Airtel Afrika yaitaja Tanzania Miongoni mwa nchi Tatu kuwashwa Masafa ya Teknolojia ya Mawasiliano ya kasi ya 5G

     
  • Airtel Tanzania miongoni mwa himaya tatu za Airtel zitakazohamia teknolojia ya 5G hivi karibuni
Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam

Airtel Africa, kampuni inayoongoza katika kutoa huduma za mawasiliano na za kuhamisha pesa kwa kutumia simu za mkononi, ikiwa imejikita katika nchi 14 barani Afrika, leo hii nchini Nigeria imezindua mchakato wa kuhamia masafa ya mtandao wa 5G ili kutoa huduma za kisasa na kasi Zaidi kwa wateja wake wote huku ikibainisha Tanzania itafuta kuwashwa kwa teknolojia hiyo ya mawasiliano ya kisasa ya 5G.

Uzinduzi wa masafa hayo ya mtandao wa 5G utafanyika awali katika nchi tatu ikianza Nigeria, ikifuatiwa na Tanzania na Zambia, huku mipango ikiwa inaandaliwa ya kusambaza maeneo yaliyobaki kwenye soko zima.

Kwa kutumia 5G, wateja sasa wanaweza kufurahia kuangalia video zikiwa ngáavu zaidi ya ilivyo sasa, kufurafia kutazama michezo mtandaoni, kurusha matukio mubashara Pamoja na kufurahia kasi zaidi wakiwa popote. Kutokana na kwamba wigo wa mawasiliano utapanuka zaidi kutokana na teknolojia ya kisasa ya 5G pia shughuli za biashara zitaimarika hasa zile zinazotumia mtandao kutoa huduma zake, pamoja na kufanikisha mikutano ya mbali mubashara kupitia mtandao.

Mkurugenzi Mkuu Mtendaji wa Airtel Afrika Group, Segun Ogunsanya alisema: “Kupitia mtandao wa 5G, tunawapa wateja wetu fursa ya kuishi kidijitali kwa kufurahia maajabu yanayoweza kufanywa na mtandao huu wa teknolojia ya mawasiliano ya kisasa ya 5G. Kwa kukamilisha hili kwa nchi zetu hizi tatu Ikiwemo Tanzania tunadhihirisha tunadhihirisha dhamira yetu tuliyojiwekea ya kuwekeza katika teknolojia ya mtandaoni ya kisasa zaidi ili kufungua wigo mpana na kutoa fursa kwa watumiaji kufanya makubwa, tunawezesha kuiunganisha dunia kidijitali pamoja na wateja wetu kukamilisha maono waliyonayo.

Mtandao wa 5G utajikita zaidi katika maeneo maalum, mfano maeneo ya makazi yenye msongamano mkubwa wa watu na yale yenye huduma kama maduka, hospitali, maeneo ya kati ya mji na maeneo makuu ya kibiashara na mjini. Wakiwa katika maeneo haya mahsusi ya 5G ambayo yatatambulika rasmi na kuwekewa alama, wateja wanaweza kufurahia mtandao kwa kasi ya mara kumi zaidi ya kawaida, na kurusha picha za video za ubora wa hali juu mubashara bila ya kukatika katika. Mtandao wa 5G unaweza kuunganishwa tu kupitia vifaa vinavyoendana nao.
Share:

Mheshimiwa Spika akutana na Uongozi wa juu wa Benki ya Absa Tanzania na kufanya mazungumzo

  
Mheshimiwa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Tulia Ackson (kulia) akisalimiana na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Obedi Laiser, wakati yeye na ujumbe wake ukimtembelea ofisini kwake, bungeni, Dodoma Jana.
Mheshimiwa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Tulia Ackson (kushoto) kuzungumza na na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Obedi Laiser, wakati yeye na ujumbe wake ukimtembelea ofisini kwake, bungeni, Dodoma Jana.
Mheshimiwa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Tulia Ackson (wa tatu kushoto) akipiga picha ya kumbukumbu pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Obedi Laiser (kulia kwake), wakati yeye na ujumbe wake ukimtembelea ofisini kwake, bungeni, Dodoma Jana.
Share:

