Benki ya Absa kuendelea kuunga mkono maendeleo ya wanawake mahali pa kazi

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Mhe. Ridhiwani Kikwete (kushoto), akikabidhi cheti Kwa Mkurugenzi Mtendaji wa benki ya Absa Tanzania, Bw. Obedi Laiser, kwa kutambua mchango wa benki hiyo kama mdau muhimu wa Programu ya Mwanamke Kiongozi inayoratibiwa na Chama Cha Waajiri Tanzania (ATE), katika hafla ya maadhimisho na mahafali ya 10 ya programu hiyo, jijini Dar es Salaam, hivi karibuni.

Na mwandishi wetu, Dar es Salaam

Benki ya Absa Tanzania imesema itaendelea kuunga mkono juhudi mbalimbali zenye lengo la kuhakikisha wanawake wa Tanzania wanapiga hatua za kimaendeleo mahali pa kazi.

Hayo yalisemwa na Mkurugenzi Mtendaji wa benki hiyo, Bw. Obedi Laiser, jijini Dar es Salaam hivi karibuni, wakati wa maadhimisho ya miaka 10 na mahafali ya 10 ya programu ya Mwanamke Kiongozi, inayoratibiwa na Chama cha Waajiri Tanzania (ATE).

Sisi Absa tuna kitu tunaita ahadi yetu ya chapa inayosema ‘Stori yako ina thamani’, kwa kuendana na ahadi yetu hii tunaamini kwamba story za wanawake wa Tanzania zina thamani na ndio maana tuliamua kuungana na ATE kusapoti jambo ili kama wadhamini, lakini pia tumekua wadau wa karibu sana na ATE kwa miaka 10 tumeweza kuweka wahitimu wengi, leo hii tukiwa na wahitimu kama wanne."

Sababu kubwa inayotufanya tuendelee kusapoti juhudi hizi ni kwamba kwenye miaka hivi karibuni tumekuwa na mafanikio makubwa sana katika utendaji, wale ambao mnafuatilia nadhani mtakuwa mashahidi na sababu kubwa ya kwanini tumefanikiwa kwa kiasi kikubwa ni kwa sababu tumekuwa na viongozi wanawake kwenye timu ya uongozi."

Sisi Absa, tuna idara mbalimbali, tuna idara nne za biashara, kati ya hizo, tatu zinaongozwa na wakurugenzi wanawake, wamepata promosheni hivi karibuni kuingia katika ngazi ya ukurugenzi, hawa ndio wakurugenzi wa biashara, hivyo basi mafanikio ya benki yetu hayawezi kabisa kutenganishwa na uwepo wa viongozi wanawake”, alisema Bw. Laiser.

Mmoja wa wahitimu wa programu hiyo, kutoka Benki ya Absa, Ikunda Kishimbo, ambayo tokea ianzishwe jumla ya washiriki 462 kutoka sekta binafsi na umma wamehitimu alisema, programu hiyo imewajengea washiriki kujiamini na kuwapa uwezo wa kiutendaji katika maeneo yao ya kazi.

Mafunzo yanayotolewa kupitia Programu ya Mwanamke Kiongozi pamoja na kuwa na lengo la kuongeza ujuzi wa wanawake viongozi, lakini pia yanasaidia kuongeza msukumo wa suala la usawa wa kijinsia katika mahali pa kazi.
Mkurugenzi Mtendaji wa benki ya Absa Tanzania, Bw. Obedi Laiser, akizungumza machache kuhusu huduma mbalimbali za kibenki zitolewazo na benki hiyo, wakati wa maadhimisho na mahafali ya 10 ya Programu ya Mwanamke Kiongozi inayoratibiwa na Chama Cha Waajiri Tanzania (ATE), katika hafla iliyofanyika jijini Dar es Salaam hivi karibuni.
Baadhi ya wahitimu wa Programu ya Mwanamke Kiongozi inayoratibiwa na Chama Cha Waajiri Tanzania (ATE) kutoka Benki ya Absa Tanzania, Ikunda Kishimbo na Vailet Ephata, wakipozi kwa picha katika hafla ya maadhimisho na mahafali ya 10 ya programu hiyo, jijini Dar es Salaam hivi karibuni.
Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dr. Samia Suluhu Hassan (katikati), Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Mhe. Ridhiwani Kikwete (kulia kwake), wakipiga picha ya kumbukumbu pamoja na wadhamini na viongozi mbalimbali, muda mfupi mara baada ya kukamilika kwa hafla ya maadhimisho na mahafali ya 10 ya Programu ya Mwanamke Kiongozi iliyoratibiwa na Chama Cha Waajiri Tanzania (ATE), jijini Dar es Salaam hivi karibuni.
Share:

Benki ya Absa ya endelea kusambaza upendo wa Siku ya Wapendanao kwa wajasiriamali

Meneja wa Masuala Endelevu na Matukio wa Benki ya Absa Tanzania, Bi. Abigail Lukuvi, akichagua maua, wakati baadhi ya wafanyakazi wa benki hiyo, wakitembelea eneo maarufu la biashara ya maua, Mbuyuni, Namanga jijini Dar es Salaam jana, Ili kuendelea kusambaza upendo wa Siku ya Wapendanao kwa wajasiriamali hao, na pia kuwaelezea huduma mbalimbali za kibenki zitolewazo na Absa.

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam

KATIKA kile kilichoelezwa kuwa ni kujali stori za maisha ya wajasiriamali wadogo wanaojishughulisha na uchuuzi wa maua, Benki ya Absa Tanzania imewatembelea wafanyabiashara hao, kuzungumza nao na kuwapa motisha mbalimbali, ikiwa ni sehemu ya kuadhimisha Siku ya Wapendanao iliyoadhimishwa duniani kote hivi karibuni.

Akizungumza katika hafla hiyo katika eneo maarufu kwa biashara hiyo la Mbuyuni, Namanga jijini Dar es Salaam jana, Meneja wa Masuala Endelevu na Matukio wa Benki ya Absa Tanzania, Bi. Abigail Lukuvi, alisema Absa imeamua kuwatembelea wajasiriamali hao kama njia ya kusambaza upendo, kwa kuwa ni kati ya makundi yanayosahaulika, wakati wanahusika kwenye kusambaza upendo kwa kuuza maua.

Kama mnavyofahamu ahadi mpya ya chapa yetu isemayo ‘stori yako ina thamani’, ndiyo maana Absa tukaamua kuendelea kusambaza upendo wa Siku hii ya Wapendao kwa kipekee kabisa kwa kuwatembelea hawa wafanyabiashara wadogowadogo hapa Mbuyuni kuonesha kuwa stori za wafanyabiashara hawa wa maua zina thamani sana na zina umuhimu kwetu."

Hawa wafanyabiashara ndio watu muhimu sana katika kusambaza upendo, lakini mara nyingi husahaulika, hutumia siku yao nzima katika kuuza maua na kusambaza upendo kwa wengine, lakini wao wenyewe wanasahaulika, kwa hiyo Absa imeamua kuwatembelea ili wasijisikie wapweke bali wajisikie kuguswa na upendo”, alisema Bi. Abigail.

Mmoja wa wafanyabiashara hao wa maua, Robert Mwita Nyamkama, huku akiishukuru benki hiyo kwa kuwatembelea, alisema biashara ya mwaka huu imeshamiri ikilinganishwa na mwaka jana, hali inayotokana na watu wengi zaidi kuwa na mwamko wa kupeleka zawadi ya maua kwa wapendwa wao.

Tunaishukuru Absa kwa kutukumbuka na kuja kututembelea tukiwa kwenye biashara zetu, hii imetuthibitishia kuwa benki hiyo inatuthamini, na ni ishara thabiti kuwa kauli ya benki hiyo ya stori yako ina thamani kwetu ni ya ukweli kabisa,” alisema.

