Absa Bank Tanzania yasisitiza dhamira yake kuendeleza ukuaji wa uchumi halisi nchini Tanzania

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara, Dk. Suleiman Hassan Serera (kushoto), akikabidhi cheti cha shukurani kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Obedi Laiser, kwa kutambua mchango wa benki hiyo kama mdhamini mkuu wa Kongamano la Biashara la tatu la Maofisa Watendaji Wakuu (200 CEO Business Forum), lililofanyika jijini Dar es Salaam jana.

Benki ya Absa Tanzania imeendelea kusisitiza dhamira yake ya kuendeleza ukuaji wa uchumi halisi wa nchini Tanzania, ikidhamini jukwaa mahsusi linalowakutanisha watendaji wakuu wa makampuni nchini, likijulikana kwa jina la ‘The 200 CEOs Business Forum’.

Jukwaa hilo la ngazi ya juu lilihudhuriwa na Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Viwanda na Biashara, Dkt Suleiman Hassan Serera, sambamba na viongozi wengine waandamizi wa Serikali akiwemo Kamishna wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), na wengineo.

Akizungumza katika hafla hiyo, Mgeni rasmi Dkt. Serera alisitiza umuhimu wa hatua za pamoja ili kupanua ajira na mauzo ya nje huku Benki Kuu ya Tanzania ikitoa mrejesho wa mwelekeo wa uchumi unaosaidia kupanga maamuzi ya bodi, na uwasilisho wa udhamini wa Absa ukugusia suluhisho za kifedha ambazo benki ya Absa inatoa kuwawezesha kampuni kuendesha na kusimamia biashara kwa urahisi ambapo katika mijadala mitatu iliyofanyika ikijikita katika uongozi na utawala bora, afya na uimara wa rasilimali watu, pamoja na njia za ufadhili zinazofungua ukuaji na kuhitimishwa na dira ya PPP.

Akizungumza katika hafla hiyo, Bw. Obedi Laiser, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania alisema Jukwaa hili si mkutano wa mawazo pekee bali ni chombo cha maamuzi yanayosukuma mitaji, kuunda ajira, kurasimisha minyororo ya thamani na kufungua fursa za mauzo ya nje akisema kama Absa, wanajivunia kusimama pamoja na viongozi wa biashara wa Tanzania katika wakati huu nyeti hususani kupitia dhamira yao ya “Kuiwezesha Afrika ya Kesho, Pamoja… hatua moja baada ya nyingine”.

Stori yako ina thamani” si ahadi tu, ndivyo tunavyojitokeza, tumesikiliza kwa makini vipaumbele na mahitaji ya wakurugenzi wakuu, na kwa kujibu tunawasilisha suluhisho zinazochochea kasi ya biashara, zikiwemo Absa Infinite Card, Absa Business Credit Card, Vehicle Asset Finance (VAF), uwezo mpana wa Cash Management & Payments, Trade & Working Capital, Treasury & Risk Management, pamoja na majukwaa yetu ya kidijitali ya benki kwa makampuni yanayosaidia idara za fedha kufanya kazi kwa kasi na udhibiti.

Tunawezesha malengo ya Watendaji wakuu (CEOs) na wajasiriamali kupitia suluhisho bora za kifedha, zenye bei shindani na zinazotolewa kwa wakati na umahiri.” Bw. Laiser aliongeza.

Udhamini huu mkubwa wa Absa unaonesha ushirikiano wa muda mrefu wa benki na Serikali na sekta binafsi wa kuharakisha ukuaji jumuishi. Kuwakutanisha watunga sera na viongozi wa viwanda katika ukumbi mmoja kunawawezesha kuoanisha kanuni, kuandaa miradi inayoweza kufadhiliwa na kuweka mifumo inayochochea uwekezaji kwa kiwango kikubwa - kigeuza dhamira kuwa utekelezaji.

Aidha watendaji hao walipata nafasi za kuzungumza na wafanyakazi wa Absa wakioneshwa suluhisho mbalimbali za kifedha zinazorahisisha maisha yao. Miongono mwa hizo ni huduma ya kifahari inayorahisisha safari za kimataifa kupitia Absa Infinite Card, udhibiti wa matumizi ya kampuni kwa Absa Business Credit Card, udhamini wa manunuzi ya magari binafsi na ya kibiashara kupitia Vehicle & Commercial Asset Finance. Ulinzi wa hatari na mipango ya ukwasi kupitia Bancassurance na Flexi Fixed Deposit, huduma za Prestige na Premier kwa wateja wa hadhi ya juu, Diaspora Banking ikirahisisha miamala ya kuvuka mipaka, na kwa upande wa sekta ya umma, e-Loans, yote yakithibitisha ahadi ya Absa kwamba Stori yako ina thamani.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Obedi Laiser (kushoto), akichangia mada isemayo “Fedha kama chachu ya ukuaji wa biashara Tanzania; Mikakati na Fursa”, wakati wa Kongamano la Biashara la tatu la Maofisa Watendaji Wakuu (200 CEO Business Forum), lililofanyika jijini Dar es Salaam jana.
Share:

Coca-Cola Kwanza hosts Minister of Industry and Trade

The Minister of Industry and Trade Seleman Said Jafo (center) and Coca-Cola Kwanza Ltd Public Affairs, Communications and Sustainability Director Salum Nassor (right) admire a bottle of Coca-Cola drink during the Minister’s tour to the company’s manufacturing plant in Dar es Salaam over the weekend as a part of the government efforts on creating a solid relationship with the private sector. A part from the visit, the Minister also had an opportunity to get insights into the company’s operations, contributions to the Tanzanian economy, and its role in driving shared value creation. Left is Coca-Cola Kwanza Ltd Managing Director David Chait.

Dar es Salaam, Tanzania, Sunday 24 August 2025 - Coca-Cola Kwanza Ltd proudly hosted the Minister of Industry and Trade, Dr Seleman Said Jafo (MP) at its Dar es Salaam facility.

The visit provided a valuable opportunity to showcase the company’s commitment to doing business the right way - guided by integrity, shared value creation, and a deep respect for the communities it serves.

The Minister’s visit included a plant tour and strategic boardroom session, where Coca-Cola Kwanza Ltd, a company in the Coca-Cola Beverages Africa (CCBA) group, shared insights into its operations, contributions to the Tanzanian economy, and its role in driving shared value creation.

This engagement reflects CCBA’s ongoing commitment to strengthening its social license to operate. By leading in environmental, social, and governance (ESG) standards, CCBA aims to create lasting positive impact and contribute to a better shared future.

We believe that by following our values, we can drive sustainable growth and societal progress,” said David Chait, General Manager for Coca-Cola Kwanza Ltd.

People are at the centre of everything we do, from our employees to those who touch our business to the communities we call home. Community involvement allows us to bring positive, measurable change to both the communities in which we operate and to our business,” said David Chait.

Our aspiration is not only to reflect the diversity of the communities where we operate but also to lead and advocate for a better shared future. We aim to create access to equal opportunities and become more inclusive. We embrace differences in backgrounds and support economic inclusion for under-served communities, especially women, youth and people with disabilities.

CCBA looks forward to continuing to build meaningful partnerships that support inclusive economic development and responsible business practices.
Coca-Cola Kwanza Ltd Managing Director David Chait (left) stresses a point to the Minister of Industry and Trade Seleman Said Jafo as he toured the company’s manufacturing plant in Dar es Salaam over the weekend as a part of the government efforts on creating a solid relationship with the private sector. A part from the visit, the Minister also had an opportunity to get insights into the company’s operations, contributions to the Tanzanian economy, and its role in driving shared value creation. Right is Coca-Cola Kwanza Ltd Public Affairs, Communications and Sustainability Director Salum Nassor.
Share:

AGRA, Sahara Accelerator kunufaisha vijana wengi kupitia kilimo

  

Na Mwandishi Wetu

Kilimotech Accelerator kupitia Youth Entrepreneurship for the Future of Food and Agriculture (YEFFA) inayodhaminiwa na shirika la AGRA Tanzania na kutelekelezwa na Sahara Accelerator inatarajia kunufaisha vijana wapatao 265,000 wanaojihusisha na masuala ya kilimo.

Akizungumza wakati wakijadili na vijana kuhusu fursa hiyo jijini Dar es Salaam, Adam Mbyallu wa Sahara Accelerator alisema fursa hiyo itatoa kiasi cha dola milioni 20 kwa bunifu za kilimo zinazojumisha mnyororo wa thamani kwa mazao manne ambayo ni mbogamboga na matunda, alizeti, mpunga na mahindi.

"Tuna hakikisha namna gani tunaweza kusaidia upatikanaji wa vifaa vya kilimo kupitia teknolojia za kidigitali tunasaidia vijana wenye bunifu mbalimbali zinzojibu changamoto za upatikanaji wa vifaa za kilimo," alieleza Mbyallu.

Alisema kupitia bunifu hizo watawapatia vijana hao mafunzo,mentorship na kuwaunganisha wa wadau mbalimbali na kusaidia kwenda shambani kwenye kilimo na kujiuza.
Alifafanua kuwa bunifu wanazotafuta zitajibu changamoto za kilimo kama vifaa,mafundi,masoko,udhibiti wa mazao,uharibifu wa mazao baada ya mavuno changamoto ambazo wadau wa kilimo walisema zipo.

