Benki ya DCB kupitia mfuko wake wa kuisaidia jamii wa DCB FOUNDATION wasaidia kampeni ya usafi wa mazingira Temeke.

      
Mkuu wa Wilaya ya Temeke, Jokate Mwegelo (wa tatu kushoto) akifanya usafi pamoja na wafanyakazi wa Benki ya Biashara ya DCB katika siku ya usafi ya mwisho wa mwezi iliyofanyika kiwilaya katika kata ya Keko jijini Dar es Salaam jana. DCB imeshiriki kampeni hiyo kupitia mfuko wake wa kusaidia jamii wa DCB Foundation kwa kufanya usafi na kukabidhi msaada wa vifaa vya kufanyia usafi.
Mkuu wa Wilaya ya Temeke, Jokate Mwegelo (katikati), Meneja Mahusiano wa Benki ya Biashara ya DCB, Brino Londo (kulia) na Ofisa Masoko wa benki hiyo, Agness Ntabaye wakifanya usafi katika siku ya usafi ya mwisho wa mwezi iliyofanyika kiwilaya katika kata ya Keko jijini Dar es Salaam jana. DCB imeshiriki kampeni hiyo kupitia mfuko wake wa kusaidia jamii wa DCB Foundation kwa kufanya usafi na kukabidhi msaada wa vifaa vya kufanyia usafi.
Meya wa Manispaa ya Temeke, Abdallah Mtinika (kulia) akipokea sehemu ya vifaa vya kufanyia usafi kutoka kwa Meneja Mahusiano wa Benki ya Biashara ya DCB, Brino Londo katika siku ya usafi ya mwisho wa mwezi iliyofanyika kiwilaya katika kata ya Keko jijini Dar es Salaam jana. DCB imeshiriki kampeni hiyo kupitia mfuko wake wa kusaidia jamii wa DCB Foundation kwa kufanya usafi na kukabidhi msaada wa vifaa vya kufanyia usafi.
Meya wa Manispaa ya Temeke, Abdallah Mtinika (kulia) akipokea sehemu ya vifaa vya kufanyia usafi kutoka kwa Meneja wa Benki ya Biashara ya DCB Tawi la Temeke, Loyce Lwiza katika tukio la siku ya usafi ya mwisho wa mwezi lililofanyika kiwilaya katika kata ya Keko jijini Dar es Salaam jana. Benki ya DCB chini ya mfuko wake wa kusaidia jamii wa DCB Foundation wasaidia usafi wa mazingira ya Wilaya ya Temeke.
Mkuu wa Wilaya ya Temeke, Jokate Mwegelo (katikati) akishikana mikono na Meneja Mahusiano wa Benki ya Biashara ya DCB, Brino Londo baada ya kukabidhiwa vifaa vya kufanyia usafi katika siku ya usafi ya mwisho wa mwezi iliyofanyika kiwilaya katika kata ya Keko jijini Dar es Salaam jana. DCB imeshiriki kampeni hiyo kupitia mfuko wake wa kusaidia jamii wa DCB Foundation kwa kufanya usafi na kukabidhi msaada wa vifaa vya kufanyia usafi.
Mkuu wa Wilaya ya Temeke, Jokate Mwegelo (wa tatu kushoto), Ofisa Masoko wa benki hiyo, Agness Ntabaye (wa pili kushoto) na Meneja Mahusiano wa Benki ya Biashara ya DCB, Brino Londo wakiwa pamoja wakati wa zoezi la siku ya usafi ya mwisho wa mwezi ambapo kiwilaya ilifanyika katika Kata ya Keko jijini Dar es Salaam. DCB imeshiriki kampeni hiyo kupitia mfuko wake wa kusaidia jamii wa DCB Foundation kwa kufanya usafi na kukabidhi msaada wa vifaa vya kufanyia usafi.
Share:

DCB KUWAWEZESHA WANAWAKE KIUCHUMI

  
Mjumbe wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya Biashara ya DCB, Pamela Nchimbi (kushoto) akizungumza katika kongamano la wanawake lililoandaliwa na Kampuni ya ushauri wa masuala ya fedha ya Bridge Consult kwa udhamini mkuu wa Benki ya DCB jijini Dar es Salaam jana. Lengo la jukwaa hilo ni kubadilishana mawazo na kupeana ujuzi wa masuala ya kifedha, uwekezaji pamoja na maendeleo endelevu.
Mkuu wa Wateja Binafsi wa Benki ya Biashara ya DCB, Fortunata Benedict akitoa elimu ya maswala ya fedha katika kongamano la wanawake lililoandaliwa na Kampuni ya ushauri wa masuala ya Kifedha ya Bridge Consult kwa udhamini mkuu wa Benki ya DCB jijini Dar es Salaam jana. Lengo la jukwaa hilo ni kubadilishana mawazo na kupeana ujuzi wa masuala ya kifedha, uwekezaji pamoja na maendeleo endelevu.
Mjumbe wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya Biashara ya DCB, Dk. Anna Abdul akizungumza katika kongamano la wanawake lililoandaliwa na Kampuni ya ushauri wa masuala ya kifedha ya Bridge Consult kwa udhamini mkuu wa Benki ya DCB jijini Dar es Salaam jana. Lengo la jukwaa hilo ni kubadilishana mawazo na kupeana ujuzi wa masuala ya kifedha, uwekezaji pamoja na maendeleo endelevu.
Mjumbe wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya Biashara ya DCB, Pamela Nchimbi (wa pili kulia) akitoa elimu ya masuala ya maendeleo endelevu katika kongamano la wanawake lililoandaliwa na Kampuni ya ushauri wa masuala ya kifedha ya Bridge Consult kwa udhamini mkuu wa Benki ya DCB jijini Dar es Salaam jana. Lengo la jukwaa hilo ni kubadilishana mawazo na kupeana ujuzi wa masuala ya kifedha, uwekezaji pamoja na maendeleo endelevu. Kutoka kulia ni Mtaalamu wa masuala ya Kimaisha, Mihaela Marcu, Mshauri wa masuala ya afya kwa jamii, Naomi Serbantez na Mkurugenzi wa Mgahawa wa Terrace, Sarah Raqey.
Baadhi ya washiriki wakichangia mada katika kongamano la wanawake lililoandaliwa na Kampuni ya ushauri wa masuala ya kifedha ya Bridge Consult kwa udhamini mkuu wa Benki ya DCB jijini Dar es Salaam jana. Lengo la jukwaa hilo ni kubadilishana mawazo na kupeana ujuzi wa masuala ya kifedha, uwekezaji pamoja na maendeleo endelevu.
Share:

TANZANIA COMMERCIAL BANK YATINGA KIBABE KATAVI YAFUNGUA TAWI JIPYA

 .com/img/a/

Mkuu wa Mkoa wa Katavi, Mh. Mwamvua Mrindoko (kushoto),  akikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa Tawi jipya la Tanzania Commercial Bank (TCB) katika Manispaa ya Mpanda  mjini mkoani Katavi,  kulia ni  Mkuu wa Halmashauri ya Wilaya ya Mpanda Onesmo Buswelu  Meneja wa Tawi la Mpanda Julius Mlang'a  pamoja na maofisa wa kamati ya ulinzi ya mkoa..com/img/a/Mkuu wa Mkoa wa Katavi, Mh. Mwamvua Mrindoko wa  (kushoto),  akipokea kadi ya ATM kutoka kwa Afisa Mtendaji Mkuu wa Tanzania Commercial Bank TCB,  Sabasaba Moshingi, alipofungua akaunti alipoalikwa kuwa mgeni rasmi wakati wa hafla ya uzinduzi wa Tawi jipya la Tanzania Commercial Bank  lililofunguliwa katika Manispaa ya Mpanda  mjini mkoani Katavi jana  wengine pichani ni Mkuu wa Halmashauri ya Wilaya ya Mpanda Onesmo Buswelu  Meneja wa Tawi la Mpanda Julius Mlang'a  pamoja na maofisa wa wengite kutoka TCB

.com/img/a/

Tanzania Commercial Bank (TCB)  imezindua tawi jipya Mkoa wa Katavi Wilaya ya Mpanda ikiwa ni jitihada za kusogeza huduma za kibenki kwa wateja na Wananchi kwa ujumla.

