Benki ya Absa Tanzania kuendelea kusaidia wanafunzi wenye mahitaji maalumu

Meneja Huduma za Jamii wa Benki ya Absa Tanzania, Bi. Abigail Lukuvi (wa pili kushoto) , Mwanafunzi wa Shule ya Uhuru Mchanganyiko, Crispian Thomas na Mkuu wa Shule ya Uhuru Mchanganyiko, Sezaria Kiwango wakikata utepe kuashiria uzinduzi wa kisima kilichojengwa na wafanyakazi wa benki hiyo jijini Dar es Salaam jana. Ni mwendelezo wa wafanyakazi wa benki hiyo kufanya huduma za kijamii katika shule hiyo Kwa takriban miaka mitatu sasa. Kutoka Kushoto ni Mameneja Rasilimali Watu wa benki hiyo, Bw. Hance Mapunda na Bi. Anna Chacha.
Meneja Rasilimali Watu wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Hance Mapunda (kushoto), Meneja Huduma za Jamii wa Benki ya Absa, Bi. Abigail Lukuvi (wa pili kushoto) , Mwanafunzi wa Shule ya Uhuru Mchanganyiko, Crispian Thomas, Mkuu wa Shule ya Uhuru Mchanganyiko, Bi. Sezaria Kiwango na Meneja Rasilimali Watu mwingine wa benki hiyo, Bi. Anna Chacha wakishangilia baada ya kuzindua kisima kilichojengwa na wafanyakazi wa benki hiyo jijini Dar es Salaam jana.
Meneja Huduma za Jamii wa Benki ya Absa Tanzania, Bi. Abigail Lukuvi (kushoto) akikabidhi kisima kilichojengwa na wafanyakazi wa benki hiyo kwa Mwanafunzi wa Shule ya Uhuru Mchanganyiko, Nabili Tuli jijini Dar ea Salaam jana.
Mkuu wa Shule ya Uhuru Mchanganyiko, Bi. Sezaria Kiwango (kulia), akikabidhi cheti cha shukurani kwa maofisa wa Benki ya Absa Tanzania, mara baada ya kupokea msaada wa kisima Cha maji kilichojengwa na wafanyakazi hao, katika hafla iliyofanyika shuleni hapo, Dar es Salaam jana.
Share:

BENKI YA DCB KUONGEZA MTAJI WA SH BILIONI 10.7

Mkurugenzi wa Usimamizi wa Masoko na Uchunguzi wa Mamlaka ya Masoko ya Mitaji na Dhamana (CMSA), Bw. Exaut Julius (katikati), akikata utepe, kuashiria uzinduzi rasmi wa zoezi la uuzaji wa Hisa za Upendeleo za Benki ya Biashara ya DCB, jijini Dar es Salaam leo. Wa nne kushoto ni Mwenyekiti wa Bodi ya DCB, Bi. Zawadia Nanyaro na wa tatu kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa benki hiyo, Bw. Sabasaba Moshingi pamoja na wawakilishi wa taasisi nyingine waliohudhuria.

*Ni kwa kupitia uuzaji wa Hisa za Upendeleo

BENKI ya Biashara ya DCB, imezindua zoezi ya uuzaji wa Hisa za Upendeleo, ikitarajia kupata zaidi ya sh bilioni 10.7 ili kuongeza kiasi cha mtaji wake unaofikia sh bilioni 15 kwa sasa, ili pamoja na mambo mengine kukidhi vigezo vilivyowekwa na Benki Kuu ya Tanzania (BoT), pamoja na kuwaletea wanahisa wake na watanzania kwa ujumla tija za kiuchumi.

Akizungumza katika hafla ya uzinduzi rasmi wa uuzaji wa hisa hizo jijini Dar es Salaam leo, Mwenyekiti wa Bodi ya DCB, Bi. Zawadia Nanyaro alisema uamuzi huo unaenda sambamba na mikakati yao ya maendeleo ya miaka mitano katika kuongeza mtaji wake kutoka ulipo sasa hadi kufikia sh bilioni 61.

Bodi ya Wakurugenzi ya DCB iliidhinisha mpango mkakati wa miaka mitano ukijikita kwenye mambo makuu Matano; Kwanza kukuza mtaji wa benki kutoka shs bilioni 15 (2024) hadi kufikia shs bilioni 61 ifikapo mwaka 2028, pili ukusanyaji wa amana nafuu za benki kupitia wanahisa wakuu na wateja wetu, tatu kuongeza wigo wa mikopo bora itakayotolewa kwa ufanisi na umahiri, nne utaoaji wa mikopo kwa wateja wadogo wadogo na wa kati ili kuendelea kutimiza lengo la kuanzishwa kwa benki yetu na tano, kuboresha njia za utoaji huduma na kuongeza bidhaa zinazotolewa kwa njia za kijiditali."

Tukio la leo linaenda kuandika historia ya benki na kuanza kutimiza mkakati wa kwanza wa kuongeza mtaji wa benki, hivi sasa, mtaji wa benki uko kwenye kima cha chini kilichowekwa na Benki Kuu ya Tanzania, na ili kuweza kusimama imara kama benki, ongezeko la mtaji ni muhimu sana, benki inadhamiria kufanya biashara kubwa ambapo ili kufanikisha lengo hili, kuna ulazima wa kuongeza mtaji”, alisema Bi. Zawadia.

