Absa Bank Tanzania yasisitiza dhamira yake kuendeleza ukuaji wa uchumi halisi nchini Tanzania

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara, Dk. Suleiman Hassan Serera (kushoto), akikabidhi cheti cha shukurani kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Obedi Laiser, kwa kutambua mchango wa benki hiyo kama mdhamini mkuu wa Kongamano la Biashara la tatu la Maofisa Watendaji Wakuu (200 CEO Business Forum), lililofanyika jijini Dar es Salaam jana.

Benki ya Absa Tanzania imeendelea kusisitiza dhamira yake ya kuendeleza ukuaji wa uchumi halisi wa nchini Tanzania, ikidhamini jukwaa mahsusi linalowakutanisha watendaji wakuu wa makampuni nchini, likijulikana kwa jina la ‘The 200 CEOs Business Forum’.

Jukwaa hilo la ngazi ya juu lilihudhuriwa na Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Viwanda na Biashara, Dkt Suleiman Hassan Serera, sambamba na viongozi wengine waandamizi wa Serikali akiwemo Kamishna wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), na wengineo.

Akizungumza katika hafla hiyo, Mgeni rasmi Dkt. Serera alisitiza umuhimu wa hatua za pamoja ili kupanua ajira na mauzo ya nje huku Benki Kuu ya Tanzania ikitoa mrejesho wa mwelekeo wa uchumi unaosaidia kupanga maamuzi ya bodi, na uwasilisho wa udhamini wa Absa ukugusia suluhisho za kifedha ambazo benki ya Absa inatoa kuwawezesha kampuni kuendesha na kusimamia biashara kwa urahisi ambapo katika mijadala mitatu iliyofanyika ikijikita katika uongozi na utawala bora, afya na uimara wa rasilimali watu, pamoja na njia za ufadhili zinazofungua ukuaji na kuhitimishwa na dira ya PPP.

Akizungumza katika hafla hiyo, Bw. Obedi Laiser, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania alisema Jukwaa hili si mkutano wa mawazo pekee bali ni chombo cha maamuzi yanayosukuma mitaji, kuunda ajira, kurasimisha minyororo ya thamani na kufungua fursa za mauzo ya nje akisema kama Absa, wanajivunia kusimama pamoja na viongozi wa biashara wa Tanzania katika wakati huu nyeti hususani kupitia dhamira yao ya “Kuiwezesha Afrika ya Kesho, Pamoja… hatua moja baada ya nyingine”.

Stori yako ina thamani” si ahadi tu, ndivyo tunavyojitokeza, tumesikiliza kwa makini vipaumbele na mahitaji ya wakurugenzi wakuu, na kwa kujibu tunawasilisha suluhisho zinazochochea kasi ya biashara, zikiwemo Absa Infinite Card, Absa Business Credit Card, Vehicle Asset Finance (VAF), uwezo mpana wa Cash Management & Payments, Trade & Working Capital, Treasury & Risk Management, pamoja na majukwaa yetu ya kidijitali ya benki kwa makampuni yanayosaidia idara za fedha kufanya kazi kwa kasi na udhibiti.

Tunawezesha malengo ya Watendaji wakuu (CEOs) na wajasiriamali kupitia suluhisho bora za kifedha, zenye bei shindani na zinazotolewa kwa wakati na umahiri.” Bw. Laiser aliongeza.

Udhamini huu mkubwa wa Absa unaonesha ushirikiano wa muda mrefu wa benki na Serikali na sekta binafsi wa kuharakisha ukuaji jumuishi. Kuwakutanisha watunga sera na viongozi wa viwanda katika ukumbi mmoja kunawawezesha kuoanisha kanuni, kuandaa miradi inayoweza kufadhiliwa na kuweka mifumo inayochochea uwekezaji kwa kiwango kikubwa - kigeuza dhamira kuwa utekelezaji.

Aidha watendaji hao walipata nafasi za kuzungumza na wafanyakazi wa Absa wakioneshwa suluhisho mbalimbali za kifedha zinazorahisisha maisha yao. Miongono mwa hizo ni huduma ya kifahari inayorahisisha safari za kimataifa kupitia Absa Infinite Card, udhibiti wa matumizi ya kampuni kwa Absa Business Credit Card, udhamini wa manunuzi ya magari binafsi na ya kibiashara kupitia Vehicle & Commercial Asset Finance. Ulinzi wa hatari na mipango ya ukwasi kupitia Bancassurance na Flexi Fixed Deposit, huduma za Prestige na Premier kwa wateja wa hadhi ya juu, Diaspora Banking ikirahisisha miamala ya kuvuka mipaka, na kwa upande wa sekta ya umma, e-Loans, yote yakithibitisha ahadi ya Absa kwamba Stori yako ina thamani.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Obedi Laiser (kushoto), akichangia mada isemayo “Fedha kama chachu ya ukuaji wa biashara Tanzania; Mikakati na Fursa”, wakati wa Kongamano la Biashara la tatu la Maofisa Watendaji Wakuu (200 CEO Business Forum), lililofanyika jijini Dar es Salaam jana.
Share:

