KILA JAMBO JIPYA MAISHANI LINA VITA VIPYA

        
Na Mwandishi Wetu | Arusha | Wakristo kote ulimwenguni wametakiwa kujiandaa na kutambua kuwa kila jambo jipya linalotokea katika maisha ya Mtu linakuwa na vita vipya.

Wito huo umetolewa na Askofu Joseph Lai Laizer wakati akihubiri neno la Mungu lililokuwa na kichwa cha somo kisemacho “Jambo Jipya na Vita vipya” katika Kanisa la Christian Life Church Sinai Mlima wa Washindi lililopo Kiranyi Mkoani Arusha.

Askofu Laizer amesema kuwa kila jambo jipya linalotokea katika maisha ya Wakristo lazima yawe na vita vipya hivyo Wakristo wanapaswa kujiandaa kupambana na vita hivyo kwa silaha ya maombi pamoja na kumtolea Mungu sadaka.

Lazima uombe maombi ya vita huku ukiambatanisha na sadaka, sadaka ni kitu cha muhimu sana

Jambo jengine katika kuvishinda vita hivi, yakupasa kumpata Kuhani atakayesema na kutoa matamshi juu ya hivyo vita vyako

"Wakati Mfalme wa Israel alipoingia vitani na vita kuwa vikali alilikumbuka hili umuhimu wa kuwa na Kuhani katika vita vyako vipya ......Lakini Yehoshafati akasema, Je! Hapana hapa nabii wa Bwana, ili tumwulize Bwana kwa yeye? Akajibu mtumishi mmoja wa mfalme wa Israeli, akasema, Yupo hapa Elisha mwana wa Shafati, aliyekuwa akimimina maji juu ya mikono yake Eliya..... 2Wafalme 3:11"

Napenda kuwaasa watu wa Mungu, kuwa usifurahi sana kuwa kuna jambo jipya linakwenda kutokea kwasababu Unabii umetoka, au kwasababu Mungu amesema kupitia watumishi wake yakupasa kujiandaa na vita vipya

Hata mwaka kuna mambo Mungu anakwenda kufanya kwako lakini lazima ujiandae kwasababu kila jambo jipya lina vita yake” alisema Askofu.

Laiton Deo Shinze mmoja wa Waumini wa Kanisa hilo waliohudhuria Ibada hiyo alitoa maoni yake kuhusu somo hili na kusema “Kwa kweli neno la Mungu alilotufundisha leo Askofu Lai, limetufundisha kwakila jambo yatupasa tumtegemee Mungu

Nae Bi Flomena Fredrick aliongeza kuhusu neno alilofundisha Askofu Lai “Neno la leo limenibariki sana. Mtumishi wa Mungu alikuwa anatufundisha jinsi ya kutoka hatua moja kwenda hatua nyingine, yakwamba kila unapotoka hatua moja kwenda nyingine unajenga kitu kipya na kila kitu kipya huja na changamoto mpya, hivyo kuelekea hatua nyingine hupaswi kulegea, unahitajika kupambana ili kuyafikia yale mafanikio yaliyokusudiwa

Ibada hiyo iliitimishwa kwa maombi maalumu kwaajili ya Wakristo wote Ulimwenguni. Kanisa la ‘Christian Life Church’ Sinai Mlima wa Washindi ni huduma inayopatikana katika jiji la vArusha maeneo ya Kiranyi, Sakina. Engi wanapokea na kushuhudia ukuu wa Mungu kupitia Mtumishi wake Askofu Joseph Lai Laizer.
Share:

AKIBA COMMERCIAL BENKI YAIPIGA JEKI TAASISIS YA FATA VICOBA ENDELEVU YADHAMINI MKUTANO WA MWAKA

 
Meneja wa Benki ya Akiba Commercial Benki PLC (ACB), Tawi la Kijitonyama Joachim Mowo (kushoto) akizungumza na wanachama wa Taasisi ya fata vicoba endelevu wakati wa halfa ya Mkutano wao wa mwisho wa mwaka wa Taasisi hiyo ambapo mkutano huo uliodhaminiwa na Benki ya ACB kwa lengo la kukuza nakunufaisha wajasiliamali wadogo na wakubwa. Hafla hiyo imefanyika leo katika ukumbi wa 361 uliyopo mwenge jijini Dar es Salaam (wapili lishoto) ni Mwenyekiti wa Taasisi futa vicoba endelevu Hanipha Tarimo, katibu wa Taasisi hiyo Rehema Sombi pamoja na Mtunza fedha Jefferson Makubo. Katika hafla hiyo mgeni rasmi alikuwa Mwanasheria Mkuu kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Godfrey Songolo
Meneja Masoko wa Benki ya Akiba Commercial Bank PLC (ACB), Innocent Ishengoma akizungumza na wanachama wa Taasisi ya fata vicoba endelevu wakati wa halfa ya Mkutano wao wa mwisho wa mwaka wa Taasisi hiyo ambapo mkutano huo uliodhaminiwa na Benki ya ACB kwa lengo la kukuza nakunufaisha wajasiliamali wadogo na wakubwa ili watimize ndotozao kupitia benki ya ACB. Hafla hiyo imefanyika leo katika ukumbi wa 361 uliyopo mwenge jijini Dar es Salaam. Katika hafla hiyo mgeni rasmi alikuwa Mwanasheria Mkuu kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Godfrey Songolo
Mwanasheria Mkuu kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Godfrey Songolo ambae pia alikuwa Mgeni rasmi katika hafla ya Mkutano wao wa mwisho wa mwaka wa Taasisi ya fata vicoba endelevu mkutano uliodhaminiwa na Benki ya ACB kwa lengo la kukuza nakunufaisha wajasiliamali wadogo na wakubwa ili waweze kutimiza ndotozao kupitia Benki hiyo. Hafla hiyo imefanyika leo katika ukumbi wa 361 uliyopo mwenge jijini Dar es Salaam
Mwenyekiti wa Taasisi futa vicoba endelevu Hanipha Tarimo akitoa ufafanuzi kuhusu Taasisi hiyo wakati wa halfa ya Mkutano wao wa mwisho wa mwaka wa Taasisi hiyo ambapo mkutano huo uliodhaminiwa na Benki ya ACB kwa lengo la kukuza nakunufaisha wajasiliamali wadogo na wakubwa ili watimize ndotozao kupitia benki ya ACB. Hafla hiyo imefanyika leo katika ukumbi wa 361 uliyopo mwenge jijini Dar es Salaam. Kutoka kushoto ni Afisa Maendeleo ya Jamii Manispaa ya Kinondoni kaya ya Mwananyamala Mulinga Samangwa, Meneja wa Benki ya Akiba Commercial Benki PLC (ACB),Tawi la Kijitonyama Joachim Mowo, katibu wa Taasisi ya fata vicoba endelevu Rehema Sombi, pamoja na Mtunza fedha wa Taasisi hiyo Jefferson Makubo. Katika hafla hiyo mgeni rasmi alikuwa Mwanasheria Mkuu kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Godfrey Songolo
Baadhi ya wanachama wa Taasisi ya fata vicoba endelevu na wateja wa Benki ya ACB wakiwa katika hafla ya Mkutano wao wa mwisho wa mwaka Uliodhaminiwa na Benki hiyo.
Picha ya Pamoja
Share:

Absa Tanzania Yashinda Tuzo Ya Benki Bora Ya Kimataifa nchini Tanzania

Naibu Waziri wa Wizara ya Viwanda na Biashara, Mhe Exaud Silaoneka Kigahe (wa pili kulia) akikabidhi cheti cha shukrani kwa kutambua mchango wa Benki ya Absa Tanzania kama mdhamini mkuu wa tuzo za kila mwaka za walaji (Tanzania Consumer Choice Awards), kwa Ofisa Fedha Mkuu wa benki hiyo, Obedi Laiser katika hafla hiyo iliyofanyika jijini Dar es Salaam jana. Kushoto ni Meneja Mwendeshaji wa Kampuni ya Lavine International Agency, Albert Makoye na Mwanzilishi wa tuzo hizo, Diana Laiser.
Mkuu wa Masoko na Mawasiliano wa Benki ya Absa Tanzania, Aron Luhanga (katikati ) akikabidhi tuzo ya kampuni bora ya vinywaji laini nchini kwa Meneja Mkuu wa Kundi la Mampuni ya Vinywaji ya Sayona, Nitin Menon na Meneja Mkuu wa Uzalishaji, Shahid Choudhary wakati wa hafla ya Tuzo bora za mwaka za Walaji (Tanzania Consumer Choice Awards), iliyofanyika jijini Dar es Salaam jana. Absa ilikuwa mdhamini mkuu wa tuzo hizo ikitoa jumla ya shs milioni 20 kuzidhamini.
Mkurugenzi wa Kitengo cha Wateja Binafsi wa Benki ya Absa Tanzania, Oscar Mwamfwagasi (katikati) akikabidhi tuzo ya kampuni bora ya bima nchini kwa Meneja Mkuu Msaidizi wa Kampuni ya Bima ya Jubilee Insurance, Abdul Rauf Suleiman wakati wa hafla ya Tuzo bora za mwaka za Walaji (Tanzania Consumer Choice Awards), iliyofanyika jijini Dar es Salaam jana. Kushoto ni Mkuu wa Masoko wa kampuni hiyo, Marco Yambi. Absa ilikuwa mdhamini mkuu wa tuzo hizo ikitoa jumla ya shs milioni 20 kuzidhamini.
Ofisa Fedha Mkuu wa Benki ya Absa Tanzania, Obedi Laiser (wa pili kulia) akikabidhi tuzo ya kampuni bora ya mafuta na gesi nchini kwa Mkurugenzi wa Kampuni ya Mafuta ya Lake Oil, Frank Nyabundege wakati wa hafla ya utoaji tuzo bora za walaji za kila mwaka (Tanzania Consumer Choice Awards), iliyofanyika jijini Dar es Salaam jana. Wengine ni Maofisa wa kampuni hiyo. Benki ya Absa ni mdhamini mkuu wa tuzo hizo. Absa ilikuwa mdhamini mkuu wa tuzo hizo ikitoa jumla ya shs milioni 20 kuzidhamini.
Naibu Waziri wa Wizara ya Viwanda na Biashara, Exaud Silaoneka Kigahe (wa tatu kulia) akikabidhi tuzo ya Benki Bora ya Kimataifa ya Mwaka nchini kwa Ofisa Fedha Mkuu wa Benki ya Absa Tanzania, Obedi Laiser wakati wa hafla ya utoaji wa tuzo bora za walaji za kila mwaka (Tanzania Consumer Choice Awards) iliyofanyika jijini Dar es Salaam jana. Wengine ni wakuu wa vitengo mbalimbali wa benki hiyo. Absa ilikuwa mdhamini mkuu wa tuzo hizo ikitoa jumla ya shs milioni 20 kuzidhamini.
Share:

Waziri Mkuu Mstaafu Mizengo Pinda Apongeza Uwezeshaji Unaofanywa Na Benki Ya CRDB Kwa Wanawake

Waziri Mkuu Mstaafu Mhe. Mizengo Pinda akipata maelezo kutoka kwa Meneja Mahusiano Tawi la Oysterbay, Witness Kileo kuhusu uwezeshaji unaofanywa na Benki yetu kwa Wanawake kupitia CRDB Malkia wakati wa Mkutano Mkuu wa Pili na Madirisha uliofanyika jumamosi hii katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere jijini Dar es Salaam. 

Waziri Mkuu Mstaafu Mheshimiwa Mizengo Pinda amepongeza jitihada zinazofanywa na Benki ya CRDB katika kuwawezesha wanawake wajasiriamali nchini kupitia huduma ya CRDB Malkia. Mheshimiwa Pinda ametoa pongezi hizo wakati akifungua Mkutano Mkuu wa Pili wa Jukwaa la Uwezeshaji Wanawake la MADIRISHA uliofanyika katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere (JNICC) ambapo Benki ya CRDB ilikuwa ni mdhamini mkuu. 

Nimefurahishwa kusikia hapa tayari mmeshafanya uwezeshaji wa zaidi ya shilingi bilioni 600 kwa wanawake wajasiriamali kupitia CRDB Malkia. Uwezeshaji huu unaleta chachu ya wanawake wengi zaidi kushiriki katika shughuli za Maendeleo katika taifa letu. Hongereni sana,” alitoa pongezi Mheshimiwa Pinda.

Waziri Mkuu Mstaafu Mhe. Mizengo Pinda akizungumza katika Mkutano Mkuu wa Pili na Madirisha uliofanyika jumamosi hii katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere jijini Dar es Salaam.

Mheshimiwa Pinda aliipongeza Benki hiyo pia kwa ushiriki wake katika makangamano na semina mbalimbali za uwezeshaji akisema kwa kufanya hivyo kunasaidia kufikisha elimu ya ujasirimali na masuala ya fedha kwa wanawake zaidi. Tafiti zinaonyesha ni asilimia 60 tu ya Wanawake ndio waliofikiwa na huduma za kifedha huku wengi wao wakiwa nyuma katika shughuli za ujasiriamali kutokana na kukosa elimu.