Siku ya Wapendanao, ambayo hujulikana sana kama Valentine, huadhimishwa tarehe 14 Februari kila mwaka, ambapo hutiwa nakshi na utamaduni maarufu wa wapendanao kupelekeana zawadi za vitu mbalimbali vikiwemo kadi na maua yenye rangi mekundu.
Mchuuzi wa maua, Bw. Robert Byamukama akikabidhi Kwa mmoja wateja, Vivian mwamanda, wakati baadhi ya wafanyakazi wa benki hiyo, wakitembelea eneo maarufu la biashara ya maua, Mbuyuni, Namanga jijini Dar es Salaam jana, Ili kuendelea kusambaza upendo wa Siku ya Wapendanao kwa wajasiriamali hao, na pia kuwaelezea huduma mbalimbali za kibenki zitolewazo na Absa.
Mmoja wa wateja wa maua, Daniel Mgedule (kulia), akipokea ua kutoka Kwa mmoja wa wachuuzi wa maua katika eneo maarufu la biashara ya maua, Mbuyuni, Namanga, Dar es Salaam jana, wakati baadhi ya wafanyakazi wa benki hiyo, wakitembelea eneo hilo, kuendelea kusambaza upendo wa Siku ya Wapendanao kwa wajasiriamali hao, na pia kuwaelezea huduma mbalimbali za kibenki zitolewazo na Absa.
Share:

AKIBA COMMERCIAL BANK AWARDS WINNERS "TWENDE KIDIJITALI" CAMPAIGN



Six customers from various branches of Akiba Commercial Bank Plc have been awarded cash prizes and other rewards after emerging as winners in the "Twende Kidijitali – Tukuvushe Januari" campaign. The winners were recognized for their high usage of the bank’s digital services, including ACB Mobile, Internet Banking, and VISA card.


Speaking during the prize-giving ceremony, Akiba Commercial Bank’s Chief Commercial Officer, Ms. Wezi Olivia Mwazani, congratulated the winners and thanked them for their participation. She emphasized that the campaign was designed to encourage customers to embrace digital banking solutions, which enhance financial accessibility and improved transaction security.


"We congratulate our winners for being part of our digital transformation journey. Through services such as ACB Mobile, Internet Banking, and VISA card, our customers have been able to conduct transactions quickly, securely, and conveniently. We encourage more customers to continue using these services for their benefit," said Ms. Wezi.

Some of the campaign winners expressed their excitement and appreciation, stating that they were delighted to be recognized and rewarded for using digital banking services. They also affirmed their commitment to continuing to use these services due to their ease and convenience.

The Twende Kidijitali – Tukuvushe Januari campaign is part of Akiba Commercial Bank’s strategy to promote digital banking adoption, offering customers modern and efficient financial solutions.
Share:

Benki ya Absa Tanzania yazindua akaunti ya akiba ya kikundi.

Mkurugenzi wa Kitengo cha Wateja Binafsi wa Benki ya Absa Tanzania, Bi. Ndabu Swere (katikati), akizungumza na waandishi wa habari wakati wa uzinduzi rasmi wa akaunti ya akiba ya kikundi ya benki hiyo jijini Dar es Salaam leo. Wanaoshuhudia ni Meneja wa Huduma za Jamii wa Absa, Bi. Abigail Lukuvi (kushoto) na Mkuu wa Mikakati na Bidhaa za Wateja Binafsi wa benki hiyo, Heristraton Genesis.

Benki ya Absa Tanzania imezindua bidhaa mpya, Akaunti ya Akiba ya Kikundi, inayolenga kuwawezesha watu wanaokusudia kufikia malengo ya kifedha ya pamoja kuweza kuweka akiba na kuwekeza, ikiwa ni sehemu ya juhudi za benki hiyo kuharakisha ajenda ya ujumuishaji wa kifedha nchini Tanzania.

Akizungumza katika hafla ya uzinduzi jijini Dar es Salaam leo, Mkurugenzi wa Kitengo cha Wateja Binafsi wa Benki hiyo, Bi. Ndabu Swere alisema: “Akaunti ya Akiba ya Kikundi ya Absa inakusudiwa kwa ajili ya vikundi; kupitia akaunti hii, tunaviwezesha vikundi kuweka akiba, kuwekeza, na kupata riba.

Alibainisha kuwa akaunti hiyo ina faida kadhaa, kubwa ikiwa ni urahisi wake unaowawezesha wamiliki kufanya miamala popote kwa kutumia mifumo ya kidijitali ya benki, benki wakala, au hundi.

Aliongeza: “Akaunti hii pia ni wazi, kwani wamiliki wanapata taarifa kuhusu kinachoendelea kwenye akaunti, kama vile uwekaji na utoaji pesa, wanaweza kuona akaunti na pia kupata taarifa za mara kwa mara.

