Airtel Africa Foundation unveils plan for improving 10 million lives in Africa by 2030

Airtel Africa Foundation, the philanthropic arm of Airtel Africa plc, today unveiled its plans to directly improve the lives of 10 million people across the continent by 2030. The strategy will be delivered through targeted initiatives under four core pillars namely Financial Empowerment, Education, Environmental Protection and Digital Inclusion (FEED).

Outlining the ambitious target, Dr. Segun Ogunsanya, Chairman of the Airtel Africa Foundation, stated, “Our 2030 vision is a transformed Africa where over 10 million lives are directly improved through our interventions. We are not just donating resources, we are building a pipeline of talent and fostering innovation to ensure the global digital revolution leaves no African behind. This is a strategic, measurable commitment to unlocking the continent's demographic dividend.

The Foundation’s mission will be executed by creating a cycle of empowerment through targeted programmes. These include ‘Connecting Schools’, which provides free connectivity and devices, and the ‘Airtel Africa Fellowship’, offering full undergraduate scholarships in tech and STEM fields, complemented by mentorship and internships.

A key early success underscoring the Foundation's impact is its ongoing partnership with UNICEF. This collaboration has already connected more than 1,800 schools, benefitted over one million students, and trained more than 17,000 teachers in digital education across the Foundation’s 14 markets of operation.

In addition, the Foundation will leverage its dedicated Employee Volunteer Programme, channelling the skills and passion of its people directly into community initiatives. For the 2025/26 financial year, the Foundation has set specific expansion targets, with programmes now active across all its operating countries, from Nigeria to Zambia, Malawi, Rwanda, and the Democratic Republic of the Congo.

Commenting on the company's support for the Foundation, Airtel Africa’s Chief Executive Officer, Sunil Taldar, said, “We cannot thrive in a place that is not thriving. This understanding is the very reason the Airtel Africa Foundation was born. It is our vehicle to catalyse transformation, by systematically investing in the pillars that underpin a resilient and dynamic society. We have remained dedicated to transforming lives both as a business imperative as well as our overarching philosophy. For us, helping to connect the unconnected, banking the unbanked and enabling businesses and economies to thrive are the three most significant objectives of our business.
Share:

LG Electronics yafungua duka jipya la kisasa jijini Dar es Salaam

Kutoka Kushoto ni Meneja Mkaazi wa kampuni ya LG Tanzania, Aashim Wadhw, Afisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Mohammed Enterprises Tanzania (MeTL) Indrabhuwan Singh, na Mkurugenzi wa F&S, Frank Rwamlima, pamoja na Mkurugenzi wa Masoko wa kampuni ya (MeTL) Fatma Dewji, wakikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi Duka jipya la LG Electronics Mlimani City, Dar es Salaam.”

Dar es Salaam, Septemba 24, 2025 – Kampuni ya LG Electronics Kanda ya Afrika Mashariki imezindua duka jipya la bidhaa zake (brandshop) katika Kituo cha Ununuzi cha Mlimani City jijini Dar es Salaam, ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuimarisha uwepo wake kwenye soko la Afrika Mashariki.

Duka hilo jipya limefunguliwa kwa ushirikiano na kampuni ya F&S pamoja na msambazaji rasmi wa bidhaa za LG nchini, METL. Hatua hiyo inalenga kuongeza urahisi wa upatikanaji wa bidhaa za LG huku wateja wakipewa huduma za kisasa zenye viwango vya kimataifa.

Akizungumza wakati wa uzinduzi, Meneja wa LG Electronics Tanzania, Aashim Wadhwa alisema“Duka hili jipya ni uthibitisho wa dhamira ya LG kuendelea kuwapatia wateja wa Tanzania teknolojia za kisasa na huduma bora zaidi. Dar es Salaam ni jiji lenye kasi kubwa ya ukuaji, na tunaona fursa kubwa ya kushirikiana na ukuaji huo kwa kuwakaribia zaidi wateja wetu na kuhakikisha wanapata msaada wa baada ya mauzo kwa kiwango cha juu.”

Katika duka hili, wateja wataweza kushuhudia na kutumia moja kwa moja ubunifu wa hivi karibuni wa LG, ikiwemo vifaa vya nyumbani (home appliances), vifaa vya burudani majumbani (home entertainment systems) na suluhisho za hali ya hewa (HVAC). Pia kutakuwa na huduma ya haraka, usaidizi wa baada ya mauzo na uhakika wa kupata bidhaa halisi.

