Huawei: Uboreshaji Wa Uwekezaji Ili Kukuza Uthibiti Wa Biashara

   Eric%2BXuMwenyekiti wa kampuni ya Huawei Bw Eric Xu

Kampuni ya mawasiliano ya Huawei imebainisha mkakati wake wa kuboresha akaunti yake ya uwekezaji ili kukuza uthabiti na kukabiliana na hali ya mashaka katika biashara inayoletwa na mvutano wa kijiografia, kuibuka tena kwa virusi vya COVID-19 pamoja na kuzuiwa kufanya biashara Marekani.


Taarifa hiyo imetolewa na Mwenyekiti wa kampuni hiyo Bw Eric Xu, wakati akiwasilisha hotuba kuu katika Mkutano  wa 18 wa Wachambuzi wa kidunia. Zaidi ya watu 400, ukijumuisha wachambuzi wa tasnia na wa kifedha, viongozi wa maoni na wawakilishi wa vyombo vya habari walishiriki katika mkutano huo wa siku 3 ulioanza liyoanza Aprili 12 hadi 14, kauli mbiu ikiwa "Ujenzi wa Ulimwengu Wa Maarifa na Uliounganishwa Kikamilifu."

“Uthibiti wa kibiashara ndio kanuni inayotuongoza. Tunataka kuongeza uimara wa biashara yetu yote, na tangu mwaka jana tumekuwa tukifanya kazi kuboresha uwekezaji letu tukiwa na lengo hili akilini.” alisema Eric Xu.

Ripoti ya mwaka 2020 ya Huawei inaonyesha mapato yaliotokana na mauzo ya kampuni hiyo mnamo 2020 yanafika CNY891.4 bilioni, ikiwa ni ukuaji wa asilimia 3.8 kulinganisha na mwaka uliopita, huku faida yake kamili ilifikia CNY64.6 bilioni, ambayo ukilinganisha na ripoti ya mwaka 2019 ni ukuaji wa asilimia 3.2.

Eric Xu alisema moja ya vipaumbele ni kuongeza zaidi uwezo wa uhandisi wa programu za Huawei. "Tunatafuta fursa mpya za kibiashara katika sekta ya programu. Tunapopata kitu kinachotufaa, tutaongeza uwekezaji ili kuongeza ushiriki wa huduma za program katika vyanzo vyetu vya mapato. "alisema Eric Xu.

Mwisho wa Novemba 2018, Huawei iliamua kuwekeza kiasi cha dola za kimarekani bilioni 2 katika kuboresha uwezo wao wa uhandisi wa programu. Eric Xu alisema kampuni hiyo "inafurahishwa na matokeo hadi sasa".

Programu kwa ajili ya magari kujiendesha ni mojawapo ya malengo makuu ya uwekezaji ndani ya kampuni. Kulingana na Eric Xu, programu hiyo ipo mbioni kufikia hatua ambapo magari yatajiendesha yenyewe bila dereva kujishughulisha kwa namna yoyote ile.

"Pamoja na uwekezaji mkubwa, matumaini yetu ni kusukuma mwenendo huu mbele kwani program hizi zinawezesha ujumuishaji wa tasnia ya magari na ICT, ambayo nayo hutengeneza fursa za kimkakati za muda mrefu kwa Huawei. Mara baada ya ukamilifu wa program hiyo, kutakua na mabadiliko katika sekta zote zilizo karibu ambayo yataleta mabadiliko makubwa zaidi katika miaka 10 ijayo.” Alisema Mwenyekiti huyo.

Share:

Benki Ya Exim Yajizatiti na 'Mteja Kwanza' Utoaji Huduma Za Kidigitali.

   

Benki Ya Exim Yajizatiti na  'Mteja Kwanza' Utoaji Huduma Za Kidigitali.


Dar es Salaam: Aprili 18, 2021: Benki ya Exim imesisitiza kuhusu mkakati wake wa kuwekeza na kutanguliza zaidi maslahi ya wateja wake hususani katika mipango yake muhimu ikiwemo ile ya  uvumbuzi na utoaji wa huduma kwa wateja.


Akizungumza kuhusiana na mkakati huo jijini Dar es Salaam mwishoni nwa wiki, Ofisa Mtandaji Mkuu wa Benki hiyo Bw Jaffari Matundu alisisitiza kuwa benki hiyo imejizatiti kuhakikisha kwamba wateja wake wananufaika zaidi na ukuaji wa technolojia katika utoaji wa huduma za kibenki.


"Lengo ni kuhakikisha kwamba benki ya Exim tunatumia vyema huu ukuaji wa kidigitali katika utoaji wa huduma za kibenki kwa wateja wetu…lengo ni kuona wanaridhishwa na huduma zetu na wanazifurahia. Tunaamini kwamba furaha na ukuaji wao ndio biashara yetu,'' alisema.