Tawi hilo la kwanza kwa taasisi za fedha kuzinduliwa Mkoa Katavi Wilaya ya Mpanda, limezinduliwa rasmi na Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mhe. Mwanamvua Mrindoko .

 

Akizungumza katika uzinduzi huo, Mkurugenzi Mtendaji wa Tanzania Commercial Bank (TCB) Sabasaba Moshingi alisema huo ni mwendelezo wa Tanzania Commercial Bank katika kusogeza huduma kwa wateja wake.

 

Alisema tawi hilo jipya la Mpanda litarahisisha utoaji huduma za kibenki kwa wateja wake hali ambayo itapunguza mzunguko wa wananchi kuzifuata huduma za kibenki maeneo mengine ya mbali

Aliongeza kuwa Tanzania Commercial Bank (TCB) imezingatia shughuli za kiuchumi zinazoendeshwa Wilayani humo kwa  wafanyabiashar  wafugaji na wakulima wa na kufungua tawi hilo hivyo wateja hawatalazimika kwenda mjini kupata huduma za kibenki kama hapo awali

 

AlisemaTanzania Commercial Bank sio kwamba tu ni benki kubwa nchini, bali inatoa mchango mkubwa katika shughuli za kijamii  hasa kuinua elimu pamoja na Afya.

Kwa kuona umuhimu wa kusongeza huduma kwa wateja hasa maeneo ya vijijini Tanzania Commercial Bank (TCB) inaendelea kuwawezesha mawakala watakaosaidia kutoa huduma hizo jambo ambalo litasaidia kusogeza huduma kwa wateja wetu nchi mzima.

 

Aliongeza, kwa sasa Benki hiyo ina matawi  82 Mawakala tunao zaidi 3,800  mashine zakutolea pesa ATM zetu tunazojitegemea Kama TanzaniaCommercial Bank ni 84 lakini zile ATM ambazo tupo chini ya Umoja Switch ni zaidi ya 250.

 

Akizungumza na wadau mbalimbali wakiwemo wafanyabiashara waliohudhuria katika hafla ya uzinduzi wa Tawi jipya la Tanzania Commercial Bank  Mgeni rasmi Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mhe. Mwanamvua Mrindoko  ameupongeza uongozi wa Tanzania CVommercial Banki  kwa kuja kuwekeza katika  Mkoa huu na anaamini kwa wingi wa watu waliojitikeza katika tukio hili watakwenda kufungua akaunti.

 

Mrindoko pia ameipongeza  Tanzania Commercial  Banki (TCB)  kwa kufika Mkoani Katavi na kuwakaribisha kwani fursa zipo nyingi katika mkoa huo zikiwemo za uzalishaji wa mazao ya chakula na biashara pamoja na mazao mengine  ya kimkakati.

 

Mkuu wa Mkoa wa Katavi aliuhakikishia uongozi wa Tanzania Commercial  Banki (TCB)  kwamba Katavi ni mkoa unaokua kwa kasi sana kutokana na shughuli za uzalishaji na za kimaendeleo hivyo huduma ya  Tanzania Commercial Bank kwakfungua tawi hilo limekuja wakati muafaka

 

“Kuzinduliwa kwa Tawi la Tanzania Commercial Bank (TCB)  hapa Katavi maana yake ni kwamba huduma za kibenki zitapatikana kwa urahisi zaidi hivyo wafanyakazi, wakulima na wafanyabiashara wa Katavi jitokezeni kwa wingi wenu kuchangamkieni  fursa hii na kuja kufungua akaunti na kufanya miamala mengine kama kulipa kodi alisisitiza Mrindoko

Share:

KWAHILI WALILOFANYA TANZANIA COMMERCIAL BANK MUNGU ANAWAONA

 