Mwakilishi wa F&S alisema Frank Mwamlima-F&S Tunafurahia kushirikiana na LG na METL kuwaletea Watanzania uzoefu wa ununuzi wa kisasa.

 Duka hili litawawezesha wateja kuona na kutumia bidhaa za LG moja kwa moja, na hivyo kuwasaidia kufanya maamuzi sahihi ya ununuzi katika mazingira ya kiwango cha kimataifa.

”kwa upande wake, mwakilishi wa METL aliongeza kuwa“Uzinduzi huu ni ishara ya uhusiano unaozidi kukua kati ya METL na LG East Africa. LG ni chapa inayotambulika duniani kwa ubora na uimara wake, na duka hili linaonesha dhamira yetu ya pamoja ya kuwaletea Watanzania bidhaa zenye viwango vya juu, imara na za kuaminika.”

Kwa mujibu wa tafiti, soko la vifaa vya nyumbani Afrika Mashariki linatarajiwa kukua kwa wastani wa asilimia 6.55 kila mwaka, huku familia nyingi zikielekeza kipaumbele katika teknolojia endelevu na zenye kuokoa gharama.


Duka jipya la LG jijini Dar es Salaam ni sehemu ya mkakati mpana wa upanuzi wa kampuni hiyo katika ukanda wa Afrika Mashariki, ambapo tayari imejitanua katika nchi mbalimbali zikiwemo Kenya, Sudan, Ethiopia, Tanzania, Somalia, Uganda, Zambia, Sudan Kusini na Rwanda. Kupitia uwekezaji huu, LG inalenga kuongeza upatikanaji wa bidhaa zake, kuboresha huduma kwa wateja na kuimarisha uzoefu wa matumizi ya teknolojia za kisasa.

Share:

Airtel Tanzania yaifikisha SmartWASOMI kwa walimu wa IT visiwani Zanzibar

 

Ofisa Vifaa vya Intaneti wa Mradi wa Airtel SmartWASOMI, Bw. Harrison Isdory (kushoto), akitoa maelekezo kuhusu matumizi ya baadhi ya vifaa vya intaneti katika warsha iliyoandaliwa kwa walimu wa IT, mjini Zanzibar hivi karibuni, iliyoandaliwa na Airtel Tanzania kupitia Airtel Africa Foundation, kwa kushirikiana na Shirika la Kimataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF) na Wizara ya Elimu, chini ya mpango wa Airtel SmartWASOMI, unaolenga kuboresha elimu ya kidigitali kwa kuwawezesha walimu na wanafunzi kupata maudhui ya kielimu kupitia maktaba mtandao ya Taasisi ya Elimu Tanzania na Shule Direct bila gharama ya vifurushi vya data.

Airtel Tanzania, kupitia Airtel Africa Foundation na kwa kushirikiana na UNICEF pamoja na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, imeendesha warsha ya mafunzo kwa walimu wa Zanzibar mwishoni mwa wiki, ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa mpango wa Airtel SmartWASOMI. Mpango huu wa elimu ya kidijitali unalenga kuongeza upatikanaji wa elimu bora kupitia teknolojia kote nchini Tanzania.

Warsha hiyo iliwaunganisha walimu 36 kutoka shule mbalimbali za sekondari ambazo tayari zimeunganishwa na jukwaa la Airtel SmartWASOMI. Tangu uzinduzi wake mwezi Mei 2024 na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, mpango wa Airtel SmartWASOMI umefikia zaidi ya shule 400 na umeleta athari chanya kwa maelfu ya walimu na wanafunzi nchini. Jukwaa hili linatoa huduma ya bure ya mtandao kwa rasilimali muhimu za kielimu, ikiwa ni pamoja na maudhui yaliyoidhinishwa na Taasisi ya Elimu Tanzania (TIE) na Shule Direct, hivyo kuwawezesha walimu na wanafunzi kujifunza bila wasiwasi wa gharama za data.

Mgeni rasmi katika tukio hilo, Mkurugenzi wa Elimu ya Sekondari Zanzibar, Bi. Asia Iddy Issa, alisifu mpango huo na kusisitiza kwamba unakwenda sambamba na malengo ya kitaifa.