Aliongeza kuwa agenda ya uvumbuzi imebaki kuwa kipaumbele cha benki hiyo katika kuelekea kwenye lengo lake la msingi ambalo ni kuifanya benki hiyo kuwa ya kidigitali zaidi huku kipaumbele kikibaki kuwa ni 'mteja kwanza'.


Katika kabiliana na changamoto ya COVID 19 benki hiyo mapema mwaka jana ilizindua kampeni ya "Maliza Kirahisi Kidigitali' iliyodumu katika kipindi cha mwaka mmoja ikilenga kubadilisha tabia ya wateja na kuongeza kasi ya mabadiliko yanayoendelea ya nchi kutoka katika kutumia pesa taslimu kwenda malipo ya dijiti.


"Kampeni hiyo pia inakwenda sambamba na kuunga mkono mkakati wa Serikali wa kuhamasisha matumizi ya kidigitali katika kufanya miamala uchumi pamoja na  kuhakikisha wateja wetu wanahudumiwa bila kwenda kwenye matawi" aliongezea.


Ili kurahisisha zaidi miamala na kuifanya bora zaidi na rahisi kwa wateja, benki ina chaguzi kadhaa za huduma kupitia simu na kidigitali ambazo wateja wanaweza kuzitumia kupata huduma na kufanya miamala muda wowowte katika siku saba za wiki Katika kuhakikisha kwamba huduma za benki hiyo zinakuwa jumuishi, huduma ya USSD ndio ilihusika katika kuipamba kampeni hiyo.


''Kila mwingiliano na mteja ni nafasi kwetu kuwaelewa vizuri wateja wetu na namna ya kuwahudimia kulingana na mahitaji yao. Tunapoendelea kupanua huduma zetu, tunaweza kuona jinsi kila huduma inatimiza mahitaji ya watumiaji. Ni suala la kuendelea kujifunza na uvumbuzi. ’


"Zaidi, kusikiliza kwa karibu maoni ya wateja hutusaidia kupata mrejesho unaotuwezesha kufanya maboresho na uvumbuzi ili kuimarisha huduma tunazowapatia. Lengo ni kufanya maisha yao yawe rahisi. Tunazingatia urahisi wa matumizi, na kufanya huduma zetu kuwa thabiti, salama, na haraka.'' alisema.

Share:

BENKI YA NBC YATINGA KIBITI YAWAPA SOMO WAJASIRIAMALI WANAWAKE

  nbc%2B1

Mkuu wa Wilaya ya Kibiti Bw Gullamhussein Kifu (watatukushoto) akipokea msaada wa madawati  viti pamoja na meza 500 kwa ajili ya shule za wilaya hiyo kutoka kwa Mkurugenzi wa Wateja wa wadogo wa Benki ya NBC Bw Elibariki Masuke(wa pili kulia) msaada huo ukilenga kuboresha sekta ya elimu  Wengine pichani ni Mbunge wa jimbo la Kibiti Bw Twaha Mpembenwe (kushoto),Mkurugenzi wa Idara ya Masoko na Mawasiliano wa Benki ya NBC Bi Neema Singo (wa pili kushoto) pamoja na Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi CCM Wilaya ya Kibiti Bw Abduljabir Marombwa hafla hiyo imefanyika hivi karibuni wilayani kibiti.nbc%2B3

Mkurugenzi wa Wateja wa wadogo wa benki ya NBC Bw Elibariki Masuke akizungumza na wajasiriamali wanawake wilayani Kibiti wakati wa mafunzo ya kibiashara na ujasiriamali kwa  wanawake wajasiriamali 150 wilayani humo ili kuwajengea uwezo wa kuemdesha biashara zao kwa ufanisi huku wakizingatia nidhamu ya fedha kabla hawajapatiwa mikopokwa ajili ya kukuza mitaji yao na benki hiyo.
NBC%2B5
M
eneja Bidhaa na Huduma za Kibenki kutoka Benki ya NBC Bw Jonathan Bitababaje akitoa mafunzo kwa wajasiriamali hao.

Kibiti, Pwani:  April 17, 2021: Benki ya Taifa ya Biashara (NBC) imetoa msaada wa madawati 250, viti viti pamoja na meza 250 wilayani Kibiti mkoni Pwani ikiwa ni sehemu ya Mpango wa kipekee wa uwajibikaji wa Jamii (CSR) ambao unaplenga kuchangia utoaji wa elimu bora nchini.

 

Zaidi, benki hiyo pia imetoa mafunzo ya kibiashara na ujasiriamali kwa  wanawake wajasiriamali 150 wilayani humo ili kuwajengea uwezo wa kuemdesha biashara zao kwa ufanisi huku wakizingatia nidhamu ya fedha kabla hawajapatiwa mikopokwa ajili ya kukuza mitaji yao.