Mwenyekiti huyo aliongeza kuwa ili kuweza kuhakikisha mtaji wa benki unaendelea kukua mwaka hadi mwaka baada ya zoezi hili na pia kutumiza malengo ya benki, Bodi ya Wakurugenzi iliona ni muhimu kufanya mabadiliko machache ya kiutawala katika menejimenti ya benki yetu, na kumteu Ndugu Sabasaba Moshingi kama Mkurugenzi Mtendaji wa benki mwenye uzoefu wa zaidi ya miaka 20 katika tansia ya benki, huku mabadiliko mengine yakifanyika katika idara ya biashara, mikopo na uendeshaji na teknolojia, idara zote hizi kwa ujumla ni nguzo muhimu katika biashara ya benki.

Alisema uuzaji wa Hisa za upendelo unatarajia kuwaletea wanahisa na watanzania kwa ujumla tija za kiuchumi, baada ya kuongeza mtaji wa benki ambapo unalenga kukuza biashara na kuwapatia wafanyabiashara wadogo wadogo na wa kati mitaji ya kukuza biashara zao na upande mwingine umiliki wa hisa za benki ya DCB unaunga mkono juhudi zinazoendelea za serikali ya awamu ya sita chini ya uongozi shupavu wa Mheshimiwa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan za kuwaletea watu wake maendeleo.

Bodi ya DCB pamoja na Menejimenti ya benki ilipendekeza na kuidhinisha uuzaji wa Hisa za Upendeleo 97,646,913 zenye thamani ya shs 10,741,160,430 kwa bei ya punguzo ya shs 110 kwa kila hisa moja, kinyume na shs 160 iliyopo sokoni, ni matumaini yetu zoezi hii litapata muitikio mkubwa kutoka kwa wanahisa wetu, ambao wana imani na benki hii, bodi na menejimenti yake kwa ujumla."

Benki imerahisisha ununuzi wa hisa kwa kuruhusu ununuzi kwa njia za kidigitali ili kuongeza wigo wa ushiriki wa wanahisa, natoa rai kwa wanahisa kuchangamkia fursa hii ya kununua hisa kwa njia za kidigitali, au kupitia mawakala wa Soko la Hisa la Dar es Salaam au kwa kufika kwenye matawi yetu ya benki”, aliongeza Bi. Nanyaro.

Akizungumza katika hafla hiyo, Mkurugenzi wa Usimamizi wa Masoko na Uchunguzi wa Mamlaka ya Masoko ya Mitaji na Dhamana (CMSA), Bw. Exaut Julius aliipongeza Benki ya DCB kwa uamuzi huo uliofanyika kwa weledi na ufanisi mkubwa na kupata idhini kutoka CMSA.

Akimwakilisha Ofisa Mtendaji Mkuu wa mamlaka hiyo, CPA Nicodemus Mkama, Bwana Julius alisema, serikali kupitia Mamlaka ya Masoko ya Mitaji na Dhamana ina jukumu la kuendeleza na kusimamia masoko ya mitaji hapa nchini, ikiwa ni pamoja na kuhakikisha kwamba shughuli katika masoko ya mitaji zinafanyika kwa kufuata sheria, taratibu na miongozo ili kuleta uwazi na haki kwa washiriki wote.

Mamlaka ya Masoko ya Mitaji na Dhamana itaendelea kujenga mazingira wezeshi na shirikishi ili kuwezesha taasisi katika sekta ya umma na binafsi kutumia masoko ya mitaji kupata fedha za kutekeleza miradi na shughuli za maendeleo ikiwa ni pamoja na kuuza hisa kwa umma, hatifungani za miundombinu, hatifungani rafiki za mazingira, hatifungani za bluu, hatifungani za jamii na hatifungani za taasisi za serikali”, alisema Bw. Julius.

Awali akizungumza katika hafla hiyo, Mkurugenzi Mtendaji wa benki hiyo, Bw. Sabasaba Moshingi alisema, yeye pamoja na menejimenti yote ya DCB wamejipanga kuhakikisha hadi kufikia Mwaka 2028 wanaandika upya historia ya benki hiyo sambamba na mkakati wa miaka mitano wa maendeleo ya benki hiyo wa kuhakikisha benki inaendelea kukua na kupata faida.

Alisema kwa kuthibitisha hayo, benki hiyo imeweza kutengeneza faida katika robo ya pili na ya tatu huku ikiendelea kutoa huduma za kibenki bila kusahau jukumu la kuanzishwa kwake takribani miaka 22 iliyopita ikiweka mkazo mkubwa katika huduma zake za kidigitali ili kuhakikisha watanzania wengi wanafikiwa na huduma za kibenki.

Tumejipanga kuhakikisha benki yetu inaendeleza maono ya kuanzishwa kwake ambayo ni kusaidia miradi ya kupunguza umasikini kwa kutoa mikopo ya mitaji kwa wajasiriamali wadogo na wa kati waliokosa huduma hizi kutokana na kutokidhi vigezo vya benki ya kibiashara za wakati ule."