Benki ya Absa yajitosa kuokoa maisha ya Watoto Njiti

Rais Mstaafu wa awamu ya nne, Mhe. Dk. Jakaya Mrisho Kikwete (kulia), akisalimiana na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Obedi Laiser katika hafla ya makabidhiano wa msaada wa vifaa vitakavyosaidia huduma za watoto wanaozaliwa kabla ya muda (Njiti) wakiwa hospitalini. Benki ya Absa imetoa ufadhili wa kiasi cha shs milioni 30 kwa taasisi ya Doris Mollel Kwa ajili hiyo. Kushoto ni Mkurugenzi wa taasisi hiyo, Doris Mollel.
Rais Mstaafu wa awamu ya nne, mhe. Dk. Jakaya Mrisho Kikwete akizunguza katika hafla ya makabidhiano wa msaada wa vifaa vitakavyosaidia huduma za watoto wanaozaliwa kabla ya muda (Njiti) wakiwa hospitalini. Benki ya Absa imetoa ufadhili wa kiasi cha shs milioni 30 kwa taasisi ya Doris Mollel kwa ajili hiyo.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Obedi Laiser(katikati), akizungumza katika hafla ya makabidhiano wa msaada wa vifaa vitakavyosaidia huduma za watoto wanaozaliwa kabla ya muda (Njiti) wakiwa hospitalini. Benki ya Absa imetoa ufadhili wa kiasi cha shs milioni 30 kwa taasisi ya Doris Mollel Kwa ajili hiyo. Kushoto kwake ni Rais Mstaafu wa awamu ya nne, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete.
Rais Mstaafu wa awamu ya nne, mhe. Dk. Jakaya Mrisho Kikwete (katikati), akikata utepe kuzindua hafla ya makabidhiano ya msaada wa vifaa vitakavyosaidia huduma za watoto wanaozaliwa kabla ya muda (Njiti) wakiwa hospitalini. Benki ya Absa imetoa ufadhili wa kiasi cha shs milioni 30 kwa taasisi ya Doris Mollel kwa ajili hiyo.
Mkurugenzi wa taasisi ya Doris Mollel Foundation, Doris Mollel akitoa shukurani Kwa mgeni rasmi, benki ya Absa na wote wakiofanikisha upatikanaji wa vifaa hivyo vitakavyosaidia kuokoa maisha ya watoto nyiti wakiwa hospitalini.
Share:

Benki ya DCB yazidi kujiimarisha kimtaji na kuendelea kupata faida

  
Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Benki ya Biashara ya DCB, Alexander Sanga (wa tatu kushoto) akiwa na baadhi ya wajumbe wa bodi ya benki hiyo wakati wa Mkutano Mkuu wa 21 wa Mwaka wa Wanahisa wa benki hiyo 2023 jijini Dar es Salaam jana. Kutoka kushoto ni Mwanasheria wa benki hiyo, Alex Mgongolwa, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji, Isidori Msaki na wajumbe wengine; Dk. Amina Baamary, Cliff Maregeli na David Shambwe.
Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Benki ya Biashara ya DCB, Alexander Sanga akifungua Mkutano Mkuu wa 21 wa Mwaka wa Wanahisa wa benki hiyo jijini Dar es Salaam jana
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Biashara ya DCB, Isidori Msaki akizungumza wakati wa Mkutano Mkuu wa 21 wa Mwaka wa Wanahisa wa benki hiyo jijini Dar es Salaam jana
Mjumbe wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya Biashara ya DCB, Dk. Amina Baamary (kulia) akizungumza na baadhi ya wanahisa na wajumbe wengine wa bodi hiyo, baada ya kumaliza Mkutano Mkuu wa 21 wa Mwaka wa Wanahisa wa benki hiyo jijini Dar es Salaam Jana.
Sehemu ya wanahisa wa Benki ya DCB wakihudhuria Mkutano Mkuu wa 21 wa Mwaka wa Wanahisa wa benki hiyo, jijini Dar es Salaam jana.

Na Mwandishi Wetu,

BENKI ya Biashara ya DCB imeendelea kujivunia kuongezeka kwa mtaji wake huku ikijiendesha kwa faida inayoongezeka kila mwaka licha ya changamoto kadhaa za kiuchumi, wanahisa wa benki hiyo wameelezwa jijini Dar es Salaam jana

Akizungumza wakati wa Mkutano Mkuu wa 21 wa Mwaka wa Wanahisa wa DCB, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa benki hiyo, Bi. Zawadia Nanyaro alisema benki yao ipo imara kimtaji unaofikia kiasi cha shs 28.5 bilioni unaovuka vigezo vya Benki Kuu ya Tanzania (BoT) vya shs 15 bilioni vilivyowekwa kwa benki za biashara.