 

Madawati hayo yalikabidhiwa na Mkurugenzi wa Idara ya wateja wadogo wa benki hiyo Bw Elibariki Masuke wakati wa hafla fupi ya makabidhiano iliyofanyika kwenye ofisi ya Mkuu wa Wilaya Hiyo Bw Gullamhussein Kifu . Hafla hiyo pia ilihudhuriwa na Mbunge wa jimbo la Kibiti Bw Twaha Mpembenwe pamoja na maafisa wengine wa wilaya hiyo akiwemo  Mkurugenzi Mtendaji.

 

Bwana Masuke alisema kuwa benki hiyo imejitolea kusaidia katika kuboresha ustawi wa jamii kupitia misaada ya kijamii ikiwemo elimu na kwamba wameguswa sana na suala la changamoto ya madawatikwenye baadhi ya maeneo hapa nchini sababu iliyosababisha wao kuchukua hatua hiyo ili kuboresha  zaidi sekta hiyomuhimu.

 

"Ni furaha kwetu kuwa sehemu ya kutatua changamoto kwenye sekta muhimu kama hii. Kupitia ushirikiano na ushawishi tunaoupata kutoka kwa Mbunge wa Kibiti na ofisi ya Mkuu wa wilaya tunaahidi kuendelea kushirikiana na jamii ya wana Kibiti huku pia tukifikiria namna kufungua tawi letu wilayani  Kibiti kufuatia fursa mbalimbali tunazoziona ikiwemo kilimo na mradi wa kituo cha kupozea umeme wa Mradi wa Bwawa la Mwalimu Nyerere,’’ alisema.

 

Alishauri pia wanafunzi na walimu watakaonufaika na msaada huo kutunza madawati na meza hizo ili viweze kutumika kwa muda mrefu na hivyo kusaidia walengwa wengi zaidi.

 

Kuhusu mafunzo kwa wajasiriamali wanawake  Bwana Masuke alisema kuwa miongoni mwa sababu zinazokwamisha utoaji wa mikopo kwa wajasiriamali wengi ni pamoja na wao kuendesha biashara zao bila kuzingatia misingi ya kifedha ikiwemo kutunza kumbukumbu za mahesabu ikiwemo mapato na matumizi.

 

Kwa mujibu wa Bw Masuke ni kutokana na uwepo wa changamoto hiyo ndio sababu benki hiyo imekuwa ikishirikiana na taasisi nyingine ikiwemo TanTrade, SIDO, VETA na washauri binafsi kuelimisha wajasiriamali kuhusu namna bora ya kusimamia na kuendesha biashara zao ili kuwajengea uwezo kabla ya kuwapatia mikopo.

 

"Tumekuwa tukishirikiana na washirika wengine kutoa mafunzo kwa wajasiriamali na wafanyabiashara kwenye maeneo kama usimamizi wa hesabu, utunzaji wa vitabu na uongozi, ili tuwaweke vizuri kwa ufikiaji rahisi wa mikopo", Masuke alisema.

 

Akizungumza mara tu baada ya kupokea msaada huo Mkuu wa Wilaya ya Kibiti Bw Gullamhussein Kifu pamoja na kuishukuru benki ya NBC kwa kutoa msaada kwa wakati haswa unaohitajika, aliiomba benki hiyo ifungue tawi lake wilayani humo mapema iwezeknavyo ili iweze kuwasaidia wakulima na wafanyabiashara husani wadogo.

 

"Msaada huu utasaidia kupunguza changamoto ya uhaba wa madawati katika baadhi ya shule zetu…tunashukuru sana NBC tunaomba muendelee kusaidia kwenye maeneo mengine pia ikiwemo sekta ya afya ." Alisema.

 

Akizungumzia mafunzo kwa wajasiriamali wanawake wilayani humo Bw Kifu alitoa wito kwa washiriki kuhakikisha wanayatumia vyema kwa kuwa yanalenga kuwasaidia katika upatikanaji wa mikopo sambamba na kuendesha biashara zao kwa ufanisi na kwa faida

 

“Kibiti ni wilaya  changa inayohitaji watu wake ili kuendelea. Kabla hatujapokea wawekezaji kutoka nje ni lazima tuanze sisi wenyewe humu ndani. Kupitia mafunzo haya tunakwenda kupata wajasiriamali na wafanyabaishara wenye weledi wa kutosha kutambua fursa zilizopo na kuzitumia,’’ alisema.


Kwa upande wake Mbunge wa jimbo hilo Bw Twaha Mpembenwe aliiomba benki hiyo iendelee kuwekeza zaidi wilayani humo kwa kufungua tawi lake sambamba na kuwasaidia wajasiriamali na wakulima hususani wa zao la ufuta pamoja na vijana ambao kwasasa wanakibiliwa na changamoto ya huduma za kifedhaikiwemo mikopo na elimu ya biashara na kilimo cha kisasa.