Coca-Cola Kwanza hosts Minister of Industry and Trade

The Minister of Industry and Trade Seleman Said Jafo (center) and Coca-Cola Kwanza Ltd Public Affairs, Communications and Sustainability Director Salum Nassor (right) admire a bottle of Coca-Cola drink during the Minister’s tour to the company’s manufacturing plant in Dar es Salaam over the weekend as a part of the government efforts on creating a solid relationship with the private sector. A part from the visit, the Minister also had an opportunity to get insights into the company’s operations, contributions to the Tanzanian economy, and its role in driving shared value creation. Left is Coca-Cola Kwanza Ltd Managing Director David Chait.

Dar es Salaam, Tanzania, Sunday 24 August 2025 - Coca-Cola Kwanza Ltd proudly hosted the Minister of Industry and Trade, Dr Seleman Said Jafo (MP) at its Dar es Salaam facility.

The visit provided a valuable opportunity to showcase the company’s commitment to doing business the right way - guided by integrity, shared value creation, and a deep respect for the communities it serves.

The Minister’s visit included a plant tour and strategic boardroom session, where Coca-Cola Kwanza Ltd, a company in the Coca-Cola Beverages Africa (CCBA) group, shared insights into its operations, contributions to the Tanzanian economy, and its role in driving shared value creation.

This engagement reflects CCBA’s ongoing commitment to strengthening its social license to operate. By leading in environmental, social, and governance (ESG) standards, CCBA aims to create lasting positive impact and contribute to a better shared future.

We believe that by following our values, we can drive sustainable growth and societal progress,” said David Chait, General Manager for Coca-Cola Kwanza Ltd.

People are at the centre of everything we do, from our employees to those who touch our business to the communities we call home. Community involvement allows us to bring positive, measurable change to both the communities in which we operate and to our business,” said David Chait.

Our aspiration is not only to reflect the diversity of the communities where we operate but also to lead and advocate for a better shared future. We aim to create access to equal opportunities and become more inclusive. We embrace differences in backgrounds and support economic inclusion for under-served communities, especially women, youth and people with disabilities.

CCBA looks forward to continuing to build meaningful partnerships that support inclusive economic development and responsible business practices.
Coca-Cola Kwanza Ltd Managing Director David Chait (left) stresses a point to the Minister of Industry and Trade Seleman Said Jafo as he toured the company’s manufacturing plant in Dar es Salaam over the weekend as a part of the government efforts on creating a solid relationship with the private sector. A part from the visit, the Minister also had an opportunity to get insights into the company’s operations, contributions to the Tanzanian economy, and its role in driving shared value creation. Right is Coca-Cola Kwanza Ltd Public Affairs, Communications and Sustainability Director Salum Nassor.
Share:

AGRA, Sahara Accelerator kunufaisha vijana wengi kupitia kilimo

  

Na Mwandishi Wetu

Kilimotech Accelerator kupitia Youth Entrepreneurship for the Future of Food and Agriculture (YEFFA) inayodhaminiwa na shirika la AGRA Tanzania na kutelekelezwa na Sahara Accelerator inatarajia kunufaisha vijana wapatao 265,000 wanaojihusisha na masuala ya kilimo.

Akizungumza wakati wakijadili na vijana kuhusu fursa hiyo jijini Dar es Salaam, Adam Mbyallu wa Sahara Accelerator alisema fursa hiyo itatoa kiasi cha dola milioni 20 kwa bunifu za kilimo zinazojumisha mnyororo wa thamani kwa mazao manne ambayo ni mbogamboga na matunda, alizeti, mpunga na mahindi.

"Tuna hakikisha namna gani tunaweza kusaidia upatikanaji wa vifaa vya kilimo kupitia teknolojia za kidigitali tunasaidia vijana wenye bunifu mbalimbali zinzojibu changamoto za upatikanaji wa vifaa za kilimo," alieleza Mbyallu.

Alisema kupitia bunifu hizo watawapatia vijana hao mafunzo,mentorship na kuwaunganisha wa wadau mbalimbali na kusaidia kwenda shambani kwenye kilimo na kujiuza.
Alifafanua kuwa bunifu wanazotafuta zitajibu changamoto za kilimo kama vifaa,mafundi,masoko,udhibiti wa mazao,uharibifu wa mazao baada ya mavuno changamoto ambazo wadau wa kilimo walisema zipo.

