BENKI YA TCB YATINGA MWANZA YAWAFUNDA WANAWAKE WAJASIRIAMALI.

.com/img/a/Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa wa Benki ya Biashara ya Tanzania TCB Bw Moses Manyatta, akizungumza wakati wa hafla ya uzinduzi rasmi wa kongamano lenye lengo la kutoa elimu ya ujasiriamali kwa wanawake wafanya biashara lililoandaliwa na Benki ya TCB kwaajili ya kuwainua na kuwawezesha wanawake wajasiriamali Mkoa wa Mwanza.

01


Naibu Waziri, Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Bi Angelina Mabula (wapili kulia), pamoja na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa wa Benki ya Biashara ya Tanzania TCB Bw Moses Manyatta, wakikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa kongamano lenye lengo la kutoa elimu ya ujasiriamali lililoandaliwa na Benki ya TCB kwaajilio yakuwainua na kuwawezesha wanawake wafanya biashara Mkoa wa Mwanza, wengine pichani kutoka kushoto ni Meneja Masoko wa Benki hiyo Grace Majige na Meneja wa Bima wa TCB Emanuel Kaganda na kulia ni Mkurugenzi wa Sheria wa Benki ya Biashara ya Tanzania TCB Bi Mystica Mapunda Ngongi, hafla hiyo imefanyika leo jijini Mwanza.


.com/img/a/Naibu Waziri, Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Bi Angelina Mabula, akikagua bidhaa alipotembelea moja ya banda la mfanya biashara na mjasiriamali na mteja wa Benki ya TCB wakati wa uzinduzi rasmi wa kongamano lenye lengo la kutoa elimu ya ujasiriamali kwa wanawake wafanya biashara lililoandaliwa na Benki ya TCB kwaajili ya kuwainua na kuwawezesha wanawake wajasiriamali Mkoa wa Mwanza, wengine ni maofisa wa Benki hiyo.
.com/img/a/ 

Naibu Waziri, Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Bi Angelina Mabula akizungumza wakati wa hafla ya uzinduzi rasmi wa kongamano lenye lengo la kutoa elimu ya ujasiriamali kwa wanawake wafanya biashara lililoandaliwa na Benki ya TCB kwaajili ya kuwainua na kuwawezesha wanawake wajasiriamali Mkoa wa Mwanza


Benki ya Biashara ya Tanzania (TCB) imedhamiria kuinua hadhi ya wanawake nchini kifedha kwa kuwawezesha kiuchumi na kuwasaidia kuwa wajasiriamali shupavu kupitia mikakati mbalimbali endelevu.



Taasisi hiyo kongwe ya fedha nchini imeweka bayana dhamira hiyo wakati wa Kongamano la Wanawake na Biashara la tatu ililoliandaa hapa jana kuwasaidia akinamama kuzing’amua na kuzitumia fursa za kibenki kwa ajili ya maendeleo yao binafsi na taifa kwa ujumla.



TCB imesema itatekeleza jukumu hilo adhimu kwa kuwa kinara wa huduma jumuishi za kifedha za akinamama na kiongozi mbunifu wa huduma hizo sokoni.



Wakiongea kwenye kongamano hilo, maofisa wake waandamizi walisema mafanikio ya jitihada hizo yatatokana na mpango mkakati wa TCB wa kufanya mapinduzi makubwa ya kuwahudumia akinamama.



Aidha, benki hiyo itawaonyesha fursa zinazopatikana TCB na kuwaelimisha jinsi ya kufanya biashara zenye tija. Pia suluhishi za kibenki zilizopo na mpya za kisasa zaidi zitatumika kumkomboa mwanamke kifedha na kumshirikisha kikamilifu katika ujenzi wa taifa.



Wataalamu hao walisema benki hiyo imejiandaa vizuri kwa hilo. Iko imara kifedha, ni uhodari kidijitali na bingwa wa ubunifu ikiwa na wigo mpana wa huduma na mtandao mkubwa wa kuzifikisha popote kwa wakati.