Share:

BILIONI 20 KUTUMIKA KUWANUFAISHA WAKULIMA

  _E1A1886Mkurugenzi wa Biashara wa Benki ya Taifa ya Biashara NBC Elvis Ndunguru  (katikati), akizungumza na waandishi wa habari wakati wa kutia saini mikataba kwaajili kuingia makubaliano yakufanya kazi pamoja na Benki ya Taifa ya Biashara NBC yenyelengo la  kuwawezesha maelfu ya wakulima wadogo katika minyororo ya thamani ya kilimo wengine pichani kulia ni  maofisa wa Benki ya TADB._E1A1889Mkurugenzi wa Biashara wa Benki ya Taifa ya Biashara NBC ElvisNdunguru (kulia), akizungumza na waandishi wa habari wakati wa  hafla yakuingia makubaliano  yakufanya kazi pamoja na Benki ya Maendeleo ya kilimo TADB yenyelengo la  kuwawezesha maelfu ya wakulima wadogo katika minyororo ya thamani ya kilimo kushoto ni Mkurugenzi wa Fedha wa Benki ya Maendeleo ya Kilimo TADB, Derick Lugemala.

_E1A1922

Mkurugenzi wa Biashara wa Benki ya Taifa ya Biashara NBC ElvisNdunguru wapili (kushoto waliokaa) pamoja na Mkurugenzi wa Fedha wa Benki ya Maendeleo ya Kilimo TADB, Derick Lugemala wakitia saini Mkataba wa makubaliano wa kufanya kazi pamoja kwaajili ya kuwawezesha wakulima wadogo katika minyororo ya dhamani ya kilimo wanaoshuhudia kulia ni Meneja wa Mfuko maalum wa dhamana kwa wakulima wadodo kutoka TADB  Asha Tarimo pamoja na Mkurugenzi wa sheria wa TADB Edson Rwechungura Picha na Brian Peterdownloaddownload




TADB na NBC kuwawezesha maelfu ya wakulima kupata mikopo nafuu

·         Zadhamiria kukuza mitaji na kuleta mageuzi katika kilimo, uvuvi na ufugaji

Dar es Salaam. Jumanne, 13 April, 2021. Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) imeingia katika makubaliano na benki ya biashara NBC kuwawezesha maelfu ya wakulima wadogo wadogo nchini kupata mikopo yenye riba nafuu ili kuweza kukuza biashara zao na kufanya mageuzi katika sekta ya kilimo, uvuvi na ufugaji.


Makubaliano haya, yaliyosainiwa leo katika makao makuu ya TADB jijini Dar es Salaam, yataiwezesha benki hiyo kutoa dhamana kwa wakulima watakaoenda kuomba mikopo NBC kufanya shughuli za kilimo, ufugaji pamoja na uvuvi kwa riba nafuu ya asilimia kumi na nne (14%) tu. Dhamana hii inaratibiwa na TADB chini ya mfuko maalum wa dhamana kwa wakulima wadogo nchini ‘SCGS’.  


“Kwa muda mrefu tumeona wakulima wetu nchini wakipata changamoto ya mitaji. Wengi wakilazimika kukopa kwa riba za kibiashara ambapo wengi wao wamekuwa wakipata changamoto ya kuhimili riba hizo kubwa. Hivyo, kama taasisi ya maendeleo ya kifedha, kupitia mfuko wa dhamana kwa wakulima wadogo, tumeona umuhimu wa kutoa mikopo hii nafuu kwa kushirikiana na NBC ili kuwawezesha wakulima wengi zaidi kupata mitaji,” alieleza Derick Lugemala, Mkurugenzi wa Fedha kutoka TADB.


Kwa upande wake, Elvis Ndunguru, Mkuu wa Biashara za Kibenki kutoka NBC, alisema kwamba mikopo hiyo watakayokuwa wanatoa kwa dhamana ya TADB itawawezesha kuwakopesha wakulima wadogo mikopo ya mtaji hadi kiwango cha shilingi 50 milioni kwa mkulima mmoja mmoja, shilingi 500 milioni kwa vikundi na vyama vya wakulima, na hadi shilingi 1 bilioni kwa kampuni ambazo miradi yake inawaunganisha na kuwanufaisha wakulima wadogo wengi.


Akieleza vigezo vya kupata mikopo hiyo, Ndunguru alisema:

“Ili kukidhi vigezo vya kupata mikopo hii, mkulima anahitajika kuwa amefanya biashara ya kilimo kwa kipindi kisichopungua miaka mitatu, awe na leseni ya biashara. Awe na kumbukumbu ya taarifa za kifedha. Mikopo hii inapatikana katika matawi yote ya arobaini na saba (47) ya NBC yaliyopo Tanzania bara na Zanzibar. Tunatoa rai kwa wakulima wote wadogo kuchangamkia fursa hii.”

 

Hapo awali, Lugemala alisema, lengo la mikopo hii yenye masharti nafuu ni kuchagiza benki za kibiashara na taasisi za kifedha kutoa mikopo zaidi kwa wakulima na kuwezesha ukuaji wa minyororo yote ya thamani yanayohusiana na kilimo, uvuvi na ufugaji nchini.