.com/img/a/Katibu Tawala Mkoa wa Kagera Prof: Faustin Kamuzora (wa pili kulia), akikata utepe wakati akikabidhiwa msaada wa jengo la madarasa, Vyoo, pamoja na Madawati mapya 50 lililokarabatiwa na Tanzania Commercial Bank (TCB) Hafla ya makabidhiano hayo yalifanyika katika Shule ya Msingi Kitunga iliyopo wilaya ya Muleba mkoani Kagera kushoto ni Mkurugenzi wa BiasharaWateja Wakubwa wa Tanzania Commercial Bank Adolfina William, Mkurugenzi wa Mipango na Mikakati wa Benki hiyo Muondakweli Kaniki pamoja na Mkuu wa Shule hiyo Hashim Kibaiza, Tanzania Commercial Bank kupitia mpango wake wa kusaidia jamii (CSR) imetumia zaidi kiasi cha shs milioni 36 kukamilisha ujenzi wa Madawati pamoja na choo   Madawati pamoja na choo cha walimu chenye matundu mawili 

.com/img/a/


Mkurugenzi wa Biashara Wateja Wakubwa wa Tanzania Commercial Bank Adolfina William,akizungumza wakati wa hafla ya kukabidhi msaada wa jengo la madarasa, Vyoo, pamoja na Madawati mapya 50 lililokarabatiwa na Tanzania Commercial Bank (TCB) Hafla ya makabidhiano hayo yalifanyika katika Shule ya Msingi Kitunga iliyopo wilaya ya Muleba mkoani Kagera kupitia mpango wake wa kusaidia jamii (CSR) imetumia zaidi kiasi cha shs milioni 36 kukamilisha ujenzi wa madarasa Madawati pamoja na choo.

.com/img/a/

Katibu Tawala wa Mkoa wa Kagera Prof Faustin Kamuzora amewataka wazazi na wakazi wa Mkoa wa Kagera kusaidiana na serikali katika kutatua changamoto za walimu.

Hayo ameyasema wakati wa kukabidhiwa ukarabati wa madarasa, madawati na Choo cha matundu mawili kilichojengwa na Tanzania Commercial Bank (TCB) kitakachosaidia kuboresha mazingira rafiki ya walimu kufundisha.

Prof Kamuzora amesema, wazazi na walezi wengi wa watoto wamesoma katika shule hiyo ila walimu wamekuwa na changamoto ya mazingira ambayo si rafiki na inaweza kupelekea walimu hao kuondoka na kwenda sehemu zingine.

“Walimu hawa wakiondoka tutakosa wa kuwafundisha watoto wetu, nyie wazazi wengi mmesoma hapa na mtu aliyesoma miaka ya nyuma akija hapa atapashangaa ila tusiwaachie serikali peke yake ila tushirikiane pamoja na wadau wa elimu pia,” amesema Prof Kamuzora.

Amesema, Benki ya TCB wamekuja na kujenga choo ila hii isiwe mwisho katika kutoa msaada bali walimu pia wanahitaji elimu ya fedha sababu wengi wamekuwa wanaingia katika mikopo inayowadidimiza kimaslahi.

Aidha, Prof Kamuzora ameitaka elimu ya fedha kuanza kutolewa mashuleni ili wanafunzi waanze kuwa na uelewa mkubwa na itawasaidia baadae.

“Na kwa upande wa walimu, haimaanishi ndio unajua kila kitu nao ni muhimu kuwa uelewa juu ya elimu ya fedha,”Mkurugenzi wa Wateja Wakubwa wa Tanzania Commercial Bank Adolphina William amesema wananchi wa Kijiji cha Msole wameweza kufurahia mradi wa kukarabati madarasa, kukabidhi madawati na walimu kupata choo cha kisasa.



Amesema, mradi huo uliofanyika katika Shule ya Kituga umeweza kugharimu kiasi cha Milioni 36.3 hadi kukamilika kwake.



“Tanzania Commercial Bank imekuwa inatenga fedha kila mwaka kwa ajili ya kusaidia jamii na mwaka huu tumetenga takribani Milioni 500 na kujikita zaidi katika sekta ya elimu na afya,” amesema Adolphina.