Faida nyingine, alibainisha, ni kwamba wamiliki wanapata bima, ambayo inaweza kutoa fidia endapo kutatokea matukio yasiyotabirika kama kifo cha mmiliki wa akaunti au ndugu zao wa karibu.

Akaunti hii pia inajenga hisia kubwa ya uwajibikaji ambayo haiwezekani kwa mtu mmoja mmoja; kama kikundi, wanaweza kuweka akiba na kufanikiwa, kwa sababu kila mwanachama anahisi wajibu wa kufanya kazi kuelekea kufanikisha malengo ya pamoja yaliyokubaliwa.

Faida nyingine ya akaunti hii ni usalama, kwani akaunti itakuwa salama kutokana na ukweli kwamba mifumo ya Absa imeundwa kuhakikisha usalama wa fedha za wateja; majukwaa yetu ni salama kabisa.

Natoa wito kwa vikundi visivyo na akaunti, vikundi vyenye akaunti lakini ambazo hazina sifa za Akaunti ya Akiba ya Kikundi ya Absa, na watu binafsi wasio na vikundi kufanya maamuzi ya kutumia pendekezo hili lenye thamani,” alisema Bi. Ndabu.

Alibainisha kuwa bidhaa hii mpya ni sehemu ya juhudi za benki hiyo sambammba na lengo kuu la benki hiyo la ‘kuiwezesha Afrika ya kesho pamoja – hatua moja baada ya nyingine’ kusaidia bara hili kushinda changamoto zake za kijamii na kiuchumi.

Iwapo wateja wetu watafanikiwa kufikia malengo yao ya pamoja kupitia Akaunti ya Akiba ya Kikundi ya Absa, tutakuwa tumeweza kuiwezesha Afrika,” alisema Bi. Ndabu.

Akizungumza katika hafla hiyo, Mkuu wa Mikakati na Bidhaa za Wateja Binafsi, Bw. Heristraton Genesis, alisema uzinduzi wa Akaunti ya Akiba ya Kikundi ya Absa, ambayo inaweza kufunguliwa na angalau watu watatu, ulikuwa ni mwitikio wa mahitaji ya soko.

Tumekuwa tukipokea mapendekezo ya kufungua akaunti ya kikundi; kama taasisi ya kifedha makini, tumejibu haraka mahitaji hayo,” alisema Bwana Genesis, akibainisha kuwa akaunti hiyo ilikuwa ni mfano mseto, ikiwa na kazi za Akaunti ya Akiba ya kawaida na Akaunti ya Kikundi.

Alifafanua kuwa ili kufungua akaunti hiyo, kikundi kinapaswa kuwa na katiba, kumbukumbu za mkutano wa kuidhinisha katiba, majina ya watia saini, na barua ya utambulisho.

Alisema wamiliki wa Akaunti ya Akiba ya Kikundi ya Absa wanaanza kupata riba baada ya amana kufikia Tsh 200,000, na kwamba amana ikizidi Tsh 1,000,000, ada zote za benki zinaondolewa na inakuwa huduma ya bure.

Alibainisha kuwa akaunti hiyo ilikuwa ni sehemu ya juhudi za benki hiyo kuhakikisha kuwa vikundi rasmi, na vile visivyo rasmi vyenye angalau barua ya utambulisho kutoka kwa Mamlaka za Serikali za Mitaa, vinapata huduma za kibenki.

Madhumuni makuu ya Akaunti ya Akiba ya Kikundi ya Absa ni kuwawezesha watu kuunganishwa na huduma rasmi za kibenki tunapochukua hatua za kusaidia juhudi za ajenda ya ujumuishaji wa kifedha zinazoratibiwa na serikali ya Awamu ya Sita,” alisema.
Mkuu wa Mikakati na Bidhaa za ya Wateja Binafsi wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Heristraton Genesis (kulia), akizungumza na waandishi wa habari wakati wa uzinduzi rasmi wa akaunti ya akiba ya kikundi ya benki hiyo jijini Dar es Salaam leo. Wanaoshuhudia ni Meneja wa Huduma za Jamii wa Benki ya Absa, Bi. Abigail Lukuvi (kushoto), na Mkuu wa Kitengo cha Benki za Wateja Binafsi wa benki hiyo, Bi. Ndabu Lilian Swere.
Baadhi ya wanahabari wakiwa kazini wakati wa uzinduzi rasmi wa akaunti ya akiba ya kikundi ya Benki ya Absa Tanzania, jijini Dar es Salaam leo. Mkurugenzi wa Kitengo cha Benki za Wateja Binafsi wa benki hiyo, Bi. Ndabu Lilian Swere alifanya uzinduzi huo.
Share:

Minister officially launches real estate giant Coldwell Banker Tanzania and Zanzibar

 

Zanzibar Minister for Labour, Economy, and Investment, Shariff Ali Shariff addresses guests during the launch of Coldwell Banker Tanzania and Zanzibar over the weekend. Centre is the company’s CEO Gina Washington and Miguel Pilgram, CEO of Pilgram Group, a property development company based in the Isles.

By GUARDIAN Reporter

ZANZIBAR Ministry of Labour, Economy, and Investment has said that it will continue to expedite the issuance of investment permits without bureaucracy so that investors can start doing business with ease for the economic development of the Isles.


Speaking during the launch of international real estate investment company Coldwell Banker Tanzania and Zanzibar Real Estate which has a presence in more than 20 countries in the world, Minister Shariff  Ali Shariff said that investment in the property market has huge potential to foster Zanzibar’s economic growth.


The company’s Chief Executive Officer (CEO), Gina Washington, echoed a similar opinion, adding that the market has the potential to provide more employment opportunities for young people.


According to the Zanzibar Investment Promotion Authority (ZIPA), 30 percent of the authority’s registered projects are in real estate, making it a promising area for further investments.


He said that the official launch of the company is a milestone that signifies not only the growth of a world-class real estate brand in our region but also the vast opportunities Zanzibar offers in the investment and property market. 


“Zanzibar is experiencing a transformative era, driven by strategic economic reforms, increased investor confidence, and a forward-thinking government agenda.

 This event is a testament to our collective commitment to fostering a business-friendly environment that attracts global players while ensuring sustainable development that benefits both local and international stakeholders,” he said.


He added that the investment landscape has never been more promising with the government positioning investment as a key pillar for economic diversification and long-term prosperity. 


“The rapid development of infrastructures, streamlined regulatory frameworks, and enhanced ease of doing business has made Zanzibar an attractive destination for investors across various sectors, including real estate,” he noted.


With tourism, and blue economy initiatives driving growth, the real estate sector remains a critical enabler of the vision to provide high-quality residential, commercial, and mixed-use developments that cater to our growing economy and international market demand, he said.


“In the last four years under the 8th Phase of the Revolutionary Government of Zanzibar, Zanzibar Investment Promotion Authority (ZIPA) has registered more than 430 investment projects account for a staggering 5.9 billion US dollars’ worth of capital and are expected to create more than 22,000 direct jobs to the locals. 


With tourism projects leading the charts which accounts for more than 38 percent of all registered projects followed by real estate sector which accounts for more than 22 percent of all registered project. About 78 percent of real estate registered projects was registered in the last four years, this shows the readiness and willingness of our government in supporting the real estate business in Zanzibar.


For her part, Washington said that for over 119 years, Coldwell Banker has been a global leader in real estate, known for trust, integrity, and innovation. 


“Today, as we establish Coldwell Banker in this region, our mission is clear—we are here to bring a new level of professionalism and transparency to the market, helping investors, developers, and agents to thrive,” she said.


Naimah Kunambi, Associate Broker and Sales Manager | Coldwell Banker Islemark Realty said that the launch is more than just the opening of a real estate brokerage but the beginning of a new standard in real estate, one built on excellence, professionalism, and a commitment to serving our clients, agents, and community at the highest level.


“I want to take a moment to acknowledge and sincerely thank everyone who has played a role in making today possible—our dedicated team, our partners, our clients, and all of you here today. Your support and belief in our vision mean everything,” she said
Share:

LILIAN-FAVOUR MAKAWA

LILIAN-FAVOUR MAKAWA

Popular Posts

Blog Archive

Labels

Recent Posts

Label Cloud

BIASHARA (260) BURUDANI (4) KIMATAIFA (10) KITAIFA (114) MICHEZO (38) SIASA (3)

Pages