AKIBA COMMERCIAL BANK PLC YAANDAA JUKWAA LA WATEJA MKOANI MBEYA ZAIDI YA WATEJA 150 WASHIRIKI.

   Tanzania – 18 Juni 2025 – Akiba Commercial Bank Plc (ACB) iliandaa mkutano Maalum wa Wateja jijini Mbeya lililowakutanisha zaidi ya wateja 150 kutoka sekta mbalimbali, kwa lengo la kuimarisha mahusiano na kuwataarifu wateja kuhusu maendeleo ya Benki pamoja na fursa mbali mbali za kuwainua wateja kiuchumi.

Jukwaa hili lililenga kutoa taarifa kuhusu maendeleo ya hivi karibuni ya benki, hususan katika huduma za kidijitali na maboresho ya uzoefu wa wateja. Aidha, lilitumika kama jukwaa la kutoa elimu ya kifedha kwa wateja ili kuwasaidia kufanya maamuzi sahihi ya kifedha. Wateja walishiriki kikamilifu kwa kutoa maoni, mrejesho na mapendekezo kuhusu huduma za benki.


Benki ilitumia fursa hiyo kusikiliza, kujifunza na pia kutoa shukrani kwa wateja wake kwa uaminifu na ushirikiano wao wa muda mrefu. Akizungumza katika tukio hilo, Bi. Wezi Mwazani, Afisa Mkuu wa Biashara wa Benki ya Akiba, alitoa pongezi kwa mwitikio mkubwa na kusema: "Mwonekano wa ushiriki huu mkubwa unatupa faraja kuwa wateja wetu wanatuamini na wamechagua Akiba kama Benki yao pendwa. Hatuchukulii jambo hili kuwa la kawaida, na tunaendelea kujitolea kuwahudumia kwa ubora siku zote.


" Bw. Ntupa, Kiongozi wa Jumuiya ya Wafanyabiashara wa Soko la Mbeya, alipongeza juhudi za Benki kwa kuandaa jukwaa lenye maana kubwa, hasa kwa kuweka kipaumbele kwenye elimu ya kifedha. "Majukwaa kama haya ni muhimu kwa maendeleo ya biashara, yanatoa maarifa kwa wateja wetu na kuimarisha uhusiano wa kuaminiana kati ya benki na jamii ya wafanyabiashara," alisema Bw. Mtupa. Akihitimisha tukio hilo,
Afisa Biashara Mkuu wa Akiba Commercial Bank Plc Bi. Wezi Mwazani akifungua mkutano wa wateja ulioandaliwa na benki hiyo mkoani mbeya.

Bw. Humphrey Nyandidi, Meneja wa Tawi la Mbeya, alishukuru wateja kwa ushirikiano wao na kuahidi kuendelea kuwahudumia kwa bidii na kujituma. "Tunathamini sana uaminifu wenu, na tunaahidi kuendelea kuwahudumia kwa ari na moyo wa dhati ili kutimiza matarajio yenu na hata kuvuka kiwango hicho," alisema. Jukwaa hili la wateja ni sehemu ya mkakati mpana wa Benki ya Akiba wa kuimarisha mahusiano na wateja wake kupitia majukwaa ya majadiliano na mirejesho kutoka kwa wateja. Benki inaendelea kujikita katika kutoa huduma shirikishi za kifedha pamoja na elimu ya fedha.

Share:

AKIBA COMMERCIAL PLC YASHIRIKIANA NA TIA KUPANDA MITI 1,500 KATIKA KAMPENI YA UTUNZAJI WA MAZINGIRA

Dar es Salaam, 13 Juni 2025: Akiba Commercial Plc imeonyesha dhamira yake endelevu ya kutunza mazingira kupitia zoezi la kupanda miti kwa ushirikiano na Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA) katika kampasi ya Kurasini, Dar es Salaam. Miti 1,500 imepandwa kama sehemu ya mpango wa Uwajibikaji kwa Jamii (CSR) unaolenga kukuza utunzaji wa mazingira na kuimarisha ustawi wa jamii. Zoezi hilo liliongoza na Afisa Biashara Mkuu wa Benki hiyo Bi. Wezi Mwazani (Picha ya kwanza) kwa kushirikiana na wafanya kazi wengine pamoja na wanafunzi wa TIA.