“Mpaka Desemba 2020, mfuko huu wa dhamana ulikwisha toa mikopo katika miradi ya kilimo, uvuvi na ufugaji yenye thamani ya shilingi bilioni 66 na kuwafikia wanufaikaji zaidi ya 9000 moja kwa moja na wasionufaika moja kwa moja 750,000. Baadhi ya miradi tuliyowezesha ni pamoja na kwenye korosho, mpunga, kahawa, miwa, mahindi, mihogo, pamba na ufugaji wa kuku,” alifafanua Lugemala.


Kutokana na taarifa kutoka TADB, mfuko huu wa dhamana ulianzishwa Februari 2018. Na katika kipindi cha miaka mitatu sasa, TADB imeshashirikiana na benki na taasisi za kifedha kama NMB, CRDB, Azania, Benki ya Posta (TPB), Stanbic, FINCA Microfinance, UCHUMI Commercial Bank, Tandahimba Community Bank (TACOBA), Mufindi Community Bank (MUCOBA) na NBC.


“TADB inaamini kwamba kupitia mtandao huu wa ushirikiano wa kimkakati, idadi kubwa ya wakulima wadogo watafikiwa na kuwezeshwa,” alisisitiza Lugemala.

xxxx Mwisho xxxx

Kuhusu TADB:

Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) ni benki ya umma yenye malengo ya kuongoza mikakati ya kujenga uwezo na mipango ya kuimarisha mnyororo wa thamani wa kilimo na kuunga mkono Serikali ya Tanzania katika kuunda na kutekeleza sera za kilimo na mikopo ya vijijini. Mpaka Desemba 2020, TADB imekwisha nufaisha wakulima 1,788,202 na kutoa mikopo yenye thamani ya shilingi bilioni 300 katika mikoa 26 ya Tanzania Bara na Zanzibar. Mikopo hii imewezesha kukua kwa minyororo ya thamani kwenye sekta ya kilimo, mifugo na uvuvi.

 

Kuhusu NBC:

Benki ya NBC ni benki pekee ya kimataifa inayopatikana katika mikoa na maeneo mbalimbali nchini ikiwa na matawi 47 na mashine za ATM zaidi ya 180, pamoja na Mawaka zaidi ya 3,000. Benki ya NBC inatoa huduma mbalimbali za ukusanyaji fedha za huduma nyingine za kibenki kwa wateja mbalimbali kwa zaidi ya miaka 54 nchini . Benki ya NBC sasa imeajiri wafanyakazi takriban 1,100 nchi nzima.

 

Kwa maelezo zaidi au msaada tupigie +255 76 898 4000/4011 | +255 22 219 3000 | +255 22 551 1000 or email us NBC_Marketingdepartment@nbc.co.tz

Kwa taarifa zaidi:

Amani Nkurlu, Meneja Mahusiano na Masoko – TADB

Barua pepe: amani.nkurlu@tadb.co.tz                                                                                                                                Simu: +255 754 878 385 au +255 712 223 839

 

David Raymond, Meneja Mwandamizi-Chapa na Mawasiliano

National Bank of Commerce Limited (NBC)

Barua pepe: david.raymond@nbc.co.tz

Simu: +255 717 742832

Share:

Benki ya NBC yawafunda Wanawake Kuhusu Ubora wa Bidhaa ya Mikopo

 PIC%2B1.

Mkurugenzi wa Taasisi ya Wafanyabiashara wanawake Tanzania (TABWA) Bi Noreen Mawala (kushoto), akikabidhi zawadi kwa niamba ya wanawake wajasiliamali nchini kwenda kwa Meneja Mahusiano wa Benki ya NBC, Bi Consolatha Shayo (Kulia) na Meneja Bidhaa na Huduma za Kibenki kutoka Benki ya hiyo Bw Jonathan Bitababaje (katikati) ikiwa ni ishara ya kutambua mchango wa benki hiyo katika kuwasaidia na kuwawezesha wanawake wajasiliamali nchini. Makabidhiano hayo yalifanyika jana wakati wa kufunga Maonesho ya Wafanyabiashara wanawake Tanzania yaliyodhaminiwa na Benki ya NBC, yaliyofanyika jijini Dar es Salaam.PIC%2B2.Meneja Mahusiano wa Benki ya NBC, Bi Consolatha Shayo akizungumza WANAWAKE WAFANYA BIASHARA  na washiriki wa maonesho hayo waliohudhulia mafunzo ya ujasiliamali yaliyodhaminiwa na benki ya NBC kwa kushirikiana na TABWA pamoja na wadau wengine ili kuwatia shime wanawake katika ujasiliamaliPIC%2B9.

Meneja Mahusiano wa Benki ya NBC, Bi Consolatha Shayo (kushoto), akikabidhi cheti cha ushiriki wa mafunzo hayo kwa mmoja kati ya washiriki  waliohudhuria semina hiyo.


