Airtel Tanzania Yawapa Walimu Mafunzo ya Ujuzi wa Kidijitali Kupitia Mpango wa SmartWASOMI

Mkurugenzi wa Machapisho na Utafiti kutoka Taasisi ya Elimu Tanzania (TET), Bw. Kwangu Zabron Masalu (Katikati), akizungumza jijini Dar es Salaam jana, wakati wa warsha iliyoandaliwa kwa walimu wa IT, iliyoandaliwa na Airtel Tanzania kupitia Airtel Africa Foundation, kwa kushirikiana na UNICEF na Wizara ya Elimu, chini ya mpango wa Airtel SmartWASOMI, unaolenga kuboresha elimu ya kidigitali kwa kuwawezesha walimu na wanafunzi kupata maudhui ya kielimu kupitia maktaba mtandao ya Taasisi ya Elimu Tanzania na Shule Direct bila gharama ya vifurushi vya data. Kushoto ni Bw. Audax Tibuhinda kutoka Unicef na kulia Bw. Jackson Mmbando, Meneja Mahusiano wa Airtel Tanzania.

Airtel Tanzania kupitia Airtel Africa Foundation, kwa kushirikiana na UNICEF na Wizara ya Elimu, imeandaa warsha ya mafunzo kwa walimu wa IT chini ya mpango wa Airtel SmartWASOMI, mradi wa kisasa wa ujifunzaji wa kidijitali unaolenga kuboresha upatikanaji wa elimu bora kupitia teknolojia.

Warsha hiyo imewakutanisha walimu 60 kutoka shule za msingi na sekondari ambazo tayari zimeunganishwa na mpango wa Airtel SmartWASOMI. Mpango huu ulizinduliwa mwezi Mei 2024 na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, ikiwa ni ushirikiano kati ya Airtel Tanzania kupitia Airtel Africa Foundation, UNICEF na Serikali ya Tanzania. Zaidi ya shule 400 kote nchini zimeunganishwa na jukwaa hili, likiwa na huduma ya bure ya mtandao (zero-rated) kwa majukwaa ya mitaala ya Taasisi ya Elimu Tanzania (TET) na Shule Direct, hivyo kuwapa maelfu ya wanafunzi na walimu fursa ya kupata rasilimali za ujifunzaji wa kidijitali bila gharama za data.

Akizungumza na waandishi wa habari katika mkutano uliofanyika leo jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Kampuni wa Airtel Tanzania, Bi. Beatrice Singano, alisisitiza umuhimu wa walimu katika mafanikio ya mpango huo.

Walimu ndio msingi wa mfumo wetu wa elimu, lengo la warsha hii ya mafunzo ni kuongeza uwezo wa walimu katika kufundisha kwa njia ya kidijitali na kuboresha matokeo ya elimu kwa wanafunzi wa shule za sekondari. Tunawekeza kikamilifu katika kuboresha elimu kupitia kuwaandaa walimu kutoa elimu bora inayojumuisha matumizi ya teknolojia,” alifafanua.

Bi. Singano aliongeza kuwa Airtel SmartWASOMI imeondoa kikwazo kikubwa cha ujifunzaji wa kidijitali kwa kutoa huduma ya kuingia kwenye maudhui ya elimu bila gharama ya data kupitia mtandao wa Airtel, hivyo kuwapa wanafunzi na walimu njia rahisi na ya uhakika ya kufikia vifaa vya kujifunzia vilivyokubaliwa na serikali.

Katika mafunzo ya leo, walimu walipata uzoefu wa moja kwa moja wa kutumia zana za ujifunzaji wa kidijitali kupitia jukwaa la Airtel SmartWASOMI, ikiwa ni pamoja na kufikia maudhui ya mitaala, rasilimali shirikishi, na mbinu za kuingiza zana hizi kwenye ufundishaji wa kila siku darasani. Hii itasaidia walimu kurahisisha upangaji wa masomo, kuboresha ufundishaji kwa kutumia maudhui ya kidijitali, kutoa kazi shirikishi, na kufuatilia maendeleo ya wanafunzi kwa ufanisi zaidi, hivyo kuongeza ushirikiano na ubora wa ufundishaji darasani,” alisema.

Akizungumza katika hafla hiyo, Mkurugenzi wa Machapisho na Utafiti kutoka Taasisi ya Elimu Tanzania (TET), Bw. Kwangu Zabron Masalu, akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa taasisi hiyo, Dk. Aneth Komba, alisema kuwa mafunzo hayo ni sehemu ya utekelezaji wa juhudi kubwa zinazofanywa na Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan, ambaye amesisitiza sana matumizi ya teknolojia ya mawasiliano. Matokeo yake, masomo ya teknolojia sasa yanafundishwa kuanzia elimu ya awali hadi ngazi ya chuo kikuu.

