA YANGU na CHANJO NI MAISHA

Mkazi wa Jiji la Dar es Salaam akipata vipimo vya afya wakati wa hafla ya uzinduzi wa michuano ya Ndondo Cup 2024. Serikali ya Marekani, kwa kushirikiana na Wizara ya Afya na Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) nchini Tanzania, imetangaza ushirikiano na mashindano ya Ndondo Cup 2024  kupitia kampeni zake mashuhuri za ‘SITETEREKI’, ‘FURAHA YANGU’ na ‘CHANJO NI MAISHA’ ili kuchochea huduma za VVU na chanjo. Mashindano haya yatafanyika katika mikoa nane nchini Tanzania, ikiwemo Dar es Salaam, Dodoma, Mwanza, Mbeya, Iringa, Ruvuma, Pwani na Kagera.

Wizara ya Afya, Ofisi ya Rais – TAMISEMI na Serikali ya Marekani (USAID na PEPFAR) kupitia mradi wa Breakthrough ACTION, wameungana na kamati ya maandalizi ya Ndondo Cup, na wadhamini wengineo ikiwemo CRDB na ASAS, kusogeza huduma za afya hasa huduma za VVU na chanjo. Ushiriki huu kwenye Ndondo Cup 2024, unafanywa kupitia kampeni ya afya ya vijana iitwayo SITETEREKI, kampeni ya wanaume kupambana na VVU iitwayo FURAHA YANGU na Kampeni yab chanjo ya kitaifa iitwayo CHANJO NI MAISHA. Mashindano ya Ndondo Cup 2024 yatafanyika katika mikoa nane ya Tanzania - Dar es Salaam, Iringa, Mbeya, Ruvuma, Kagera, Dodoma, Mwanza, na Pwani.

Mashindano yalianza rasmi Juni 30, 2024, na mechi ya ufunguzi ya kusisimua kati ya Manzese Warriors na Makuburi FC kwenye Uwanja wa Kinesi, kata ya Sinza. Washiriki walipata huduma kamili za afya, ikiwa pamoja na vipimo vya VVU na matibabu na huduma za chanjo. Mgeni rasmi aliyefurahishwa na mpango huu wa ubunifu, aliipongeza kamati ya maandalizi na wadhamini kwa kujumuisha burudani na huduma za afya.

"Tumejitolea kubuni mbinu zinazotoa matokeo halisi ya kiafya," alisema Evangelina Chihoma kutoka Ofisi ya PEPFAR.

"Tunaamini kwamba michezo inaweza kuongeza nguvu kubwa katika kuleta mabadiliko ya tabia na kuboresha upatikanaji wa huduma, na tunafurahia kushirikiana na Ndondo Cup na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kufanikisha mashindano haya."

Lulu Msangi, Mtaalamu wa Programu kutoka Shirika la maendeleo la Marekani (USAID) aliongezea, "Tunatumia michezo kuhamasisha Watanzania kupata chanjo na kulinda familia zao."