Uuzaji huu wa Hisa za Upendeleo ambao sasa benki yetu inafanya kwa mara ya nne kwa vipindi tofauti utasaidia kuongeza uwezo wa benki yetu katika kuwahudumia wateja wetu na ni imani yetu pia kuanzia mwakani wanahisa wetu wataweza kuanza kupata gawio hivyo tunaomba waendelee kutuunga mkono”, alisema.
Mkurugenzi wa Usimamizi wa Masoko na Uchunguzi wa Mamlaka ya Masoko ya Mitaji na Dhamana (CMSA), Bw. Exaut Julius (katikati), Mwenyekiti wa Bodi ya DCB, Bi. Zawadia Nanyaro (wa nne kushoto), Mkurugenzi Mtendaji wa benki hiyo, Bw. Sabasaba Moshingi (wa tatu kulia), Ofisa Mtendaji Mkuu wa Soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE), Bw. Peter Nalitolela, wakionesha kitabu chenye taarifa muhimu kuhusu Hisa wakati wa uzinduzi rasmi wa zoezi la uuzaji wa Hisa za Upendeleo za Benki ya DCB, jijini Dar es Salaam leo. Kulia ni Mkurugenzi wa Idara ya Sheria wa DCB, Bi. Regina Mduma, pamoja na wawakilishi kutoka taasisi nyingine waliohudhuria hafla hiyo.
Mkurugenzi wa Biashara wa Benki ya DCB, Bw. Ramadhan Mganga, akizungumza katika hafla hiyo, jijini Dar es Salaam leo.
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Benki ya DCB, Bi. Zawadia Nanyaro, akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa Hisa za Upendeleo za benki hiyo, jijini Dar es Salaam leo. Alisema Bodi na Menejimenti ya benki ilipendekeza na kuidhinisha uuzaji wa Hisa za Upendeleo 97,646,913 zenye thamani ya shs 10,741,160,430 kwa bei ya punguzo ya shs 110 kwa kila hisa moja. Huku bei ya soko ikiwa shs 160.
Share:

STANBIC BANK TANZANIA AND GAIN LAUNCH COHORT 7 OF THE SUPPLIER DEVELOPMENT PROGRAM FOR LOCAL SMES

Head of the Business Incubator Unit from Stanbic Bank Tanzania, Kai Mollel (second right) and the Head of Projects from the Global Alliance for Improved Nutrition (GAIN), Winifrida Mayilla signing the Memorandum of Understanding (MOU) for cooperation in the training phase 7 of the Supplier Development Program. The training aims to empower 50 women and youth, food business owners and operators. The event took place on Wednesday witnessed by the employees of Stanbic Bank Tanzania and GAIN Tanzania.
Head of Business Incubator, From Stanbic Bank, Kai Mollel presents the seventh cohort of the Supplier Development Program, in partnership with GAIN. The program equips women-led SMEs engaged in the food and nutrition sector in Tanzania with specialized training, mentorship, and networking that will help them achieve business scaling in a sustainable manner and drive positive change.
  • Stanbic and GAIN partner to boost SME capacity in Tanzania’s food sector for economic impact.
  • Program enhances women-led businesses with expertise in food nutrition, safety, and market strategies.
  • Launch aligns with Stanbic’s commitment to sustainable growth and empowering local enterprises.
Dar es Salaam, Tanzania: Stanbic Bank Tanzania, in partnership with the Global Alliance for Improved Nutrition (GAIN), has launched the seventh cohort of the Supplier Development Program under the Stanbic Business Incubator (BSI). This collaboration focuses on empowering Small and Medium Enterprises (SMEs), particularly women-led businesses in the food and nutrition sector, to develop more sustainable and scalable business models, contributing to Tanzania’s broader economic growth goals.

GAIN’s participation reflects its commitment to enhancing food security and nutrition in Tanzania by empowering local businesses to adopt better food safety and quality standards. By integrating training on nutrition and food safety, GAIN aims to ensure that Tanzanian food producers meet industry standards and promote healthier food practices. GAIN’s support will not only strengthen these businesses but also improve the nutritional value of food products available to Tanzanian communities, contributing to a healthier nation.

XXXX XXXX at GAIN Tanzania, “Our collaboration with Stanbic will not only enhance the competitiveness of Tanzanian SMEs but also uplift communities through better nutrition and food security. This partnership is a step towards achieving GAIN’s mission to make nutritious foods more accessible and affordable for all.

Participants in this cohort will receive specialized training that extends beyond basic business skills to address key areas that impact their businesses directly. The expanded curriculum includes advanced topics in food nutrition, safety, and strategic marketing. This will equip trainees with the knowledge needed to improve their production quality, enhance food safety practices, and effectively market their products.

Through Stanbic and GAIN’s combined efforts, participants will gain the tools needed to implement safe and nutritious food production practices, ensuring their businesses comply with health and quality standards. This foundational knowledge in food safety is key to building credibility and trust among consumers. Additionally, the program will help participants strengthen their marketing strategies, enabling them to reach broader markets and compete more effectively within the industry. By adopting robust marketing techniques, they can increase visibility and attract a wider customer base. Furthermore, participants will learn to build resilient business models that prioritize sustainability and incorporate local content, fostering a greater sense of economic inclusivity. This approach not only supports their long-term success but also contributes to a more equitable and sustainable economic landscape in Tanzania.

The program offers six months of dedicated coaching, providing participants with ongoing mentorship to help them navigate market challenges and grow their businesses sustainably. In addition, graduates will join an extensive network within the Stanbic Business Incubator and GAIN communities, giving them access to valuable connections and potential partnerships.

XXXX XXXX of Stanbic Bank Tanzania, stated, “The Stanbic Business Incubator is more than just a training ground—it is a platform where local businesses find the resources, networks, and guidance needed to scale. Through partnerships like this with GAIN, we are creating sustainable opportunities that empower businesses and build a stronger, healthier Tanzania.

Since its inception in 2022, the Stanbic Business Incubator has served as a cornerstone of Stanbic Bank Tanzania’s commitment to supporting local enterprises. BSI programs focus on empowering SMEs through tailored capacity-building initiatives, enabling them to participate meaningfully in key sectors such as agriculture, manufacturing, and now, food and nutrition. With over 200 SMEs trained and more than 500 jobs created to date, BSI Supplier Development Program has demonstrated its impact across six cohorts, contributing significantly to Tanzania’s economic resilience and job creation.