“Tuna mtandao wa matawi makubwa 46, matawi madogo 36, ofisi za wakala za Shirika la Posta Tanzania 120, ATM 84 ambazo zimeunganishwa na ATM 350 za mtandao wa Umoja Switch,” Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu wa TCB, Bw Moses Manyatta alibainisha.



Alisema itakuwa rahisi kuwafikia wanawake wengi na kusaidia kuwawezesha kupitia matawi na vituo vyake vya huduma vilivyosambaa kote Tanzania Bara na Visiwani.



"Pamoja na vikwazo vingi vya kiuchumi wanavyokumbana navyo wanawake na changamoto za kifedha walizonazo, tutahakikisha ajenda ya kuwezesha kiuchumi inafikia malengo yaliyokusudiwa," Bw Manyatta alitabainisha.



"Kupitia makongamano haya, tunataka kubainisha mahitaji maalumu ya kifedha ya akinamama na kuihudumia sehemu hii kubwa ya soko kwa namna ya kipekee,” aliongeza.



Mikutano kama hiyo pia itaandaliwa Zanzibar, Tanga, Arusha na Dar es Salaam kama jukwaa la kuwakutanisha akinamama kujifunza mambo mbalimbali na kuijua zaidi Benki ya TCB na huduma zake.



Kongamano la Wanawake na Biashara la TCB la ufunguzi lilifanyika mwanzoni mwa mwezi huu jijini Dodoma. La jana lililofunguliwa rasmi na Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Angeline Mabula (MB), na liliwajumuisha washiriki wapatao 400 waliotumia mijadala ya pamoja kubadilishana uzoefu, kujuana na kujifunza kutoka kwa wajasiriamali waliofanikiwa.



“Lengo kuu la kuwa na utaratibu huu wa makongamano ya akinamama ni kusaidia kuongeza mchango wao katika uchumi wa taifa kupitia fursa mbalimbali hasa zile zinazopatikana TCB,” Bw Manyatta alifafanua katika wasilisho lake.

Kiongozi huyo alitumia takwimu za mafanikio ya TCB kwa kipindi cha mwaka 2007 hadi 2020 kuonyesha uwezo wa kifedha wa benki hiyo kutimiza jukumu hilo.

Mizania ya TCB ilikua kwa zaidi ya asilimia 1,000 hadi takribani TZS trilioni 1.04 huku mikopo ikiongezeka kwa zaidi ya TZS bilioni 580. Hadi sasa akinamama ambao ni nusu ya wateja milioni moja wa TCB wamekopeshwa zaidi ya TZS bilioni 120.



Kuhusu makongamano hayo ambayo mada yake kuu ni “Nafasi ya Mwanamke katika Kukuza Uchumi wa Taifa”, Mhe. Mabula alisema yamekuja wakati muafaka na yataisadia serikali kuhakikisha hakuna mwanamke anayeachwa nyuma kiuchumi na kimaendeleo.



"Kupitia mpango huu, TCB itatoa mchango mkubwa katika kubadilisha hadhi ya wanawake nchini kifedha na kiuchumi. Nawapongeza kwa kuja na wazo hili na kuwekeza muda na rasilimali kuhakikisha linafanikiwa," alisema Mhe. Mabula.



Aidha, aliitaka benki hiyo isitoe mikopo yake kiholela bila kuhakiki miradi tarajiwa na kutoa miongozo ya kuitumia mikopo hiyo vizuri.



Wachokoza mada ambao wote walikuwa wafanyakazi wanawake wa TCB walisema mikutano hiyo inalenga kuonyesha utayari na uwezo wa benki hiyo kuwasaidia wanawake wajasiriamali.



Walisema TCB inazo fursa lukuki za kibiashara na uwezeshaji kwa ajili yao kupitia huduma maalumu kama akaunti ya Tabasamu na suluhishi mbalimbali kama zile za bima za Nishike Mkono Bima na Kinamama Policy (sera).