Mpango huu unasaidia ndoto yetu ya kuunda kizazi chenye uelewa wa kidijitali na unatatua changamoto zilizokwamisha upatikanaji wa nyenzo bora za kujifunzia, hasa katika maeneo yenye uhitaji mkubwa kwa kuwajengea uwezo walimu na kuondoa kikwazo cha gharama za data, tunapunguza pengo kati ya mbinu za kiasili za ufundishaji na ufundishaji wa kisasa,” alisema Asia.

Akaendeleo kusema, “Tunakaribisha kwa moyo mmoja suluhisho kama hili bunifu, kwani linakamilisha juhudi zetu za kuimarisha mfumo wa elimu kwa njia ya kidijitali, tunatarajia kuona shule nyingi zaidi Zanzibar zikifaidi kupitia Airtel SmartWASOMI, na tumejizatiti kushirikiana na wadau wote kuhakikisha kuna matokeo ya kudumu.

Akizungumza kwa niaba ya Wizara ya Elimu, Mkuu wa Idara ya Elimu ya Sekondari Zanzibar, Mfaume Jaffary Mfaume ambaye pia alifungua warsha hiyo, alisisitiza umuhimu wa kuwaunga mkono walimu katika mabadiliko ya kidijitali.

Warsha hii inawawezesha walimu kutumia kwa ufanisi zana za kidijitali ili kuboresha utoaji wa somo, kurahisisha upangaji wa masomo, na kuleta matokeo bora ya kujifunza, Airtel SmartWASOMI ni njia rahisi, thabiti na jumuishi ya kuwaunganisha walimu na wanafunzi na rasilimali bora za kujifunzia bila gharama za data,” alisema.

Katika warsha hiyo, walimu walipata mafunzo ya vitendo kuhusu namna ya kuvinjari maudhui ya mitaala, kuunganisha rasilimali za kidijitali katika masomo yao, na kufuatilia ushiriki wa wanafunzi kwa ufanisi zaidi. Pia walihimizwa kujifunza kwa kushirikiana, kushirikiana mawazo, na kujenga mtandao wa walimu waliowezeshwa kwa njia ya kidijitali.

Walimu waliohudhuria walielezea shukrani zao kwa Airtel Africa Foundation, UNICEF na serikali kwa kuanzisha mpango unaosaidia mbinu za kisasa, zinazopatikana kwa urahisi na zenye ufanisi katika shule.

Kwa upande wake, Yussuf Mwadini Haji, mwalimu wa Shule ya Sekondari Hamamni, alisema, “Kabla ya warsha hii, wengi wetu hatukujua uwezo mkubwa wa zana za kidijitali. Sasa najisikia kuwa na ujasiri na hamasa ya kufanya masomo yangu yawe ya kuvutia zaidi kwa wanafunzi.

Mwalimu mwingine, Amina Hamza Shaabani kutoka Shule ya Sekondari Forodhani, aliongeza, “Airtel SMARTWASOMI imefungua fursa mpya. Sasa tunapata maudhui ya kisasa bila gharama za data, jambo ambalo limepunguza mzigo mkubwa.