Lengo ni kuhakikisha kuwa fursa hii inaleta mapinduzi katika mfumo wa elimu wa Tanzania, tukizingatia kuwa elimu yetu kwa sasa inalenga zaidi kuzalisha wahitimu wenye ujuzi na umahiri katika kila ngazi,” alisema Bw. Masalu.

Walimu walioshiriki warsha hiyo waliupokea mpango huo kwa furaha kubwa, kwa wengi, ilikuwa mara yao ya kwanza kushiriki kwenye jukwaa kubwa la kidijitali linalolenga shule za sekondari nchini Tanzania.

Bi. Neema Avumba, mwalimu kutoka Shule ya Msingi TEGETA A, jijini Dar es Salaam alisema: “Ningependa kutoa shukrani zangu kwa Airtel Tanzania, UNICEF na serikali kwa kuandaa mafunzo haya leo, kabla ya warsha hii, wengi wetu hatukujua uwezo wa zana za kidijitali, sasa najihisi nimewezeshwa kuleta mbinu mpya darasani, tayari naona jinsi zitakavyowavutia na kuwashirikisha wanafunzi kwa njia ambayo hatukuweza hapo awali.

Kwa upande wake, Bw. Nassoro Shamsi, mwalimu kutoka Shule ya Msingi Mji Mwema, Kigamboni, nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam, aliongeza kwa kusema: “SmartWASOMI imefungua fursa mpya. Sasa tunapata maudhui ya mtaala yaliyowezeshwa na nyenzo za kufundishia bila gharama za data kwa kutumia mtandao wa Airtel. Nimefurahi sana kuanza kutumia ipasavyo jukwaa hili baada ya mafunzo haya.

Mbali na mafunzo ya kiteknolojia, warsha hiyo pia iliwawezesha walimu kushirikiana, kuuliza maswali na kubadilishana uzoefu. Lengo si kuongeza ujuzi tu, bali pia kuunda mtandao wa mabalozi wa ujifunzaji wa kidijitali kote nchini.

Mpango wa Airtel Tanzania ni kufikia zaidi ya shule 1,000 ifikapo mwisho wa mwaka 2025, kwa kuendelea kuwekeza katika miundombinu ya kidijitali, ushirikiano madhubuti na jamii pamoja na msaada kutoka kwa wadau muhimu. Juhudi hizi zinaendana na ajenda ya kitaifa ya kukuza upatikanaji jumuishi wa elimu bora ya kidijitali na kuchangia malengo mapana ya kukabiliana na upungufu wa walimu wenye sifa, kuongeza uelewa wa kidijitali kwa wanafunzi, na kuhakikisha usawa katika upatikanaji wa rasilimali za elimu katika mikoa yote.
Ofisa Vifaa vya Intaneti wa Mradi wa SmartWASOMI, Bw. Harrison Isdory (kulia), akitoa mafunzo kuhusu matumizi ya baadhi ya vifaa hivyo katika wakati wa warsha iliyoandaliwa kwa walimu wa IT, iliyoandaliwa na Airtel Tanzania kupitia Airtel Africa Foundation, kwa kushirikiana na UNICEF na Wizara ya Elimu, chini ya mpango wa Airtel SmartWASOMI, unaolenga kuboresha elimu ya kidigitali kwa kuwawezesha walimu na wanafunzi kupata maudhui ya kielimu kupitia maktaba mtandao ya Taasisi ya Elimu Tanzania na Shule Direct bila gharama ya vifurushi vya data. Hafla hiyo ilifanyika jijini Dar es Salaam jana.
Share:

Airtel Money na TCDC Waingia Ubia Kuboresha Sekta ya Kilimo Kidijitali

      

Mkurugenzi wa Airtel Money, Bw. Andrew Rugamba (wa pili kushoto), akisaini makubaliano (MoU) na Mrajis na Mtendaji Mkuu wa Tume ya Maendeleo ya Ushirika Tanzania (TCDC), Dk. Benson Ndiege, ili kuboresha sekta ya kilimo kupitia huduma za mawasiliano na huduma fedha kidijitali. Ushirikiano huu unalenga kuwawezesha wakulima kupata huduma salama na za haraka za malipo, kuongeza ujumuishwaji wa kifedha na kupanua upatikanaji wa pembejeo kwa gharama nafuu, hususan katika maeneo ya vijijini. Waliosimama wakishuhudia kutoka kushoto ni Mkurugenzi wa Sheria wa Airtel Tanzania, Bw. David Lema(kushoto), na Mwanasheria wa TCDC, Bw. Harry Mbogoro. Hafla hiyo ilifanyika mjini Dodoma jana.