Akizungumza kwa niaba ya benki katika tukio hilo, Bwana Emmanuel Mseti, Meneja Mwandamizi wa Kitengo cha Wateja Binafsi, alitoa shukrani za dhati kwa uongozi, wafanyakazi na wanafunzi wa TIA kwa mapokezi na ushirikiano mzuri uliowezesha mafanikio ya shughuli hiyo ya kimazingira. Alibainisha kuwa zoezi hili si ishara tu bali ni kitendo kinachoonyesha imani ya Benki kwamba kulinda mazingira ni jukumu la pamoja.
Shughuli hii ni mfano halisi wa imani yetu kuwa kulinda mazingira ni jukumu la kila mmoja wetu. Jukumu letu halikomi tu kwenye kupanda miti peke yake bali, tunaendelea kuhimiza huduma rafiki kwa mazingira kupitia huduma zetu za kidijitali kama ACB Mobile, Internet Banking na Akiba Wakala, ambazo si tu huongeza urahisi na ufanisi, bali pia hupunguza matumizi ya karatasi na kuunga mkono utunzaji wa mazingira,” alisema Bwana Mseti.
Benki pia ilibainisha juhudi zake nyingine za utunzaji wa mazingira ikiwemo jukumu endelevu la kutunza na kuboresha Viunga vya Independence Square jijini Dodoma. Katika tukio hilo, Bwana Mseti aliwahimiza wanafunzi wa TIA kuchukua jukumu la kulinda miti iliyopandwa na kuhakikisha inakua vizuri kwa faida ya vizazi vijavyo.

Pia aliwahakikishia kuwa Benki itaendelea kushirikiana na TIA katika kampeni za mazingira katika kampasi zake nyingine pindi itakapohitajika.

Kwa mtazamo wa Uwajibikaji kwa Jamii, Akiba Commercial inaamini kuwa kwao kurudisha kwa jamii si chaguo bali ni wajibu.

Kupitia sekta za afya, elimu, uwezeshaji wa kiuchumi, na utunzaji wa mazingira, Benki imejitolea katika maendeleo jumuishi na endelevu yanayonufaisha jamii inayoihudumia.

Ili kupata taarifa zaidi kuhusu ushiriki wetu katika maswala ya kijamii na huduma za kibenki kwa ujumla, tafadhali skani QR yetu hapa chini.
Share:

UWT TANGA YAKUNWA NA UCHAPAKAZI WA MBUNGE UMMY MWALIMU

Na - Mwandishi Wetu, TANGA

Jumuiya ya Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) imempongeza Mbunge wa Jimbo la Tanga Mjini, Ummy Mwalimu, kwa uchapakazi na uwajibikaji wake wa kuwaletea wananchi maendeleo na namna anavyoilea Jumuiya hiyo muhimu kwa uhai wa Chama.

Pongezi hizo zimetolewa na Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo wilaya ya Tanga, Bi. Moza Seif, katika Baraza lake la Kikanuni lililokaa Juni 12, 2025 katika Ukumbi wa CCM wilaya ya Tanga ambapo pamoja na mambo mengine, Baraza hilo lilikuwa na ajenda ya kusoma Utekelezaji wa Ilani kwa Madiwani wa Viti Maalum wa Jiji la Tanga.

Bi. Moza amempongeza Mbunge Ummy Mwalimu ambaye amekuwa bega kwa bega na Jumuiya hiyo katika kusukuma gurudumu la maendeleo ndani ya Jiji la Tanga. Katika kuunga mkono juhudi za maendeleo zinazofanywa na Mbunge huyo, uongozi wa UWT Tanga ulimpatia Mbunge Ummy Mwalimu Zawadi mbalimbali za Pongezi ambazo zilipokelewa na Bi. Mwanahawa Mwalimu kwa niaba ya Mbunge.