For more information, please contact:

Name: Azda Nkullo

Title: Business Marketing Manager at Stanbic Bank Tanzania


About Stanbic Bank Tanzania Stanbic Bank Tanzania is a leading financial services provider in Tanzania, offering a comprehensive range of products and services to personal, business, and corporate clients. As a subsidiary of Standard Bank Group, Stanbic Bank Tanzania leverages its deep local knowledge and expertise with the global reach and capabilities of Standard Bank to support the growth and development of its clients.

About the Global Alliance for Improved Nutrition (GAIN) The Global Alliance for Improved Nutrition (GAIN) is an international organization founded by the United Nations to address global nutrition challenges. GAIN works with governments, the private sector, and civil society to make nutritious foods more accessible, affordable, and desirable for vulnerable populations worldwide. By enhancing the food supply chains of local businesses, GAIN contributes to creating healthier, more resilient communities, advancing both public health and economic development.
Share:

Benki ya Absa Tanzania yafanya uwekezaji mkubwa katika huduma za kidigitali

Mkuu wa Kitengo cha Wateja Binafsi wa Benki ya Absa Tanzania, Bi. Ndabu Lilian Swere (wa pili kushoto) akionyesha jina la mshindi wa droo ya kwanza ya kampeni ya Tumia na Ushinde 'Spend & Win' ambapo mkazi wa Dar es Salaam Bw, Rashid Nassoro Said aliibuka kidedea kwa kujishindia gari jipya aina ya Subaru Forester 2024 lenye thamani ya zaidi ya shs milioni 40. Kampeni hiyo inayochezeshwa kila mwezi kwa kwa muda wa miezi mitatu, inahamasisha matumizi ya kadi na hduma za kidigitali katika kufanya miamala mbalimbali ya kibenki. Hafla hiyo ilifanyika jijini Dar es Salaam jana.

Benki ya Absa Tanzania imesema imefanya uwekezaji mkubwa katika huduma zake za kibenki kwa njia za kidigitali ili kuunga mkono juhudi za serikali ya awamu ya sita ya Rais Samia Suluhu Hassan katika kuhakikisha huduma za kibenki zinawafikia watanzania wengi na kwa gharama nafuu.

Hayo yalisemwa na Mkuu wa Kitengo cha Wateja Binafsi wa benki hiyo, Bi. Ndabu Lilian Swere wakati wa droo ya kwanza ya Kampeni ianyoendelea ya ‘Tumia Ushinde’ (Spend & Win), ambayo lengo lake kubwa ni kuhamasisha wateja wa benki hiyo na watanzania kufanya miamala mbalimbali ya kibenki kwa kutumia kadi ama huduma za kibenki kwa njia za kidigitali.

Kampeni hii ya miezi mitatu ina lengo la kuwazawadia gari wateja wetu wanaofanya miamala ya kibenki kwa kutumia kadi za ATM ama huduma za kidigitali kwa kutumia mifumo yetu inayowawezesha wateja kupata huduma kiuharaka na kiurahisi hivyo kutimiza malengo yao."

Sisi kama Absa Benki Tanzania tumeimarisha huduma zetu za kidigitali ili kwenda sambamba na jitihada zinazofanywa na serikali kusaidia kufikisha huduma za kibenki kwa wale ambao hawajafikiwa na huduma hizi huku wakiendelea kutumia mifumo ya kibenki ya kiasili."

Mifumo ya kidigitali ya benki yetu ni ya haraka na tumeimarisha kwa kiwango cha kimataifa mifumo ya usalama hivyo tunapenda kuwatoa hofu wateja wetu wote kuendelea kufanya miamala kwa kutumia mifumo yetu ya kidigitali bila hofu yoyote”, alisema Bi. Ndabu.

Naye Mkuu wa Masoko na Mawasiliano wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Aron Luhanga alisema kampeni hiyo inaenda sambamba na lengo kuu la kuwepo kwa benki hiyo ambalo ni kuiwezesha Afrika na Tanzania ya Kesho, hatua moja baada ya nyingine ikiwezeshwa na chapa mpya ya benki hiyo isemayo ‘Stori yako ni ya thamani’.

Tunapotoa zawadi hii kwa wateja wetu na huku tukiboresha huduma zetu kwa njia za kidigitali tunaamini kuwa tunasaidia kuandika stori mbalimbali za washindi na wateja wetu, lakini pia tunaisaidia serikali yetu kuandika stori yake ya kuona huduma za kibenki zinawafikia watanzania wengi kila kona ya nchi yetu”, alisema Bw. Luhanga.