Airtel Money Tanzania imesaini makubaliano ya kuingia katika ushirikiano wa kimkakati na Tume ya Maendeleo ya Ushirika Tanzania (TCDC) kwa lengo la kuboresha sekta ya kilimo kupitia huduma za mawasiliano na huduma fedha kidijitali. Ushirikiano huu unalenga kuwawezesha wakulima kupata huduma salama na za haraka za malipo, kuongeza ujumuishwaji wa kifedha na kupanua upatikanaji wa pembejeo kwa gharama nafuu, hususan katika maeneo ya vijijini.

Akizungumza wakati wa kutangaza ushirikiano huo, Mkurugenzi wa Airtel Money Tanzania, Bw. Andrew Rugamba alisema: “Kwa mujibu wa Shirika la Chakula na Kilimo (FAO), kilimo kinachangia takribani asilimia 30 ya Pato la Taifa na kuajiri zaidi ya asilimia 75 ya Watanzania. Hata hivyo, bado wakulima wengi wadogo hawajafikiwa na huduma rasmi za kifedha. Kupitia ushirikiano huu, Airtel Money itatoa suluhisho la malipo ya kidijitali kwa wakulima na vyama vya ushirika, kuwezesha ununuzi wa pembejeo, upatikanaji wa simu janja za bei nafuu, pamoja na kujenga historia ya matumizi ya kifedha. Pia tutatoa elimu ya fedha na huduma kwa wateja kupitia mtandao wetu mpana wa mawakala.

Ushirikiano huu unafikiwa kutokana na mafanikio ya majaribio yaliyofanyika na Airtel kwa kushirikiana na Vyama vya Ushirika vya Masoko ya Mazao (AMCOS), mkoani Morogoro, ambapo Airtel Money lengo lake ni kurahisisha malipo ya pembejeo kidijitali. Matokeo ya awali yalionesha mafanikio makubwa kwa kuongeza uwazi, ufanisi, na upatikanaji wa huduma kwa wakulima wadogo, huku yakipunguza changamoto za kifedha zilizokuwa kikwazo kwa maendeleo yao.

Bw. Rugamba aliongeza: “Kupitia ushirikiano huu, tunaweza kupanua huduma hizi na kuwafikia maelfu ya wakulima nchini kote. Tunajibu moja kwa moja wito wa Waziri wa Kilimo, Mhe. Hussein Bashe, alioutoa Desemba 2023, akiitaka sekta binafsi kushirikiana kwa karibu na wakulima wadogo ambao wengi wao hulima chini ya ekari 2.5, na wanahitaji msaada wa kubadilika kibiashara.

Kwa upande wake, Kamishna na Mtendaji Mkuu wa TCDC, Dkt. Benson Ndiege, alisema: “Makubaliano haya yanaashiria hatua muhimu katika kuimarisha maendeleo ya sekta ya ushirika na kilimo nchini. Kwa kushirikiana na Airtel Money, tunatoa fursa kwa wakulima wetu kustawi na kuendelea kuchangia kikamilifu katika uchumi wa taifa.

Ushirikiano huu pia utawezesha ushiriki wa Airtel Money katika majukwaa mbalimbali ya kitaifa ya kilimo kama vile Maonesho ya Nane Nane, Siku ya Kimataifa ya Ushirika (ICUD), na matukio mengine muhimu yanayoandaliwa na TCDC, hivyo kusaidia kupanua zaidi wigo wa ujumuishwaji wa kifedha vijijini.