Share:

BENKI YA TCB YAAZIMISHA WIKI YA MTEJA KWA KUTOA VYETI KWA WATEJA WAKE

1E1A3180
Afisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya Biashara Tanzania (TCB), Bw Sabasaba Moshingi, (wa pili kulia) akiongoza zoezi la kugongesha glasi kuashiria upendo na furaha kwa wateja wa benki hiyo wakati hafla ya uzinduzi wa Wiki ya Huduma kwa Wateja iliyofanyika leo Jumatano Oktoba 6, 2021 katika makao makuu ya Benki hiyo jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Mkurugenzi Rasilimali watu na Utawala Diana Myonga.
1E1A3188
Afisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya Biashara Tanzania (TCB), Bw Sabasaba akimkabidhi cheti Mteja wa Benki hiyo Goodluck Luhanjo, wakati hafla ya uzinduzi wa Wiki ya Huduma kwa Wateja iliyofanyika leo Jumatano Oktoba 6, 2021 katika makao makuu ya Benki hiyo jijini Dar es Salaam.


BENKI ya Biashara Tanzania TCB imesema hatua ya serikali kuweka mifumo imara ya kifedha imezidi kuziboresha huduma za kifedha nchini ikiwemo kuongeza namba ya watu wanaotumia mifumo rasmi ya kifedha.

Akizungumza katika hafla ya kuadhimisha wiki ya huduma Kwa wateja Mkurugenzi mkuu wa Benki hiyo Sabasaba Moshingi amesema Nia Yao ni kutoa huduma hasa kuwapa fursa wateja wadogo wadogo ambao ndiyo azma ya Serikali na Benki hiyo ya Biashara ya Tanzania.

Moshingi amesema kuwa nia yao nikusogeza huduma rafiki kwa wateja wake ili kuhakikisha kuwa kila mtanzania wa hali ya chini anatumia benki hiyo kwaajili ya uendeshaji wa biashara zao katika Nyanja tofauti.

Kwa upande wao baadhi ya wateja na watumiaji wa mifumo ya kibenki wamesema kitendo Cha baadhi ya taasisi kuanzisha huduma za kuwajali wastaafu imezidi kuongeza weledi hivyo wameishukuru Benki ya TCB kwakuendelea kuwaamini nakuwawezesha kupata mikopo kwa wakati na kwamashart rafiki
Share:

ATE INA MATUMAINI THABITI YA KUTEKELEZA MALENGO NA DIRA YAKE KATIKA USAWA WA KIJINSIA

 WhatsApp%2BImage%2B2021-09-27%2Bat%2B4.16.13%2BPMWaziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera,Bunge,Kazi,Vijana, na Wenye Ulemavu Mh. Jenista Mhagama (MB), akihutubia wageni waalikwa wakati wa kumpongeza na kumuaga Mkurugenzi Mtendaji Mkuu wa Chama cha Waajiri Tanzania (ATE) Dkt. Aggrey Mlimuka, ambaye amemaliza muda wake wa utumishi katika chama hicho. Hafla hiyo iliandaliwa na Chama cha Waajiri Tanzania (ATE) katika Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam jana.WhatsApp%2BImage%2B2021-09-27%2Bat%2B4.16.13%2BPM%2B%25281%2529Mkurugenzi Mtendaji Mkuu wa Chama cha Waajiri Tanzania (ATE) Dkt. Aggrey Mlimuka, akizungumza wakati alipokuwa akiwaaga wafanyakazi wa chama hicho pamoja na wadau mbalimbali baada ya kumaliza muda wake wa utumishi katika chama hicho, katika hafla hiyo Mgeni rasmi alikuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera,Bunge,Kazi,Vijana, na wenye Ulemavu Mh. Jenista Mhagama Hafla hiyo iliandaliwa na Chama cha Waajiri Tanzania (ATE) katika Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam jana.WhatsApp%2BImage%2B2021-09-27%2Bat%2B4.16.14%2BPM%2B%25281%2529

Mkurugenzi Mtendaji mpya wa Chama cha Waajiri Tanzania (ATE)  Wakili Suzanne Ndomba, akihutubia wageni waalikwa wakati wa hafla ya kumpongeza na kumuaga mtanguliziwake, Mkurugenzi Mtendaji Mkuu wa Chama hicho Dkt. Aggrey Mlimuka, ambae amemaliza muda wake wa utumishi wake, kwenye hafla iliyoandaliwa na Chama cha Waajiri Tanzania (ATE) katika Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam jana.
WhatsApp%2BImage%2B2021-09-27%2Bat%2B4.16.14%2BPM%2B%25282%2529