"Maeneo hayo yote kama vinavifaa vya kilimo vingesaidia sana vijana kujiajiri kwenye kilimo kama watajiajiri tunaangalia jinsi ya kuwawezesha kupitia teknolojia ya kidijitali," aliongeza.

Mbyallu alisema ili kufanikisha upatikanaji wa bunifu hizo wamefungua dirisha la usajili wa bunifu kwa muda wa miezi miwili ambapo itafungwa Agosti 18, 2025 na zitachujwa kuangalia kama bunifu hizo zinakidhi vigezo na baada ya hapo watawaunga mkono.

"Tutawaunga mkono Kwa mafunzo,mentorship,changamoto na kuwaunganisha na wadau watakaowasaidia bunifu zao kwenda soko kama wadau wanaouza zana za kilimo,mafundi wa zana za kilimo,wanaotengeneza zana za kilimo,taasisi za fedha na wadau wengine," alisisitiza.
Aliongeza: "Bunifu zitakwenda kwenye mazao manne yamegawiwa katika kanda kuna miradi kulingana na mazao ya eneo mfano Morogoro wanajikita na mbogamboga na alizeti ,Mbeya wana mbogamboga na mpunga, Njombe mbogamboga na mahindi, Singida ni alizeti kila kanda imepewa aina ya zao… tunakwenda kote."
Share:

Airtel Money na Benki ya I&M Wazindua Mpango wa Elimu ya kifedha kuwawezesha Wajasiriamali Wanawake

 

Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Airtel Tanzania, Bw. Charles Kamoto (kulia), akishikana mikono na Mkurugenzi Mtendaji wa I&M Bank Tanzania, Bw. Zahid Mustafa, wakati wa uzinduzi rasmi wa mpango unaolenga kuwawezesha wanawake wajasiriamali nchini kwa elimu ya kifedha na nyenzo nyingine muhimu za kukuza biashara zao. Hafla hiyo ilifanyika jijini Dar es Salaam jana. Katikati ni mmoja wa wanawake wajasiriamali waliohudhuria semina iliyofanyika pamoja na uzinduzi huo, Bi. Virginia Gift.

Airtel Money kwa kushirikiana na Benki ya I&M wamezindua rasmi mpango unaolenga wanawake wajasiriamali ukiwa na malengo ya kuwawezesha wanawake hao nchini kwa elimu ya kifedha na nyenzo muhimu za kukuza biashara zao hivyo kuweza kuboresha maisha yao.

Mpango huu ni sehemu muhimu ya Mkakati wa Uendelevu wa Benki ya I&M Tanzania unaojikita kwenye nguzo tatu kuu ambazo ni ujumuishaji wa kifedha, elimu ya kifedha, na uwajibikaji wa mazingira, ukiendana na Malengo ya Maendeleo Endelevu ya Umoja wa Mataifa (SDGs), hususan SDG 5 (Usawa wa Kijinsia) na SDG 13 (Hatua dhidi ya Mabadiliko ya Tabia nchi).

Kupitia huduma ya Kamilisha, iliyoundwa kwa pamoja kati ya Airtel Money na Benki ya I&M, huwapa wateja uwezo wa kupata mikopo midogo midogo kupitia simu zao ili kukamilisha miamala muhimu kama kutuma pesa au kulipa bili, hata wanapokosa salio kwenye akaunti zao za Airtel Money.

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Mkurugenzi Mtendaji wa Airtel Tanzania, Bw. Charles Kamoto alisema, “kuna matumizi mkubwa ya Airtel Money na ndio tunalenga kujenga uwezo ili kupunguza pengo la matumizi, tunataka kuhakikisha kuwa wateja wetu, hasa wanawake, wana ujasiri na ujuzi wa kutumia huduma za kifedha kidijitali kwa ufanisi.

Kamoto alieleza kuwa zaidi ya asilimia 65 ya watu wazima Tanzania wanakabiliwa na upatikanaji mdogo wa huduma za kifedha, huku wanawake wakiwa katika hali mbaya zaidi.

Kupitia mpango huu, tunasaidia kupunguza pengo la elimu ya kifedha na kusaidia uimara wa kifedha wa muda mrefu, kwa kuwa chini ya asilimia 30 ya wanawake Tanzania wanamiliki simu janja, tumejumuisha mafunzo ya moja kwa moja ya matumizi ya programu za kifedha ili kuwajengea ujasiri watumiaji wapya,” aliongeza Bw. Kamoto.