Mafunzo haya ni sehemu ya dhamira pana ya Airtel Tanzania ya kuunganisha zaidi ya shule 1,000 ifikapo mwisho wa mwaka 2025. Kampuni hiI ya mawasiliano inaendelea kuwekeza katika miundombinu ya kidijitali, ushirikiano na jamii, pamoja na kushirikiana kwa karibu na wadau ili kupanua wigo na manufaa ya mpango wa Airtel SmartWASOMI. Mpango huu unachangia moja kwa moja malengo ya taifa ya kuboresha uelewa wa kidijitali, kupunguza pengo la elimu, na kuhakikisha walimu na wanafunzi katika maeneo yote wanapata elimu bora ya kidijitali.
Mkurugenzi wa Elimu ya Sekondari visiwani Zanzibar, Bi. Asia Iddy Issa, akizungumza katika katika warsha iliyoandaliwa kwa walimu wa IT, mjini Zanzibar hivi karibuni, iliyoandaliwa na Airtel Tanzania kupitia Airtel Africa Foundation, kwa kushirikiana na Shirika la Kimataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF) na Wizara ya Elimu, chini ya mpango wa Airtel SmartWASOMI, unaolenga kuboresha elimu ya kidigitali kwa kuwawezesha walimu na wanafunzi kupata maudhui ya kielimu kupitia maktaba mtandao ya Taasisi ya Elimu Tanzania na Shule Direct bila gharama ya vifurushi vya data.
Ofisa Vifaa vya Intaneti wa Mradi wa Airtel SmartWASOMI, Bw. Harrison Isdory (kushoto), na Mratibu wa Elimu wa Taasisi ya Elimu Tanzania (TIE), Bw. Charles Manyama (kulia), wakiangalia wakati Mwalimu wa Shule ya Sekondari Hammamni ya mjini Zanzibar, Bw. Yussuf Mwadini Haji, akifanya usajili katika mfumo wa TIE, wakati wa warsha iliyoandaliwa kwa walimu hao, visiwani humo, jana, iliyoandaliwa na Airtel Tanzania kupitia Airtel Africa Foundation, kwa kushirikiana na Shirika la Kimataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF) na Wizara ya Elimu, chini ya mpango wa Airtel SmartWASOMI, unaolenga kuboresha elimu ya kidigitali kwa kuwawezesha walimu na wanafunzi kupata maudhui ya kielimu kupitia maktaba mtandao ya Taasisi ya Elimu Tanzania na Shule Direct bila gharama ya vifurushi vya data.
Ofisa Vifaa vya Intaneti wa Mradi wa Airtel SmartWASOMI, Bw. Harrison Isdory (kulia), akizungumza na baadhi ya walimu wa IT mjini Zanzibar, katika warsha iliyoandaliwa kwa walimu hao, na Airtel Tanzania kupitia Airtel Africa Foundation, kwa kushirikiana na Shirika la Kimataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF) na Wizara ya Elimu, chini ya mpango wa Airtel SmartWASOMI, unaolenga kuboresha elimu ya kidigitali kwa kuwawezesha walimu na wanafunzi kupata maudhui ya kielimu kupitia maktaba mtandao ya Taasisi ya Elimu Tanzania na Shule Direct bila gharama ya vifurushi vya data.
Baadhi ya walimu wa IT mjini Zanzibar hivi karibuni, wakiwa katika warsha iliyoandaliwa kwa walimu hao na Airtel Tanzania kupitia Airtel Africa Foundation, kwa kushirikiana na Shirika la Kimataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF) na Wizara ya Elimu, chini ya mpango wa Airtel SmartWASOMI, unaolenga kuboresha elimu ya kidigitali kwa kuwawezesha walimu na wanafunzi kupata maudhui ya kielimu kupitia maktaba mtandao ya Taasisi ya Elimu Tanzania na Shule Direct bila gharama ya vifurushi vya data.
Share:

Absa Bank Tanzania yasisitiza dhamira yake kuendeleza ukuaji wa uchumi halisi nchini Tanzania

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara, Dk. Suleiman Hassan Serera (kushoto), akikabidhi cheti cha shukurani kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Obedi Laiser, kwa kutambua mchango wa benki hiyo kama mdhamini mkuu wa Kongamano la Biashara la tatu la Maofisa Watendaji Wakuu (200 CEO Business Forum), lililofanyika jijini Dar es Salaam jana.

Benki ya Absa Tanzania imeendelea kusisitiza dhamira yake ya kuendeleza ukuaji wa uchumi halisi wa nchini Tanzania, ikidhamini jukwaa mahsusi linalowakutanisha watendaji wakuu wa makampuni nchini, likijulikana kwa jina la ‘The 200 CEOs Business Forum’.

Jukwaa hilo la ngazi ya juu lilihudhuriwa na Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Viwanda na Biashara, Dkt Suleiman Hassan Serera, sambamba na viongozi wengine waandamizi wa Serikali akiwemo Kamishna wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), na wengineo.

Akizungumza katika hafla hiyo, Mgeni rasmi Dkt. Serera alisitiza umuhimu wa hatua za pamoja ili kupanua ajira na mauzo ya nje huku Benki Kuu ya Tanzania ikitoa mrejesho wa mwelekeo wa uchumi unaosaidia kupanga maamuzi ya bodi, na uwasilisho wa udhamini wa Absa ukugusia suluhisho za kifedha ambazo benki ya Absa inatoa kuwawezesha kampuni kuendesha na kusimamia biashara kwa urahisi ambapo katika mijadala mitatu iliyofanyika ikijikita katika uongozi na utawala bora, afya na uimara wa rasilimali watu, pamoja na njia za ufadhili zinazofungua ukuaji na kuhitimishwa na dira ya PPP.