Benki yetu ilipata faida baada ya kodi ya shs 747 milioni kwa mwaka 2022, faida iliyochangiwa na mapato yasiyotokana riba ya shs 10.3 bilioni ambayo ni mafanikio ya asilimia 111 ya malengo tuliyojiwekea kwa mwaka 2022, huku mapato yatokanayo na riba yakifika shs 28.6 bilioni ikiwa ni asilimia 86 ya malengo tuliyojiwekea".

Mazingira ya uendeshaji wa taasisi za fedha kwa mwaka 2022 yaliendelea kuwa tulivu huku thamani ya shilingi ya kitanzania ikiendelea kuimarika dhidi ya mataifa mengine, uchumi ukikua tena baada ya janga la Uviko-19, mfumuko wa bei ukiendelea kuwa chini kwa mwaka mzima, mafanikio katika sekta ya utalii na kufunguliwa kwa milango ya biashara kumechagiza kwa DCB kuendelea kufanya vizuri sokoni”,

Akizungumzia utendaji wa benki, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa wa benki hiyo Bw. Isidori Msaki alisema DCB imekuwa makini katika kusimamia mikakati yake ya muda mrefu jambo linaloleta matokeo chanya ikiwemo kukua kwa mali za benki.

Mwaka 2022 mali za benki zimekuwa hadi kufikia shs 211 bilioni kutoka shs 192 bilioni kwa mkwa 2021, ukuaji ulioitoa benki yetu kutoka kwenye kundi la benki ndogo za biashara hadi kufikia benki za kati nchini."

DCB imeendelea kulinda thamani ya wanahisa wake kwa kukuza mapato yasiyotokana na riba kutoka asilimia 30 ya mapato yote mwaka 2021 hadi kufikia asilimia 49 kwa mwaka 2022 ongezeko lililotokana na kuimarika kwa mifumo ya kidigitali inayochangia kwa kiasi kikubwa ongezeko la miamala kwa zaidi ya asilimia 135”, alisema Bwana Msaki.

Akizungumzia baadhi ya vipaumbele vya benki hadi ifikapo mwaka 2025 kwa wanahisa waliofurika katika ukumbi wa JK Nyerere International Conference Centre jijini humo mkurugenzi huyo alisema ni kuhakikisha huduma za benki hiyo zinapatikana nchi nzima na hiyo inawezekana kwa kupitia hatua mbalimbali zinazoendelea kuchukuliwa ikiwa ni pamoja na kuimarisha huduma zake kwa njia za kidigitali.

Tumeanzisha vituo vidogo vya huduma katika maeneo ya kimkakati, huduma za mawakala zaidi ya 700 nchini kote pamoja na mtandao wa matawi saba ndani na nje ya mkoa wa Dar es Salaam".

Benki yetu inalenga kuongeza wigo wa kutoa mikopo kwa njia za kidigitali kwa kiwango kikubwa ifikapo mwaka 2025, mwaka 2022 tulitoa mikopo isiyopungua shs 1.2 bilioni, mikopo hii ni salama zaidi kwa sababu inalipwa ndani ya kipindi cha mwezi mmoja” , aliongeza mkurugenzi huyo.

Aidha mkurugenzi huyo alisema DCB inaendelea na mkakati wake wa kuhakikisha inapata faida mwaka hadi mwaka ili kufikia thamani ya hisa ya asilimia 18.9 na kuendelea kupunguza uwiano wa mikopo chechefu hadi kufikia chini ya asilimia 5 na pia kuongeza idadi ya wateja.

Aliwaomba wanahisa hao kuzidi kuwekeza ndani ya benki yao na kuzidi kuiamini menejimenti na bodi kwani uwekezaji wao umeleta faida kubwa kwa maisha ya watoto wa watanzania kwani umewawezesha kutoa msaada wa madawati kwa shule zenye uhitaji mkubwa jambo linalowapa amani watoto hao kusoma katika mazingira bora.