"Maeneo hayo yote kama vinavifaa vya kilimo vingesaidia sana vijana kujiajiri kwenye kilimo kama watajiajiri tunaangalia jinsi ya kuwawezesha kupitia teknolojia ya kidijitali," aliongeza.

Mbyallu alisema ili kufanikisha upatikanaji wa bunifu hizo wamefungua dirisha la usajili wa bunifu kwa muda wa miezi miwili ambapo itafungwa Agosti 18, 2025 na zitachujwa kuangalia kama bunifu hizo zinakidhi vigezo na baada ya hapo watawaunga mkono.

"Tutawaunga mkono Kwa mafunzo,mentorship,changamoto na kuwaunganisha na wadau watakaowasaidia bunifu zao kwenda soko kama wadau wanaouza zana za kilimo,mafundi wa zana za kilimo,wanaotengeneza zana za kilimo,taasisi za fedha na wadau wengine," alisisitiza.
Aliongeza: "Bunifu zitakwenda kwenye mazao manne yamegawiwa katika kanda kuna miradi kulingana na mazao ya eneo mfano Morogoro wanajikita na mbogamboga na alizeti ,Mbeya wana mbogamboga na mpunga, Njombe mbogamboga na mahindi, Singida ni alizeti kila kanda imepewa aina ya zao… tunakwenda kote."
Share:

Airtel Money na Benki ya I&M Wazindua Mpango wa Elimu ya kifedha kuwawezesha Wajasiriamali Wanawake

 

Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Airtel Tanzania, Bw. Charles Kamoto (kulia), akishikana mikono na Mkurugenzi Mtendaji wa I&M Bank Tanzania, Bw. Zahid Mustafa, wakati wa uzinduzi rasmi wa mpango unaolenga kuwawezesha wanawake wajasiriamali nchini kwa elimu ya kifedha na nyenzo nyingine muhimu za kukuza biashara zao. Hafla hiyo ilifanyika jijini Dar es Salaam jana. Katikati ni mmoja wa wanawake wajasiriamali waliohudhuria semina iliyofanyika pamoja na uzinduzi huo, Bi. Virginia Gift.

Airtel Money kwa kushirikiana na Benki ya I&M wamezindua rasmi mpango unaolenga wanawake wajasiriamali ukiwa na malengo ya kuwawezesha wanawake hao nchini kwa elimu ya kifedha na nyenzo muhimu za kukuza biashara zao hivyo kuweza kuboresha maisha yao.

Mpango huu ni sehemu muhimu ya Mkakati wa Uendelevu wa Benki ya I&M Tanzania unaojikita kwenye nguzo tatu kuu ambazo ni ujumuishaji wa kifedha, elimu ya kifedha, na uwajibikaji wa mazingira, ukiendana na Malengo ya Maendeleo Endelevu ya Umoja wa Mataifa (SDGs), hususan SDG 5 (Usawa wa Kijinsia) na SDG 13 (Hatua dhidi ya Mabadiliko ya Tabia nchi).

Kupitia huduma ya Kamilisha, iliyoundwa kwa pamoja kati ya Airtel Money na Benki ya I&M, huwapa wateja uwezo wa kupata mikopo midogo midogo kupitia simu zao ili kukamilisha miamala muhimu kama kutuma pesa au kulipa bili, hata wanapokosa salio kwenye akaunti zao za Airtel Money.

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Mkurugenzi Mtendaji wa Airtel Tanzania, Bw. Charles Kamoto alisema, “kuna matumizi mkubwa ya Airtel Money na ndio tunalenga kujenga uwezo ili kupunguza pengo la matumizi, tunataka kuhakikisha kuwa wateja wetu, hasa wanawake, wana ujasiri na ujuzi wa kutumia huduma za kifedha kidijitali kwa ufanisi.

Kamoto alieleza kuwa zaidi ya asilimia 65 ya watu wazima Tanzania wanakabiliwa na upatikanaji mdogo wa huduma za kifedha, huku wanawake wakiwa katika hali mbaya zaidi.

Kupitia mpango huu, tunasaidia kupunguza pengo la elimu ya kifedha na kusaidia uimara wa kifedha wa muda mrefu, kwa kuwa chini ya asilimia 30 ya wanawake Tanzania wanamiliki simu janja, tumejumuisha mafunzo ya moja kwa moja ya matumizi ya programu za kifedha ili kuwajengea ujasiri watumiaji wapya,” aliongeza Bw. Kamoto.