Kampeni ya Spend & Win itadumu kwa muda wa miezi mitatu na ikishuhudia kila mwezi mshindi mmoja akiibuka na gari jipya aina ya Subaru Forester lenye thamani za zaidi sh shs milioni 40, ambapo mshindi hutakiwa kufanya miamala kila wakati kwa kutumia kadi ama huduma za kibenki kwa njia ya mtandao. Katika hafla ya jana, mkazi wa Dar es Salaam, Rashidi Nassoro Saidi aliibuka kidedea na kujishindia moja ya zawadi hiyo ya gari.
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Masoko wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Aron Luhanga (kulia) akizungumzai jijini Dar es Salaam jana wakati wa droo ya kwanza ya kampeni ya Tumia na Ushinde 'Spend & Win' ambapo mkazi wa Dar es Salaam Bw, Rashid Nassoro Said aliibuka kidedea kwa kujishindia gari jipya aina ya Subaru Forester 2024 lenye thamani ya zaidi ya shs milioni 40. Kampeni hiyo inayochezeshwa kila mwezi kwa kwa muda wa miezi mitatu, inahamasisha matumizi ya kadi na huduma za kidigitali katika kufanya miamala mbalimbali ya kibenki. Hafla hiyo ilifanyika jijini Dar es Salaam jana.
Share:

Wafanyabiashara waipongeza serikali kushughulikia changamoto za kikodi

    

Mkuu wa Kitengo cha Shughuli za Kibenki wa Benki ya Absa Tanzania, Alred Urasa (kushoto), akizungumza wakati wa mkutano wa Jukwaa la Wafanyabiashara wa Afrika Kusini nchini Tanzania (SABFT), uliodhaminiwa na benki hiyo, jijini Dar es Salaam jana. SABFT moja ya malengo yake makuu ni kuwaunganisha wawekezaji kutoka nchini huko na wawekezaji wa Tanzania wenye ni ya kuwekeza nchini Afrika Kusini kunufaika na fursa zinazopatikana katika pande zote mbili.

Na mwandishi wetu, Dar es Salaam

WAFANYABIASHARA wanachama wa Jukwaa la Wafanyabiashara wa Afrika Kusini nchini Tanzania (SABFT), wametoa pongezi za serikali za nchi zote mbili kwa kushughulikia changamoto ya kero za kikodi zilizokuwa zikiwakabili kwa muda mrefu.

Akizungumza jijini Dar es Salaam jana wakati wa mkutano wa wafanyabiashara hao, uliofanyika kwa udhamini wa Benki ya Absa kwa kushirikiana na Shirika la Ndege la Afrika Kusini (SAA), Mwenyekiti wa Jukwaa hilo, Bw. Manish Thakrar alisema changamoyo ya kodi kutozwa mara mbili imekuwa kilio cha muda mrefu kwao lakini kutoka juhudi zinazoendelea kufanywa kwa ushirikiano wa serikali za Tanzania na Afrika Kusini, chemba za biashara na wadau wengine ni imani yao hadi kufikia mwisho wa mwaka huu kero hizo zitakuwa zimeondolewa kabisa.

Alisema Jukwaa la Wafanyabiashara wa Afrika Kusini nchini Tanzania (SABFT) lilianzishwa miaka 24 iliyopita kwa lengo kubwa la kuwaunganisha wawekezaji kutoka nchini huko na wawekezaji wa Tanzania wenye ni ya kuwekeza nchini Afrika Kusini hivyo kunufaika na fursa zinazopatikana katika pande zote mbili.

Kipindi kutoka mwaka 1997 kupitia mpango wa ubinafsishaji, kimsingi kumekuwa na ongezeko kubwa la uwekezaji wa wafanyabiashara kutoka Afrika Kusini katika miradi mikubwa katika sekta za mawasiliano, uzalishaji, vinywaji na vyakula, hivyo kutoa fursa za ajira kwa watanzania pia kunufaisha wafanyabiashara wa ndani.

Natoa shukurani za kipekee kwa Benki ya Absa Tanzania kwa udhamini mkubwa katika tukio hili, lakini pia tunaipongeza benki hii kwa jinsi inavyoweka juhudi katika kutoa huduma na bidhaa pamoja na masuluhisho mbalimbali katika kusaidia mahitaji ya kifedha kwa wafanyabiasha wa Afrika Kusini na wa Tanzania”, alisema Bw. Thakrar.

Akizungumza wakati wa mkutano huo, Mkurugenzi wa Masoko ya Fedha za Kigeni wa Benki ya Absa Tanzania, Bi. Irene Rwegalulira akimwakilisha Mkurugenzi Mtendaji wa benki hiyo, Bw. Obedi Laiser alisema, wamejipanga vizuri katika kuhudumia wateja wao kutoka nje ya Tanzania kwa ubunifu zaidi ikiwa na masuluhisho tofauti ya huduma za kibenki kwa wateja wadogo, wa kati na wakubwa.

Majukwaa kama haya yana faida sana kwani sisi benki tunakuja kama kiunganishi ili tuweze kuwasaidia katika biashara zao zinazohitaji huduma za kifedha kama vile mikopo, fedha za kigeni, pamoja na ushauri wa namna bora ya kufanya biashara nchini Tanzania kulingana na taratibu na miongozo ya serikali.

Absa inafanya biashara sambamba na lengo kuu la kuanzishwa kwake ambalo ni Kuiwezesha Afrika na Tanzania ya Kesho Pamoja, hatua moja baada ya nyingine, huku tukiongozwa na ahadi mpya ya chapa ya benki yetu isemayo ‘Story yako ina thamani’ hivyo kwa kutoa huduma bora za kibenki kwa wafanyabiashara hawa, tunaamini tunasaidia kuandika story za mafanikio za wateja wetu kwa manufaa yao na maslahi mapana ya Tanzania na Afrika Kusini”, alisema Bi. Irene.