Ni kwa uwekezaji wenu wanahisa wetu uliotuwezesha pia kutoa elimu ya ujasiriamali kwa watanzania, elimu hii ni muhimu katika maendeleo ya biashara na maisha yao, tutaendelea kuimarisha ufanisi wa utendaji kazi wetu ili kuendelea kuleta matokeo chanya”, alisema.

Pamoja na kupata faida ya baada ya kodi ya sh 747 milioni 2022, na kwa kuzingatia sheria ya Benki Kuu, Bodi ya Wakurugenzi ya DCB imependekeza faida iliyopatikana ikaongeze fedha za wanahisa badala ya kutoa gawio.
Share:

KIWANGO CHA SIMENTI NCHINI – UKWELI NI HUU HAPA

 

Ninaendelea kusikia na kuona mengi juu ya huu muunganiko wa kampuni za simenti na ninazidi kushangaa kwa nini kuna habari nyingi tofauti kwenye vyombo vya habari? Nimeamua kufanya utafiti kuhusu uwezo wa makampuni ya simenti Tanzania na picha yake inanivutia.

Ngoja nikwambie, kwanza nimeanza kwa kutazama hotuba ya Mheshimiwa Waziri wa Uwekezaji, Viwanda na Biashara Dk Ashantu Kijaji na nimesikia machache….

Alisema, wizara hiyo ilifuata sheria na kanuni zote baada ya kupokea ombi la muunganiko. Unaposoma kifungu cha 11 kifungu kidogo cha 2 cha sheria ya Tume ya Ushindani (FCC) ya mwaka 2018 pamoja na kifungu cha 1 kifungu kidogo cha 2 kinatoa vigezo kwa kampuni zinazoungana na zimekidhi vigezo vyote vilivyowekwa hapo juu ili kuwasilisha ombi lao bila kujali ombi lao la awali kukataliwa au kukubaliwa. Hii inamaanisha kuwa kampuni mpya haiwezi kuwa na zaidi ya asilimia 35 ya soko.

Tangu ombi hilo, nimekuja kujua kuwa serikali ilifanya utafiti na uchunguzi ili kuhakikisha muunganiko huo hautakuwa mbaya kwa Tanzania. Na ndo sababu waliidhinisha ombi hilo, nami nikaanza safari yangu.

Watu wengine wanasema kuwa kampuni hii mpya itatawala soko, lakini mimi binafsi silioni hilo. Nikawapigia simu marafiki wachache wanaofanya kazi viwanda vya simenti pamoja na kupitia / kusoma mitandaoni, nilipata yafuatayo na kuwasilisha kupitia jedwali lifuatalo.

Lazima niwe muwazi na kusema kwamba kiwanda cha simenti cha maweni nimewasilisha kiwango chake ambacho ni pamoja na ujenzi wa tanuru lao jipya la tani milini nne (mil 4) kwa mwaka. Nilipata taarifa hizo lakini sikuweza kupata taarifa ya tathmini ya athari za mazingira ya tanuru hilo. Nikazungumza na baadhi ya watu na kuwahoji kama wanaona tanuru likiendelea.


Uwezo wa viwanda vya Simenti Tanzania

Kampuni
Uwezo
(tani kwa mwaka)
Asilimia ya Usambazaji
Maweni Limestone (Huaxin

2,200,000
20%
Dangote Cement
2,200,000
20%

Tanzania Portland Cement (Twiga)
2,100,000
19%

Tanga Cement (Simba)

1,200,000
11%
Mbeya (Bamburi)
700,000
6%

DSM Cement (Camel)
700,000
6%

Lake Cement (Nyati)
660,000
6%

Kisarawe Cement

300,000
3%

Fortune Cement
300,000
3%

Sungura Cement
300,000
3%

Moshi Cement


300,000
3%

Rufiji / Mtwara Cement
100,000
1%

Arusha Cement

100,000
1%

Chalinze Cement

ZERO

ZERO

Kwahiyo nilichokiona katika kuthibitisha kile alichoongea Mheshimiwa Waziri. Muunganiko hautaweza kutawala soko. Kuongeza asilimia 19 kwenye asilimia 11 kutafikia asilimia 30 tu. Hii imekuwa wazi kwangu sasa. Pia niliona mara nyingi sana Tanga na Twiga wakisaidia jamii mbalimbali nchini, huku viwanda vingine vikiwa havifanyi hivyo.