Kwa kuweka malipo ya wakulima kwenye mfumo wa kidijitali, na kutoa elimu na nyenzo za kifedha, ushirikiano huu kati ya Airtel Money na TCDC unatarajiwa kubadilisha maisha ya wakulima wa vijijini, kuongeza tija ya kilimo, na kuchochea mabadiliko ya kweli katika mustakabali wa sekta ya kilimo nchini Tanzania.
Mkurugenzi wa Airtel Money, Bw. Andrew Rugamba (wa pili kushoto), akibadilishana hati za makubaliano (MoU) na Mrajis na Mtendaji Mkuu wa Tume ya Maendeleo ya Ushirika Tanzania (TCDC), Dk. Benson Ndiege, katika hafla ya utiaji saini makubaliano hayo yenye lengo la kuboresha sekta ya kilimo kupitia huduma za mawasiliano na huduma fedha kidijitali. Ushirikiano huu unalenga kuwawezesha wakulima kupata huduma salama na za haraka za malipo, kuongeza ujumuishwaji wa kifedha na kupanua upatikanaji wa pembejeo kwa gharama nafuu, hususan katika maeneo ya vijijini. Wengine ni Mkurugenzi wa Sheria wa Airtel Tanzania, Bw. David Lema (kushoto), na Mwanasheria wa TCDC, Bw. Harry Mbogoro. Hafla hiyo ilifanyika mjini Dodoma jana.
Mrajis na Mtendaji Mkuu wa Tume ya Maendeleo ya Ushirika Tanzania (TCDC), Dk. Benson Ndiege (kulia), akizungumza katika hafla ya utiaji saini hati za makubaliano kati ya tume hiyo na Kampuni ya Airtel Tanzania yenye lengo la kuboresha sekta ya kilimo kupitia huduma za mawasiliano na huduma fedha kidijitali. Ushirikiano huu unalenga kuwawezesha wakulima kupata huduma salama na za haraka za malipo, kuongeza ujumuishwaji wa kifedha na kupanua upatikanaji wa pembejeo kwa gharama nafuu, hususan katika maeneo ya vijijini. Kushoto ni Mkurugenzi wa Airtel Money, Bw. Andrew Rugamba. Hafla hiyo ilifanyika mjini Dodoma jana.
Mrajis na Mtendaji Mkuu wa Tume ya Maendeleo ya Ushirika Tanzania (TCDC), Dk. Benson Ndiege (aliyeketi kulia), Mkurugenzi wa Airtel Money, Bw. Andrew Rugamba (aliyeketi Katikati), wakipiga picha ya kumbukumbu katika hafla ya utiaji saini hati za makubaliano kati ya tume hiyo na Kampuni ya Airtel Tanzania yenye lengo la kuboresha sekta ya kilimo kupitia huduma za mawasiliano na huduma fedha kidijitali. Ushirikiano huu unalenga kuwawezesha wakulima kupata huduma salama na za haraka za malipo, kuongeza ujumuishwaji wa kifedha na kupanua upatikanaji wa pembejeo kwa gharama nafuu, hususan katika maeneo ya vijijini. Hafla hiyo ilifanyika mjini Dodoma jana.
Share:

Airtel UNICEF waunganisha shule 30 Mkoani Dodoma na intaneti ya BURE

Mwakilishi wa Afisa Elimu Sekondari Mkoa wa Dodoma, Bi. Grace Samweli, (Kulia) akipokea moja ya vifaa vya intaneti kutoka kwa Meneja wa Kanda wa Biashara wa Airtel Tanzania, Salum Ngururu, wakati wa hafla ya makabidhiano ya vifaa zaidi ya 30 kwa ajili ya shule za sekondari iliyofanyika mkoani Dodoma mwishoni mwa wiki. Msaada wa vifaa hivyo ni sehemu ya utekelezaji wa mradi wa Airtel SmartWASOMI ili kurahisisha upatikanaji wa nyenzo za kufundishia na kusomea kidijitali bila gharama yoyote kwa shule zote za sekondari nchini.

Kampuni ya Airtel Tanzania na Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF) kupitia mradi wake wa kijamii wa Airtel SmartWASOMI, imekabidhi na kufunga vifaa vya intaneti ya kasi kwa shule 30 za sekondari mkoani Dodoma. Vifaa hivi vitawawezesha walimu na wanafunzi kupata huduma ya intaneti bure, ili kujisomea bure kupitia maktaba mtandaoni ya Taasisi ya Elimu Tanzania na majukwaa ya elimu.

Akizungumza katika hafla ya makabidhiano iliyofanyika katika Shule ya Sekondari Mtemi Mazengo, Mkoani Dodoma mwishoni mwa wiki, Meneja wa Kanda ya Airtel Tanzania Dodoma, Bw. Salum Ngururu alisema, SmartWASOMI siyo tu mtandao, bali ni mfumo wa kidijitali unaoleta vifaa, maudhui ya kielimu yanayolingana na mtaala, na jukwaa la usomaji na ufundishaji wa kisasa

Mpango huu unaunga mkono jitihada za Serikali kupitia Wizara ya Mawasiliano katika kutumia teknolojia ya mawasiliano (TEHAMA) kwenye sekta ya elimu,” alisema meneja huyo.

Naye Bi. Grace Samwel akizungumza wa niaba ya Afisa Elimu wa Mkoa wa Dodoma,aliishukuru Airtel na kusema, “Shule zetu sasa zinaweza kusoma kidijitali kwenye maktaba mtandao ya Taasisi ya Elimu (TET) au kupata maudhui kutoka maktaba mtandao ya Shule Direct bila bila gharama ya bando, tunawashukuru Airtel kwa kuwezesha elimu ya kidijitali kufika hadi kwa wanafunzi wetu bila gharama yoyote.