Dar es Salaam: Machi 8, 2021: Wanawake wajasiliamali na wafanyabiashara nchini wameshauriwa kuongeza jitiahada zao zaidi katika kuboresha zaidi mawazo ya biashara sambamba na kuongeza ubora za wa bidhaa zao ili kuongeza ushawishi kwa taasisi za kifedha nchini ziweze kuwakopesha kwa urahisi.


Akizungumza wakati wa kufunga Maonesho ya Wafanyabiashara wanawake Tanzania yaliyofanyika jijini Dar es Salaam kwa siku nne, Meneja Mahusiano wa Benki ya NBC, Bi Consolatha Shayo alisema taasisi za kifedha zinashawishika zaidi kutoa mikopo kwa kuzingatia ubora wa wazo la biashara na sio jina au jinsia ya mkopaji.


Alisema hiyo ndio sababu benki hiyo imekuwa mstari wa mbele kuhakikisha inaendelea kuwaongezea ujuzi wajasiliamali hao ili kuboresha mawazo na bidhaa zao ili kuwajengea uwezo utakaowezesha kufanya biashara zao kwa weledi na kutengeneza faida itayowawezesha kurejesha mikopo yao.


“Ndio maana kupitia wataalamu ambao tunawatumia kutoa elimu kwa wajasiliamali kupitia maonesho kama haya, tumekuwa tukifundisha na kusisitiza sana juu ya umuhimu wa kujenga zaidi majina ya bidhaa zao kuliko majina yao binafsi kwa kuwa taasisi za kifedha zinatazama zaidi biashara zao na sio jinsia wala majina yao binafsi,’’ alisema  Consolatha.


Pamoja na kudhamini maonesho hayo, benki hiyo pia iliandaa programu kadhaa za mafunzo kwa wajasiliamali ikiwemo kliniki ya biashara kwa kushirikisha taasisi na mamlaka mbalimbali ikiwemo Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (Brela) na Shirika la Viwango Tanzania (TBS).


Zaidi benki hiyo ilitumia fursa hiyo kutangaza huduma zake mahususi kwa ajili ya wanawake na wajasiliamali zikiwemo akaunti za NBC Kua Nasi na akaunti mpya ya Johari.


“NBC Kua Nasi ni akaunti maalum kabisa kwa wote wanaojihusisha na biashara ndogo ndogo kama vile mama na baba lishe, wenye maduka ya reja reja, wasindikaji wa vyakula na mazao, bodaboda, wazabuni wa taasisi mbalimbali wakati akaunti ya Johari ni mahususi kwa ajili ya wanawake na inawezesha kuweka akiba kidogo kidogo kwa kianzio cha shilingi 10,000 tu. Akaunti zote hizi hazina makato ya mwezi,’’ alisema.


Kwa upande wake Mkurugenzi wa Taasisi ya Wafanyabiashara wanawake Tanzania (TABWA) Bi Noreen Mawala ambae taasisi yake ndio iliratibu maonesho hayo pamoja na kuipongeza benki ya NBC pamoja na wadau wengine kwa kufanikisha maonesho hayo, alisema taasisi hiyo kwasasa inaandaa safari ya mafunzo na maonesho ya biashara katika nchi za Oman na Comoro ili kutoa fursa kwa wafanyabiashara hao kutangaza biashara zao katika mataifa hayo.


“Baada ya mafanikio kupitia maonesho haya yaliyokwenda sambamba na maadhimisho ya siku ya mwanamke Duniani  tunatarajia kuwa na safari za maonesho ya biashara zetu katika nchi za Oman na Comoro ili kufungua milango zaidi ya kutangaza biashara zetu nje nchi,’’ alisema.

Share:

BENKI YA NBC YADHAMINI MAONESHO YA WAFANYA BIASHARA WANAWAKE TANZANIA

Waziri wa Nchi Ofisi ya Raisi (Uwekezaji) Kitila Mkumbo (kushoto), akizungumza wakati wa hafla ya uzinduzi wa wafanya biashara wanawake yaliyodhaminiwa na Benki ya NBC yenye kauli mbiu MWANAMKE MILIKI KIWANDA KWA UCHUMI ENDELEVU, maonesho yaliyozinduliwa na waziri huyo katika viwanja vya mlimani city jijini Dar es Salaam. Kulia ni Mkuu wa Kitengo cha Wajasiliamali wa Benki ya Taifa ya Biashara NBC Mussa Mwinyidaho.
Mkuu wa Kitengo cha Wajasiliamali wa Benki ya Taifa ya Biashara NBC Mussa Mwinyidaho akizungumza wakati wa hafla ya uzinduzi wa maonesho ya wafanya biashara wanawake Tanzania yaliyodhaminiwa na Benki hiyo ambapo katika uzinguzi huo mgeni rasmi alikuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Raisi (Uwekezaji) Kitila Mkumbo halfla ya uzinduzi huo umefanyika katika viwanja vya mlimani city jijini Dar es Saalam.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Raisi (Uwekezaji) Kitila Mkumbo (katikati) akipokea zawadi ya kifungashio kilichotengenezwa na wajasiliamali wakitanzania wakati wa hafla ya uzinduzi wa maonesho ya wafanya bishara wanawakeTanzania yaliyodhaminiwa na Benki ya NBC kutoka kwa Mkurugenzi wa Chama cha Wafanyabiashara Tanzania (Tabwa), Noreen Mawalla (kushoto) ni Mkuu wa Kitengo cha Wajasiliamali wa Benki ya Taifa ya Biashara NBC Mussa Mwinyidaho
Baadhi ya wanawake waliohudhulia hafla ya uzinduzi huo wakifurahia jambo kutoka kwa mgeni rasmi.
Picha ya pamoja waziri pamoja na wadhamini wa maonesho hayo.