Sambamba na hilo, Madiwani wa Viti Maalum wa Jiji la Tanga walisoma Utekelezaji wa Ilani ambapo kazi nyingi na miradi mingi ya maendeleo imefanyika katika kipindi cha uongozi wao. Aidha, wanachama wameaswa kuwa wamoja kuelekea Uchaguzi Mkuu Mwezi Oktoba, 2025 kwa kuepuka fitna, majungu na makundi.

Katika hatua nyingine, Baraza hilo lilihudhuriwa viongozi mbalimbali wa Chama wakiwemo Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Tanga, Meja Mstaafu Hamisi Bakari Mkoba ambaye alikuwa Mgeni Rasmi pamoja na Katibu wa CCM wilaya ya Tanga, Jamal Khimji.
Share:

Mkurugenzi wa Benki ya DCB, Sabasaba Moshingi aongoza wafanyakazi wa benki hiyo kujitolea damu wakiadhimisha Siku ya Wachangia damu Duniani

Ofisa Mtendaji Mkuu wa Hospitali ya Aga Khan, Bw. Sisawo Konteh (Kulia) akishikana mikono na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya DCB, Bw.Sabasaba Moshingi, wakati yeye na baadhi ya wafanyakazi wa benki hiyo walipofika hospitalini hapo kujitolea damu kuadhimisha Siku ya Wachangiaji Damu Duniani, jijini Dar es Salaam Leo.

BENKI ya Biashara ya DCB imesema itaendelea kufanya jitihada tofauti katika kusaidia afya za watanzania wenye uhitaji wa kupata damu kutokana na kukabiliwa na changamoto mbalimbali imeelezwa jijini Dar es Salaam leo.

Akizungumza katika zoezi la kujitolea damu kama sehemu ya maadhimisho ya Siku ya Wachangia Damu Duniani, jijini Dar es Salaam leo, Mkurugenzi Mtendaji wa DCB, Bw. Sabasaba Moshingi alisema yeye pamoja na baadhi ya wafanyakazi wenzake wameamua kujitolea damu kwani licha ya benki yao kujishughulisha na utoaji wa huduma za kifedha lakini pia wanabeba jukumu la kuhakikisha watu wanaohitaji damu salama mahospitalini wanazipata bila kuwa na haja ya kusubiria ndugu waje kujitolea.

Leo tupo hapa pamoja na washirika wenzetu hospitali ya Aga Khan kwa lengo la kuchangia damu, tutaendelea kushiriki matukio mengine kama haya na mengineyo yenye lengo la kusaidia kuokoa maisha ya watanzania wenzetu wenye uhitaji wa damu na mahitaji mengine ya kibidamu”, alisema Bw. Moshingi.

Akizungumza katika hafla hiyo Mkuu wa Kitengo cha Maabara katika Hosptali ya Aga Khan, Dk. Caroline Ngimba alitoa hamasa kwa watanzania wote nchini kuwa na moyo na utamaduni wa kujitolea damu bila kusubiri siku rasmi za kitaifa ama kimataifa bali liwe ni jambo endelevu kwani uhitaji wa damu upo kila siku mahospitalini.

Uzuri ukichangia damu kama afya inaruhusu kila baada ya miezi mitatu unaweza kuchangia tena, tungeomba tabia hii iwe endelevu kwani hakuna kiwanda cha kutengeneza damu, damu inayopewa mwanadamu inatoka kwa mwanadamu”, alisema Dk. Caroline.