Leo hii mmetoa elimu nzuri sana juu ya fursa za uwezeshaji zinazotolewa na Benki hii. Niwapongeze lakini niwasihi mfikishe elimu hii kwa wanawake wengi zaidi mjini na vijijini,” aliongezea Mheshimiwa Pinda. 

Akizungumzia kuhusiana na huduma za uwezeshaji kwa Wanawake zinazotolewa na Benki ya CRDB, Mheshimiwa Pinda alipongeza hatua ya Benki hiyo kupunguza riba ya mikopo inayotolewa kwa wanawake wajasiriamali kutoka asilimia 24 hadi asilimia 14.

.. Kupungua huku kwa riba na masharti mengine yaambatanayo kunatoa fursa kwa Wanawake wengi zaidi kunufaika na CRDB Malkia,” alisema Mheshimiwa Pinda huku akiwahamasisha Wanawake wote kujitokeza kwa wingi kuchangamkia fursa hizo zinazotolewa na Benki yao ya CRDB.


Akiwasilisha mada katika mkutano huo, Meneja Uwezeshaji Wanawake Benki ya CRDB, Rehema Shambwe alisema huduma ya CRDB Malkia imelenga katika kumtambua, kumpa nafasi na kumuwezesha mwanamke wa Kitanzania kufikia malengo yake kupitia mikopo ya biashara na ujasiriamali, kujiwekea akiba kwa akaunti ya Malkia na mafunzo ya uendeshaji biashara. 

“Mpaka kufikia mwishoni mwa mwezi June mwaka huu, Benki yetu tayari ilikuwa imekwisha toa mikopo yenye thamani ya shilingi bilioni 600 kwa wanawake zaidi ya elfu 55,” alisema Rehema huku akibainisha kuwa zaidi ya wanawake 30,000 tayari wameshajiunga na akaunti ya Malkia. 

Rehema alisema pamoja na mafanikio ambayo Benki ya CRDB imeyapata katika kumuwezesha mwanamke, bado idadi ndogo ya wanawake wamekuwa wakijitokeza kupata huduma kutokana na changamoto ya riba, masharti magumu ya dhamana na kukosa uelewa wa huduma za kifedha.


Tukiwa Benki ya kizalendo inayothamini mchango wa wanawake katika maendeleo ya taifa letu, tukasema ni vyema tukatafuta suluhisho la changamoto hizi ili kuweza kumsaidia mwanamke kufankisha malengo yake zaidi,” alisisitiza Rehema. 

CRDB Malkia sasa hivi inawawezesha wanawake kupata mikopo kwa riba ndogo ya asilimia 14 kulinganisha na asilimia 24 iliyokuwa ikitozwa mwanzo huku masharti ya upatikanaji wa mikopo yakirahisishwa kwa kiasi kikubwa. 

Kupungua kwa riba kuna maana wanawake sasa wanaweza kukopa zaidi na kwa gharama nafuu kulinganisha na mwanzo hivyo kusaidia kufanikisha malengo yao kwa uharaka zaidi,” alisema Rehema.  

Rehema alibainisha kuwa kupitia CRDB Malkia, Benki ya CRDB pia imeanzisha huduma ya Malkia Rafiki katika mitandao wake wa matawi ambao watakuwa wanawasidia wanawake kupata huduma stahili kwa uharaka na elimu juu ya huduma hizo ili kuwawezesha kufikia lengo.


Naye Muanzilishi na Mwenyekiti wa Jukwaa la MADIRISHA, Fatma Kange aliishukuru Benki ya CRDB kwa udhamini iliyoutoa kufanikisha Mkutano Mkuu huo ambao kwa mara ya kwanza umeweza kuhudhuriwa na wanawake zaidi 1,000.

.. Wanawake sasa tumepata Benki kimbilio na sehemu ya kuelezea mahitaji yetu. Tuishukuru Benki ya CRDB kwa kutushika mkono na kwa kutuheshimisha Wanawake kupitia CRDB Malkia,” alisema Fatma Kange huku Akitoa rai kwa Wanawake wote kuchangamkia fursa zinazotolewa na Benki hiyo.