Akizungumza katika hafla hiyo, Bw. Obedi Laiser, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania alisema Jukwaa hili si mkutano wa mawazo pekee bali ni chombo cha maamuzi yanayosukuma mitaji, kuunda ajira, kurasimisha minyororo ya thamani na kufungua fursa za mauzo ya nje akisema kama Absa, wanajivunia kusimama pamoja na viongozi wa biashara wa Tanzania katika wakati huu nyeti hususani kupitia dhamira yao ya “Kuiwezesha Afrika ya Kesho, Pamoja… hatua moja baada ya nyingine”.

Stori yako ina thamani” si ahadi tu, ndivyo tunavyojitokeza, tumesikiliza kwa makini vipaumbele na mahitaji ya wakurugenzi wakuu, na kwa kujibu tunawasilisha suluhisho zinazochochea kasi ya biashara, zikiwemo Absa Infinite Card, Absa Business Credit Card, Vehicle Asset Finance (VAF), uwezo mpana wa Cash Management & Payments, Trade & Working Capital, Treasury & Risk Management, pamoja na majukwaa yetu ya kidijitali ya benki kwa makampuni yanayosaidia idara za fedha kufanya kazi kwa kasi na udhibiti.

Tunawezesha malengo ya Watendaji wakuu (CEOs) na wajasiriamali kupitia suluhisho bora za kifedha, zenye bei shindani na zinazotolewa kwa wakati na umahiri.” Bw. Laiser aliongeza.

Udhamini huu mkubwa wa Absa unaonesha ushirikiano wa muda mrefu wa benki na Serikali na sekta binafsi wa kuharakisha ukuaji jumuishi. Kuwakutanisha watunga sera na viongozi wa viwanda katika ukumbi mmoja kunawawezesha kuoanisha kanuni, kuandaa miradi inayoweza kufadhiliwa na kuweka mifumo inayochochea uwekezaji kwa kiwango kikubwa - kigeuza dhamira kuwa utekelezaji.

Aidha watendaji hao walipata nafasi za kuzungumza na wafanyakazi wa Absa wakioneshwa suluhisho mbalimbali za kifedha zinazorahisisha maisha yao. Miongono mwa hizo ni huduma ya kifahari inayorahisisha safari za kimataifa kupitia Absa Infinite Card, udhibiti wa matumizi ya kampuni kwa Absa Business Credit Card, udhamini wa manunuzi ya magari binafsi na ya kibiashara kupitia Vehicle & Commercial Asset Finance. Ulinzi wa hatari na mipango ya ukwasi kupitia Bancassurance na Flexi Fixed Deposit, huduma za Prestige na Premier kwa wateja wa hadhi ya juu, Diaspora Banking ikirahisisha miamala ya kuvuka mipaka, na kwa upande wa sekta ya umma, e-Loans, yote yakithibitisha ahadi ya Absa kwamba Stori yako ina thamani.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Obedi Laiser (kushoto), akichangia mada isemayo “Fedha kama chachu ya ukuaji wa biashara Tanzania; Mikakati na Fursa”, wakati wa Kongamano la Biashara la tatu la Maofisa Watendaji Wakuu (200 CEO Business Forum), lililofanyika jijini Dar es Salaam jana.
Share:

Coca-Cola Kwanza hosts Minister of Industry and Trade

The Minister of Industry and Trade Seleman Said Jafo (center) and Coca-Cola Kwanza Ltd Public Affairs, Communications and Sustainability Director Salum Nassor (right) admire a bottle of Coca-Cola drink during the Minister’s tour to the company’s manufacturing plant in Dar es Salaam over the weekend as a part of the government efforts on creating a solid relationship with the private sector. A part from the visit, the Minister also had an opportunity to get insights into the company’s operations, contributions to the Tanzanian economy, and its role in driving shared value creation. Left is Coca-Cola Kwanza Ltd Managing Director David Chait.

Dar es Salaam, Tanzania, Sunday 24 August 2025 - Coca-Cola Kwanza Ltd proudly hosted the Minister of Industry and Trade, Dr Seleman Said Jafo (MP) at its Dar es Salaam facility.