Naye mtaalamu wa utoaji damu kutoka Mpango wa Taifa wa Damu Salama, Peter Chami alitoa shukurani kwa Benki ya DCB, huku akizitaka taasisi nyingine kuiga mfano wa benki hiyo ili kuokoa maisha ya watanzania wenye shida ya damu kwani mahitaji ya damu ni makubwa sana.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya DCB, Bw.Sabasaba Moshingi, akifanyiwa uchunguzi wa afya yake kabla hajajitolea damu katika Hospitali ya Aga Khan, Dar es Salaam leo, alipongoza baadhi ya wafanyakazi wa benki hiyo kujitolea damu, kuadhimisha Siku ya Wachangiaji Damu Duniani. Picha nyingine zikionesha matukio mbalimbali katika hafla hiyo.
Mkurugenzi wa Mikopo wa Benki ya DCB, Bw. Deogratius Thadei, akijitolea damu katika hafla ya maadhimisho ya Siku ya Wachangiaji Damu Duniani, katika Hospitali ya Aga Khan, Dar es Salaam leo, ambako yeye pamoja na baadhi ya wafanyakazi wenzake walishiriki. Kushoto ni Mkuu wa Kitengo cha Maabara, Dk. Caroline Ngimba na kulia ni Mtaalamu wa mishipa Kutoka Mpango wa Taifa wa Damu Salama, Bw. Peter Chami.
Baadhi ya wakurugenzi wa Benki ya DCB, waliojitolea damu pamoja na baadhi ya wafanyakazi wengine wa benki hiyo wakati wa maadhimisho ya Siku ya Wachangia damu Duniani katika Hospitali ya Aga Khan, Dar es Salaam, leo.
Baadhi ya wafanyakazi wa Benki ya DCB, wakishiriki zoezi la uchangiaji damu Ili kusaidia wenye uhitaji ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Siku ya Wachangia damu Duniani, jijini Dar es Salaam leo.
Baadhi ya wafanyakazi wa Benki ya DCB, wakijitolea damu kusaidia wenye uhitaji ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Siku ya Wachangia damu Duniani, jijini Dar es Salaam leo.
Share:

Benki ya Absa Tanzania Yathibitisha Uwazi na Dhamira ya Ukuaji Katika Mkutano na Gavana wa BoT

Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Bw. Emmanuel Tutuba (katikati), akizungumza na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Obedi Laiser (wa tatu kutoka kushoto), wakati wa ziara yao katika ofisi ya gavana jijini Dar es Salaam jana. Ujumbe huo ulifanya mazungumzo ya kina na gavana, ukimpa taarifa kuhusu masuala muhimu yakiwemo utendaji wa kifedha wa benki hiyo, sera za faragha na ulinzi wa taarifa, mipango ya ukuaji na upanuzi, maendeleo ya udhibiti, na maeneo mengine muhimu ya kipaumbele kama Utawala wa Mazingira, Jamii na Uongozi (ESG) pamoja na huduma za kijamii, ikionesha dhamira thabiti ya taasisi hiyo ya kifedha kwa uwazi, ulinganifu wa udhibiti na ukuaji endelevu. Kutoka kushoto ni Kaimu Mkurugenzi wa Kitengo cha Sheria na Udhibiti wa Benki ya Absa, Bw. Alistides Kashasira na Afisa Mkuu wa Uendeshaji, Bw. Oscar Mwamfwagasi. Kulia ni baadhi ya maafisa kutoka Benki Kuu.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Obedi Laiser (wa tatu kutoka kushoto), akizungumza na Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Bw. Emmanuel Tutuba (kulia), wakimtembelea gavana ofisi kwake, jijini Dar es Salaam jana. Ujumbe huo ulifanya mazungumzo ya kina na gavana, ukimjulisha kuhusu masuala muhimu yakiwemo utendaji wa kifedha wa benki hiyo, sera za faragha na ulinzi wa taarifa, mipango ya ukuaji na upanuzi, maendeleo ya udhibiti, na maeneo mengine muhimu ya kipaumbele kama Utawala wa Mazingira, Jamii na Uongozi (ESG) pamoja na huduma za kijamii, yakionesha dhamira ya benki hiyo katika uwazi, kuzingatia kanuni na ukuaji endelevu. Kutoka kushoto ni Kaimu Mkurugenzi wa Kitengo cha Sheria na Udhibiti wa Absa, Bw. Alistides Kashasira na Afisa Mkuu wa Uendeshaji, Bw. Oscar Mwamfwagasi.
Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Bw. Emmanuel Tutuba (kulia), akiagana na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Obedi Laiser (kushoto), pamoja na ujumbe wake, mara baada ya kikao kilichofanyika katika ofisi ya gavana jijini Dar es Salaam jana. Ujumbe huo ulifanya mazungumzo ya kina na gavana, ukimpa taarifa juu ya masuala muhimu yakiwemo utendaji wa kifedha wa benki, sera za faragha na ulinzi wa taarifa, mipango ya ukuaji na upanuzi, maendeleo ya udhibiti, pamoja na maeneo mengine muhimu kama Utawala wa Mazingira, Jamii na Uongozi (ESG) na huduma za kijamii, yakionesha dhamira thabiti ya benki hiyo kwa uwazi, ulinganifu wa udhibiti na maendeleo endelevu.
Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Bw. Emmanuel Tutuba (wa nne kutoka kushoto), na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Obedi Laiser (wa tatu kutoka kushoto), wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya maafisa waandamizi kutoka Benki ya Absa na Benki Kuu jijini Dar es Salaam jana, wakati wa ziara ya ujumbe wa Absa katika ofisi ya gavana. Kupitia mazungumzo ya wazi na ushirikiano na benki kuu, Benki ya Absa inaendelea kulinganisha malengo yake na vipaumbele vya kitaifa na kuchangia kikamilifu katika mustakabali wa kifedha wa nchi.
Share:

Akiba Commercial Bank Yakutana na Wateja wa Mwanza: Zaidi yaWateja 250 Wahudhuria Mkutano wa Mahusiano

Mkurugenzi Mtendaji wa Akiba Commercial Bank Plc, Bw. Silvest Arumasi (katikati), akizungumza na wateja wa Benki hiyo mkoa wa Mwanza wakati wa hafla ya kukuza na kuimarisha mahusiano na wateja hao pamoja na kupokea mrejesho kwa ajili ya kufanya maboresho ya bidhaa pamoja na viwango vya huduma. wengine pichani kutoka kushoto ni Afisa Biashara Mkuu wa ACB, Bi. Wezi Mwazani pamoja na mwakilishi wa wafanya Biashara wa soko kuu la Mwanza.
Meneja wa Akiba Commercial Bank Tawi la Mwanza Bw.Emmanuel Makula akitambulisha timu yake ya ushindi ya Tawi hilo Wakati wa hafla ya kukuza na kuimarisha mahusiano na wateja wa benki hiyo mkoa wa mwanza.

Benki ya Akiba imeendelea kuonyesha dhamira yake ya kuwa karibu na wateja kwa kuandaa mkutano maalum na wateja wa Mwanza uliofanyika tarehe 22 Mei 2025 katika ukumbi wa Gold Crest Hotel.

Tukio hili lilivutia zaidi ya wateja 250, ikiwa ni ishara ya hamasa kubwa na utayari wa jamii ya Kanda ya Ziwa kunufaika na huduma Benki hiyo.

Katika mkutano huo wa ana kwa ana, wateja walipata nafasi ya kuzungumza moja kwa moja na viongozi waandamizi wa benki, kutoa maoni yao kuhusu huduma, kueleza changamoto wanazokutana nazo katika shughuli za kifedha, pamoja na kujifunza kuhusu huduma na bidhaa mpya za benki.

Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Akiba, Bw. Silvest Arumasi, alipata nafasi ya kuzungumza na wateja na kueleza kuwa mkutano huu ni sehemu ya mikakati ya Benki katika kuimarisha mawasiliano na wateja wake. Alisema:

Benki ya Akiba inaamini katika kusikiliza wateja wake. Lengo letu ni kuelewa vizuri zaidi mahitaji yao halisi ili tuweze kutoa huduma zinazogusa maisha yao kwa namna chanya, hasa katika mazingira yao ya kila siku.

Bw. Arumasi aliongeza kuwa benki inaendelea kuweka mkazo katika kutoa msaada kwa wafanyabiashara wadogo na wa kati kwa kuwapa jukwaa la kuzungumza moja kwa moja na wataalamu wa kifedha na kupata ushauri wa kibiashara wenye manufaa ya moja kwa moja.