Serikali imewataka wanawake kuchangamkia fursa zinazotolewa katika mikoa wanayoishi ili kutatua changamoto mbalimbali zinazowakabili hasa kwenye swala zima la mitaji.

Hayo yameelezwa leo jijini Dar es Salaam na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (uwekezaji), Profesa Kitila Mkumbo ambae pia ni Mbunge wa Jimbo la Ubumgo wakati alipoalikwa kuwa Mgeni rasmi na kuzindua maonyesho ya biashara za wanawake Tanzania yaliyodhaminiwa na Benki ya Taifa ya bishara NBC,kwa lengo mahususi la kuwainua wanawake kiuchumi yanayofanyika Mlimani City kwa siku tatu mfurulizo.

Waziri Mkumbo amesema Serikali kwa kutambua umuhimu na mchango wa maendeleo kwa wanawake kwa Taifa, letu na Serikali inayoongozwa na jemedali wetu Rais John Pombe Magufuli wameanzisha dirisha maalumu la mikopo kwa halmashauri zote nchini kwa ajili ya kuwainua wanawake na vijana.

"Tunatambua jitihada zenu na malengo yenu lakini Serikali tunatoa wito kwa wanawake wote nchini kuchangamkia fursa zinazotolewa kupitia mikoa yao ziweze kuwasaidia kwenye changamoto zinazowakabili,” amesema Waziri Mkumbo.

Waziri huyo pia ameishukuru Benki ya Taifa ya Biashara NBC ambayo ndio mdhamini mkuu wa maonesho hayo kwa uzalendo walioufanya kutambua kuwa hakuna maendeleo bila wanawake na kulibeba hili ili wanawake waweze na vijana waweze kwenda sawa na spidi ya uchumi wa kati na kuzitaka Taasisi nyengine kuiga mfano huo kwani utaleta matokeo nyanya katika sekta ya uwekezaji.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Chama cha Wafanyabiashara Tanzania (Tabwa), Noreen Mawalla aliiomba Serikali kuwasaidia majengo ya wazi ili wanawake wafanyie biashara zao katika mazingira mazuri na salama yatakayowawezesha kulipa kodi kwa wakati.

Nae Mkuu wa Kitengo cha Wajasiliamali wa Benki ya Taifa ya Biashara NBC Mussa Mwinyidaho katika uzinduzi huo leo, amemwambia Waziri kuwa lengo kuu la udha mini wa benki hiyo kwa maoneso ya wanawake wafanya biashara tanzania ni kuwawezesha wajasiliamari wadogo na wa kati ambao ndiyo walengwa wakuu wa maonesho haya.

NBC ni Benki inayo wajali wateja wake na watanzania wote kwa ujumla hivyo ili waweze kuwa wafanyabiashara bora nilazima wapate elimu ya kifedha hivyo tunawakaribisha NBC waje wapate elimu pia kujionea huduma mbalimbali zinazotolewa na Benki hiyo alisema mwinyidaho.
Share:

AKIBA COMMERCIAL BANK YAPATA MBIA WA KIMKAKATI (STRATEGIC INVESTOR) AMBAYE NI NATIONAL BANK OF MALAWI YA NCHINI MALAWI

01
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Akiba Commercial Bank, Juliana Swai (kulia), akizungumza na wanahabari wakati wa hafla ya kutangaza kuwa Benki hiyo imepata mbia wa kimkakati ambaye ni National Bank of Malawi. Kushoto ni Mkuu wa Kitengo cha Masoko na Mawasiliano wa Benki hiyo, Dora Saria.
02
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Akiba Commercial Bank Juliana Swai (kulia), pamoja na Mkuu wa Kitengo cha Masoko na Mawasiliano wa Benki hiyo, Dora Saria wakinyanyua mikono yao kwa pamoja kuashiria mafanikio kwa benki hiyo mara baada ya kumtangaza mbia wao mpya, National Bank of Malawi.