Kwa upande wa Mkuu wa shule Hashim kibaiza ameishukuru Tanzania Commercial Bank kwa kufanikisha mradi huo ambao utaenda kuboresha mazingira bora ya walimu katika kuinua taaluma.

Ameomba wadau mbalimbali kuiga mfano kwa Tanzania Commercial Banki ili kuendelea kujikita katika kusaidia jamii ikiwemo shule yao ya Kitunga.



Tanzania Commercial Bank imekabidhi ukarabati wa madarasa mawili, ujenzi wa choo cha walimu pamoja na kuchangia madawati 50 katika shule ya Msingi Kitunga iliyopo Muleba, mkoani Kagera mradi umegharimu Milioni 36,274,500 pesa za kitanzania.
Share:

ACEX CEO URGES LOCAL INVESTORS TO USE DIGITAL PLATFORM IN TRADING EFFECTIVELY

     
African Consolidated Exchange (ACEX) Chief Executive Officer, Peter Mucheru (right), toasts with some of Acex's co-workers, during the official launching of unified exchange platform, ACEX that will allow people to buy and sell assets such as stocks, bonds, forex, cryptocurrencies and other traditional commodities. A brief occasion was held in Nairobi recently.

Tanzanians have been called upon taking advantage offered by the newly launched unified exchange platform, the African Consolidated Exchange (ACEX) that will allow people to buy and sell assets such as stocks, bonds, forex, cryptocurrencies and other traditional commodities.

The trailblazing digital infrastructure would also allow investors to stake in real estate, Venture Capital, Micro-funding, mining and exploration among other projects while earning dividends on trading.

According to ACEX's chief executive officer, Mr Peter Mucheru, the platform intends to rewrite African history by revolutionizing the finance ecosystem through digital means.

Speaking during an exclusive interview with this paper, during the launching event that was conducted in Kenyan capital Nairobi, the chief executive told the paper that ACEX will be the first exchange where native producers from Africa can list their produce, fix their competitive price and earn direct rewards from their efforts.

African products such as cobalt, cocoa, and timber will be synthetically indexed and offered as quotes for traders to take advantage of, he says.

"We also have a microfinancing model, which allows us to partner with local microfinance institutions and facilitate them with funds to provide as credits to micro, small and medium enterprises," he said.

Mr Mucheru said for Tanzania, ACEX are currently reviewing some few microfinance institutions - that when approved will start empowering MSMEs with capital access.

"We understand there is still faint knowledge when it comes to digital economy, with many people in the region fearing scams and online fraudsters. The platform offers education materials and through our local franchises, we ensure that one is well informed before they start trading, " he said.

To start tapping on the company potentials one will need to purchase an initial investment of 100 of Temcoin ($XTEM) which is the native cryptocurrency of ACEX.

Tanzanian Digital trader Mr Elibariki Shilla, who has had near three years experience with the ACEX's potential company TE Markets said that stakeholders and investors can take advantage of the centralized platform because it offers multiple assets trading options unlike any other consolidated market in the world.

"For those who fear the digital trading initiatives, there are experts who offer knowledge and understanding on how to properly exploit the opportunity, as one can also trade by following what the verified traders do, step by step," he said.

Another digital entrepreneur Mr Joshua Fanuel also insisted on the youth using this platform to fully exploit the digital opportunities and overcome the unemployment challenges.

He however said in doing so, one need to make sure they gain enough information so that they can make informed and profitable trading decisions.

"Like in any business, before you put your money one needs to know everything there is about that business. Same for this, you need to be well informed and understand how it goes then start trading, " said Fanuel.

In the ACEX platform there will be a handful of verified people who will be known as merchants who will be allowed to engage in the business of converting $XTEM to fiat (nationally issued currencies) and vice versa.