Afisa Mkuu wa Biashara, Bi. Wezi Mwanzani, alieleza kuwa mwitikio mkubwa wa wateja wa Mwanza ni ushahidi wa Imani ya Wakazi wa Mwanza kwa Benki ya Akiba pamoja na uhitaji mahitaji mkubwa wa huduma za kifedha. Alisema

Tunashukuru kwa mwitikio mzuri kutoka kwa wateja wa Mwanza. Kama benki, tutaendelea kutoa huduma bunifu na zinazolenga kumsaidia mteja katika uhalisia wa biashara zake. Mwanza ni sehemu muhimu ya mpango wetu wa kuhakikisha huduma zetu zinawafikia watu wote.

Bi. Wezi alisisitiza kuwa dhamira ya benki ni kuijenga jamii jumuishi kifedha, kwa kuhakikisha watu wote wanapata nafasi sawa ya kutumia huduma za kifedha kama njia ya kujikwamua kiuchumi.

Mbali na majadiliano, tukio hili pia liliambatana na utoaji wa elimu ya kifedha. Wateja walielimishwa kuhusu usimamizi wa fedha binafsi na za biashara, matumizi salama ya huduma za kidijitali kama benki mtandao na miamala kwa njia ya simu, pamoja na mbinu bora za kukuza biashara kwa njia endelevu.
Share:

Startups reimagining farming through digital mechanization.

In the heart of the country, where smallholder farmers have long relied on traditional tools like hoes and ox-plows, a new generation of agricultural startups is sowing the seeds of transformation.


Young entrepreneurs are reimagining farming by introducing affordable mechanization solutions that are bridging the productivity gap and driving food security.


One such trailblazer is Greenbiz Limited, a startup based in Kisongo, Arusha. This is a platform that captures what farmers are already doing, how much they save weekly, how they repay loans, and their farming activities and turns that into a digital credit profile.


Co-founder Daniel Elibariki says that the idea was born from a simple but powerful realization: rural farmers, especially women, were doing everything right; saving weekly, working hard, and forming cooperative groups, yet remained locked out of formal finance because they lacked collateral. 
“We saw these groups, known as Village Community Bank (VICOBA), as a foundation we could build on.
 By digitizing their financial records and aggregating their data, we realized we could build a trust bridge between these farmers and banks. That’s how the journey started out of a desire to make finance fairer and more inclusive for the people who need it most,” he says.


The startup addresses the financing gap for smallholder farmers, particularly the lack of access to credit due to traditional collateral requirements.


Agriculture contributes over 25 percent to Tanzania’s GDP, yet most smallholder farmers still rely on informal lending or personal savings. Without finance, there's no mechanization, no inputs, and no scaling. Given the growing threats from climate change and food insecurity, closing this gap has never been more urgent.


The company uses the profiles to secure collateral-free loans from partner banks and integrates agricultural advisory and sensor technology to help farmers make data-driven decisions and the result is that a farmer wakes up not just hoping for rain, but knowing when to plant, how much to borrow, and where to improve.

 
“We are focused on micro-mechanization, tools and technologies that fit the scale and budget of smallholder farmers. Things like soil sensors, drip irrigation kits, and precision planting tools. These might seem small, but for a farmer using only hand tools, they’re game-changers. We're filling the gap between traditional labor and full-scale mechanization, which is often unaffordable or unsuitable for small farms,” Elibariki says.
Elibariki says that one of the biggest hurdles in their operations has been digital and financial literacy.


“Farmers need to understand not just how to use our platform or devices, but why they matter. That’s why training is central to our model. We host in-person sessions and partner with local leaders and youth to serve as digital champions in each village. Building trust has also been key, most rural communities have been burned by “solutions” that disappeared after a pilot,” he adds.