WhatsApp%2BImage%2B2021-09-27%2Bat%2B4.16.15%2BPM
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera,Bunge,Kazi,Vijana, na wenye Ulemavu Mh. Jenista Mhagama (MB) (wapilikushoto), akikabidhi zawadi kwa Mkurungezi Mtendaji wa Chama cha Waajiri Tanzania (ATE) Dkt. Aggrey Mlimuka, iliyotolewa na Chama hicho wakati wa hafla ya kumpongeza na kumuaga mara baada yakumaliza muda wake wa utumishi katika chama hicho kushoto ni Mwenyekiti wa Bodi wa Chama hicho Bi jayne Nyimbo pamoja na Mke wa Dkt. Aggrey Mlimuka.
 


CHAMA cha Waajiri Tanzania (ATE) wamefanikisha tukio kubwa na la kihistoria katika utaratibu wake wa kupokezana uongozi wa ngazi za juu, ambapo Mkurugenzi Mtendaji na Ofisa Mkuu Mtendaji Dk. Aggrey Mlimuka anastaafu na kutoa  fursa kwa awamu mpya ya uongozi chini ya mrithi wake, Suzanne Ndomba.



Pamoja na mabadiliko hayo ni jambo la  kujivunia kwamba katika uwepo wake, ATE imefanikiwa katika kupevuka kishughuli kiasi cha malengo yake kupanuka zaidi ya lile la kudumisha uhusiano kazini, na sasa ni mdau thabiti katika kuhakikisha mazingira ya kufanya biashara Tanzania yanaboreshwa.



Pamoja na hayo, ATE kama taasisi mama inayounganisha waajiri imefanikiwa kuongeza idadi ya wanachama, na vilevile imekuwa ikiibua miradi mbalimbali ambayo imekuwa ikitekelezwa kwa kushirikian na wadau nawashirika mbalimbali.



Mkurugenzi Mtendaji anayemaliza muda wake Dk. Aggrey Mlimuka alisema : “ Mafanikio yaliyofikiwa katika awamu yangu ya uongozi yamewezekana kutokana na ushirkiano wa uongozi    wa sasa na uliopita, pamoja na bodi, na nina wiwa kuona nao pia wanapokea shukurani zao zinazostahili”



Dk.Mlimuka alibainisha kuwa ATE inazo changamoto zake zandani ya taasisi, mojawapo na kubwa zaidi ni ulipaji mdogo wa ada za wanachama. “ Tunatakiwa kufanya mabadiliko makubwa kwenye vyanzo vyetu vya fedha na kuondoa hali ya sasa ambapo pamoja na kwamba ATE ni chama chenye wanachama matajir ilakini  chenyewe kinabakia kuw nimasikini” alisema Dk Mlimuka.



Kama taasisi inayojihusisha na ajira, ATE inaona haya ya sheria za nchi kuhusiana na maswala ya ajira kufanyiwa mabadiliko ili kuendana na hali halisi ilivyo duniani, hasa kutokana na mabadiliko yaliyoletwa na utandawazi. “ Sheria zetu zimepitwa na wakati na hazishabihiani na haliiliyopo. Baadhi ya sheria zilitungwazaidi ya miaka 17 iliyopita na zina mapungufu. Sheria za ajira  hazina budi kuendana na hali halisi ya kisiasa na kiuchumi”, alisema Dk. Mlimika.



“ Nina matumaini kuwa Sheria ya Ajira na Uhusiano Kazini itafanyiwa marekebisho yapasayo ili kuboresha na kuleta ulinganifu katika wajibu na haki za waajiri na wafanyakazi. Natumaini vilevile kuwa ATE  itashiriki ipasavyo na kutoa mchango ili kurekebisha hali hiyo na hivyo kusaidia kupanua ajira. Waajiri hawana budi sasa kuitambua ATE.”