Jukwaa na Wafanyabiashara wa Afrika Kusini kwa sasa lina jumla ya wanachama 100 kutoka katika sekta mbalimbali kama vile mabenki, madini, mawasiliano, viwanda vya uzalishaji, maduka makubwa na nyinginezo.
Mkurugenzi wa Masoko ya Fedha za Kigeni wa Benki ya Absa Tanzania, Bi. Irene Rwegalulira, akizungumza wakati wa mkutano wa Jukwaa la Wafanyabiashara wa Afrika Kusini nchini Tanzania (SABFT), uliodhaminiwa na benki hiyo, jijini Dar es Salaam jana. SABFT moja ya malengo yake makuu ni kuwaunganisha wawekezaji kutoka nchini huko na wawekezaji wa Tanzania wenye ni ya kuwekeza nchini Afrika Kusini kunufaika na fursa zinazopatikana katika pande zote mbili.
Mkurugenzi wa Masoko ya Fedha za Kigeni wa Benki ya Absa Tanzania, Bi. Irene Rwegalulira (kushoto), akizungumza wakati wa mkutano wa Jukwaa la Wafanyabiashara wa Afrika Kusini nchini Tanzania (SABFT), uliodhaminiwa na benki hiyo, jijini Dar es Salaam jana. SABFT moja ya malengo yake makuu ni kuwaunganisha wawekezaji kutoka nchini huko na wawekezaji wa Tanzania wenye ni ya kuwekeza nchini Afrika Kusini kunufaika na fursa zinazopatikana katika pande zote mbili.
Mkurugenzi wa Masoko ya Fedha za Kigeni wa Benki ya Absa Tanzania, Bi. Irene Rwegalulira (kushoto), akizungumza wakati wa mkutano wa Jukwaa la Wafanyabiashara wa Afrika Kusini nchini Tanzania (SABFT), uliodhaminiwa na benki hiyo, jijini Dar es Salaam jana. SABFT moja ya malengo yake makuu ni kuwaunganisha wawekezaji kutoka nchini huko na wawekezaji wa Tanzania wenye ni ya kuwekeza nchini Afrika Kusini kunufaika na fursa zinazopatikana katika pande zote mbili.
Baadhi wa wafanyabiashara na wajumbe wa Jukwaa la Wafanyabiashara wa Afrika Kusini nchini Tanzania (SABFT), wakihudhuria mkutano wa jukwaa hilo uliodhaminiwa na Benki ya Absa Tanzania, jijini Dar es Salaam jana. SABFT moja ya malengo yake makuu ni kuwaunganisha wawekezaji kutoka nchini huko na wawekezaji wa Tanzania wenye ni ya kuwekeza nchini Afrika Kusini kunufaika na fursa zinazopatikana katika pande zote mbili.
Mwenyekiti wa Jukwaa la Wafanyabiashara wa Afrika Kusini nchini Tanzania (SABFT), Bw. Manish Thakrar (katikati), pamoja na baadhi ya viongozi wa jukwaa hili, wakikata keki kufurahia mafanikio ya jukwaa hilo, wakati wa mkutano wao, uliodhaminiwa na Benki ya Absa Tanzania jijini Dar es Salaam jana. SABFT moja ya malengo yake makuu ni kuwaunganisha wawekezaji kutoka nchini huko na wawekezaji wa Tanzania wenye ni ya kuwekeza nchini Afrika Kusini kunufaika na fursa zinazopatikana katika pande zote mbili.
Share:

Rais wa Zanzibar aipongeza Benki ya Absa Tanzania kuboresha afya ya mama na mtoto

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi ya Zanzibar, Mhe. Dk. Hussein Ali Mwinyi (wa pili kulia), akikabidhi cheti cha shukurani kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Obedi Laiser kwa kutambua mchango wa benki hiyo katika kuwezesha kampeni ya ‘Uzazi ni Maisha’ iliyoanzishwa na Shirika la Amref Tanzania kwa kushirikiana na Wizara ya Afya ya Zanzibar. Ilikuwa ni katika hafla ya shukurani na uchangishaji fedha iliyofanyika katika Ikulu ya Zanzibar, jana. Wengine kutoka kushoto ni, Waziri wa Afya Zanzibar, Mhe. Nassor Mazrui, Mwenyekiti wa Bodi ya Amref, Bw. Anthony Chamungwana na Mkurugenzi Mkazi wa Amref Tanzania, Dk. Florence Temu.

Na mwandishi wetu, Zanzibar

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi ya Zanzibar, Mhe. Dk. Hussein Ali Mwinyi, ameipongeza Benki ya Absa Tanzania kwa mchango wake wa shs milioni 150 kuchangia kampeni ya ‘Uzazi ni Salama’ yenye lengo la kuboresha afya ya mama na mtoto wakati wa ujauzito na kujifungua.

Mheshimiwa Rais Mwinyi alitoa pongezi hizo katika hafla ya tatu ya shukurani na uchangishaji fedha wa kampeni hiyo, iliyoandaliwa na Shirika la Amref Tanzania, Wizara ya Afya Zanzibar, kwa udhamini mkuu wa Benki ya Absa Tanzania na kufanyika katika Ikulu ya Zanzibar, jana.

Leo tumekusanyika hapa kwa lengo la kuunga mkono juhudi za kuokoa maisha kupitia kampeni hii, iliyoanzishwa mwaka 2020 ikiwa na lengo la kukusanya fedha kiasi cha shs Bilioni 1."

Aidha nimefahamishwa, mwezi juni mwaka huu, Amref, wizara yetu ya afya pamoja na Benki ya Absa Tanzania wakiungwa mkono na wadau kadhaa walitoa vifaa tiba vyenye thamani ya shs milioni 262.6 kwa ajili ya vituo vya afya 28 katika mikoa mitano ya Zanzibar, niwashukuru Amref Tanzania, wadhamini wakuu Benki ya Absa Tanzania na wadau wote kwa kujitolea kuunga mkono jitihada ya serikali ya Zanzibar katika kuboresha huduma za afya”, alisema Rais Mwinyi.