Pia Airtel imeeleza kuwa mradi wa Airtel SmartWASOMI tayari umeshatekelezwa katika mikoa ya Zanzibar, Kilimanjaro, Arusha, Tabora, Mbeya na sasa Dodoma, ikiwa ni sehemu ya mpango mpana wa kuunganisha shule 3,000 nchini kwa kushirikiana na Serikali na UNICEF.

Kwa upande wake, Mwalimu Florian Kashasila alisema; “Vifaa vya intaneti ya kasi ya Airtel tulivyopatiwa leo vitasaidia sana walimu na wanafunzi kupata nyenzo za kufundishia na kujifunzia, ambazo awali hazikupatikana kirahisi shuleni.

Airtel Tanzania imesisitiza dhamira yake ya kuendelea kuwa sehemu ya mabadiliko ya elimu nchini kwa kuhakikisha shule haziachwi nyuma katika safari ya ujumuishaji wa kidijitali.
Mwakilishi wa Afisa Elimu Sekondari Mkoa wa Dodoma, Bi. Grace Samweli, (kushoto) akimkabidhi Mwalimu Mkuu wa Shule ya Fufu Sekondari, Mohammed Hassan, vifaa vya intaneti vya Airtel Tanzania wakati wa hafla ya makabidhiano ya vifaa zaidi ya 30 kwa ajili ya shule za sekondari iliyofanyika mkoani Dodoma mwishoni mwa wiki. Msaada wa vifaa hivyo ni sehemu ya utekelezaji wa mradi wa Airtel SmartWASOMI ili kurahisisha upatikanaji wa nyenzo za kufundishia na kusomea kidijitali bila gharama yoyote kwa shule zote za sekondari nchini.
Mwakilishi wa Afisa Elimu Sekondari Mkoa wa Dodoma, Bi. Grace Samweli, (kushoto) akimkabidhi Mwalimu Mkuu wa Shule ya Sekondari Mwanakianga, Bi. Theresia Mdemu, vifaa vya intaneti vya Airtel Tanzania wakati wa hafla ya makabidhiano ya vifaa zaidi ya 30 kwa ajili ya shule za sekondari iliyofanyika mkoani Dodoma mwishoni mwa wiki. Msaada wa vifaa hivyo ni sehemu ya utekelezaji wa mradi wa Airtel SmartWASOMI ili kurahisisha upatikanaji wa nyenzo za kufundishia na kusomea kidijitali bila gharama yoyote kwa shule zote za sekondari nchini.
Afisa wa Kitengo cha Ufundi wa Airtel Tanzania, Bw. Harrison Isdory (aliyesimama), akitoa maelezo kwa wakuu wa shule za sekondari mkoani Dodoma kuhusu mradi wa Airtel SmartWASOMI na jinsi vifaa vya intaneti vya Airtel Tanzania vitakavyoboresha ufundishaji na usomaji kwa njia ya kidijitali katika shule za sekondari mkoani humo. Kushoto ni Meneja wa Kanda wa Biashara wa Dodoma wa Airtel Tanzania, Bw. Salum Ngururu, na upande wa kulia ni, Mwakilishi wa Afisa Elimu Sekondari wa Mkoa wa Dodoma, Bi. Grace Samweli.
Mwakilishi wa Afisa Elimu Sekondari Mkoa wa Dodoma, Bi. Grace Samweli, (kushoto) akimkabidhi Mwalimu Mkuu wa Shule ya Sekondari Pandambili, Bw. Mengi Lekuchela, vifaa vya intaneti vya Airtel Tanzania wakati wa hafla ya makabidhiano ya vifaa zaidi ya 30 kwa ajili ya shule za sekondari iliyofanyika mkoani Dodoma mwishoni mwa wiki. Msaada wa vifaa hivyo ni sehemu ya utekelezaji wa mradi wa Airtel SmartWASOMI ili kurahisisha upatikanaji wa nyenzo za kufundishia na kusomea kidijitali bila gharama yoyote kwa shule zote za sekondari nchini.
Mwakilishi wa Afisa Elimu Sekondari Mkoa wa Dodoma, Bi. Grace Samweli (Kulia), Meneja Biashara wa Kanda wa Airtel Tanzania, Salum Ngururu (kushoto) na Afisa wa Kitengo cha Ufundi wa Airtel Tanzania, Bw. Harrison Isdory (Katikati) wakiwa kwenye picha ya pamoja na wakuu wa shule za sekondari jijini Dodoma, mara baada ya makabidhiano ya vifaa vya Intaneti chini ya mpango wa Airtel SmartWASOMI. Msaada wa vifaa hivyo ni sehemu ya utekelezaji wa mradi wa Airtel SmartWASOMI ili kurahisisha upatikanaji wa nyenzo za kufundishia na kusomea kidijitali bila gharama yoyote kwa shule zote za sekondari nchini.
Share:

AKIBA COMMERCIAL BANK PLC YAANDAA JUKWAA LA WATEJA MKOANI MBEYA ZAIDI YA WATEJA 150 WASHIRIKI.