Mpango huu wa ubunifu utatekelezwa kwenye ngazi ya kitaifa na jamii, ukilenga kuwafikia vijana wanaoshiriki shughuli za kimichezo kupata elimu na huduma za afya hasa zinazohusu VVU na chanjo. Kwa kuingiza huduma za afya katika burudani, mpango huu unalenga upokeaji wa huduma za afya miongoni mwa wavulana na wanaume kwa kutumia umaarufu wa soka.
Mashabiki wa mpira wa miguu kutoka maeneo mbali mbali ya jiji la Dar es Salaam wakifuatilia uzinduzi wa michuano ya Ndondo Cup 2024. Serikali ya Marekani, kwa kushirikiana na Wizara ya Afya na Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) nchini Tanzania, imetangaza ushirikiano na mashindano ya Ndondo Cup 2024 kupitia kampeni zake mashuhuri za ‘SITETEREKI’, ‘FURAHA YANGU’ na ‘CHANJO NI MAISHA’ ili kuchochea huduma za VVU na chanjo. Mashindano haya yatafanyika katika mikoa nane nchini Tanzania, ikiwemo Dar es Salaam, Dodoma, Mwanza, Mbeya, Iringa, Ruvuma, Pwani na Kagera.
Evangelina Chihoma ambaye ni Mtaalamu wa taarifa za mkakati kutoka PEPFAR akizungumza wakati wa uzinduzi wa michuano ya Ndondo Cup 2024. Serikali ya Marekani, kwa kushirikiana na Wizara ya Afya na Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) nchini Tanzania, imetangaza ushirikiano na mashindano ya Ndondo Cup 2024 kupitia kampeni zake mashuhuri za ‘SITETEREKI’, ‘FURAHA YANGU’ na ‘CHANJO NI MAISHA’ ili kuchochea huduma za VVU na chanjo. Mashindano haya yatafanyika katika mikoa nane nchini Tanzania, ikiwemo Dar es Salaam, Dodoma, Mwanza, Mbeya, Iringa, Ruvuma, Pwani na Kagera.
Share:

Benki ya Absa kuendelea kudhamini Absa Dar City Marathon

Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Obedi Laiser akiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa benki hiyo walioshiriki mbio za Absa Dar City Marathon zilizofanyika Kwa udhamini mkuu wa benki hiyo jijini Dar es Salaam Jana. Wafanyakazi 200 wa Absa walishiriki katika mashindano hayo yaliyoshirikisha wakimbiaji zaidi ya 3000.
Mshindi wa Kwanza wa Mbio za Absa Dar City Marathon, , Augustino Sulle ( kulia) akipokea zawadi kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Obedi Laiser mara baada ya kufanyika Kwa kinyang'anyiro hicho jijini Dar es Salaam Jana. Kulia ni Mkuu wa Masoko na Mahusiano wa Benki hiyo, Aron Luhanga. Benki ya Absa ilikuwa mdhamini mkuu wa mbio hizo ikitoa kiasi cha shs milioni 45 kufanikisha mashindano hayo.
Mshindi wa nne wa Mbio za Absa Dar City Marathon, Oscar Shananga ( kulia) akipokea zawadi kutoka kwa Mkuu wa Masoko na Mahusiano wa Benki ya Absa Tanzania, Aron Luhanga mara baada ya kufanyika Kwa kinyang'anyiro hicho jijini Dar es Salaam Jana. Kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Benki hiyo, Obedi Laiser. Benki ya Absa ilikuwa mdhamini mkuu wa mbio hizo ikitoa kiasi cha shs milioni 45 kufanikisha mashindano hayo.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Obedi Laiser (kushoto) pamoja na washiriki wengine wakipoza viungo muda mfupi baada ya kumalizika Kwa mbio za Absa Dar City Marathon zilizofanyika Kwa udhamini mkuu wa benki hiyo jijini Dar es Salaam Jana.
Mkuu wa Kitengo cha Masoko na Mawasiliano wa Benki ya Absa Tanzania, Aron Luhanga (kushoto), Meneja Mahusiano wa benki hiyo, Theresia Kahesa (katikati) pamoja na wakimbiaji wengine wakishiriki mbio za Kilomita 21 za Absa Dar City Marathon zilizofanyika jijini Dar es Salaam jana. Benki ya Absa ilikuwa mdhamini mkuu wa mbio hizo ikitoa kiasi cha shs milioni 45 kufanikisha mashindano hayo.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Obedi Laiser (katikati) akipozi kwa picha ya kumbukumbu na baadhi ya wakimbiaji baada ya kumalizika kwa mbio za Absa Dar City Marathon zilizofanyika Kwa udhamini mkuu wa benki hiyo jijini Dar es Salaam Jana.
Mkuu wa Masoko na Mahusiano wa Benki ya Absa Tanzania, Aron Luhanga (kushoto), akipokea cheti cha shukurani kutoka Kwa mmoja wa maofisa wa The Runners Club, Kwa kutambua mchango wa Absa kama mdhamini Mkuu wa mbio za mwaka huu.