Grenbiz Limited is among the beneficiaries of KilimoTech Accelerator. The brainchild of Youth Entrepreneurship for the Future of Food and Agriculture (YEFFA), the strategic initiative is supported by Alliance for a Green Revolution in Africa (AGRA) and implemented by Sahara Accelerator and aims to accelerate digital innovations in agricultural mechanization for Tanzania's smallholder farmers.

Emmanuel Senzighe, Kilimotech Accelerator Project Manager, says that The project focuses on enhancing productivity and sustainability in the sunflower, maize, horticulture, and rice value chains by supporting Agritech startups (Agripreneurs) and fostering partnerships among key stakeholders.


The program focuses on scaling Agritech startups (Agripreneurs) by providing tailored support, technical and business diagnostics, and technical mentorship. By connecting young women and men SMEs to mechanization, irrigation, and financial service providers, Kilimotech Accelerator fosters a vibrant ecosystem of innovators, startups, and key stakeholders.


This comprehensive approach aims to enhance the productivity of Tanzania’s agriculture sector by leveraging digital platforms to address key barriers such as high equipment costs, limited system integration, and restricted access to financing.


It further enables the most underserved farmers, particularly youth and smallholders, to leapfrog into modern mechanization by making essential technologies more accessible, affordable, and readily available.

   
“GreenBiz is one of nine innovative solutions currently being accelerated with tailored support to refine their offerings and develop proof-of-concept models that can enable scalable impact. The Accelerator is committed to driving sustainable growth and market readiness for these startups through mentorship, targeted workshops, ecosystem engagement, and strategic collaboration, ultimately aiming to expand youth employment and enhance access to mechanization services,” he adds.
      
As for Elibariki, KilimoTech has been instrumental in the growth of their startup and they see a brighter future on the horizon.


“The mentorship helped us refine our product-market fit, the network connected us with potential partners, and the exposure has opened doors to potential investors and partners we wouldn’t have accessed on our own. It’s been a catalyst for our next phase of growth,” he says. 
He notes that they expect a twofold impact from their operations: increased productivity through timely decision-making and smart investments, and a shift in labor dynamics where technology eases the burden on women and youth.

 
“With access to finance and mechanization tools, farmers can cultivate more land, reduce post-harvest losses, and generate higher incomes. Over time, we hope to see less outmigration of rural youth and more pride in farming as a tech-driven profession,” he says.


According to Elibariki, despite their expectations, their journey has not been devoid of surprises or memorable moments.


“One Maasai woman in our pilot group told us that for the first time in her life, she feels like a "bankable" person. That word “bankable” really stuck with us.


 It’s not just about money. It’s about dignity, confidence, and a sense of being seen and valued by the formal system,” he says.


Still, challenges remain. Agritech is tough because you’re dealing with two notoriously hard sectors, agriculture and finance.

 Getting banks to trust community data and getting farmers to trust tech requires patience and consistency, says Elibariki.


“We’ve faced setbacks in infrastructure, resistance to change, and even skepticism from funders. But the impact we’ve seen makes it all worthwhile,” he adds.


Mechanization has traditionally been the missing link in Africa’s agricultural development. 
According to the UN Food and Agriculture Organization, over 60 percent of sub-Saharan farmers still rely on hand tools. But startups are now stepping into this gap with technology tailored to local realities.


Creating an enabling environment for agri-tech startups means investing not just in individual ventures but in the ecosystem itself. 


Governments, donors, and private sector actors have a role to play in supporting research, building infrastructure (like rural connectivity), and shaping policies that promote innovation.


As the digital revolution sweeps through agriculture, the startups that will succeed are those with both the tools to build and the vision to lead. 


By equipping innovators with the right mix of business savvy and technical depth, we can unlock the full potential of technology to power a more resilient and productive future for farming.
And hopefully, somewhere out there, investors are taking note.
Share:

LILIAN-FAVOUR MAKAWA

LILIAN-FAVOUR MAKAWA

Popular Posts

Blog Archive

Labels

Recent Posts

Label Cloud

BIASHARA (275) BURUDANI (4) KIMATAIFA (10) KITAIFA (119) MICHEZO (38) SIASA (3)

Pages