The visit provided a valuable opportunity to showcase the company’s commitment to doing business the right way - guided by integrity, shared value creation, and a deep respect for the communities it serves.

The Minister’s visit included a plant tour and strategic boardroom session, where Coca-Cola Kwanza Ltd, a company in the Coca-Cola Beverages Africa (CCBA) group, shared insights into its operations, contributions to the Tanzanian economy, and its role in driving shared value creation.

This engagement reflects CCBA’s ongoing commitment to strengthening its social license to operate. By leading in environmental, social, and governance (ESG) standards, CCBA aims to create lasting positive impact and contribute to a better shared future.

We believe that by following our values, we can drive sustainable growth and societal progress,” said David Chait, General Manager for Coca-Cola Kwanza Ltd.

People are at the centre of everything we do, from our employees to those who touch our business to the communities we call home. Community involvement allows us to bring positive, measurable change to both the communities in which we operate and to our business,” said David Chait.

Our aspiration is not only to reflect the diversity of the communities where we operate but also to lead and advocate for a better shared future. We aim to create access to equal opportunities and become more inclusive. We embrace differences in backgrounds and support economic inclusion for under-served communities, especially women, youth and people with disabilities.

CCBA looks forward to continuing to build meaningful partnerships that support inclusive economic development and responsible business practices.
Coca-Cola Kwanza Ltd Managing Director David Chait (left) stresses a point to the Minister of Industry and Trade Seleman Said Jafo as he toured the company’s manufacturing plant in Dar es Salaam over the weekend as a part of the government efforts on creating a solid relationship with the private sector. A part from the visit, the Minister also had an opportunity to get insights into the company’s operations, contributions to the Tanzanian economy, and its role in driving shared value creation. Right is Coca-Cola Kwanza Ltd Public Affairs, Communications and Sustainability Director Salum Nassor.
Share:

AGRA, Sahara Accelerator kunufaisha vijana wengi kupitia kilimo

  

Na Mwandishi Wetu

Kilimotech Accelerator kupitia Youth Entrepreneurship for the Future of Food and Agriculture (YEFFA) inayodhaminiwa na shirika la AGRA Tanzania na kutelekelezwa na Sahara Accelerator inatarajia kunufaisha vijana wapatao 265,000 wanaojihusisha na masuala ya kilimo.

Akizungumza wakati wakijadili na vijana kuhusu fursa hiyo jijini Dar es Salaam, Adam Mbyallu wa Sahara Accelerator alisema fursa hiyo itatoa kiasi cha dola milioni 20 kwa bunifu za kilimo zinazojumisha mnyororo wa thamani kwa mazao manne ambayo ni mbogamboga na matunda, alizeti, mpunga na mahindi.

"Tuna hakikisha namna gani tunaweza kusaidia upatikanaji wa vifaa vya kilimo kupitia teknolojia za kidigitali tunasaidia vijana wenye bunifu mbalimbali zinzojibu changamoto za upatikanaji wa vifaa za kilimo," alieleza Mbyallu.

Alisema kupitia bunifu hizo watawapatia vijana hao mafunzo,mentorship na kuwaunganisha wa wadau mbalimbali na kusaidia kwenda shambani kwenye kilimo na kujiuza.
Alifafanua kuwa bunifu wanazotafuta zitajibu changamoto za kilimo kama vifaa,mafundi,masoko,udhibiti wa mazao,uharibifu wa mazao baada ya mavuno changamoto ambazo wadau wa kilimo walisema zipo.

"Maeneo hayo yote kama vinavifaa vya kilimo vingesaidia sana vijana kujiajiri kwenye kilimo kama watajiajiri tunaangalia jinsi ya kuwawezesha kupitia teknolojia ya kidijitali," aliongeza.

Mbyallu alisema ili kufanikisha upatikanaji wa bunifu hizo wamefungua dirisha la usajili wa bunifu kwa muda wa miezi miwili ambapo itafungwa Agosti 18, 2025 na zitachujwa kuangalia kama bunifu hizo zinakidhi vigezo na baada ya hapo watawaunga mkono.