Taasisi ya ATE  bado itaendelea kuimarisha uhusiano kati yake na serikali na wafanyakazi. Maboresho hayo yatasaidia kwa kiasi kikubwa katika kukuza ufanisi kazini, kuongeza kipato cha wafanyakazi na kwa upande wao wafanyakazi watazalisha zaidi, kodi itaongezeka  na kufanya hali ya kifedha ya serikali iimarike. Kuboresha uhusiano kutasaidia kuwepo kwa ajira endelevu na ya uhakika. Wafanyakazi wote katika sekta zote bila kubagua watafaidika na mahusiano mazuri maeneo ya uzalishaji.



Alisema Dk Mlimuka : “ Hadi sasa uhusiano na serikali umekuwa ni mzurisana, kwa kuwa ATE imekuwa ikifanya kazi kwa karibu zaidi na wizara mama, viongozi wa ngazi za juu wa serikali  na muungano wa wafanyakati yaani TUCTA.  Kwa mfano, ATE ni mjumbe wa bodi mbalimbal I za taasisi za umma.”



Kwa upande wa miradi, ATE imekuwa ikiendesha program za  kuzuia ajira za watoto kwa kushirikiana na shirika la Umoja wa Mataifa la maendeleo ya watoto, yaani UNICEF. Vilevile ATE imekuwa ikishiriana na vyama visivyokuwa  vya kiserikali ili kuongeza tija kwa walemavu na kuwaandaa wawe na sifa za kuajirika. Eneo lingiine limekuwa ni katika kuwawezesha wanawake kushika nyadhifa za uongozi,  ambapo mafunzo mbalimbali yamekuwa yakiendeshwa kwa lengo la kuwapa wanawake sifa  zitakazowawezesha kukwea hadi ngazi za juu kabisa za uongozi.



Alisema Mlimuka, “ Kwa siku za usoni, tunategemea kupanua wigo wa mradi huu wa wanawake kujumuisha wanasiasa, ambapo tumepanga kuendesha mafunzo kwa Wabunge wanawake kwa upande wa Tanzania Bara na Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi kwa upande wa Visiwani.”



Hivyo basi, ikiwa imejipanga vyema kutekeleza malengo yake, ATE leo inastahili kuwa na fahari wakati inamkaribisha Mkurugenzi Mtendaji na Ofisa Mkuu Mtendaji mpya, Suzanne Ndomba, ambaye ni matokeo ya program hiyo ya ATE ya kuwawezesha  wanawake na kuwaweka tayari kushika nyadhifa za juu za uongozi.



“ ATE imefanya kwa vitendo falsafa yake kwa kutumia mafunzo hayo vyema. Nikiwa moja wa waliofaidika na program hiyo, itoshe kusema tuna uwezo, weledi, uzoefu na sifa ambavyo vinatuwezesha kushika nyadhifa za juu za unongozi vyema,” alisema Suzanne Ndomba. “ Nina msimamo wangu na nina uwezo wa kufanya maamuzi, hata hivyo ninakaribisha maoni na ushauri kutoka kwa wadau mbalimbali. Uongozi unahitaji ushirikiano, na kiongozi si lazima  awe anafahamu kila kitu.”



Akigusia kuhusu dira ya ATE, Suzanne alisema dira hiyo imebeba azma ya ATE ya kuhakikisha inatoa mchango kwenye kuboresha mazingira ya kufanya biashara Tanzania. “ Tutahakikisha tunatekelzea dira hiyo, na nichukue fursa hii kuwahakikishia wadau ya kuwa ATE itaendelea kuwa sauti ya waajiri Tanzania,” alisema.



“Tutaendeela kufanya kazi kwa karibu zaidi na serikali katika kuboresha mazingira ya kufanya biashara nchini. Kwa Upande wetu, ATE tunaridhishwa na hatua ambazo zimekwisha chukuliwa na Rais Samia Suluhu Hassan kuboresha mazingira ya kufanya biashara Tanzania.”

Kuhusiana na kupanua wigo wa wanachama, Mkurugenzi Mtendaji na Ofisa Mkuu Mtendaji mpya Suzanne Ndomba amesisitiza haja ya waajiri kujiunga na ATE.  Alisema kama taasisi mama inayounganisha waajiri wote, shughuli za ATE  zinazaa manufaa yasiyobabu ambayo mwisho  siku yananufaisha waajiri wote katika sekta zote.