BENKI ya Absa Tanzania imesema itaendelea kudhamini mbio za Absa Dar City Marathon ikiwa kama mdhanini mkuu kutokana na faida za mbio hizo kwa ustawi wa afya za watanzania.

Akizungumza wakati wa mbio hizo zilizotimua vumbi jijini Dar es Salaam leo, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa, Obedi Laiser alisema kama Absa wanaamini kukimbia kunaleta fursa nyingi katika maisha ikiwa ni pamoja na afya njema jambo muhimu katika ufanisi wa shughuli za uzalishaji mali.

Katika kukimbia tunajenga afya zetu, ili tuweze kufanya shughuli zetu, tuweze kuishi kwa muda mrefu, ni dhana mojawapo ambayo sisi Absa tunaiishi na ndio maana tukaungana na The Runners Club ili tuweze kuboresha maisha ya watanzania,” alisema Bwana Laiser.

Alisema Absa kama benki kongwe kuliko zote Tanzania ikitoa shughuli za kibenki tokea mwaka 1925 ni imani yao kwa kushirikiana na waandaaji wa mbio hizo, Klabu ya The Runners mbio hizo zitaendelea kukua na kufikia viwango vya Kimataifa.

The Runners Club ni wabobezi katika marathon na sisi kama Absa ni wabobezi hasa inapokuja katika utoaji wa huduma bora za kibenki hivyo tunaamini kwa pamoja tunaweza kuifikisha marathon hii mbali zaidi,” alisema mkurugenzi huyo.

Katika mbio hizo Mkuu wa Kitengo cha Habari cha Runners Club, alisema pamoja na mambo mengine mbio hizo zina malengo ya kutangaza vivutio vya utalii wa Jiji la Dar es Salaam na ndio sababu zilianzia katika Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini humo na kuzunguuka katika mitaa na barabara mbalimbali maarufu jijini humo.

Zaidi ya wanariadha 3000 kutoka mikoa mbalimbali nchini walipimana ubavu wakishindana katika mbio za km 21, 10 na 5 huku washindi walikabidhiwa zawadi ya za medali na pesa taslimu.
Share:

WANAWAKE KANISA LA KKKT KWENYE MATEMBEZI YA SHUKURANI

 

.com/img/a/

Mchungaji Kiongozi wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Usharika wa Boko, Ambakisye Lusekelo (wa pili kulia) akiongoza matembezi ya Shukrani ya kilometa 5 yaliyoanzia Kanisa la KKKT - Boko na kuishia katika ufukwe wa Ndege Beach Mbweni jijini Dar es Salaam leo Machi 12, 2022. Matembezi hayo yakiwa ni sehemu ya Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Dunia ambapo Umoja wa Wanawake wa Usharika huo wametumia fursa hiyo kuhamasishana katika kuwachangia watoto waliolazwa katika hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) ambao wakisumbuliwa na ugonjwa wa saratani.

.com/img/a/
Mwenyekiti wa Wanaumoja wa Wanawake wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Sylvia Lupembe, akizungumza wakati wa matembezi ya shukrani 2022 yaliyowashirikisha wanawaka wa kanisa hilo.
.com/img/a/
.com/img/a/
.com/img/a/
.com/img/a/
.com/img/a/
.com/img/a/
Share:

KP MOTORZ YANG’ARISHA FAMILIA MARATHON 2021 YAKABIDHI GARI KWA MSINDI WA KM 21 WANAWAKE

    
Mkuu wa Mauzo na Uendeshaji wa Kampuni ya Kuagiza na Kuuza Magari ya KP Motorz, Lucas Mwamfupe (kulia), akikabidhi funguo ya gari jipya aina ya Toyota Passo lenye thamani ya shs milioni 9.5 kwa mshindi wa kwanza wa KM 21 Wanawake wa mbio za Familia Marathon 2021, Aisha Ibrahim, jijini Dar es Salaam leo. Wanaoangalia kutoka kushoto ni Meneja Mauzo kwa Makampuni wa KP Motorz, Protas Mbeya na Mwenyekiti wa Familia Marathon, Francisca Alphonce
Mkuu wa Mauzo na Uendeshaji wa Kampuni ya Kuagiza na Kuuza Magari ya KP Motorz, Lucas Mwamfupe (kushoto), akikabidhi cheti kwa mshindi wa kwanza wa KM 21 Wanawake wa mashindano ya mbio za Familia Marathon 2021, Aisha Ibrahim, wakati wa mashindano hayo jijini Dar es Salaam leo. Kulia ni Mwenyekiti wa Familia Marathon, Francisca Alphonce.
Mkuu wa Mauzo na Uendeshaji wa Kampuni ya Kuagiza na Kuuza Magari ya KP Motorz, Lucas Mwamfupe (kushoto), akikabidhi cheti kwa mshindi wa pili wa KM 21 Wanawake wa mashindano ya mbio za Familia Marathon 2021, Jamila Abdallah, wakati wa mashindano hayo jijini Dar es Salaam leo. Kulia ni Mwenyekiti wa Familia Marathon, Francisca Alphonce.
Mkuu wa Mauzo na Uendeshaji wa Kampuni ya Kuagiza na Kuuza Magari ya KP Motorz, Lucas Mwamfupe (kushoto), akikabidhi cheti kwa mshindi wa tatu wa KM 21 Wanawake wa mashindano ya mbio za Familia Marathon 2021, Verah Mrema, wakati wa mashindano hayo jijini Dar es Salaam leo. Kulia ni Mwenyekiti wa Familia Marathon, Francisca Alphonce.
Mkuu wa Mauzo na Uendeshaji wa Kampuni ya Kuagiza na Kuuza Magari ya KP Motorz, Lucas Mwamfupe (kushoto), akikabidhi cheti kwa mshindi wa nne wa KM 21 Wanawake wa mashindano ya mbio za Familia Marathon 2021, Shameeza Mukhi, wakati wa mashindano hayo jijini Dar es Salaam leo. Kulia ni Mwenyekiti wa Familia Marathon, Francisca Alphonce.
Mkuu wa Mauzo na Uendeshaji wa Kampuni ya Kuagiza na Kuuza Magari ya KP Motorz, Lucas Mwamfupe (kushoto), akikabidhi cheti kwa mshindi wa tano wa KM 21 Wanawake wa mashindano ya mbio za Familia Marathon 2021, Nimishal Ladha, wakati wa mashindano hayo jijini Dar es Salaam leo. Kulia ni Mwenyekiti wa Familia Marathon, Francisca Alphonce.
Mshindi wa Mbio za KM 21 Wanawake za Familia Marathon 2021, Aisha Ibrahim akijaribu kuwasha gari lake mara baada ya kukabidhiwa na wadhamini, Kampuni ya Magari ya KP Motorz mara baada ya kumalizika kwa mbio hizo jijini Dar es Salaam leo. Aisha atakuwa pia balozi wa KP Motorz kwa muda wa mwaka mmoja.
Mwenyekiti wa Familia Marathon 2021, Francisca Alphonce (wa nne kushoto), akikabidhi tuzo kwa Mkuu wa Mauzo na Uendeshaji wa Kampuni ya Magari ya KP Motorz, Lucas Mwamfupe ya kutambua mchango wa udhamini wa kampuni hiyo katika mbio za mwaka huu za Familia Marathon zilizotimua vumbi jijini Dar es Salaam leo zikifanyika eneo la Msasani Beach Club. KP Motorz ilitoa gari jipya aina ya Toyota Passo kwa mshindi wa pili wa KM 21 Wanawake.
Mshindi wa Mbio za KM 21 za Familia Marathon 2021, Aisha Ibrahim akipozi kwa picha mbele ya gari lake, Toyota Passo lililotplewa zawadi na Kampuni ya kuagiza na kuuza magari ya KP Motorsz mara baada ya kuibuka kidedea katika mbio hizo jijini Dar es Salaam leo.
Share:

FAMILIA MARATHON 2021 KUTIMUA VUMBI JUMAMOSI DISEMBA 11

Mwenyekiti wa mbio za Familia Marathon 2021, Bi. Francisca Alphonce (wa tatu Kulia), akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo kuhusu mbio hizo zinazotarajiwa kufanyika jijini Dar es Salaam Disemba 11, jumamosi. Wengine ni wawakilishi wa Kampuni zinazodhamini mbio hizo.
Mkuu wa Masoko, Mawasiliano na Uhusiano wa Benki ya KCB, Christina Manyenye (wa nne kushoto), akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo kuhusu udhamini wao katika mbio za Familia Marathon 2021 zinazotarajiwa kutimua vumbi lake jijini Dar es Salaam jumamosi wiki hii. Usajili unaendelea kufanyika katika Tawi la KCB Mlimani City.
Ofisa Habari Familia Marathon (kushoto), akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo kuhusu mbio hizo zinazotarajiwa kufanyika jijini Dar es Salaam Disemba 11, jumamosi. Mbio zitaanzia Msasani Beach Club kuanzia saa 12 asubuhi zikijumuisha mbio za 21km -half marathon, 10km- Corporate Run na 5km -Social Run.
Mkurugenzi Mtendaji was Kampuni ya magari ya KP Motors, Anita Kisima (kushoto), akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo kuhusu udhamini wao katika mbio za Familia Marathon 2021 zinazotarajiwa kutimua vumbi lake jijini Dar es Salaam jumamosi wiki hii. KP Motors itatoa zawadi ya gari aina ya Passo mpya kwa mshindi mwanamke kati ya washindi kumi atakayeshinda mbio za KM 21. Kushoto kwake ni Mkuu wa Masoko Mawasiliano na Uhusiano wa Benki ya KCB, Christina Manyenye na Ofisa Masoko wa UTT Amis, Rahim Mwanga.
Mkurugenzi Uendeshaji wa Planet Fitness, Ramadhani Mdula (kushoto), akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo kuhusu udhamini wao katika mbio za Familia Marathon 2021 zinazotarajiwa kufanyika jijini Dar es Salaam jumamosi wiki hii.
Meneja wa Kampuni ya Rani Sanitary Pads, Mawi Zahor (kulia ), akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo kuhusu udhamini wao katika mbio za Familia Marathon 2021 zinazotarajiwa kufanyika jijini Dar es Salaam jumamosi wiki hii.
Waandaaji na wadhamini wa Familia Marathon 2021 wakionyesha kwa waandishi habari, Dar es Salaam leo, medani na baadhi ya zawadi watakazopewa washiriki wa mbio hizo zitakazofanyika kwa mtindo wa kutembea na kukimbia jijini humo jumamosi wiki hii. Mbio za mwaka huu zimedhaminiwa na KCB Bank, KP Motors, UTT Amis, Premier Security, Optical Centre, Rani Sanitary Pads, Planet Fitness, Knight Support na Xpress Rent.
Share:

Baada ya Ushindi, Yanga Yatahadharishwa!

Kocha mkuu wa KMC Habibu Kondo, amewatahadharisha Yanga kutokwenda na matokeo kichwani katika mechi dhidi yao itakayochezwa Jumapili ya tarehe 25 /10/2020 jijini Mwanza.
 
Tunashukuru Mwenyezi Mungu tumefika salama tangu jana, na kwa sasa tumeshakuwa wenyeji hapa Mwanza, tumepata nafasi ya kufanya mazoezi jana na tumefanya mazoezi tena leo kuanzia saa 9:00 hadi saa11:00 jioni ili kuendelea kuzoea hali ya hewa, kiufundi timu tumeiandaa vyema”, alisema.
 