"Tutawaunga mkono Kwa mafunzo,mentorship,changamoto na kuwaunganisha na wadau watakaowasaidia bunifu zao kwenda soko kama wadau wanaouza zana za kilimo,mafundi wa zana za kilimo,wanaotengeneza zana za kilimo,taasisi za fedha na wadau wengine," alisisitiza.
Aliongeza: "Bunifu zitakwenda kwenye mazao manne yamegawiwa katika kanda kuna miradi kulingana na mazao ya eneo mfano Morogoro wanajikita na mbogamboga na alizeti ,Mbeya wana mbogamboga na mpunga, Njombe mbogamboga na mahindi, Singida ni alizeti kila kanda imepewa aina ya zao… tunakwenda kote."
Share:

Airtel Money na Benki ya I&M Wazindua Mpango wa Elimu ya kifedha kuwawezesha Wajasiriamali Wanawake

 

Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Airtel Tanzania, Bw. Charles Kamoto (kulia), akishikana mikono na Mkurugenzi Mtendaji wa I&M Bank Tanzania, Bw. Zahid Mustafa, wakati wa uzinduzi rasmi wa mpango unaolenga kuwawezesha wanawake wajasiriamali nchini kwa elimu ya kifedha na nyenzo nyingine muhimu za kukuza biashara zao. Hafla hiyo ilifanyika jijini Dar es Salaam jana. Katikati ni mmoja wa wanawake wajasiriamali waliohudhuria semina iliyofanyika pamoja na uzinduzi huo, Bi. Virginia Gift.

Airtel Money kwa kushirikiana na Benki ya I&M wamezindua rasmi mpango unaolenga wanawake wajasiriamali ukiwa na malengo ya kuwawezesha wanawake hao nchini kwa elimu ya kifedha na nyenzo muhimu za kukuza biashara zao hivyo kuweza kuboresha maisha yao.

Mpango huu ni sehemu muhimu ya Mkakati wa Uendelevu wa Benki ya I&M Tanzania unaojikita kwenye nguzo tatu kuu ambazo ni ujumuishaji wa kifedha, elimu ya kifedha, na uwajibikaji wa mazingira, ukiendana na Malengo ya Maendeleo Endelevu ya Umoja wa Mataifa (SDGs), hususan SDG 5 (Usawa wa Kijinsia) na SDG 13 (Hatua dhidi ya Mabadiliko ya Tabia nchi).

Kupitia huduma ya Kamilisha, iliyoundwa kwa pamoja kati ya Airtel Money na Benki ya I&M, huwapa wateja uwezo wa kupata mikopo midogo midogo kupitia simu zao ili kukamilisha miamala muhimu kama kutuma pesa au kulipa bili, hata wanapokosa salio kwenye akaunti zao za Airtel Money.

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Mkurugenzi Mtendaji wa Airtel Tanzania, Bw. Charles Kamoto alisema, “kuna matumizi mkubwa ya Airtel Money na ndio tunalenga kujenga uwezo ili kupunguza pengo la matumizi, tunataka kuhakikisha kuwa wateja wetu, hasa wanawake, wana ujasiri na ujuzi wa kutumia huduma za kifedha kidijitali kwa ufanisi.

Kamoto alieleza kuwa zaidi ya asilimia 65 ya watu wazima Tanzania wanakabiliwa na upatikanaji mdogo wa huduma za kifedha, huku wanawake wakiwa katika hali mbaya zaidi.

Kupitia mpango huu, tunasaidia kupunguza pengo la elimu ya kifedha na kusaidia uimara wa kifedha wa muda mrefu, kwa kuwa chini ya asilimia 30 ya wanawake Tanzania wanamiliki simu janja, tumejumuisha mafunzo ya moja kwa moja ya matumizi ya programu za kifedha ili kuwajengea ujasiri watumiaji wapya,” aliongeza Bw. Kamoto.

Katika mafunzo ya siku moja yaliyofanyika jijini Dar es Salaam kama sehemu ya uzinduzi wa mpango huu, zaidi ya wanawake 50 walikusanyika kwa mafunzo shirikishi juu ya usimamizi wa fedha, matumizi ya fedha kidijitali, na mbinu endelevu za biashara, lengo ikiwa siyo tu kutoa ujuzi wa kiufundi, bali pia kuunganisha uwezeshaji wa kiuchumi na maendeleo jumuishi yanayostahimili mabadiliko ya tabianchi.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa I&M Bank Tanzania, Bw. Zahid Mustafa alisema, “Hii ni sehemu ya dhima yetu ya kufanya benki kuwa jukwaa la kuleta mabadiliko, tunajivunia kuongoza mpango huu kwa ushirikiano na Airtel Tanzania, leo tukianza safari hii kwa kutoa mafunzo ya siku moja ya elimu ya kifedha kwa wanawake 60 hapa Dar es Salaam, kwa udhamini kamili, mtaala wa mafunzo haya umetayarishwa kwa kushirikiana na Grant Thornton na utaendelea kuboreshwa kwa kuzingatia mrejesho kutoka kwa washiriki.