   Tanzania – 18 Juni 2025 – Akiba Commercial Bank Plc (ACB) iliandaa mkutano Maalum wa Wateja jijini Mbeya lililowakutanisha zaidi ya wateja 150 kutoka sekta mbalimbali, kwa lengo la kuimarisha mahusiano na kuwataarifu wateja kuhusu maendeleo ya Benki pamoja na fursa mbali mbali za kuwainua wateja kiuchumi.

Jukwaa hili lililenga kutoa taarifa kuhusu maendeleo ya hivi karibuni ya benki, hususan katika huduma za kidijitali na maboresho ya uzoefu wa wateja. Aidha, lilitumika kama jukwaa la kutoa elimu ya kifedha kwa wateja ili kuwasaidia kufanya maamuzi sahihi ya kifedha. Wateja walishiriki kikamilifu kwa kutoa maoni, mrejesho na mapendekezo kuhusu huduma za benki.


Benki ilitumia fursa hiyo kusikiliza, kujifunza na pia kutoa shukrani kwa wateja wake kwa uaminifu na ushirikiano wao wa muda mrefu. Akizungumza katika tukio hilo, Bi. Wezi Mwazani, Afisa Mkuu wa Biashara wa Benki ya Akiba, alitoa pongezi kwa mwitikio mkubwa na kusema: "Mwonekano wa ushiriki huu mkubwa unatupa faraja kuwa wateja wetu wanatuamini na wamechagua Akiba kama Benki yao pendwa. Hatuchukulii jambo hili kuwa la kawaida, na tunaendelea kujitolea kuwahudumia kwa ubora siku zote.


" Bw. Ntupa, Kiongozi wa Jumuiya ya Wafanyabiashara wa Soko la Mbeya, alipongeza juhudi za Benki kwa kuandaa jukwaa lenye maana kubwa, hasa kwa kuweka kipaumbele kwenye elimu ya kifedha. "Majukwaa kama haya ni muhimu kwa maendeleo ya biashara, yanatoa maarifa kwa wateja wetu na kuimarisha uhusiano wa kuaminiana kati ya benki na jamii ya wafanyabiashara," alisema Bw. Mtupa. Akihitimisha tukio hilo,
Afisa Biashara Mkuu wa Akiba Commercial Bank Plc Bi. Wezi Mwazani akifungua mkutano wa wateja ulioandaliwa na benki hiyo mkoani mbeya.

Bw. Humphrey Nyandidi, Meneja wa Tawi la Mbeya, alishukuru wateja kwa ushirikiano wao na kuahidi kuendelea kuwahudumia kwa bidii na kujituma. "Tunathamini sana uaminifu wenu, na tunaahidi kuendelea kuwahudumia kwa ari na moyo wa dhati ili kutimiza matarajio yenu na hata kuvuka kiwango hicho," alisema. Jukwaa hili la wateja ni sehemu ya mkakati mpana wa Benki ya Akiba wa kuimarisha mahusiano na wateja wake kupitia majukwaa ya majadiliano na mirejesho kutoka kwa wateja. Benki inaendelea kujikita katika kutoa huduma shirikishi za kifedha pamoja na elimu ya fedha.

Share:

AKIBA COMMERCIAL PLC YASHIRIKIANA NA TIA KUPANDA MITI 1,500 KATIKA KAMPENI YA UTUNZAJI WA MAZINGIRA

Dar es Salaam, 13 Juni 2025: Akiba Commercial Plc imeonyesha dhamira yake endelevu ya kutunza mazingira kupitia zoezi la kupanda miti kwa ushirikiano na Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA) katika kampasi ya Kurasini, Dar es Salaam. Miti 1,500 imepandwa kama sehemu ya mpango wa Uwajibikaji kwa Jamii (CSR) unaolenga kukuza utunzaji wa mazingira na kuimarisha ustawi wa jamii. Zoezi hilo liliongoza na Afisa Biashara Mkuu wa Benki hiyo Bi. Wezi Mwazani (Picha ya kwanza) kwa kushirikiana na wafanya kazi wengine pamoja na wanafunzi wa TIA.