Akiba Commercial Bank (ACB) imepata mbia wa kimkakati (Strategic Investor) ambaye ni National Bank of Malawi (NBM) ya nchini Malawi iliyoingia makubaliano yakuwekeza katika ACB ili kuongeza mtaji wake.

Hii ni mikakati mbalimbali ya kimaendeleo ndani ya Akiba Commercial Bank ambayo itapelekea kuleta mabadiliko makubwa na yenye tija hasa katika sekta ya kifedha kwa benki hiyo.

Akizungumza na wanahabari makao makuu ya benki hiyo Dar es salaam,  Kaimu Mkurugenzi wa Akiba Commercial Bank Bi. Juliana Swai amesema kupitia mbia huyu Benki hiyo sasa imeweza kuimarisha mtaji wake na kukidhi vigezo vya Benki Kuu hususani swala zima la mtaji wa uendeshaji wa Benki ya Biashara baada ya mbia wake National Bank of Malawi NBM kuwekeza kiasi cha shilingi billion 17 za kitanzania.

Bi swai amesema lengo kuu la mkakati huu ni kuimarisha mtaji wa Benki lakini pia benki imekuwa ikiangalia mahitaji ya soko lake na kuona kuwa kuna haja ya kupata mwekezaji au mbia wa kimkakati kwa ajili ya kuifanya benki iwe imara zaidi na kuweza kuboresha huduma zake na kuanzisha huduma nyingi zaidi ambazo zinahitajika kwenye soko la Tanzania

“Kupitia Ubia huu naomba niwaahidi wateja wetu na Watanzania wote kwa ujumla mabadiliko makubwa na chanya katika huduma zetu na mifumo yetu ya utoaji huduma yanakuja.

Tunaamini kuwa tutaweza kuwahudumia wateja wetu kwa weledi zaidi kupitia utalaamu na uzoefu wa taasisi hizi mbili makini kwenye sekta ya fedha” amesema Bi Juliana Swai.

Ameongeza kuwa benki hiyo inatambua mahusiano mazuri na undugu kati ya nchi hizi mbili ambazo pia zina mahusiano makubwa ya kibiashara na faida mojawapo ya wazi ni kuwepo kwa mazingira wezeshi ya kufanya biashara kati ya nchi hizi mbili kupitia huduma za kifedha ambazo zitapatikana kwa urahisi zaidi.

Bi Juliana amesema aidha uwekezaji huu utasaidia pia kuwepo kwa mazingira wezeshi ya ufanyaji biashara kwa nchi ambazo zipo kusini mwa bara la Afrika wakiwepo wanachama wa SADC

Malawi ni moja ya nchi zilizoko kusini mwa Afrika zinazotumia bandari ya Dar es Salaam kama lango kuu la kibishara hii itarahisisha huduma za kifedha kwa wafanyabiashara wa Tanzania na Malawi wanaotumia bandari ya Dar es Salaam .

NBM ilianzishwa mwaka 1971 baada ya muungano wa Barclays Bank DCO na Benki ya Standard ya Afrika Kusini, ni moja ya benki kubwa nchini Malawi inayotoa huduma za benki ikiwemo rejareja yaani (Personal and Retail banking), wateja wakubwa (Corporate banking), huduma za kibenki za uwekezaji na udalali katika soko la hisa na mitaji.

Sasa Akiba Commercial Benki imekuwa mhimili imara katika sekta ya fedha na imefungua ukurasa mpya kibiashara. Nawakaribisha Watanzania wote wafike Akiba Commercial Bank ili waweze kufaidika na fursa mbalimbali kwa maendeleo ya maisha yao na biasharazao

Akiba Commercial bank ni Benki ya biashara ambayo tangu kuanzishwa kwake mnamo mwaka 1997 imekuwa ikitoa huduma zake kwa wateja wengi wakiwani wajasiriamali wadogo, wakati na wajuu;yaani Micro, Small and Medium entrepreneurs (MSMEs)

Benki imeweza kuwafikia zaidi ya Watanzania 200,000 katika mikoa ya Dar es Salaam, Arusha, Mwanza, Mbeya, Kilimanjaro, na Dodoma. Watanzania hawa wameweza kufaidika na huduma za mikopo mbalimbali ya kijasiriamali,pamoja na kuweka amana zao benki kwenye akaunti kulingana na matakwa yao. Aina za akaunti ni kuanzia zawatoto wadogo, vijana,watu wazima, na za biashara na makampuni. Aidha, huduma za benki kupitia simu za mikononi yaani Akiba Mobile zimeleta unafuu na urahisi zaidi katika kuwafikia wateja wetu popote pale walipo.

 

Share:

LILIAN-FAVOUR MAKAWA

LILIAN-FAVOUR MAKAWA

Popular Posts

Blog Archive

Labels

Recent Posts

Label Cloud

BIASHARA (275) BURUDANI (4) KIMATAIFA (10) KITAIFA (119) MICHEZO (38) SIASA (3)

Pages