Nimeshawishika na kufurahishwa na serikali yetu na kazi kubwa wanayofanya ya kusaidia uchumi wa Tanzania.

Kila la kheri la Muunganiko wenu!
Share:

Absa Dar City Marathon 2023 donates hospital equipment to Mnazi Mmoja Hospital

Absa Bank Tanzania Chief Internal Auditor, George Binde (fourth left), hands over medical equipment for Mnazi Mmoja Hospital to Dar es Salaam City Council non-communicable diseases cordinator, Dr Milka Mathania, donated by Absa to support the government efforts to provide quality health services in the country.

Dar Es Salaam, Wednesday, 17 May 2023 | Absa Dar City Marathon donated hospital equipment to Mnazi Mmoja Hospital in Dar es Salaam to support the government efforts to provide quality health services to all Tanzanians. This follows from the successful event that was held on 7 May 2023 in Dar es Salaam. The occasion was running in parallel with a blood donation campaign organized by the Club with the support of the marathon sponsors, partners, vendors, services providers and the general public.

The handover of the hospital equipment was attended by In-charge of Mnazi Mmoja Hospital, Dr. Delila Moshi, Ilala Municipal NCDs Coordinator, Dr. Milka Mathania, leaders and members of The Runners Club and representatives of the sponsors of the marathon, Absa Bank Tanzania Limited, Britam Insurance Tanzania Limited, Alliance Life Assurance Limited and Gardaworld Security Services Limited.

Speaking at the occasion, Dr. Delila expressed her gratitude to Absa Dar City Marathon for choosing Mnazi Mmoja Hospital as their preferred institution for their charitable donation and urged them to continue supporting the hospital in the coming marathons. She also praised The Runners Club blood donation campaign, informing that lack of adequate blood is one of the major challenges of the hospital which admits more than 200 expecting mothers in the maternity ward and attends to more than 400 children daily in their reproductive health clinic. On her side, the Ilala Municipal NCDs Coordinator, Dr. Milka advised that NCDs is one of the major challenges of public health in Dar es Salaam and urged The Runners Club to continue with this initiative for the greater benefit of the community.

The spokesperson of the Runners Club, Mr. Godfrey Mwangungulu informed the audience that Absa Dar City Marathon that was held on Sunday, 7 May 2023 at Mnazi Mmoja Grounds, Dar es Salaam was the 3rd edition and attracted more than 2,500 runners in the 21.1km, 10km and 5km race categories. Theme of the marathon was aligned with the Club’s vision of healthy lifestyles aiming at preventing non-communicable diseases (NCDs) through running and the donation of hospital equipment to Mnazi Mmoja Hospital NCDs Clinic was to fulfil that vision. The selection of Mnazi Mmoja Hospital was in line with the saying that charity begins at home given the close proximity of the hospital to Mnazi Mmoja Grounds, the venue of the marathon for the past three events.

The representative of Absa Bank Tanzania Limited, the main sponsors of the marathon, Mr. George Binde, said that Absa supports The Runners Club’s vision to prevent non-communicable diseases (NCDs) through running, and this was one of the main reasons for sponsoring the marathon, which included this charitable donation of hospital equipment. In addition, Absa motivates and promotes healthy lifestyles amongst its staff members and clients through the Absa Health Club. This donation is also aligned with our Citizenship agenda of being a force for good to our communities and play a major role in the society.

The representative of Britam Insurance Tanzania Limited, the sponsors of the 10km corporate run, Ms. Leoncia Makubo, said that the prevention of non-communicable diseases (NCDs) is aligned with the company objectives particularly in the provision of health insurances services. Healthy lifestyles reduce the usage of hospital services for preventable diseases, reserving this scarce service to those are critically in need. The company will continue to support deserving charitable activities through its CSR initiatives.

The representative of Alliance Life Assurance Limited, the sponsors of the 5km family fun run, Ms. Josephine Mfikwa said that the company supports the Runners Club vision of healthy lifestyles and this donation is a demonstration of their commitment to support the health needs of the society. As a life assurance provider, healthy lifestyles are likely to prevent untimely deaths leading to long and happy lives.