Ameongeza kuwa; ”Yanga isijiamini na matokeo iliyoyapata katika mchezo wa mwisho dhidi ya Polisi Tazania, huku sisi tukitoa sare katika mchezo wetu wa mwisho dhidi ya Ruvu Shooting, sisi tulikutana na wapinzani bora sana ndiyo maana tukapata matokeo hayo lakini dhidi ya Yanga ni mechi tofauti kabisa”.
 
KMC inajivunia kikosi chake chenye nyota kadhaa kama nahodha Juma Kaseja aliyepo kwenye kiwango bora kwa sasa, Israel Mwenda, Hassan Kapalata, Reliant Lusajo, Keny Ally Hassan Kabunda, Andew Vicent “Dante” na wengineo.
 
Katika msimu huu wa ligi 2020-2021, KMC ipo kwenye nafasi ya 6 ikiwa imecheza michezo 7, imeshinda 3 na kutoka sare 2, huku wakipoteza michezo 2 wakiwa wamefunga magoli 9 na kuruhusu kufungwa magoli 4.
 
"Tunashukuru Mwenyezi Mungu tumefika salama tangu jana, kwa sasa tumeshakuwa wenyeji hapa Mwanza, tumepata nafasi ya kufanya mazoezi jana na tumefanya mazoezi tena leo kuanzia saa 9:00 alasiri ili kuendelea kuzoea hali ya hewa, kiufundi timu tumeiandaa vyema”, alisema.
 
Ameongeza kuwa "Yanga isijiamini na matokeo iliyoyapata katika mchezo wa mwisho dhidi ya Polisi Tazania, huku sisi tukitoa sare katika mchezo wetu wa mwisho dhidi ya Ruvu Shooting, sisi tulikutana na wapinzani bora sana ndiyo maana tukapata matokeo hayo lakini dhidi ya Yanga ni mechi tofauti kabisa”.
 
KMC inajivunia kikosi chake chenye nyota kadhaa kama nahodha Juma Kaseja aliyepo kwenye kiwango bora kwa sasa, Israel Mwenda, Hassan Kapalata, Reliant Lusajo, Keny Ally Hassan Kabunda, Andew Vicent “Dante” na wengineo.
 
Katika msimu huu wa ligi 2020-2021, KMC ipo kwenye nafasi ya 6 ikiwa imecheza michezo 7, imeshinda 3 na kutoka sare 2, huku wakipoteza michezo 2 wakiwa wamefunga magoli 9 na kuruhusu kufungwa magoli 4.
Share:

Wafanyakazi wa Benki ya DCB walivyoshiriki mbio za Masaki Corporate Marathon 2020

Wafanyakazi wa Benki ya Biashara ya DCB wakinyoosha viungo mara baada ya kushiriki mbio za Masaki Corporate Marathon 2020 katika Uwanja wa The Green, Masaki jijini Dar es Salaam hivi karibuni.
Baadhi ya wafanyakazi hao wakijinyoosha ili kujiweka sawa mara baada ya kushiriki mbio hizo za mwaka huu katika Uwanja wa The Green, Masaki jijini Dar es Salaam juzi.
Baadhi ya wafanyakazi wa Benki ya DCB, wakishiriki mbio hizo zilizoanzia katika Uwanja wa The Green, Masaki, Dar es Salaam hivi karibuni.
Wafanyakazi wa Benki ya Biashara ya DCB walioshiriki mbio za mwaka huu za Masaki Corporate Marathon wakipiga picha ya kumbukumbu mara baada ya kumaliza mbio hizo katika Uwanja wa The Green Masaki, jijini Dar es Salaam hivi karibuni.
Share:

Absa Bank Tanzania sponsors celebrated local golfer

Absa Bank Tanzania Managing Director, Abdi Mohamed hands over a box contains some golf sports gears and travelling documents to Tanzania renowned golf player, Victor Mbunda (left), on his mission as Tanzania’s flag-bearer in the coming Kenya Open Golf Championship to be staged at Karen Country Club in Nairobi, Kenya on date to be disclosed soon. Mbunda participation is full sponsored by Absa Tanzania. Right is ABT Head of Marketing and Corporate Relations, Aron Luhanga and others from second left are veteran golfers, Martin Warioba and Marian Mugo. A brief occasion was held in Dar es Salaaam during the weekend.