According to ACEX these merchants will be cast across all regions of Africa to facilitate smooth financial transactions because their fee will be minimal. These merchants will additionally be solving the issue associated with foreign remittances on the African continent.
Share:

KP MOTORZ YANG’ARISHA FAMILIA MARATHON 2021 YAKABIDHI GARI KWA MSINDI WA KM 21 WANAWAKE

    
Mkuu wa Mauzo na Uendeshaji wa Kampuni ya Kuagiza na Kuuza Magari ya KP Motorz, Lucas Mwamfupe (kulia), akikabidhi funguo ya gari jipya aina ya Toyota Passo lenye thamani ya shs milioni 9.5 kwa mshindi wa kwanza wa KM 21 Wanawake wa mbio za Familia Marathon 2021, Aisha Ibrahim, jijini Dar es Salaam leo. Wanaoangalia kutoka kushoto ni Meneja Mauzo kwa Makampuni wa KP Motorz, Protas Mbeya na Mwenyekiti wa Familia Marathon, Francisca Alphonce
Mkuu wa Mauzo na Uendeshaji wa Kampuni ya Kuagiza na Kuuza Magari ya KP Motorz, Lucas Mwamfupe (kushoto), akikabidhi cheti kwa mshindi wa kwanza wa KM 21 Wanawake wa mashindano ya mbio za Familia Marathon 2021, Aisha Ibrahim, wakati wa mashindano hayo jijini Dar es Salaam leo. Kulia ni Mwenyekiti wa Familia Marathon, Francisca Alphonce.
Mkuu wa Mauzo na Uendeshaji wa Kampuni ya Kuagiza na Kuuza Magari ya KP Motorz, Lucas Mwamfupe (kushoto), akikabidhi cheti kwa mshindi wa pili wa KM 21 Wanawake wa mashindano ya mbio za Familia Marathon 2021, Jamila Abdallah, wakati wa mashindano hayo jijini Dar es Salaam leo. Kulia ni Mwenyekiti wa Familia Marathon, Francisca Alphonce.
Mkuu wa Mauzo na Uendeshaji wa Kampuni ya Kuagiza na Kuuza Magari ya KP Motorz, Lucas Mwamfupe (kushoto), akikabidhi cheti kwa mshindi wa tatu wa KM 21 Wanawake wa mashindano ya mbio za Familia Marathon 2021, Verah Mrema, wakati wa mashindano hayo jijini Dar es Salaam leo. Kulia ni Mwenyekiti wa Familia Marathon, Francisca Alphonce.
Mkuu wa Mauzo na Uendeshaji wa Kampuni ya Kuagiza na Kuuza Magari ya KP Motorz, Lucas Mwamfupe (kushoto), akikabidhi cheti kwa mshindi wa nne wa KM 21 Wanawake wa mashindano ya mbio za Familia Marathon 2021, Shameeza Mukhi, wakati wa mashindano hayo jijini Dar es Salaam leo. Kulia ni Mwenyekiti wa Familia Marathon, Francisca Alphonce.
Mkuu wa Mauzo na Uendeshaji wa Kampuni ya Kuagiza na Kuuza Magari ya KP Motorz, Lucas Mwamfupe (kushoto), akikabidhi cheti kwa mshindi wa tano wa KM 21 Wanawake wa mashindano ya mbio za Familia Marathon 2021, Nimishal Ladha, wakati wa mashindano hayo jijini Dar es Salaam leo. Kulia ni Mwenyekiti wa Familia Marathon, Francisca Alphonce.
Mshindi wa Mbio za KM 21 Wanawake za Familia Marathon 2021, Aisha Ibrahim akijaribu kuwasha gari lake mara baada ya kukabidhiwa na wadhamini, Kampuni ya Magari ya KP Motorz mara baada ya kumalizika kwa mbio hizo jijini Dar es Salaam leo. Aisha atakuwa pia balozi wa KP Motorz kwa muda wa mwaka mmoja.
Mwenyekiti wa Familia Marathon 2021, Francisca Alphonce (wa nne kushoto), akikabidhi tuzo kwa Mkuu wa Mauzo na Uendeshaji wa Kampuni ya Magari ya KP Motorz, Lucas Mwamfupe ya kutambua mchango wa udhamini wa kampuni hiyo katika mbio za mwaka huu za Familia Marathon zilizotimua vumbi jijini Dar es Salaam leo zikifanyika eneo la Msasani Beach Club. KP Motorz ilitoa gari jipya aina ya Toyota Passo kwa mshindi wa pili wa KM 21 Wanawake.
Mshindi wa Mbio za KM 21 za Familia Marathon 2021, Aisha Ibrahim akipozi kwa picha mbele ya gari lake, Toyota Passo lililotplewa zawadi na Kampuni ya kuagiza na kuuza magari ya KP Motorsz mara baada ya kuibuka kidedea katika mbio hizo jijini Dar es Salaam leo.
Share:

FAMILIA MARATHON 2021 KUTIMUA VUMBI JUMAMOSI DISEMBA 11

Mwenyekiti wa mbio za Familia Marathon 2021, Bi. Francisca Alphonce (wa tatu Kulia), akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo kuhusu mbio hizo zinazotarajiwa kufanyika jijini Dar es Salaam Disemba 11, jumamosi. Wengine ni wawakilishi wa Kampuni zinazodhamini mbio hizo.
Mkuu wa Masoko, Mawasiliano na Uhusiano wa Benki ya KCB, Christina Manyenye (wa nne kushoto), akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo kuhusu udhamini wao katika mbio za Familia Marathon 2021 zinazotarajiwa kutimua vumbi lake jijini Dar es Salaam jumamosi wiki hii. Usajili unaendelea kufanyika katika Tawi la KCB Mlimani City.
Ofisa Habari Familia Marathon (kushoto), akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo kuhusu mbio hizo zinazotarajiwa kufanyika jijini Dar es Salaam Disemba 11, jumamosi. Mbio zitaanzia Msasani Beach Club kuanzia saa 12 asubuhi zikijumuisha mbio za 21km -half marathon, 10km- Corporate Run na 5km -Social Run.
Mkurugenzi Mtendaji was Kampuni ya magari ya KP Motors, Anita Kisima (kushoto), akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo kuhusu udhamini wao katika mbio za Familia Marathon 2021 zinazotarajiwa kutimua vumbi lake jijini Dar es Salaam jumamosi wiki hii. KP Motors itatoa zawadi ya gari aina ya Passo mpya kwa mshindi mwanamke kati ya washindi kumi atakayeshinda mbio za KM 21. Kushoto kwake ni Mkuu wa Masoko Mawasiliano na Uhusiano wa Benki ya KCB, Christina Manyenye na Ofisa Masoko wa UTT Amis, Rahim Mwanga.
Mkurugenzi Uendeshaji wa Planet Fitness, Ramadhani Mdula (kushoto), akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo kuhusu udhamini wao katika mbio za Familia Marathon 2021 zinazotarajiwa kufanyika jijini Dar es Salaam jumamosi wiki hii.
Meneja wa Kampuni ya Rani Sanitary Pads, Mawi Zahor (kulia ), akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo kuhusu udhamini wao katika mbio za Familia Marathon 2021 zinazotarajiwa kufanyika jijini Dar es Salaam jumamosi wiki hii.
Waandaaji na wadhamini wa Familia Marathon 2021 wakionyesha kwa waandishi habari, Dar es Salaam leo, medani na baadhi ya zawadi watakazopewa washiriki wa mbio hizo zitakazofanyika kwa mtindo wa kutembea na kukimbia jijini humo jumamosi wiki hii. Mbio za mwaka huu zimedhaminiwa na KCB Bank, KP Motors, UTT Amis, Premier Security, Optical Centre, Rani Sanitary Pads, Planet Fitness, Knight Support na Xpress Rent.
Share:

LILIAN-FAVOUR MAKAWA

LILIAN-FAVOUR MAKAWA

Popular Posts

Blog Archive

Labels

Recent Posts

Label Cloud

BIASHARA (275) BURUDANI (4) KIMATAIFA (10) KITAIFA (119) MICHEZO (38) SIASA (3)

Pages