Akizungumza kwa niaba ya benki katika tukio hilo, Bwana Emmanuel Mseti, Meneja Mwandamizi wa Kitengo cha Wateja Binafsi, alitoa shukrani za dhati kwa uongozi, wafanyakazi na wanafunzi wa TIA kwa mapokezi na ushirikiano mzuri uliowezesha mafanikio ya shughuli hiyo ya kimazingira. Alibainisha kuwa zoezi hili si ishara tu bali ni kitendo kinachoonyesha imani ya Benki kwamba kulinda mazingira ni jukumu la pamoja.
Shughuli hii ni mfano halisi wa imani yetu kuwa kulinda mazingira ni jukumu la kila mmoja wetu. Jukumu letu halikomi tu kwenye kupanda miti peke yake bali, tunaendelea kuhimiza huduma rafiki kwa mazingira kupitia huduma zetu za kidijitali kama ACB Mobile, Internet Banking na Akiba Wakala, ambazo si tu huongeza urahisi na ufanisi, bali pia hupunguza matumizi ya karatasi na kuunga mkono utunzaji wa mazingira,” alisema Bwana Mseti.
Benki pia ilibainisha juhudi zake nyingine za utunzaji wa mazingira ikiwemo jukumu endelevu la kutunza na kuboresha Viunga vya Independence Square jijini Dodoma. Katika tukio hilo, Bwana Mseti aliwahimiza wanafunzi wa TIA kuchukua jukumu la kulinda miti iliyopandwa na kuhakikisha inakua vizuri kwa faida ya vizazi vijavyo.

Pia aliwahakikishia kuwa Benki itaendelea kushirikiana na TIA katika kampeni za mazingira katika kampasi zake nyingine pindi itakapohitajika.

Kwa mtazamo wa Uwajibikaji kwa Jamii, Akiba Commercial inaamini kuwa kwao kurudisha kwa jamii si chaguo bali ni wajibu.

Kupitia sekta za afya, elimu, uwezeshaji wa kiuchumi, na utunzaji wa mazingira, Benki imejitolea katika maendeleo jumuishi na endelevu yanayonufaisha jamii inayoihudumia.

Ili kupata taarifa zaidi kuhusu ushiriki wetu katika maswala ya kijamii na huduma za kibenki kwa ujumla, tafadhali skani QR yetu hapa chini.
Share:

UWT TANGA YAKUNWA NA UCHAPAKAZI WA MBUNGE UMMY MWALIMU

Na - Mwandishi Wetu, TANGA

Jumuiya ya Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) imempongeza Mbunge wa Jimbo la Tanga Mjini, Ummy Mwalimu, kwa uchapakazi na uwajibikaji wake wa kuwaletea wananchi maendeleo na namna anavyoilea Jumuiya hiyo muhimu kwa uhai wa Chama.

Pongezi hizo zimetolewa na Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo wilaya ya Tanga, Bi. Moza Seif, katika Baraza lake la Kikanuni lililokaa Juni 12, 2025 katika Ukumbi wa CCM wilaya ya Tanga ambapo pamoja na mambo mengine, Baraza hilo lilikuwa na ajenda ya kusoma Utekelezaji wa Ilani kwa Madiwani wa Viti Maalum wa Jiji la Tanga.

Bi. Moza amempongeza Mbunge Ummy Mwalimu ambaye amekuwa bega kwa bega na Jumuiya hiyo katika kusukuma gurudumu la maendeleo ndani ya Jiji la Tanga. Katika kuunga mkono juhudi za maendeleo zinazofanywa na Mbunge huyo, uongozi wa UWT Tanga ulimpatia Mbunge Ummy Mwalimu Zawadi mbalimbali za Pongezi ambazo zilipokelewa na Bi. Mwanahawa Mwalimu kwa niaba ya Mbunge.

Sambamba na hilo, Madiwani wa Viti Maalum wa Jiji la Tanga walisoma Utekelezaji wa Ilani ambapo kazi nyingi na miradi mingi ya maendeleo imefanyika katika kipindi cha uongozi wao. Aidha, wanachama wameaswa kuwa wamoja kuelekea Uchaguzi Mkuu Mwezi Oktoba, 2025 kwa kuepuka fitna, majungu na makundi.

Katika hatua nyingine, Baraza hilo lilihudhuriwa viongozi mbalimbali wa Chama wakiwemo Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Tanga, Meja Mstaafu Hamisi Bakari Mkoba ambaye alikuwa Mgeni Rasmi pamoja na Katibu wa CCM wilaya ya Tanga, Jamal Khimji.
Share:

Mkurugenzi wa Benki ya DCB, Sabasaba Moshingi aongoza wafanyakazi wa benki hiyo kujitolea damu wakiadhimisha Siku ya Wachangia damu Duniani

Ofisa Mtendaji Mkuu wa Hospitali ya Aga Khan, Bw. Sisawo Konteh (Kulia) akishikana mikono na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya DCB, Bw.Sabasaba Moshingi, wakati yeye na baadhi ya wafanyakazi wa benki hiyo walipofika hospitalini hapo kujitolea damu kuadhimisha Siku ya Wachangiaji Damu Duniani, jijini Dar es Salaam Leo.