Katika mafunzo ya siku moja yaliyofanyika jijini Dar es Salaam kama sehemu ya uzinduzi wa mpango huu, zaidi ya wanawake 50 walikusanyika kwa mafunzo shirikishi juu ya usimamizi wa fedha, matumizi ya fedha kidijitali, na mbinu endelevu za biashara, lengo ikiwa siyo tu kutoa ujuzi wa kiufundi, bali pia kuunganisha uwezeshaji wa kiuchumi na maendeleo jumuishi yanayostahimili mabadiliko ya tabianchi.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa I&M Bank Tanzania, Bw. Zahid Mustafa alisema, “Hii ni sehemu ya dhima yetu ya kufanya benki kuwa jukwaa la kuleta mabadiliko, tunajivunia kuongoza mpango huu kwa ushirikiano na Airtel Tanzania, leo tukianza safari hii kwa kutoa mafunzo ya siku moja ya elimu ya kifedha kwa wanawake 60 hapa Dar es Salaam, kwa udhamini kamili, mtaala wa mafunzo haya umetayarishwa kwa kushirikiana na Grant Thornton na utaendelea kuboreshwa kwa kuzingatia mrejesho kutoka kwa washiriki.

Licha ya ukuaji wa huduma za fedha kidijitali, biashara ndogondogo zinazoongozwa na wanawake nchini bado zinakosa huduma rasmi kutokana na ukosefu wa elimu na mifumo ya kifedha. Mpango huu unalenga kuziba pengo hilo kwa kuwapa wanawake ujuzi wa vitendo na ujasiri zaidi kushiriki katika mfumo wa kifedha.

Tangu kuanzishwa kwake, huduma ya Kamilisha imekwisha toa mikopo yenye thamani ya zaidi ya TZS bilioni 392, ambapo asilimia 46 ya mikopo hiyo imekwenda kwa wanawake. Hadi sasa, zaidi ya Watanzania milioni tano wameingia kwenye mfumo rasmi wa kifedha kupitia huduma hii,” aliongeza Mustafa.

Kama sehemu ya mpango huu, Benki ya I&M imeahidi kupanda mti mmoja kwa kila wanawake 100 watakaokopeshwa, na inalenga kupanda miti 8,000 kwa mwaka. Jitihada hizi za kimazingira zinatekelezwa kwa kushirikiana na taasisi ya Africa Transformation Initiative (ATI), ambayo itasimamia upatikanaji, upandaji, na ufuatiliaji wa miti hiyo nchini Tanzania kwa kipindi cha miaka mitatu ijayo.
Mkurugenzi wa Airtel Money, Bw. Andrew Rugamba akizungumza katika hafla ya uzinduzi rasmi wa mpango unaolenga kuwawezesha wanawake wajasiriamali nchini kwa elimu ya kifedha na nyenzo nyingine muhimu za kukuza biashara zao katika hafla hiyo jijini Dar es Salaam jana. Mpango huo unafanyika kwa ushirikiano wa Airtel Money na I&M Bank Tanzania.
Mkurugenzi Mtendaji wa Airtel Tanzania, Bw. Charles Kamoto, akizungumza, katika hafla ya uzinduzi rasmi wa mpango unaolenga kuwawezesha wanawake wajasiriamali nchini kwa elimu ya kifedha na nyenzo nyingine muhimu za kukuza biashara zao katika hafla hiyo jijini Dar es Salaam jana. Mpango huo unafanyika kwa ushirikiano wa Airtel Money na I&M Bank Tanzania.
Mkurugenzi Mtendaji wa I&M Bank Tanzania, Bw. Zahid Mustafa, akizungumza, katika hafla ya uzinduzi rasmi wa mpango unaolenga kuwawezesha wanawake wajasiriamali nchini kwa elimu ya kifedha na nyenzo nyingine muhimu za kukuza biashara zao katika hafla hiyo jijini Dar es Salaam jana. Mpango huo unafanyika kwa ushirikiano wa benki ya I&M na Airtel Money.
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Airtel Tanzania, Bw. Charles Kamoto (walioketi wa pili kulia), Mkurugenzi Mtendaji wa I&M Bank Tanzania, Bw. Zahid Mustafa (wa pili kushoto), Mkurugenzi wa Airtel Money, Bw. Andrew Rugamba (kushoto), na Mkurugenzi Mtendaji wa Grant Thornton Tanzania, Bw. Muntazir Fazel (kulia), wakipozi mbele ya wapiga picha, mara baada ya semina na uzinduzi rasmi wa mpango unaolenga kuwawezesha wanawake wajasiriamali nchini kwa elimu ya kifedha hivyo kukuza biashara zao. Hafla hiyo iliyofanyika jijini Dar es Salaam jana. Wengine ni baadhi ya washiriki na wawezeshaji wa semina hiyo.
Share:

Akiba Commercial Bank Plc Yazungumza na Wateja Wake Mjini Moshi.

Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Akiba Commercial  Bank PLC Bw. Silvest Arumasi akifungua Mkutano wa wateja wa Benki hiyo mkoa wa Moshi wenye lengo la kusikiliza maoni yao, kushirikishana maendeleo ya Beni na kutoa elimu ya fedha. Pia ulikuwa ni jukwaa la kutoa shukrani kwa uaminifu wao tangu Benki ilipoanza kutoa huduma zake katika mkoa hu
wateja wa Benki hiyo wakifuatilia mkutano huo.

Akiba Commercial Bank Plc imeendelea kuimarisha dhamira yake ya kuwa benki inayosikiliza wateja kwa kufanya mkutano maalum na wateja wake jijini Moshi, tarehe 16 Julai 2025. Tukio hilo lilihudhuriwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki, Bw. Silvest Arumasi, kama mgeni rasmi.

Mkutano huo uliwaleta pamoja wateja wa eneo la Moshi kwa lengo la kusikiliza maoni yao, kushirikishana maendeleo ya Benki na kutoa elimu ya fedha. Pia ulikuwa ni jukwaa la kutoa shukrani kwa uaminifu wao tangu Benki ilipoanza kutoa huduma zake katika mkoa huo.

Bw. Arumasi aliwahimiza wateja kutumia majukwaa kama haya kama sauti yao ya moja kwa moja kwa Benki kwa kusema . "Kwetu ACB, kuwa karibu na mteja si kauli tu,  ni utamaduni tunaouishi. Tunathamini maoni yenu na tumejizatiti kuyawekea kazi kwa vitendo," alisisitiza.

Wateja walieleza mafanikio kadhaa ya ushirikiano wao na Benki na kutoa mapendekezo mbali mbali kwa lengo la kunufaisha pande zote mbili.  
Aidha, wateja walionesha kufurahishwa kwa kiasi kikubwa na ushiriki wa moja kwa moja wa Mkurugenzi Mtendaji katika tukio hilo, hususan kwa kujibu hoja mbalimbali papo kwa papo na kutoa maamuzi ya moja kwa moja kwa baadhi ya changamoto zilizowasilishwa. Walimtaja kuwa kiongozi wa mfano mwenye upeo mpana wa kibiashara na uwezo wa kufikiri kimkakati, kipaji na uwezo  unaosaidia  kuharakisha maamuzi muhimu kwa maendeleo ya Benki na ustawi wa wateja.

Katika hitimisho la mkutano, Akiba Commercial Bank iliahidi kufanyia kazi mapendekezo yaliyotolewa na kuendeleza utamaduni wa kusikiliza wateja kama sehemu ya mkakati wake wa kuwa Benki inayosikiliza, inayojali  na inayoleta matokeo chanya katika jamii.

Share:

AIRTEL YAZINDUA HUDUMA YA ‘AIRTEL CHAPAKAZI’ MAALUM KWA WAJASIRIAMALI

Mkurugenzi wa Biashara wa Kampuni ya Airtel Tanzania, Bw. Joseph Muhere (katikati), akizungumza na waadishi wa habari wakati wa uzinduzi wa huduma ya Airtel Chapakazi jijini Dar es Salaam leo. Airtel Chapakazi inalenga kuinua biashara ndogo ndogo kwa kuwawezesha wajasiriamali kote nchini kutumia teknolojia kama daraja la kufikia masoko mapya, wateja wapya na fursa zaidi za kukuza kipato. Kushoto ni Mkuu wa Huduma za Wajasiriamali, Bw. Charles Banduka na Meneja Mahusiano wa Kampuni hiyo, Bw. Jackson Mmbando.

Airtel Tanzania leo imezindua rasmi huduma ya Airtel Chapakazi, suluhusho jipya lililoundwa kuchochea ukuaji wa wajasiriamali na wafanyabiashara wadogo kote nchini. Uzinduzi wa huduma hiyo uliofanyika Makao makuu ya Airtel Tanzania jijini Dar es Salaam, ulionyesha dhamira ya Airtel katika kukuza maendeleo jumuishi ya kidijitali na kuunga mkono ajenda ya kukuza uchumi wa Tanzania.

Airtel Chapakazi inalenga kuinua biashara ndogo ndogo kwa kuwawezesha wajasiriamali kote nchini kutumia teknolojia kama daraja la kufikia masoko mapya, wateja wapya na fursa zaidi za kukuza kipato. Kulingana na takwimu za kitaifa, asilimia 15 tu ya biashara ndogo ndogo na za kati nchini Tanzania kwa sasa zinapata zana rasmi za masoko ya kidijitali, pengo ambalo Airtel Chapakazi inalenga kuziba. Airtel Chapakazi ni suluhisho la kibunifu linaloenda kuwapa wafanyabiashara wadogo uwezo sawa wa kidijitali unaotumiwa na makampuni makubwa.