Licha ya ukuaji wa huduma za fedha kidijitali, biashara ndogondogo zinazoongozwa na wanawake nchini bado zinakosa huduma rasmi kutokana na ukosefu wa elimu na mifumo ya kifedha. Mpango huu unalenga kuziba pengo hilo kwa kuwapa wanawake ujuzi wa vitendo na ujasiri zaidi kushiriki katika mfumo wa kifedha.

Tangu kuanzishwa kwake, huduma ya Kamilisha imekwisha toa mikopo yenye thamani ya zaidi ya TZS bilioni 392, ambapo asilimia 46 ya mikopo hiyo imekwenda kwa wanawake. Hadi sasa, zaidi ya Watanzania milioni tano wameingia kwenye mfumo rasmi wa kifedha kupitia huduma hii,” aliongeza Mustafa.

Kama sehemu ya mpango huu, Benki ya I&M imeahidi kupanda mti mmoja kwa kila wanawake 100 watakaokopeshwa, na inalenga kupanda miti 8,000 kwa mwaka. Jitihada hizi za kimazingira zinatekelezwa kwa kushirikiana na taasisi ya Africa Transformation Initiative (ATI), ambayo itasimamia upatikanaji, upandaji, na ufuatiliaji wa miti hiyo nchini Tanzania kwa kipindi cha miaka mitatu ijayo.
Mkurugenzi wa Airtel Money, Bw. Andrew Rugamba akizungumza katika hafla ya uzinduzi rasmi wa mpango unaolenga kuwawezesha wanawake wajasiriamali nchini kwa elimu ya kifedha na nyenzo nyingine muhimu za kukuza biashara zao katika hafla hiyo jijini Dar es Salaam jana. Mpango huo unafanyika kwa ushirikiano wa Airtel Money na I&M Bank Tanzania.
Mkurugenzi Mtendaji wa Airtel Tanzania, Bw. Charles Kamoto, akizungumza, katika hafla ya uzinduzi rasmi wa mpango unaolenga kuwawezesha wanawake wajasiriamali nchini kwa elimu ya kifedha na nyenzo nyingine muhimu za kukuza biashara zao katika hafla hiyo jijini Dar es Salaam jana. Mpango huo unafanyika kwa ushirikiano wa Airtel Money na I&M Bank Tanzania.
Mkurugenzi Mtendaji wa I&M Bank Tanzania, Bw. Zahid Mustafa, akizungumza, katika hafla ya uzinduzi rasmi wa mpango unaolenga kuwawezesha wanawake wajasiriamali nchini kwa elimu ya kifedha na nyenzo nyingine muhimu za kukuza biashara zao katika hafla hiyo jijini Dar es Salaam jana. Mpango huo unafanyika kwa ushirikiano wa benki ya I&M na Airtel Money.
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Airtel Tanzania, Bw. Charles Kamoto (walioketi wa pili kulia), Mkurugenzi Mtendaji wa I&M Bank Tanzania, Bw. Zahid Mustafa (wa pili kushoto), Mkurugenzi wa Airtel Money, Bw. Andrew Rugamba (kushoto), na Mkurugenzi Mtendaji wa Grant Thornton Tanzania, Bw. Muntazir Fazel (kulia), wakipozi mbele ya wapiga picha, mara baada ya semina na uzinduzi rasmi wa mpango unaolenga kuwawezesha wanawake wajasiriamali nchini kwa elimu ya kifedha hivyo kukuza biashara zao. Hafla hiyo iliyofanyika jijini Dar es Salaam jana. Wengine ni baadhi ya washiriki na wawezeshaji wa semina hiyo.
Share:

LILIAN-FAVOUR MAKAWA

LILIAN-FAVOUR MAKAWA

Popular Posts

Blog Archive

Labels

Recent Posts

Label Cloud

BIASHARA (331) BURUDANI (4) KIMATAIFA (10) KITAIFA (129) MICHEZO (41) SIASA (3)

Pages