BENKI ya Biashara ya DCB imesema itaendelea kufanya jitihada tofauti katika kusaidia afya za watanzania wenye uhitaji wa kupata damu kutokana na kukabiliwa na changamoto mbalimbali imeelezwa jijini Dar es Salaam leo.

Akizungumza katika zoezi la kujitolea damu kama sehemu ya maadhimisho ya Siku ya Wachangia Damu Duniani, jijini Dar es Salaam leo, Mkurugenzi Mtendaji wa DCB, Bw. Sabasaba Moshingi alisema yeye pamoja na baadhi ya wafanyakazi wenzake wameamua kujitolea damu kwani licha ya benki yao kujishughulisha na utoaji wa huduma za kifedha lakini pia wanabeba jukumu la kuhakikisha watu wanaohitaji damu salama mahospitalini wanazipata bila kuwa na haja ya kusubiria ndugu waje kujitolea.

Leo tupo hapa pamoja na washirika wenzetu hospitali ya Aga Khan kwa lengo la kuchangia damu, tutaendelea kushiriki matukio mengine kama haya na mengineyo yenye lengo la kusaidia kuokoa maisha ya watanzania wenzetu wenye uhitaji wa damu na mahitaji mengine ya kibidamu”, alisema Bw. Moshingi.

Akizungumza katika hafla hiyo Mkuu wa Kitengo cha Maabara katika Hosptali ya Aga Khan, Dk. Caroline Ngimba alitoa hamasa kwa watanzania wote nchini kuwa na moyo na utamaduni wa kujitolea damu bila kusubiri siku rasmi za kitaifa ama kimataifa bali liwe ni jambo endelevu kwani uhitaji wa damu upo kila siku mahospitalini.

Uzuri ukichangia damu kama afya inaruhusu kila baada ya miezi mitatu unaweza kuchangia tena, tungeomba tabia hii iwe endelevu kwani hakuna kiwanda cha kutengeneza damu, damu inayopewa mwanadamu inatoka kwa mwanadamu”, alisema Dk. Caroline.

Naye mtaalamu wa utoaji damu kutoka Mpango wa Taifa wa Damu Salama, Peter Chami alitoa shukurani kwa Benki ya DCB, huku akizitaka taasisi nyingine kuiga mfano wa benki hiyo ili kuokoa maisha ya watanzania wenye shida ya damu kwani mahitaji ya damu ni makubwa sana.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya DCB, Bw.Sabasaba Moshingi, akifanyiwa uchunguzi wa afya yake kabla hajajitolea damu katika Hospitali ya Aga Khan, Dar es Salaam leo, alipongoza baadhi ya wafanyakazi wa benki hiyo kujitolea damu, kuadhimisha Siku ya Wachangiaji Damu Duniani. Picha nyingine zikionesha matukio mbalimbali katika hafla hiyo.
Mkurugenzi wa Mikopo wa Benki ya DCB, Bw. Deogratius Thadei, akijitolea damu katika hafla ya maadhimisho ya Siku ya Wachangiaji Damu Duniani, katika Hospitali ya Aga Khan, Dar es Salaam leo, ambako yeye pamoja na baadhi ya wafanyakazi wenzake walishiriki. Kushoto ni Mkuu wa Kitengo cha Maabara, Dk. Caroline Ngimba na kulia ni Mtaalamu wa mishipa Kutoka Mpango wa Taifa wa Damu Salama, Bw. Peter Chami.
Baadhi ya wakurugenzi wa Benki ya DCB, waliojitolea damu pamoja na baadhi ya wafanyakazi wengine wa benki hiyo wakati wa maadhimisho ya Siku ya Wachangia damu Duniani katika Hospitali ya Aga Khan, Dar es Salaam, leo.
Baadhi ya wafanyakazi wa Benki ya DCB, wakishiriki zoezi la uchangiaji damu Ili kusaidia wenye uhitaji ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Siku ya Wachangia damu Duniani, jijini Dar es Salaam leo.
Baadhi ya wafanyakazi wa Benki ya DCB, wakijitolea damu kusaidia wenye uhitaji ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Siku ya Wachangia damu Duniani, jijini Dar es Salaam leo.
Share:

LILIAN-FAVOUR MAKAWA

LILIAN-FAVOUR MAKAWA

Popular Posts

Labels

Recent Posts

Label Cloud

BIASHARA (271) BURUDANI (4) KIMATAIFA (10) KITAIFA (118) MICHEZO (38) SIASA (3)

Pages