Pamoja na hayo alisema ni jambo la kutia moyo kuona Zanzibar ikiwa kwenye njia sahihi ya kufikia malengo endelevu (SDG) 2030 ya kupunguza vifo vya wajawazito hadi chini ya vifo 70 kwa vizazi hai 100, vifo vya watoto wachanga hadi kufikia 12 kwa kila vizazi 1000 na vifo vya watoto chini ya miaka mitano hadi 25 kwa kila vizazi hai 1000 kufikia 2030.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Bwana Obedi Laiser alisema wametoa msaada kuunga mkono juhudi zinazofanywa za serikali za mbili za, Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika kuwekeza katika sekta ya afya hususan katika kupunguza vifo vya akina mama na watoto.

Benki ya Absa Tanzania tunaenda sawa na lengo la taasisi yetu lisemalo ‘Kuiwezesha Afrika na Tanzania ya kesho kwa pamoja, hatua moja baada ya nyingine’ hapa tukihakikisha jamii yetu inapata huduma za afya stahiki."

Lakini pia msaada huu unaenda sambamba na ahadi yetu ya chapa tuliyoizindua hivi karibuni isemayo ‘Stori yako ina thamani’, hivyo kwa kuunga mkono juhudi hizi, tunaamini tunazisaidia serikali zetu katika kuandika stori zake zile zinazohakikisha watanzania wote wanapata huduma bora za afya”, alisema Bw. Laiser.

Awali akizungumza katika hafla hiyo, Mkurugenzi Mkazi wa Amref Tanzania, Dk. Florence Temu alimshukuru Rais Dk. Mwinyi kwa kukubali, kujitoa na kuunga mkono kampeni ya Uzazi ni Maisha tokea ilipoanzishwa mwaka 2020.

Niwashukuru pia wadhamini wakuu, Benki ya Absa pamoja na wafadhili wetu wengine waliokuwa nasi tokea mwanzo kufanikisha malengo ya kampeni hii yenye kauli mbiu ya ‘Changia Vifaa Tiba kwa Uzazi Salama’ ambapo kati ya malengo yetu ya kukusanya kiasi cha shs Bilioni 1, hadi sasa tumeshapokea ahadi zenye thamani ya shs 989,831,145, Zaidi ya asilimia 98.9 ya malengo yetu tukipokea kiasi cha shs 740,457,422 sawa na asilimia 75”, alisema Dk. Florence.

Hafla hiyo pia ilihudhuriwa na Waziri wa Afya Zanzibar, Mhe. Nassoro Mazrui, Naibu Waziri, Mhe. Hassan Khamis Hafidh, Katibu Mkuu, Dk. Mngereza Mzee Miraji, mabalozi na wawakilishi wa mashirika ya kimataifa na kitaifa ya maendeleo, watendaji na watumishi wa serikali na mashirika ya umma.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi ya Zanzibar, Mhe. Dk. Hussein Ali Mwinyi (katikati) na wengine kutoka kushoto; Mwenyekiti wa Bodi ya Amref Tanzania, Bw. Anthony Temu, Waziri wa Afya Zanzibar, Mhe. Nassor Mazrui, Mkurugenzi Mkazi wa Amref Tanzania, Dk. Florence Temu na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Obedi Laiser, wakifanya dua katika hafla ya shukurani na uchangishaji fedha wa kampeni ya ‘Uzazi ni Maisha’ iliyofanyika katika Ikulu ya Zanzibar, jana.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi ya Zanzibar, Mhe. Dk. Hussein Ali Mwinyi, akihutubia katika hafla ya shukurani na uchangishaji fedha ya kampeni ya Uzazi ni Maisha iliyofanyika katika Ikulu ya Zanzibar, jana.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Obedi Laiser, akizungumza kuhusu udhamini na malengo ya benki hiyo katika kuiwezesha kampeni ya ‘Uzazi ni Maisha’ iliyoanzishwa ma Shirika la Amref Tanzania pamoja na Wizara ya Afya Zanzibar, katika hafla ya shukurani na uchangishaji fedha kwa ajili ya kampeni hiyo katika Ikulu ya Zanzibar, jana. Kampeni hiyo ina lengo la kuboresha afya ya mama na mtoto wakati wa ujauzito na kujifungua.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi ya Zanzibar, Mhe. Dk. Hussein Ali Mwinyi (katikati),akipozi kwa picha ya kumbukubu na baadhi ya wafanyakazi wa benki ya Absa Tanzania, pamoja na viongozi wengine, mara ya baada ya hafla ya shukurani na uchangishaji fedha ya kampeni ya 'Uzazi ni Salama' iiyofanyika Ikulu ya Zanzibar, jana.
Share:

Tanzania Breweries Plc (TBL) na WWF Wakabidhi Mradi wa Maji Kijiji Cha Minazi mirefu, Ruvu Stesheni

   Katika hatua muhimu ya kuhakikisha upatikanaji endelevu wa maji kwa jamii za wenyeji na mazingira, Kampuni ya Tanzania Breweries Limited (TBL) na WWF Tanzania wamekabidhi rasmi miundombinu ya mfumo wa maji unaotumia nishati ya jua, ikijumuisha kisima, sehemu ya kunyweshea mifugo, na kituo cha maji kwa matumizi ya nyumbani katika Wilaya ya Kibaha.