Share:

Wafanyakazi wa Benki ya Absa wajitolea kusaidia watoto

Mkuu wa Huduma za Kibiashara wa Benki ya Absa Tanzania, Pius Makalle akikabidhi baadhi ya vitu walivyotoa msaada kwa Meneja wa Mahabusu ya Watoto Upanga, Darius Damas (wa tano kushoto), kituoni hapo, Upanga, Dar es Salaam Jana. Katika hafla hiyo wafanyakazi hao walikabidhi vifaa vya umeme wa sola, jokofu, vyakula na misaada mingine ya kibinadamu vyenye thamani ya zaidi ya shs milioni 6.7.
Meneja Rasilimali watu wa Benki ya Absa Tanzania, Anna Chacha, akikabidhi baadhi ya vitu walivyotoa msaada kwa Meneja wa Mahabusu ya Watoto Upanga, Darius Damas (wa tano kushoto), kituoni hapo jijini Dar es Salaam jana. Katika hafla hiyo wafanyakazi hao walikabidhi vifaa vya umeme wa sola, jokofu, vyakula, na misaada mingine ya kibinadamu vyenye thamani ya shs milioni 6.7.
Baadhi ya wafanyakazi wa Benki ya Absa Tanzania wakibeba misaada mbalimbali wakati wakiwasili katika mahabusu ya watoto Upanga jijini Dar es Salaam jana. Katika hafla hiyo wafanyakazi hao walikabidhi vifaa vya umeme wa sola, jokofu, vyakula, na misaada mingine ya kibinadamu vyenye thamani ya shs milioni 6.7.
Share:

Tanga Cement yashinda ushindi wa jumla tuzo za NBAA kwa Mwaka 2019

Kamishna wa Fedha anaesimamia sekta za maendeleo kutoka Wizara ya Fedha Dk. Charles Mwamaja (wa pili kushoto), akikabidhi tuzo ya ushindi wa kwanza wa kipengele cha Wazalishaji Bora katika tuzo za Uwasilishaji Bora wa Taarifa za Mahesabu za Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu (NBAA) ya mwaka 2019 kwa Mkuu wa divisheni ya Fedha wa Kampuni ya Tanga Cement PLC, Isaac Lupokela, katika hafla iliyofanyika jijini Dar es Salaam. Kulia ni Mthibiti Fedha wa kampuni ya Tanga Cement Emmanuel Nkonyoka.
Mkuu wa divisheni ya Fedha wa Kampuni ya Tanga Cement PLC, Isaac Lupokela (kulia) pamoja na timy ya wahasibu kutoka kampuni ya Tanga Cement PLC wakifurahia tuzo ya ushindi wa Jumla ya uwasilishaji Bora wa Taarifa ya Mahesabu za Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu (NBAA) baada ya kuibuka mshindi wa jumla katika tuzo hizo.
Kamishna wa Fedha anaesimamia sekta za maendeleo katoka Wizara ya Fedha Dk. Charles Mwamaja (wa pili kushoto), akikabidhi tuzo ya ushindi wa kwanza wa kipengele cha Wazalishaji Bora katika tuzo za Uwasilishaji Bora wa Taarifa za Mahesabu za Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu (NBAA) ya mwaka 2019 kwa Mkuu wa divisheni ya Fedha wa Kampuni ya Tanga Cement PLC, Isaac Lupokela, katika hafla iliyofanyika jijini Dar es Salaam. Wengine pichani ni Wahasibu kutoka kampuni ya Tanga Cement.
Share:

Absa Tanzania scoop NBAA award

The National Board of Accountants and Auditors Board (NBAA), Vice Chairperson, Dr. Neema Kiure presents the Best Presented Financial Statements third winner award in banking category to Absa Bank Tanzania Financial Controller, Bernard Tesha, during the NBAA annual gala dinner in Dar es Salaam yesterday.
Jubilant Absa Bank Tanzania Board Chairman, Simon Mponji (centre), Absa Tanzania Financial Controller, Bernard Tesha (right) and the bank’s official, Muhsin Kaye hold the National Board of Accountants and Auditors Board (NBAA), Best Presented Financial Statements award in banking category for the year 2019 soon after it was presented to them during the NBAA annual gala dinner in Dar es Salaam yesterday.
Share:

LILIAN-FAVOUR MAKAWA

LILIAN-FAVOUR MAKAWA

Popular Posts

Blog Archive

Labels

Recent Posts

Label Cloud

BIASHARA (275) BURUDANI (4) KIMATAIFA (10) KITAIFA (119) MICHEZO (38) SIASA (3)

Pages