Katika mafunzo ya siku moja yaliyofanyika jijini Dar es Salaam kama sehemu ya uzinduzi wa mpango huu, zaidi ya wanawake 50 walikusanyika kwa mafunzo shirikishi juu ya usimamizi wa fedha, matumizi ya fedha kidijitali, na mbinu endelevu za biashara, lengo ikiwa siyo tu kutoa ujuzi wa kiufundi, bali pia kuunganisha uwezeshaji wa kiuchumi na maendeleo jumuishi yanayostahimili mabadiliko ya tabianchi.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa I&M Bank Tanzania, Bw. Zahid Mustafa alisema, “Hii ni sehemu ya dhima yetu ya kufanya benki kuwa jukwaa la kuleta mabadiliko, tunajivunia kuongoza mpango huu kwa ushirikiano na Airtel Tanzania, leo tukianza safari hii kwa kutoa mafunzo ya siku moja ya elimu ya kifedha kwa wanawake 60 hapa Dar es Salaam, kwa udhamini kamili, mtaala wa mafunzo haya umetayarishwa kwa kushirikiana na Grant Thornton na utaendelea kuboreshwa kwa kuzingatia mrejesho kutoka kwa washiriki.

Licha ya ukuaji wa huduma za fedha kidijitali, biashara ndogondogo zinazoongozwa na wanawake nchini bado zinakosa huduma rasmi kutokana na ukosefu wa elimu na mifumo ya kifedha. Mpango huu unalenga kuziba pengo hilo kwa kuwapa wanawake ujuzi wa vitendo na ujasiri zaidi kushiriki katika mfumo wa kifedha.

Tangu kuanzishwa kwake, huduma ya Kamilisha imekwisha toa mikopo yenye thamani ya zaidi ya TZS bilioni 392, ambapo asilimia 46 ya mikopo hiyo imekwenda kwa wanawake. Hadi sasa, zaidi ya Watanzania milioni tano wameingia kwenye mfumo rasmi wa kifedha kupitia huduma hii,” aliongeza Mustafa.

Kama sehemu ya mpango huu, Benki ya I&M imeahidi kupanda mti mmoja kwa kila wanawake 100 watakaokopeshwa, na inalenga kupanda miti 8,000 kwa mwaka. Jitihada hizi za kimazingira zinatekelezwa kwa kushirikiana na taasisi ya Africa Transformation Initiative (ATI), ambayo itasimamia upatikanaji, upandaji, na ufuatiliaji wa miti hiyo nchini Tanzania kwa kipindi cha miaka mitatu ijayo.
Mkurugenzi wa Airtel Money, Bw. Andrew Rugamba akizungumza katika hafla ya uzinduzi rasmi wa mpango unaolenga kuwawezesha wanawake wajasiriamali nchini kwa elimu ya kifedha na nyenzo nyingine muhimu za kukuza biashara zao katika hafla hiyo jijini Dar es Salaam jana. Mpango huo unafanyika kwa ushirikiano wa Airtel Money na I&M Bank Tanzania.
Mkurugenzi Mtendaji wa Airtel Tanzania, Bw. Charles Kamoto, akizungumza, katika hafla ya uzinduzi rasmi wa mpango unaolenga kuwawezesha wanawake wajasiriamali nchini kwa elimu ya kifedha na nyenzo nyingine muhimu za kukuza biashara zao katika hafla hiyo jijini Dar es Salaam jana. Mpango huo unafanyika kwa ushirikiano wa Airtel Money na I&M Bank Tanzania.
Mkurugenzi Mtendaji wa I&M Bank Tanzania, Bw. Zahid Mustafa, akizungumza, katika hafla ya uzinduzi rasmi wa mpango unaolenga kuwawezesha wanawake wajasiriamali nchini kwa elimu ya kifedha na nyenzo nyingine muhimu za kukuza biashara zao katika hafla hiyo jijini Dar es Salaam jana. Mpango huo unafanyika kwa ushirikiano wa benki ya I&M na Airtel Money.
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Airtel Tanzania, Bw. Charles Kamoto (walioketi wa pili kulia), Mkurugenzi Mtendaji wa I&M Bank Tanzania, Bw. Zahid Mustafa (wa pili kushoto), Mkurugenzi wa Airtel Money, Bw. Andrew Rugamba (kushoto), na Mkurugenzi Mtendaji wa Grant Thornton Tanzania, Bw. Muntazir Fazel (kulia), wakipozi mbele ya wapiga picha, mara baada ya semina na uzinduzi rasmi wa mpango unaolenga kuwawezesha wanawake wajasiriamali nchini kwa elimu ya kifedha hivyo kukuza biashara zao. Hafla hiyo iliyofanyika jijini Dar es Salaam jana. Wengine ni baadhi ya washiriki na wawezeshaji wa semina hiyo.
Share:

LILIAN-FAVOUR MAKAWA

LILIAN-FAVOUR MAKAWA

Popular Posts

Blog Archive

Labels

Recent Posts

Label Cloud

BIASHARA (277) BURUDANI (4) KIMATAIFA (10) KITAIFA (119) MICHEZO (38) SIASA (3)

Pages