About Absa Dar City Marathon

Absa Dar City Marathon is an iconic city centre race organized annually in May by The Runners Club through the Runners Sports Agency. The marathon has both male and female categories in the 21.1km, 10km and 5km race categories. It showcases the city’s iconic landmarks including the Clock Tower, TPA Towers, PSSSF Twin Towers, Johari Rotana, St. Joseph Cathedral, Azania Front Cathedral, Askari Monument, Bank of Tanzania Towers, JNICC, the Aga Khan Hospital, Tanzanite Bridge, Coco Beach and Selander Bridge.

The third edition of the marathon was held on Sunday, 7 May 2023 at Mnazi Mmoja Grounds, Dar es Salaam and was sponsored by Absa Bank Tanzania Limited (21.1km, half marathon), Britam Insurance Tanzania Limited (10km, corporate run), Alliance Life Assurance Limited (5km, fun run) and Gardaworld Security Services Limited with the support of the City of Dar es Salaam, Mnazi Mmoja Hospital, Target Bar & Grill, Jackie’s Pub & Restaurant, The Deck Kitchen & Bar, Kilimanjaro Fresh, Swahili Sweatshop and Selous Marathon.

About The Runners Club

The Runners Club is the largest social running club in Tanzania in terms of number of members, followers and supporters. The Club is based in Dar es Salaam, Tanzania, with more than 1,000 members across the country mainly in the cities of Dar es Salaam, Morogoro, Zanzibar, Tanga, Mtwara, Moshi, Arusha, Mwanza, Dodoma, Iringa and Mbeya. The Club is incorporated under The Trustees Incorporation Act (Cap 318 R. E. 2002) as a Trust and registered under the National Sports Council of Tanzania Act, 1967 as a sports club with registration number NSC 12396 dated 31 July 2019.

The objectives of the Club are to provide sports and social health (drug abuse, non-communicable diseases) education; to provide a wholesome social sporting environment for members; and to organize, collaborate and associate with other clubs in sports activities and events throughout the country.

The Club organizes Absa Dar City Marathon in May and Dar Night Run (DNR) on the last Saturday of August every year. The Club leverages its expertise and large membership base to provide race management services to other races through partnerships and/or agency services including Kilimanjaro Marathon, DAM DAM Marathon, CRDB Bank Marathon, NBC Dodoma Marathon and UDSM Marathon.

About Absa Bank Tanzania

Absa Bank Tanzania Limited is a leading commercial bank in Tanzania that currently boasts a network of 15 branches and 62 ATMs strategically located countrywide – 21 at all our branches and 49 offsite.

The Bank is a wholly owned subsidiary of Absa Group Limited. Absa Bank Tanzania Limited, (registered number 38557), is regulated by the Bank of Tanzania.
Share:

Who is behind Chalinze Cement? What is hidden and why?

For some time now I have been following a company called Chalinze Cement and what I saw was funny. Did you know that this company does not own any land that can mine limestone for cement production? It also doesn't even have the branding they claim to have. They do not even import cement into the country through any of our ports in Tanzania.

The only thing I could find for citizens and users of cement products related to this company is a construction and paint store located in Kisutu in the Dar es Salaam region.

Nothing else! That's what happened when I asked about this group to defend consumers in the country, I didn't find the truth or anything about them.

It doesn't have members, it doesn't have an office, and it doesn't even have a registration, so I wonder how they get the right to hinder their fellow Tanzanians from this huge investment of 500 million US dollars?

Let me ask my fellow writers for something, I challenge one of you to publish pictures of Chalinze Cement workers or a picture of their cement storage bag, even a picture of their limestone mining license.

Even if they have not started mining, publish that so that the people understand that they are investors in the country.

The same goes for the Association for the Defense of Consumers in the country (TCAS). Explain the number of your members. What cases have they ever won while defending consumers in the country?

So I wonder... How come they have a chance to delay the investment of 500 million dollars between the Twiga company and Tanga Cement.

A delay that lasted more than a year and a half? We Tanzanians, how much money could we save by having that money in our country?

I have heard rumors that they are trying to put a damper on this sale by causing more delays. But it is clear that the company Twiga and Tanga Cement will not stop at that.

IMG-20230511-WA0017.jpg
Share:

LILIAN-FAVOUR MAKAWA

LILIAN-FAVOUR MAKAWA

Popular Posts

Blog Archive

Labels

Recent Posts

Label Cloud

BIASHARA (275) BURUDANI (4) KIMATAIFA (10) KITAIFA (119) MICHEZO (38) SIASA (3)

Pages