“ Hivyo basi, natoa wito kwa waajiri wasio wanachama kujiunga na ATE na kuongeza nguvu kwenye utakelezaji wa malengo yake. Ili ATE ifanikiwe, inatakiwa waajiri wote wawe wanachama wa taasisi hii,” alisema Suzanne. “ Mimi kama Mkurugenzi  Mtendaji na Ofisa Mkuu Mtendaji  mpya  nitahakikisha kuwa  naongeza idadi ya wanachama kwa kuhakikisha kila mwajiri anakuwa mwanachama wa ATE.”

Share:

TCB YABAINISHA MIKAKATI YA KUWAWEZESHA WANAWAKE KIUCHUMI

 d9695962-3f71-43d3-8b66-d2dc26f5d3a2

Naibu Spika wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Tulia Ackson (katikati) Mkuu wa Wilaya ya Mbeya Dkt Rashid Chuachua kushoto pamoja na Mtendaji Mkuu wa TCB, Bw Sabasaba Moshingi wakishangilia jambo wakati wa Kongamano la Wanawake na Biashara la pili lililoandaliwa na Benki hiyo kwa lengo la kuwasaidia wakinamama kuzing’amua na kuzitumia fursa za kibenki kwa ajili ya maendeleo yao binafsi na taifa kwa ujumla. Hafla hiyo imefanyika leo jijini mbea ambapo mgeni rasmi alikuwa Naibu Spika wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Tulia AcksonWhatsApp%2BImage%2B2021-09-24%2Bat%2B02.58.00

Naibu Spika wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Tulia Ackson (katikati) akimsikiliza mmoja wa Mteja wa Benki ya Biashara ya Tanzania na mnufaika wa huduma wa Benki hiyo wakati wa Kongamano la Wanawake na Biashara la pili lililoandaliwa na Benki hiyo kwa lengo la kuwasaidia wakinamama kuzing’amua na kuzitumia fursa za kibenki kwa ajili ya maendeleo yao binafsi na taifa kwa ujumla. wengine pichani ni Mtendaji Mkuu wa TCB, Bw Sabasaba Moshingi  pamoja na maofisa wengine kutoka TCB.WhatsApp%2BImage%2B2021-09-24%2Bat%2B02.55.49


Benki ya Biashara ya Tanzania (TCB) imedhamiria kuinua hadhi ya wanawake nchini kifedha kwa kuwawezesha kiuchumi na kuwasaidia kuwa wajasiriamali shupavu kupitia mikakati mbalimbali endelevu.


Taasisi hiyo kongwe ya fedha nchini imeweka bayana dhamira hiyo wakati wa Kongamano la Wanawake na Biashara la pili ililoliandaa hapa jana kuwasaidia akinamama kuzing’amua na kuzitumia fursa za kibenki kwa ajili ya maendeleo yao binafsi na taifa kwa ujumla.

 

TCB imesema itatekeleza jukumu hilo adhimu kwa kuwa kinara wa huduma jumuishi za kifedha za akinamama na kiongozi mbunifu wa huduma hizo sokoni.

 

Wakiongea kwenye kongamano hilo, maofisa wake waandamizi walisema mafanikio ya jitihada hizo yatatokana na mpango mkakati wa TCB wa kufanya mapinduzi makubwa ya kuwahudumia akinamama.

 

Aidha, benki hiyo itawaonyesha fursa zinazopatikana TCB na kuwaelimisha jinsi ya kufanya biashara zenye tija. Pia suluhishi za kibenki zilizopo na mpya za kisasa zaidi zitatumika kumkomboa mwanamke kifedha na kumshirikisha kikamilifu katika ujenzi wa taifa.

 

Wataalamu hao walisema benki hiyo imejiandaa vizuri kwa hilo.Iko imara kifedha, ni uhodari kidijitali na bingwa wa ubunifu ikiwa na wigo mpana wa huduma na mtandao mkubwa wa kuzifikisha popote kwa wakati.