Huduma ya Airtel Chapakazi inapatikana katika vifurushi vitano (05) vilivyoundwa kulingana na ukubwa na mahitaji na utofauti wa biashara:

● SME chap pack (TZS 100,000): Inajumuisha laini 2 za simu, kila moja ikiwa na GB10 ya data, SMS 1,000, na dakika 1,000 kwa mitandao yote. Pia kifurushi hiki kinajumuisha router ya intaneti ya bure kwa ajili ya matumizi ya ofisi yenye kasi ya 10 Mbps

 Kifurushi cha SME Bomba (TZS 150,000): Inajumuisha laini 3 za simu, kila moja ikiwa na 10GB ya data, SMS 1,000, na dakika 1,000 kwa mitandao yote. Pia kifurushi hiki kinajumuisha router ya intaneti ya bure kwa ajili ya matumizi ya ofisi yenye kasi ya 20 Mbps.

 Fahari Pack (TZS 200,000): Inajumuisha laini 5 za simu, kila moja ikiwa na 10GB ya data, SMS 1,000, na dakika 1,000 kwa mitandao yote. Pia kifurushi hiki kinajumuisha router ya intaneti ya bure kwa ajili ya matumizi ya ofisi yenye kasi ya Mbps 30 na SMS 5,000.

 Supa Pack (TZS 300,000): Inatoa laini 9 za simu zenye data sawa, SMS, na manufaa ya sauti, router ya ofisi ya bure ya Mbps 30, na SMS 10,000 kwa wingi.

● Max Pack (TZS 400,000): Inatoa laini 14 za simu, router ya ofisi ya bure yenye kasi ya Mbps 50, na SMS 15,000 — zinazofaa kwa timu kubwa yenye watu wengi au yenye ukuaji wa kasi ya juu.

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Mkurugenzi wa Biashara wa Airtel Tanzania, Joseph Muhere, alisema Airtel Chapakazi inadhihirisha dhamira ya Airtel kusaidia biashara ndogo ndogo na za kati kupitia huduma suluhishi za kidijitali.

"Kwa kutumia Airtel Chapakazi, wateja watapata msaada wa karibu kutoka kwa mawakala wetu kuanzia hatua ya mwanzo hadi kupakua programu kutoka Play Store. Baada ya taarifa hizo kuthibitishwa, mteja atapokea ujumbe mfupi wa kiunganishi wa kupakua programu ya Airtel Chapakazi kutoka Play Store, mteja atapakua programu hiyo, kuchagua kifurushi: Fahari, Supa, au Max, na kukamilisha malipo ili kuwezesha huduma.” Alieleza Muhere.

Muhere alisisitiza juu ya umuhimu wa biashara ndogo ndogo na za kati katika uchumi wa Tanzania, akibainisha kuwa kundi hilo la wafanyabiashara wajasiriamali linashikilia zaidi ya asilimia 95 ya biashara zote, limeajiri zaidi ya watu milioni 8, na linachangia takriban asilimia 35 kwenye Pato la Taifa, ilhali wengi bado hawajafikiwa na zana za kijiditali ambazo zinaweza kukuza biashara zao kwa kiasi kikubwa.

"Kwa kipindi kirefu, Airtel Tanzania ilikuwa na dhamira ya kuanzisha suluhisho la kidijitali ambalo litaboresha sekta ya biashara na kuchangia katika kukuza uchumi wa nchi na sasa ndoto hiyo imetimia kwa kupitia Airtel Chapakazi," aliongeza Muhere.

Uzinduzi wa Airtel Chapakazi ni sehemu ya dhamira kubwa ya Airtel Tanzania katika kukuza maendeleo jumuishi, yanayoendeshwa na teknolojia nchini kote kwa kuwapa wafanyabiashara wanazohitaji ili kustawi katika zama za kidijitali.
Meneja Mahusiano wa Kampuni ya Airtel Tanzani, Bw. Jackson Mmbando (kulia), akizungumza na waadishi wa habari wakati wa uzinduzi wa huduma ya Airtel Chapakazi jijini Dar es Salaam leo. Airtel Chapakazi inalenga kuinua biashara ndogo ndogo kwa kuwawezesha wajasiriamali kote nchini kutumia teknolojia kama daraja la kufikia masoko mapya, wateja wapya na fursa zaidi za kukuza kipato. Kushoto ni Mkuu wa Huduma za Wajasiriamali, Bw. Charles Banduka na Mkurugenzi wa Biashara wa Airtel, Bw. Joseph Muhere.
Mkuu wa Huduma za Wajasiriamali wa Kampuni ya Airtel Tanzania, Bw. Charles Banduka (kushoto), akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo, wakati wa uzinduzi wa huduma ya Airtel Chapakazi jijini Dar es Salaam leo. Airtel Chapakazi inalenga kuinua biashara ndogo ndogo kwa kuwawezesha wajasiriamali kote nchini kutumia teknolojia kama daraja la kufikia masoko mapya, wateja wapya na fursa zaidi za kukuza kipato. Kushoto kwake Mkurugenzi wa Biashara wa Airtel, Bw. Joseph Muhere na Meneja Mahusiano wa kampuni hiyo, Bw. Jackson Mbando.
Mkurugenzi wa Biashara wa Airtel Tanzania, Bw. Joseph Muhere (katikati), pamoja na baadhi ya wafanyakazi wengine wa Airtel, wakipiga picha nyuma ya bango lililoandaikwa 'Chapakazi' kuashiria uzinduzi rasmi wa huduma mpya ya Airtel Chapakazi, jijini Dar es Salaam leo. Airtel Chapakazi ni suluhusho jipya lililoundwa kuchochea ukuaji wa wajasiriamali na wafanyabiashara wadogo nchini kote.
Share:

Airtel Tanzania Yawapa Walimu Mafunzo ya Ujuzi wa Kidijitali Kupitia Mpango wa SmartWASOMI

Mkurugenzi wa Machapisho na Utafiti kutoka Taasisi ya Elimu Tanzania (TET), Bw. Kwangu Zabron Masalu (Katikati), akizungumza jijini Dar es Salaam jana, wakati wa warsha iliyoandaliwa kwa walimu wa IT, iliyoandaliwa na Airtel Tanzania kupitia Airtel Africa Foundation, kwa kushirikiana na UNICEF na Wizara ya Elimu, chini ya mpango wa Airtel SmartWASOMI, unaolenga kuboresha elimu ya kidigitali kwa kuwawezesha walimu na wanafunzi kupata maudhui ya kielimu kupitia maktaba mtandao ya Taasisi ya Elimu Tanzania na Shule Direct bila gharama ya vifurushi vya data. Kushoto ni Bw. Audax Tibuhinda kutoka Unicef na kulia Bw. Jackson Mmbando, Meneja Mahusiano wa Airtel Tanzania.

Airtel Tanzania kupitia Airtel Africa Foundation, kwa kushirikiana na UNICEF na Wizara ya Elimu, imeandaa warsha ya mafunzo kwa walimu wa IT chini ya mpango wa Airtel SmartWASOMI, mradi wa kisasa wa ujifunzaji wa kidijitali unaolenga kuboresha upatikanaji wa elimu bora kupitia teknolojia.

Warsha hiyo imewakutanisha walimu 60 kutoka shule za msingi na sekondari ambazo tayari zimeunganishwa na mpango wa Airtel SmartWASOMI. Mpango huu ulizinduliwa mwezi Mei 2024 na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, ikiwa ni ushirikiano kati ya Airtel Tanzania kupitia Airtel Africa Foundation, UNICEF na Serikali ya Tanzania. Zaidi ya shule 400 kote nchini zimeunganishwa na jukwaa hili, likiwa na huduma ya bure ya mtandao (zero-rated) kwa majukwaa ya mitaala ya Taasisi ya Elimu Tanzania (TET) na Shule Direct, hivyo kuwapa maelfu ya wanafunzi na walimu fursa ya kupata rasilimali za ujifunzaji wa kidijitali bila gharama za data.

Akizungumza na waandishi wa habari katika mkutano uliofanyika leo jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Kampuni wa Airtel Tanzania, Bi. Beatrice Singano, alisisitiza umuhimu wa walimu katika mafanikio ya mpango huo.

Walimu ndio msingi wa mfumo wetu wa elimu, lengo la warsha hii ya mafunzo ni kuongeza uwezo wa walimu katika kufundisha kwa njia ya kidijitali na kuboresha matokeo ya elimu kwa wanafunzi wa shule za sekondari. Tunawekeza kikamilifu katika kuboresha elimu kupitia kuwaandaa walimu kutoa elimu bora inayojumuisha matumizi ya teknolojia,” alifafanua.

Bi. Singano aliongeza kuwa Airtel SmartWASOMI imeondoa kikwazo kikubwa cha ujifunzaji wa kidijitali kwa kutoa huduma ya kuingia kwenye maudhui ya elimu bila gharama ya data kupitia mtandao wa Airtel, hivyo kuwapa wanafunzi na walimu njia rahisi na ya uhakika ya kufikia vifaa vya kujifunzia vilivyokubaliwa na serikali.

Katika mafunzo ya leo, walimu walipata uzoefu wa moja kwa moja wa kutumia zana za ujifunzaji wa kidijitali kupitia jukwaa la Airtel SmartWASOMI, ikiwa ni pamoja na kufikia maudhui ya mitaala, rasilimali shirikishi, na mbinu za kuingiza zana hizi kwenye ufundishaji wa kila siku darasani. Hii itasaidia walimu kurahisisha upangaji wa masomo, kuboresha ufundishaji kwa kutumia maudhui ya kidijitali, kutoa kazi shirikishi, na kufuatilia maendeleo ya wanafunzi kwa ufanisi zaidi, hivyo kuongeza ushirikiano na ubora wa ufundishaji darasani,” alisema.