By Staff Reporter

ABSA Bank Tanzania said it has fully sponsored local golf celebrity, Victor Mbunda,  on his mission as Tanzania’s flag-bearer in the coming Kenya Open Championship.

Speaking in Dar es Salaam yesterday, Absa Bank Tanzania Managing Director, Abdi Mohamed, said the bank was happy with Mbunda’s ambition, giving rise to the decision to support him.

“We always aim to bring possibilities into life and, knowing that Mbunda is the current number one golfer in Tanzania, it is our willingness to be part of his success story by facilitating him into this tournament,” said Mohamed.

He said the bank was always proud to be associated with sports so as to inspire Tanzanian youth, as Mbunda does, into showing they were capable to brush shoulders with world-class sportsmen.

Kenya Open is an annual golf tournament founded in 1967. It has been an event on Europe-based Challenge Tour schedule since 1991, before being affix onto the European Tour in 2019.

The tourney’s past champions include Seve Ballesteros, Ian Woosnam, Ken Brown, Christy O’Connor Jr and Trevor Immelman.

“Mbunda is a symbol of ambitions. We, Absa Bank Tanzania respect the ambitions of our customers as well as those of our nation at large. As a way of putting in action the noble aim of our ‘Africanacity’ maxim, we feel obliged to give Mbunda support, and we believe he won’t let us down,” said Mohamed.

Earlier, Absa Tanzania Head of Marketing and Corporate Relations Aron Luhanga, said Mbunda would be fully sponsored.

“We provide a return ticket to Nairobi, allowances as well as golf gears,” he said.

Luhanga urged Tanzanians to play down the misguided notion that golf was reserved for the affluent, saying it was like any other sports and was open to people from all walks of life, whether driven by the urge to keep fit or are out to make money.

Mbunda, flanked by veteran golfers Martin Warioba and Marian Mugo, thanked Absa Bank Tanzania for giving him a helping hand, and promised not to let them down.

“I am willing to be brand ambassador for Absa Bank Tanzania in the tourney as well as in other future golf   contests. You have showed the way,” he said.

The four-day regional classic is scheduled to take off at the Karen Country Club in Nairobi, Kenya on date to be disclosed soon.
Share:

Benki ya Absa Tanzania yadhamini Kili Marathon 2020 kwa mafanikio

Mkuu wa Masoko na Mawasiliano wa Benki ya Absa Tanzania, Aron Luhanga (katikati), pamoja na wafanyakazi wa benki hiyo wakishiriki mbio za Kilomita 21 za Kilimanjaro marathon pamoja na wakimbiaji wengine. Absa ilikuwa mmoja wa wadhamini ikigharamia kituo cha kutoa maji ya kunywa na viburudisho kwa wakimbiaji. Mashindano hayo yalifanyika mjini Moshi, Kilimanjaro leo.  
Mkuu wa Masoko na Mawasiliano wa Benki ya Absa Tanzania, Aron Luhanga (kushoto), akimpongeza mmoja wa wakimbiaji wao aliyeshiriki mbio za kilomita 42 wakati wa mashindano ya Kilimanjaro marathon 2020 pamoja na wakimbiaji wengine mjini Moshi, Kilimanjaro leo. Absa ilikuwa mmoja wa wadhamini ikigharamia kituo cha kutoa maji ya kunywa na viburudisho kwa wakimbiaji. Mashindano hayo yalifanyika Moshi, Kilimanjaro leo.
Mkuu wa Masoko na Mawasiliano wa Benki ya Absa Tanzania, Aron Luhanga (kushoto), pamoja na wakimbiaji wengine wakionyesha medali zao walizopewa baada ya kushiriki mshindamo ya Kilimanjaro Marathon 2020 katika Uwanja wa Chuo cha Ushirika Moshi, mkoani Kilimanjaro leo. Absa ilikuwa mmoja wa wadhamini ikigharamia kituo cha kutoa maji ya kunywa na viburudisho kwa wakimbiaji pamoja na kupeleka wafanyakazi wake kushiriki mbio hizo.
Baadhi ya wakimbiaji wa Benki ya Absa Tanzania pamoja na wakimbiaji wengine, wakitimua mbio wakati wa mashindano ya Kilimanjaro Marathon 2020 mjini Moshi Kilimanjaro leo. Absa ilidhamini mashindano hayo kwa kutoa kituo cha maji na viburudisho kwa wakimbiaji pamoja na kupeleka wafanyakazi wake kushiriki mbio hizo.
Mkimbiaji akipewa maji ili kupoza kiu katika kituo cha maji kilichowekwa kwa ufadhili wa Benki ya Absa Tanzania wakati wa mashindano ya mwaka huu ya Kilimanjaro Marathon mjini Moshi, Kilimanjaro leo.  
Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Dk. Anna Mghirwa (kulia), akikabidhi cheti cha shukurani kwa Mkuu wa Masoko na Mawasiliano wa Benki ya Absa Tanzania, Aron Luhanga kwa kutambua mchango wa benki hiyo katika kufanikisha mashindano ya mwaka huu ya Kilimanjaro Marathon yaliyofanyika leo katika Uwanja wa Chuo cha Ushirika Moshi Mkoani Kilimanjaro. Anayeshuhudia ni Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Dk. Harrison Mwakyembe.
Wakimbiaji wa Benki ya Absa Tanzania, wakipiga picha ya kumbukumbu mara baada ya kumalizika kwa mashindano ya Kilimanjaro Marathon 2020 katika Uwanja wa Chuo cha Ushirika, Mjini Moshi, Kimanjaro juzi. Absa ilidhamini mashindano hayo kwa kutoa kituo cha maji na viburudisho kwa wakimbiaji pamoja na kupeleka wafanyakazi wake kushiriki mbio hizo.
Share:

Wafanyakazi wa DCB washiriki Kilimanjaro Marathon mjini Moshi



Wafanyakazi wa Benki ya Biashara ya DCB, wakishiriki mbio za Kilomita 21 pamoja na wakimbiaji wengine katika Mashindano ya Kilimanjaro Marathon yaliyofanyika katika Uwanja wa Chuo cha Ushirika, Mjini Moshi, Kimanjaro leo.
Wakimbiaji wa Benki ya Biashara ya DCB, wakipasha viungo kabla ya kuanza mbio za Kilomita 21 za mashindano ya Kilimanjaro Marathon 2020 yaliyofanyika katika Uwanja wa Chuo cha Ushirika Mjini Moshi, Kimanjaro, leo.
Baadhi ya wakimbiaji wa Benki ya Biashara ya DCB, wakitimua mbio wakati wa mashindano ya Kilimanjaro Marathon 2020 mjini Moshi Kilimanjaro, leo.
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk. Harrison Mwakyembe (Katikati), Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Dk. Anna Mghwira (wa pili kushoto) pamoja na baadhi ya wakimbiaji wa Benki ya Biashara ya DCB wakishiriki mbio za kujifurahisha za kilomita 5 wakati wa mashindano ya Kilimanjaro Marathon 2020 yaliyofanyika katika Uwanja wa Chuo cha Ushirika Mjini Moshi, Kimanjaro leo.
Wakimbiaji wa Benki ya Biashara ya DCB, wakipiga picha ya kumbukumbu mara baada ya kumalizika kwa mashindano ya Kilimanjaro Marathon 2020 katika Uwanja wa Chuo cha Ushirika, Mjini Moshi, Kimanjaro leo.
Share:

LILIAN-FAVOUR MAKAWA

LILIAN-FAVOUR MAKAWA

Popular Posts

Blog Archive

Labels

Recent Posts

Label Cloud

BIASHARA (275) BURUDANI (4) KIMATAIFA (10) KITAIFA (119) MICHEZO (38) SIASA (3)

Pages