 

“Tuna mtandao wa matawi makubwa 46, matawi madogo 36, ofisi za wakala za Shirika la Posta Tanzania 120, ATM 84 ambazo zimeunganishwa na ATM 350 za mtandao wa Umoja,” Afisa Mtendaji Mkuu wa TCB, Bw Sabasaba Moshingi alibainisha.

 

Alisema itakuwa rahisi kuwafikia wanawake wengi na kusaidia kuwawezesha kupitia matawi na vituo vyake vya huduma vilivyosambaa kote Tanzania Bara na Visiwani.

 

"Pamoja na vikwazo vingi vya kiuchumi wanavyokumbana navyo wanawake na changamoto za kifedha walizonazo, tutahakikisha ajenda ya kuwezesha kiuchumi inafikia malengo yaliyokusudiwa," Bw Moshingi alitabainisha.

 

"Kupitia makongamano haya, tunataka kubainisha mahitaji maalumu ya kifedha ya akinamama na kuihudumia sehemu hii kubwa ya soko kwa namna ya kipekee,” aliongeza.

 

Mikutano kama hiyo pia itaandaliwa Zanzibar, Morogoro, Arusha, Mwanza na Dar es Salaam kama jukwaa la kuwakutanisha akinamama kujifunza mambo mbalimbali na kuijua zaidi Benki ya TCB na huduma zake.

 

Kongamano la Wanawake na Biashara la TCB la ufunguzi lilifanyika mwanzoni mwa mwezi huu jijini Dodoma. La jana lililofunguliwa rasmi na Naibu Spika, Dkt Tulia Ackson, na liliwajumuisha washiriki wapatao 250 waliotumia mijadala ya pamoja kubadilishana uzoefu, kujuana na kujifunza kutoka kwa wajasiriamali waliofanikiwa.

 

“Lengo kuu la kuwa na utaratibu huu wa makongamano ya akinamama ni kusaidia kuongeza mchango wao katika uchumi wa taifa kupitia fursa mbalimbali hasa zile zinazopatikana TCB,” Bw Moshingi alifafanua katika wasilisho lake.

 

Kiongozi huyo alitumia takwimu za mafanikio ya TCB kwa kipindi cha mwaka 2007 hadi 2020 kuonyesha uwezo wa kifedha wa benki hiyo kutimiza jukumu hilo.

 

Mizania ya TCB ilikua kwa zaidi ya asilimia 1,000 hadi takribani TZS trilioni 1.04 huku mikopo ikiongezeka kwa zaidi ya TZS bilioni 580. Hadi sasa akinamama ambao ni nusu ya wateja milioni moja wa TCB wamekopeshwa zaidi ya TZS bilioni 120.

 

Kuhusu makongamano hayo ambayo mada yake kuu ni “Nafasi ya Mwanamke katika Kukuza Uchumi wa Taifa”, Dkt Ackson alisema yamekuja wakati muafaka na yataisadia serikali kuhakikisha hakuna mwanamke anayeachwa nyuma kiuchumi na kimaendeleo.

 

"Kupitia mpango huu, TCB itatoa mchango mkubwa katika kubadilisha hadhi ya wanawake nchini kifedha na kiuchumi. Nawapongeza kwa kuja na wazo hili na kuwekeza muda na rasilimali kuhakikisha linafanikiwa," alisema Dk Tulia.

 

Wachokoza mada ambao wote walikuwa wafanyakazi wanawake wa TCB walisema mikutano hiyo inalenga kuonyesha utayari na uwezo wa benki hiyo kuwasaidia wanawake wajasiriamali.

 

Walisema TCB inazo fursa lukuki za kibiashara na uwezeshaji kwa ajili yao kupitia huduma maalumu kama akaunti ya Tabasamu na suluhishi mbalimbali kama zile za bima za Nishike Mkono Bima na Kinamama Policy.

Share:

LILIAN-FAVOUR MAKAWA

LILIAN-FAVOUR MAKAWA

Popular Posts

Blog Archive

Labels

Recent Posts

Label Cloud

BIASHARA (275) BURUDANI (4) KIMATAIFA (10) KITAIFA (119) MICHEZO (38) SIASA (3)

Pages