Akizungumza katika hafla hiyo, Mkurugenzi wa Machapisho na Utafiti kutoka Taasisi ya Elimu Tanzania (TET), Bw. Kwangu Zabron Masalu, akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa taasisi hiyo, Dk. Aneth Komba, alisema kuwa mafunzo hayo ni sehemu ya utekelezaji wa juhudi kubwa zinazofanywa na Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan, ambaye amesisitiza sana matumizi ya teknolojia ya mawasiliano. Matokeo yake, masomo ya teknolojia sasa yanafundishwa kuanzia elimu ya awali hadi ngazi ya chuo kikuu.

Lengo ni kuhakikisha kuwa fursa hii inaleta mapinduzi katika mfumo wa elimu wa Tanzania, tukizingatia kuwa elimu yetu kwa sasa inalenga zaidi kuzalisha wahitimu wenye ujuzi na umahiri katika kila ngazi,” alisema Bw. Masalu.

Walimu walioshiriki warsha hiyo waliupokea mpango huo kwa furaha kubwa, kwa wengi, ilikuwa mara yao ya kwanza kushiriki kwenye jukwaa kubwa la kidijitali linalolenga shule za sekondari nchini Tanzania.

Bi. Neema Avumba, mwalimu kutoka Shule ya Msingi TEGETA A, jijini Dar es Salaam alisema: “Ningependa kutoa shukrani zangu kwa Airtel Tanzania, UNICEF na serikali kwa kuandaa mafunzo haya leo, kabla ya warsha hii, wengi wetu hatukujua uwezo wa zana za kidijitali, sasa najihisi nimewezeshwa kuleta mbinu mpya darasani, tayari naona jinsi zitakavyowavutia na kuwashirikisha wanafunzi kwa njia ambayo hatukuweza hapo awali.

Kwa upande wake, Bw. Nassoro Shamsi, mwalimu kutoka Shule ya Msingi Mji Mwema, Kigamboni, nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam, aliongeza kwa kusema: “SmartWASOMI imefungua fursa mpya. Sasa tunapata maudhui ya mtaala yaliyowezeshwa na nyenzo za kufundishia bila gharama za data kwa kutumia mtandao wa Airtel. Nimefurahi sana kuanza kutumia ipasavyo jukwaa hili baada ya mafunzo haya.

Mbali na mafunzo ya kiteknolojia, warsha hiyo pia iliwawezesha walimu kushirikiana, kuuliza maswali na kubadilishana uzoefu. Lengo si kuongeza ujuzi tu, bali pia kuunda mtandao wa mabalozi wa ujifunzaji wa kidijitali kote nchini.

Mpango wa Airtel Tanzania ni kufikia zaidi ya shule 1,000 ifikapo mwisho wa mwaka 2025, kwa kuendelea kuwekeza katika miundombinu ya kidijitali, ushirikiano madhubuti na jamii pamoja na msaada kutoka kwa wadau muhimu. Juhudi hizi zinaendana na ajenda ya kitaifa ya kukuza upatikanaji jumuishi wa elimu bora ya kidijitali na kuchangia malengo mapana ya kukabiliana na upungufu wa walimu wenye sifa, kuongeza uelewa wa kidijitali kwa wanafunzi, na kuhakikisha usawa katika upatikanaji wa rasilimali za elimu katika mikoa yote.
Ofisa Vifaa vya Intaneti wa Mradi wa SmartWASOMI, Bw. Harrison Isdory (kulia), akitoa mafunzo kuhusu matumizi ya baadhi ya vifaa hivyo katika wakati wa warsha iliyoandaliwa kwa walimu wa IT, iliyoandaliwa na Airtel Tanzania kupitia Airtel Africa Foundation, kwa kushirikiana na UNICEF na Wizara ya Elimu, chini ya mpango wa Airtel SmartWASOMI, unaolenga kuboresha elimu ya kidigitali kwa kuwawezesha walimu na wanafunzi kupata maudhui ya kielimu kupitia maktaba mtandao ya Taasisi ya Elimu Tanzania na Shule Direct bila gharama ya vifurushi vya data. Hafla hiyo ilifanyika jijini Dar es Salaam jana.
Share:

LILIAN-FAVOUR MAKAWA

LILIAN-FAVOUR MAKAWA

Popular Posts

Blog Archive

Labels

Recent Posts

Label Cloud

BIASHARA (275) BURUDANI (4) KIMATAIFA (10) KITAIFA (119) MICHEZO (38) SIASA (3)

Pages