Katika tukio hilo hilo, washirika hao wawili pia walizindua mradi wa majaribio wa miradi ya urejeshaji wa mazingira chini ya mpango wa "Bankable Nature Solutions" (BNbS) ili kuimarisha usalama wa maji wa muda mrefu na ulinzi wa mazingira.

Hafla ya makabidhiano iliyofanyika Kijiji cha Minazimikinda, Wilaya ya Kibaha, ilihudhuriwa na Mkuu wa Wilaya ya Kibaha, Mheshimiwa Nickson Simon John, ambaye alisifu ushirikiano kati ya TBL na WWF. Alisisitiza umuhimu wa ushirikiano katika kukabiliana na changamoto za maji nchini, hususan katika maeneo yanayokua kwa kasi kama Pwani na Dar es Salaam.

"Maji ni rasilimali muhimu kwa ukuaji wa jamii zetu na uchumi. Ushirikiano huu unaonesha nguvu ya kufanya kazi kwa pamoja katika kutatua uhaba wa maji. Juhudi za TBL na WWF Tanzania za kuboresha usalama wa maji, hasa katika Dar es Salaam na maeneo jirani, ni za kupongezwa na ni hatua muhimu kuelekea kuhakikisha upatikanaji endelevu wa maji safi kwa wote," alisema Mkuu wa Wilaya, Mheshimiwa Nickson Simon John.

Mfumo mpya wa maji unaotumia nishati ya jua utatoa maji safi na ya kuaminika kwa jamii zinazozunguka, ukiwasaidia kaya na mifugo katika eneo hilo. Miundombinu hii inashughulikia changamoto za uhaba wa maji kwa sasa na kutumia teknolojia rafiki wa mazingira ili kuhakikisha matumizi endelevu kwa muda mrefu.
Mradi huu ni sehemu ya dhamira kubwa ya TBL kwa uendelevu, inayooana na mkakati wake wa kuleta athari chanya kwa jamii inazozihudumia huku ikiunga mkono uhifadhi wa rasilimali za asili za Tanzania. Ushirikiano na WWF Tanzania chini ya mpango wa BNbS unalenga kuhakikisha kuwa mifumo ya asili inabaki salama wakati changamoto za maji zinashughulikiwa.

Akizungumza katika hafla hiyo, Mkurugenzi Mtendaji wa TBL Michelle Kilpin, alisisitiza umuhimu wa mradi huo: "Kwa TBL, uendelevu ni msingi wa shughuli zetu. Mfumo huu wa maji unaotumia nishati ya jua, pamoja na uzinduzi wa mradi wa majaribio wa Bankable Nature Solutions, ni hatua muhimu kuelekea kuhakikisha kwamba watu na mazingira wote wananufaika na juhudi zetu. Kwa kushirikiana kwa karibu na WWF Tanzania, tunahakikisha upatikanaji wa maji kwa jamii hii na kulinda mifumo muhimu ya ikolojia ambayo ni muhimu kwa mustakabali wetu."
Mbinu ya Bankable Nature Solutions (BNbS) inatumia rasilimali za asili kwa njia endelevu, ikigeuza juhudi za uhifadhi wa mazingira kuwa miradi inayoweza kujiendesha kifedha na kuleta manufaa kwa uchumi na jamii. Kupitia mpango huu, TBL na WWF Tanzania wanalenga kuunda mfano wa kurudiwa unaoweza kutekelezwa nchi nzima ili kukabiliana na uhaba wa maji na kuimarisha uhifadhi wa mazingira.

Mkurugenzi wa Nchi wa WWF Tanzania, Dkt. Amani Ngusaru, alielezea umuhimu wa kulinda vyanzo vya maji. “Ulinzi wa vyanzo muhimu vya maji ni muhimu kwa kudumisha maisha ya binadamu na usawa wa mazingira. Kupitia mbinu za ubunifu kama Bankable Nature Solutions, tunaweza kuunda suluhisho la muda mrefu kwa ajili ya watu na mazingira.”

"Ushirikiano wetu na TBL unaonesha jinsi biashara na mashirika ya uhifadhi wa mazingira yanavyoweza kushirikiana kufanikisha matokeo ya kudumu. Kwa uzinduzi wa mradi wa majaribio wa BNbS hapa Kibaha, tunaweka msingi wa suluhisho za muda mrefu na endelevu ambazo zinalinda rasilimali zetu za asili huku zikihakikisha jamii zinapata huduma muhimu kama maji." alisema Dkt. Ngusaru

Tukio hilo lilihudhuriwa na viongozi wa eneo hilo, wanajamii, na wadau muhimu ambao walipongeza mpango huo kwa kuwa na mtazamo wa mbali na manufaa ya muda mrefu kwa jamii. Kisima cha maji cha nishati ya jua, sehemu ya kunyweshea mifugo, na kituo cha maji kwa matumizi ya nyumbani vinatarajiwa kunufaisha moja kwa moja mamia ya kaya na mifugo yao.

Ushirikiano kati ya TBL na WWF Tanzania haukabiliani tu na upungufu wa maji, bali pia unaimarisha ulinzi wa vyanzo vya maji, muhimu kwa kuhifadhi bioanuwai na kudumisha huduma za mazingira kwa vizazi vijavyo.
Share:

LILIAN-FAVOUR MAKAWA

LILIAN-FAVOUR MAKAWA

Popular Posts

Blog Archive

Labels

Recent Posts

Label Cloud

BIASHARA (275) BURUDANI (4) KIMATAIFA (10) KITAIFA (119) MICHEZO (38) SIASA (3)

Pages